Ugaidi Tanzania Unafanikiwa

Ugaidi Tanzania Unafanikiwa

Kama ugaidi haukufanikiwa awamu ya nne basi hauwezi awamu hii ya tano. Awamu ya nne watu wafitini walifugwa ili kumtawala vizuri mtanzania-divide and rule. Sasa hivi wafitini hawacheleweshwi-hata kama unajitungia tu kawimbo ka uchochezi kadogo, unashughulikiwa mpaka kuku unamuona kama mwewe.

Ugaidi wamefanyiwa CCM huko kusini,umeshwahi kulizungumzia hilo?

La Roma Mkatoliki nnalitowa kabisa kwenye ugaidi kwa kuwa nimepata habari mpya leo niliyokuwa siijuwi.
 

Attachments

  • upload_2017-4-12_14-32-3.png
    upload_2017-4-12_14-32-3.png
    60.4 KB · Views: 29
Ugaidi wamefanyiwa CCM huko kusini,umeshwahi kulizungumzia hilo?

La Roma Mkatoliki nnalitowa kabisa kwenye ugaidi kwa kuwa nimepata habari mpya leo niliyokuwa siijuwi.
Ni kweli kuna matukio yanatokea ya kuuliwa kwa viongozi mbalimbali huko kusini kiasi kwamba wengine wamefikia hatua ya kuhama makazi yao. Ni kweli pia kwamba vituo vyetu vya polisi na askari kiujumla wamekuwa wakishambuliwa kinyama. Lakin yote hayo hayafikii wakati ule mabomu yanalipuliwa na chuki kubwa iliyokuwepo katika jamii ambapo kilele kilikuwa suala la kuchinja.

Matukio yanayotokea sasa yapo ktk maeneo machache ambako visa vyake vinaweza kuelezeka, tofauti na kipindi kile ambapo wananchi waliaminishwa na kugombea haki ya kuchinja mnyama aliyefugwa na masai. Kwangu mimi, hapo palikuwa mahali pa fedheha sana tulipokuwa tumefikia kama jamii.
 
Dhanna ya Mauaji ya kimbari na matukio ya kigaidi ni vitu viwili tofauti.

Sawa jitahidi kutofautisha,

Je, na utekaji wa NIGERIA endapo wangenyamaza kimya mimi na wewe pamoja na Jumuiya za kimataifa wangejua kinachoendelea Nigeria?????

SEMA USIKIKE.......

MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!
 
Ni njia mojawapo ya kupigana na ugaidi, Watanzania wote ni ndugu na yanayowafika hata mimi yanaihusu na ndiyo maana nimeleta mjadalahuu.

Sasa unaposema tunyamaze tusiongee kuhusu ugaidi uliopo Tanzania una maana gani???

Kumbuka kuna watu ambao walikamatwa hapa Tanzania kwa ugaidi, mfano ni yale matukio ya Zanzbar,

Je, hawa nao kwa nini tusiwaseme au wasikamatwe badala yake unatuambia tusiongee kuhusu ugaidi.


Uhuru wa Mtanzania.jpg


SEMA USIKIKE..................


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Kinachoendelea sasa hivi Tanzania ni ugaidi (terrorism).

Lengo la ugaidi ni kuwatia watu hofu na kufikisha ujumbe kwa wengi kwa njia ya hofu.

Matukio yanayoongelewa sana kwenye vyombo vya habari na mitandao yote ya kijamii mpaka nchi za nje kwa sasa ni hayo, kuanzia watu kutekwa, kutolewa bastola hadharani, mauaji ya Kusini huko, watu kukutwa kwenye viroba, kupotea kwa watu na mengi mengineyo, yote yanaashiria ugaidi.

Magaidi hujitokeza na kusema sisi ndiyo tuliyoyafanya hayo ili waogopwe au matakwa yao yatimizwe au hukaa kimya na kuwachochea kivingine kwa lengo hilo hilo.

Matukio ya ugaidi yanapotokea pia hujitokeza wengine ambao hutumia fursa hiyo kufikisha ujumbe wao kwa njia tofauti.

Kwa yanayotokea Tanzania, ukweli ni kuwa, kuna wanaofanya huo ugaidi wa kutisha na kuna wanaotumia huo gaidi kama ni fursa kwao kufikisha ujumbe wao ama kwa kuongezea ugaidi mwingine au kwa kuendeleza hofu kwenye jamii na vyombo husika.

Watanzania tunachotakiwa kufanya ni kukaa kimya na kufunga hii mijadala yote na kuwacha kuripoti matukio yote ya kigaidi ili kushindana na ugaidi.

Gaidi kama matukio yake hayaongelewi kazi yake inakuwa haijafanikiwa.

Au leta mawazo yako ni njia gani zitumike kutatuwa hili tatizo "linalotukabili".

Kwa muono wangu, kila tunapoyaongea na kuyasambaza ndiyo furaha ya magaidi na ndiyo lengo lao, wengi wajawe na hofu.

Kwanini? Mie sijuwi.
Huyu Faiza Fox anakuaga na kauli za kukera lakini ana akili zaidi tunavyompa credit. Kwa mfano kwenye hii thread kaongea point tupu kwa wale tunaoelewa war on terror.
 
Na wakishawateka ndugu zetu wakawadhuru na kuwatia ulemavu tusiwapeleke hospitali wala kukaa nao karibu!!! pia wakiwaua tuwaachie wao wawazike wala tusiweke msiba!!!

Ama kitanda usichokilalia....
 
Kwanza Raisi ampangie kazi nyingine Bashite, hapo nahisi Magaidi watakosa point, maana matukio yote ya ugaidi mwisho anatajwa Bashite. Rais atafute kijana mwingine wa Kisukuma anayemwamini aanzie alipoishia Bashite

Angesakamwa kabla ya kutangaza vita vya madawa ningeelewa lakini baada ya hiyo vita, hata asemwe vipi nnaona kuwa ni vita ya madawa tu.

Ulisikia wapi kuna vita vya upande mmoja tu?
 
FaizaFoxy

Una pointi ya msingi kwamba sehemu kubwa ya lengo la ugaidi ni kuogopesha jamii na kuifanya ifuate matakwa ya magaidi.

Lengo hili linafanikishwa na kusambazwa kwa habari za ugaidi.

Hivyo, kwa upande mmoja, kukataa kuripoti habari hizi za ugaidi kunaweza kusaidia kudhoofisha kiasi cha lengo hili kufikiwa.

Vyombo vingi vya habari vimeshawahi kufanya namna ya jambo hili. Mfano mmoja ni vyombo kadhaa vya Marekani vilivyokataa kutaja jina au kutoa picha ya Adam Lanza aliyeua watu kwa kuwapiga risasi ovyo katika shule ya Sandy Hook Connecticut.

Lakini, tunapoangalia tija ya kufanya hivi, tupime kwa mizani itakayotuletea tija bila kuleta madhara mengine.

Nchi za kidemokrasia zinaendeshwa kwa misingi ya uwazi na uhuru wa habari. Wananchi wana haki ya kupewa habari. Wanahabari wana wajibu wa kutoa habari.

Zaidi, habari za ugaidi zinaweza kusambazwa katika lengo na minajili ya kumaliza ugaidi.

Mathalani, habari za ugaidi zinaweza kuenea, ikiwamo picha za magaidi, na kusaidia magaidi hao kukamatwa kwa msaada wa wananchi.

Pia, habari za ugaidi zinaweza kusambazwa na kuweza kuisaidia jamii kujihami. Mfano, kama eneo la Rufiji lina ugaidi, habari za kuwaasa wananchi kwamba wachukue tahadhari wanapotembelea eneo hilo, kwa sababu lina ugaidi, zitakuwa habari muhimu katika kuwatayarisha wananchi wajihami vizuri na kuchukua tahadhari zote kabla ya kutembelea eneo hilo.

Kwa kifupi, kwa upande mmoja kuna haja ya kuacha kuhamanika sana na kuandika habari za ugaidi ovyo kiasi cha kutisha wananchi na kuwasaidia magaidi. Kwa upande wa pili, kuacha kabisa kuandika habari za ugaidi kutaweza kusababisha matatizo vilevile.

Kuna kanuni kadhaa nzuri na muhimu katika kuamua kutoa ama kutotoa habari ya kigaidi.Chache kati ya hizo ni:-

1. Habari itasaidia kuelimisha jamii kupambana/ kujihami na ugaidi?
2. Habari itamsaidia zaidi nani? Jamii au gaidi?
3. Kamahabari ikitolewa, itolewe kwa kiwango gani? Kutoa picha za watu waliouawa kinyama kutafaa au kutakosa staha kwa umuhimu wa maisha ya binadamu?
4. Habari zimethibitishwa au hazijathibitishwa na zinaweza kusababisha kashfa isiyo kweli (libel)?
5. Habari zinaandikwa kwa ukweli (facts) tu na si kwa ushabiki.
6. Gaidi hapewi uwanja wa kujitangaza zaidi ya inavyohitajika kuihami na kuifunza jamii.
7. Habari haiingilii wala kuharibu uchunguzi wa polisi na vyombo vya usalama.
8. Habari haihatarishi usalama wa raia wasio na hatia (kama kutaja vyanzo vinavyoweza kuumizwa na magaidi)
9. Habari haihatarishi usalama wa waandishi wa habari. Ikifikia sehemu ambayo waandishi wataanza kuhatarisha usalama wao,usalama wao uwe na kipaumbele kuliko habari.
10. Mizani mizuri itumike kati ya kuchapisha habari mapema na kuihakiki vya kutosha ili isiwe na au ipunguze makosa.
 
Kinachoendelea sasa hivi Tanzania ni ugaidi (terrorism).

Lengo la ugaidi ni kuwatia watu hofu na kufikisha ujumbe kwa wengi kwa njia ya hofu.

Matukio yanayoongelewa sana kwenye vyombo vya habari na mitandao yote ya kijamii mpaka nchi za nje kwa sasa ni hayo, kuanzia watu kutekwa, kutolewa bastola hadharani, mauaji ya Kusini huko, watu kukutwa kwenye viroba, kupotea kwa watu na mengi mengineyo, yote yanaashiria ugaidi.

Magaidi hujitokeza na kusema sisi ndiyo tuliyoyafanya hayo ili waogopwe au matakwa yao yatimizwe au hukaa kimya na kuwachochea kivingine kwa lengo hilo hilo.

Matukio ya ugaidi yanapotokea pia hujitokeza wengine ambao hutumia fursa hiyo kufikisha ujumbe wao kwa njia tofauti.

Kwa yanayotokea Tanzania, ukweli ni kuwa, kuna wanaofanya huo ugaidi wa kutisha na kuna wanaotumia huo gaidi kama ni fursa kwao kufikisha ujumbe wao ama kwa kuongezea ugaidi mwingine au kwa kuendeleza hofu kwenye jamii na vyombo husika.

Watanzania tunachotakiwa kufanya ni kukaa kimya na kufunga hii mijadala yote na kuwacha kuripoti matukio yote ya kigaidi ili kushindana na ugaidi.

Gaidi kama matukio yake hayaongelewi kazi yake inakuwa haijafanikiwa.

Au leta mawazo yako ni njia gani zitumike kutatuwa hili tatizo "linalotukabili".

Kwa muono wangu, kila tunapoyaongea na kuyasambaza ndiyo furaha ya magaidi na ndiyo lengo lao, wengi wajawe na hofu.

Kwanini? Mie sijuwi.
Atleast leo wewe bibi nimeweza kuelewa kidogo uzi wako,umekuwa sasa hongera.
 
Back
Top Bottom