Ugaidi Tanzania Unafanikiwa

Ugaidi Tanzania Unafanikiwa

Kinachoendelea sasa hivi Tanzania ni ugaidi (terrorism).

Lengo la ugaidi ni kuwatia watu hofu na kufikisha ujumbe kwa wengi kwa njia ya hofu.

Matukio yanayoongelewa sana kwenye vyombo vya habari na mitandao yote ya kijamii mpaka nchi za nje kwa sasa ni hayo, kuanzia watu kutekwa, kutolewa bastola hadharani, mauaji ya Kusini huko, watu kukutwa kwenye viroba, kupotea kwa watu na mengi mengineyo, yote yanaashiria ugaidi.

Magaidi hujitokeza na kusema sisi ndiyo tuliyoyafanya hayo ili waogopwe au matakwa yao yatimizwe au hukaa kimya na kuwachochea kivingine kwa lengo hilo hilo.

Matukio ya ugaidi yanapotokea pia hujitokeza wengine ambao hutumia fursa hiyo kufikisha ujumbe wao kwa njia tofauti.

Kwa yanayotokea Tanzania, ukweli ni kuwa, kuna wanaofanya huo ugaidi wa kutisha na kuna wanaotumia huo gaidi kama ni fursa kwao kufikisha ujumbe wao ama kwa kuongezea ugaidi mwingine au kwa kuendeleza hofu kwenye jamii na vyombo husika.

Watanzania tunachotakiwa kufanya ni kukaa kimya na kufunga hii mijadala yote na kuwacha kuripoti matukio yote ya kigaidi ili kushindana na ugaidi.

Gaidi kama matukio yake hayaongelewi kazi yake inakuwa haijafanikiwa.

Au leta mawazo yako ni njia gani zitumike kutatuwa hili tatizo "linalotukabili".

Kwa muono wangu, kila tunapoyaongea na kuyasambaza ndiyo furaha ya magaidi na ndiyo lengo lao, wengi wajawe na hofu.

Kwanini? Mie sijuwi.
Kamarade, na dadaangu ktk jamvi la JF...kuna ugaidi! Na unatusulubu...lkn ukweli mbaya, na usiofurahisha ni namna wanasiasa walivyoanza cheza siasa hata ktk hili... "mmoja, mwenye asili ya kutokea pembe ya afrika, anadai hata yeye, na wenziwe, kina msukuma, na malima, "walitekwa!"....hatukubali taarifa ya kunyanyaswa kwao, kama tusivyokubali kunyanyaswa mtu mwingine yoyote.....lkn, wakati, tunatafakari masuala ya kutekwa kwa kina Roma, na Ben saa8, ....kutuletea "maugomvi, na kupishana, na kuthibitiana kichama" na kutaka kupata sympathy ile ile wanayopatata kina Ben saa8, inakuwa ni kuleta uchuro ktk maana nzima na tafsiri ya "kweli" ya kutekwa....tusipotafakari, wanasiasa siku ingine watakapozidiwa na "mambo ya ndani, ktk vibanda hasara", watatujia na kutueleza kuwa ,vibanda hasara hivyo ni njama za mahasimu wao, na vilitumika kuwateka....
...tuwe makini na wanasiasa wenye kufanya siasa kimchezomchezo, na wenye kutumia masahibu ya "mitaani", kama kifaa ktk makabiliano yao "mchezoni"...
 
Ndo mkae mkijiuliza why ben? Why Roma? Tiss sio machizi kama wengi wenu humu, wale watu sio wa mchezo wana mbinu za kiitelijensia ya hali ya juu, cha muhimu ni watu maarufu kujua mipaka yao nini wanatakiwa kusema na kwa wakati gani, hakuna aliyedhihaki serikali akabaki salama, why wakamatwe ben na roma pekee? Sio mnakurupuka tu mnafikiri Tiss ni vibaka tu wa mitaani
Kama ndio wale waliokuwa na makonda clouds basi hatuna usalama pale
 
Nimeanza kujiuliza.

Fisadi na gaidi, yupi ana nafuu?

Tukumbuke gaidi lazima awe fisadi. Lakini fisadi fisadi si lazima awe gaidi!
 
Lengo la ugaidi ni kuwatia watu hofu na kufikisha ujumbe kwa wengi kwa njia ya hofu.

Mkuu FaizaFoxy,
Kutokana na kifungu hicho hapo chenye rangi tujaribu tuyapitie matamko yafuatayo;
1 .I wish I could be IGP
2.Ningekuwa na uwezo ningeomba Malaika washuke wazime mitandao.
3. Watu wanaimba waziwazi kuwa tuna imani na fulani halafu unawaacha tu.
4.Hakuna kufanya fyoko fyoko mimi ndiye Rais sina ushirika na mtu.

:Wadau ongezeni mengine ,niliyoyasahau

 
Terrorism maana yake ni vitisho, hata nyumbani unapomkemea mwanao ni vitisho "terror".

Inabidi ubadili njia na uanze kumlea bila kutishana.

Chini hapo nimesema, sijuwi. Ni mjadala.
kwahiyo unamaanisha hata huyu kiongozi wetu anapotoa kauli za vitisho naye ni GAIDI?
 
Magaidi? Ndio nani? We mama unataka tuikimbie nchi yetu au? Kha!
 
How to fight state sponsored terrorism is the million $ question.
Certainly not by keeping quiet
 
habari za ugaidi ndio zinapendwa sana na CHADEMA na ndio wamejaa huku kwenye mitandao wanazisambaza kwa kasi sana....leo Magufuli anaweka jiwe la msingi ujenzi wa reli hakuna anaejali....CHADEMA wako busy na habari za watu kutekwa! CHADEMA ni janga la Taifa

Anayecheza mchezo wa UGAIDI anajulikana vizuri sana na system inamjua sana,anatumia MADARAKA yake kutesa na kuua,lakini mwisho wa siku hakuna siri ya watu wawili.

TUnajua hata wewe ni mmoja wa wale wanaotuhumiwa,usijekucheza na uhai wa mtu halafu unakuja kuonyesha upupu barabarani.

Mhusika mkuu ni Bashite mkemeeni aache.
 
Wewe ndo hujui, huo si ugaidi. Ugaidi una lengo la kushinikiza serikali/taasisi flani kufanya au kuwapa wanachohitaji. Sasa hawa wa tz wanahitaji nini maana hawajajitokeza.

Wanataka msiwakosoe,wanataka muwapigie makofi kwa kila jambo hata kama ni ovu.
 
Anayecheza mchezo wa UGAIDI anajulikana vizuri sana na system inamjua sana,anatumia MADARAKA yake kutesa na kuua,lakini mwisho wa siku hakuna siri ya watu wawili.

TUnajua hata wewe ni mmoja wa wale wanaotuhumiwa,usijekucheza na uhai wa mtu halafu unakuja kuonyesha upupu barabarani.

Mhusika mkuu ni Bashite mkemeeni aache.
subiri niko kwenye uzinduzi wa reli ya kati kwa maslahi ya Taifa na wananchi nikitoka hapa nitakujibu wewe mfuasi wa magaidi
 
subiri niko kwenye uzinduzi wa reli ya kati kwa maslahi ya Taifa na wananchi nikitoka hapa nitakujibu wewe mfuasi wa magaidi

Kwa kawaida MTAWALA anatumia nguvu kubwa pale Performance yake inapokuwa below 0.Mfuasi wa magaidi ni Makonda anayetumi Taasisi nyeti Kuteka,kutesa na kuua.

Tumeshabadili jina kwa sasa mnaitwa Chama Cha Mauaji
 
Tufanye nini?
Kama ulivyosema "lengo la ugaidi ni kuwatia hofu ili ujumbe ufike kwa njia ya hofu" hapo panakuwa na sababu ya wao kutenda huo ugaidi na mara nyingi inakuwa
1) Yule anaefanya ugaidi anahisi anaonewa na hasikilizwi na kila anapojaribu kujieleza angalau asikilizwe ama hasikilizwi kabisa au anasikilizwa lakini anapuuzwa, mtu au hicho kikundi hufanya vitendo vya kigaidi dhidi ya wanaowapuuza, hii imetokea sana kule Ireland kati ya wakatoliki na waprotestant, kwa bahati mbaya wengi tumekuwa na tafsiri potofu kuhusisha ugaidi na uislam, huko nyuma pia ulifanyika ugaidi dhidi ya tawala za kikoloni na kibaguzi, sababu tawala ziliwapuuza waliopaza sauti kupinga matendo ya watawala.

2) Panakuwa na kundi la utawala ambalo vitendo na maamuzi yake vinakua havikubaliki na baadhi ya raia wake, sasa wale wanaopinga na kupaza sauti wakijenga hoja zao na ikaonekana hoja zao zina mashiko na kwamba kuna dalili za raia kuwaunga mkono, hofu huwaingia na kufanya vitendo vya kigaidi dhidi ya raia, haya yalifanywa na tawala katika nchi nyingi za latin
america na baadhi ya nchi za Africa.
Nikijibu swali lako ni kwamba vitendo nilivyoongelea hapo juu vilikoma baada ya watu kuingia katika meza ya majadiliano, watawala wawasikilize hata kama ni wachache lakini waendelee na maamuzi yao ya wengi, ukiwapa watu nafasi ya kupumua na kutowatisha katika maelezo yao mengi unaweza ukaokota moja ambalo nao wataona umewajali na ukapunguza munkari wa kujiona wanaonewa na kupuuzwa, maana hapa nchini hofu ya kupinduliwa serikali iliondolewa kwa kuanzisha mfumo wa vyama vingi, na hapo presha ya serikali ikapungua kwa kiasi kikubwa, hivi sasa sielewi kwa nini watawala wanakuwa na hofu dhidi ya mawazo kinzani, serikali ina vyombo vyote vya ulinzi na usalma.
Nakumbuka huko nyuma wapinzani walikua wakizuiwa kufanya maandamano, nadhani ilikua wakati wa kamanda Maji(nisahihishwe kama nimekosea) na presha ikawa juu sana, Tibaigana alipohamishiwa hapa akasema wanaotaka kuandamana njooni tuongee maandamano yanaazia wapi, yanaishia wapi, muda na njia ya kupita, akawapa ulinzi CUF wakaandamana na kufanya mkutano pale jangwani, hapakuwa na fujo, hili joto la sasa hivi ni kwa sababu wapinzani wanataka kutoa hisia zao na watawala hawataki kusikia toka kwa wapinzani, na wao kazi yao ni siasa, na siasa bila mikutano ni ngumu, hapo ndipo ninapomkumbuka Jakaya bingwa wa siasa za Tanzania, aliwapa nafasi watoe nyongo zao na alisema maneno yao wala hayamnyimi usingizi, na baadhi ya maneno yao aliyachukua na kuyafanyia kazi na nchi imesonga mbele sana, na wapinzani wanajua kuwa Jakaya ni bingwa wa siasa pamoja na kelele zao zote.
Ugaidi unaotokea huko Pakistan na baadhi ya nchi za mashariki ya kati ni kama ule uliokuwa Ireland kuna kundi la watu wanaona kuwa wanaonewa na hawasikilizwi na mbaya zaidi baadhi ya walioko madarakani wanapandikizwa chuki na mataifa ya magharibi.
Hapa kwetu hatuna budi kusikiliza iwe ni vikundi vya dini wana mahitaji/maoni gani, iwe ni vyama vya siasa vina maoni/mahitaji yepi hapo tutapunguza shinikizo la ugaidi/usalama, lakini njia yoyote ile ya kutisha na kuwajengea hofu huwa hazifaulu ni jambo la muda tu wanaibuka wengine, mtabaki kila siku kukimbizana na watu.
Kwenye mawazo kinzani si kila anaepinga ana nia ovu, mwingine anapinga sababu haelewi na mwingine anapinga sababu anadhani njia unayotumia si sahihi japo anaweza kuwa anaunga mkono hilo jambo, mfano wote tunahitaji watoto wetu wapate elimu iliyo bora, lakini tunatekelezaje hapo ndipo pana mawazo kinzani.

Tufanye nini?
Jibu; Ni meza huru ya majadliano.
 
Ngoja siku ukitekwa wewe na sisi tukae kimya na vyombo vyote vya habari vikae kimya ili tuwakomoe magaidi.
 
Kwa kawaida MTAWALA anatumia nguvu kubwa pale Performance yake inapokuwa below 0.Mfuasi wa magaidi ni Makonda anayetumi Taasisi nyeti Kuteka,kutesa na kuua.

Tumeshabadili jina kwa sasa mnaitwa Chama Cha Mauaji
angalia hata TV uone rais wako anazindua reli ya kati sio kukalia majungu muda wote
 
habari za ugaidi ndio zinapendwa sana na CHADEMA na ndio wamejaa huku kwenye mitandao wanazisambaza kwa kasi sana....leo Magufuli anaweka jiwe la msingi ujenzi wa reli hakuna anaejali....CHADEMA wako busy na habari za watu kutekwa! CHADEMA ni janga la Taifa
Aiseee,i ddnt expect ,ndo unawaza huu ujinga!?

Hivi hao kuna bashevwanaolalamika ,nk ndo cdm?!

Kuna wakati muwe mnawaza kesho yenu sio ushabiki wa kijinga jinga
 
Kinachoendelea sasa hivi Tanzania ni ugaidi (terrorism).

Lengo la ugaidi ni kuwatia watu hofu na kufikisha ujumbe kwa wengi kwa njia ya hofu.

Watanzania tunachotakiwa kufanya ni kukaa kimya na kufunga hii mijadala yote na kuwacha kuripoti matukio yote ya kigaidi ili kushindana na ugaidi.

Gaidi kama matukio yake hayaongelewi kazi yake inakuwa haijafanikiwa.

Au leta mawazo yako ni njia gani zitumike kutatuwa hili tatizo "linalotukabili".

Kwa muono wangu, kila tunapoyaongea na kuyasambaza ndiyo furaha ya magaidi na ndiyo lengo lao, wengi wajawe na hofu

Kwanini? Mie sijuwi.

Ndugu yangu Faiza kwanza binafsi nashukuru kwa wewe pia kuliona hili, ya kuwa yanayofanyika tanzania ni ugaidi.

Lakini acha tuongee huenda hawa Magaidi wataacha au wataona AIBU kwa vitendo vyao vya Kigaidi, kwani hatujui kesho atatekwa nani huenda mimi au wewe. Na hawa magaidi wanafahamika hata walipo, hawa ni magaidi tofauti na wale Alsha-ashab, Boko Haramu, Al-Qaeda, au IS; ambao matendo yao huyafanya kwa kujificha kiasi kwamba hata askari kupambana nao ni ngumu kiasi.

Lakini magaidi wa Tanzania ni kwamba asilimia kubwa wanafahamika.

NDUGU ZANGU HIVI KUNA TOFAUTI GANI KATI YA UTEKAJI UNAOFANYWA TANZANIA NA ULE WA BOKO HARAMU WA KUTEKA WASICHANA ZAIDI YA 200 KULE NIGERIA??????

Boko Haram in Nigeria.jpg


Nigerian Girls in Boko Haram Video Identified

HIVYO NI JUHUDI ZINAHITAJIKA KATIKA KULIMALIZA HILI SUALA LA UGAIDI HAPA TANZANIA.

BINAFSI NAOMBA VYOMBO VYA DOLA TANZANIA PIA HATA JUMUIYA YA KIMATAIFA KUINGILIA KATI KAMA WANAVYOFANYA NCHI ZA SYRIA, MISRI, IRAQ, SOMALIA.

TANZANIA NI NCHI YA AMANI, HIVYO HATUJAZOEA KUISHI KWA HOFU.

MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU WABARIKI WATANZANIA



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
angalia hata TV uone rais wako anazindua reli ya kati sio kukalia majungu muda wote

Majungu yapi,unadhani nani analipa kama siyo kodi yangu?Unadhani inalipwa na mshahara wake?Acho upumbavu?Mie siwangalii watu wanaosupport mauaji ya aina yeyote ya kiakili au kimwili
 
Back
Top Bottom