Ugali unaopikwa kwa Unga wa mahindi (dona) hatari kwa afya ya binadamu

Ugali unaopikwa kwa Unga wa mahindi (dona) hatari kwa afya ya binadamu

Sio kwamba tusiile dona.Tule dona yenye zero au very small contamination ya Aspergillus au poisonous fungi wengine wanaomea sana kwenye punje za mahindi zilizohifadhiwa vibaya
 
Daaaah maisha ni magumu kama ni hivyo, ukichukua demu utaambiwa ukimwi, ukivuta sigara utaambiwa cancer, ukinywa konyagi utaambiwa livercirhosis, ukila kiti moto utaambiwa kisukali , shenzi kabisa sasa nimeamua sifuati tena maushauri yenu

Usifuate uteseke kwa magonjwa.
 
Vijijini ndo vyakula vyao na wamevitumia enzi na enzi kama ni kweli wengi wangekuwa wameshakufa


Kwani kijijini kwenu hajawahi kufa watu kwa saratani ya ini!?
 
Tufwile nyambala Kyala nnunu gwe! Hatufi kirahisi rahisi hivyo wewe njoo na style nyingine boss

Kumbe hata fungus akitokoshwa Kwenye uji hafi anazidi kuwa strong ahahahahahhaha Asante Kwa hii elimu ya fungus hafi Kwenye uji
Tatizo ni hiyo sumu iitwayo Aflatoxin itolewayo na hao fungus huwepo kwenye mahindi hata hao fungi akifaa.

Hao fungi hata kwenye karanga wapo.


Cha muhimu ni kusafisha mahindi vizuri kabla ya kusaga.
 
Kwani kijijini kwenu hajawahi kufa watu kwa saratani ya ini!?
Ni kweli mkuu,maana kijijini mihogo huvundikwa hadi ivunde na kuota fungus juu(ule utando wa juu) ndipo huwa tayari kupondwa-pondwa kwaajiri ya kutayarisha Unga!
 
Jambo lolote linaloshabikiwa na mtanzania lina madhara na hua ninajitenga nalo, learning from experience
 
Ukifuata kila linalosemwa utashindwa kuishi. Eat what you like, badilisha badilisha, fanya mazoezi, usinenepeane, kunywa pombe kwa wastani na usivute sigara. Maisha yatakwenda tu na siku yako ikifika unakwenda.

Dona mbaya miaka na miaka Wasukuma kule tunakula dona na hakukuwa na kansa wala huu upuuzi mwingine. Yamekuja haya mavyakula ya viwandani ndiyo kansa imeripuka kila kona barani Afrika kisa tunaiga wazungu. Aaaaargh!
 
Ni tetesi kwa sababu hakuna takwimu zenye kuhusisha ulaji wa ugali wa dona na kansa.

Bado ukweli ni kwamba kiini cha mahindi hutunza "fungus" na ndiyo mama wa "aflatoxin".

Kwa maeneo ya joto na unyevunyevu (kama huku TZ) kansa ni ugonjwa mkubwa kwa kula aina hiyo ya vyakula vinavyozalisha "fungus" km dona, unga wa mhogo unaovundikwa hadi kuwa mweusi nk.

...

Kwa hiyo sio tu unga wa dona, hata muhogo nao ni shida?
 
Ukifuata kila linalosemwa utashindwa kuishi. Eat what you like, badilisha badilisha, fanya mazoezi, usinenepeane, kunywa pombe kwa wastani na usivute sigara. Maisha yatakwenda tu na siku yako ikifika unakwenda.

Dona mbaya miaka na miaka Wasukuma kule tunakula dona na hakukuwa na kansa wala huu upuuzi mwingine. Yamekuja haya mavyakula ya viwandani ndiyo kansa imeripuka kila kona barani Afrika kisa tunaiga wazungu. Aaaaargh!

Umeongea point sana mkuu, sijafanya utafiti lakini hua naamini akili niliyonayo inaniwezesha kuchambua na kutafakari mambo ili kunipatia ufumbuzi wa changamoto zinazonikabili.

Kwa upande mmoja nafikiri tatizo halipo kwenye unga wa dona moja kwa moja, ila mahindi siku hizi yanahifadhiwa kwa kupuliziwa au kuchanganywa na madawa ili kuyakinga na wadudu waharibifu, kwa bahati mbaya hayo madawa ni sumu.
Vilevile njia za kuyasafisha hayo mahindi kwa kiwango cha kutoa hiyo dawa inaweza isifanyike kwa ufasaha kwa kiwango cha kuitoa dawa yote. Kwa mtazamo huo, naweza kukubaliana na mtoa mada kwamba unga wa dona huenda ukawa na madhara kwa kigezo cha madawa kubaki kwenye mahindi tofauti na yakikobolewa ambapo maganda hutolewa.
Ila ugali sidhani kama ni sahihi kusema kila ugali wa dona una madhara!

Shukrani mkuu.
 
Ukifuata kila linalosemwa utashindwa kuishi. Eat what you like, badilisha badilisha, fanya mazoezi, usinenepeane, kunywa pombe kwa wastani na usivute sigara. Maisha yatakwenda tu na siku yako ikifika unakwenda.

Dona mbaya miaka na miaka Wasukuma kule tunakula dona na hakukuwa na kansa wala huu upuuzi mwingine. Yamekuja haya mavyakula ya viwandani ndiyo kansa imeripuka kila kona barani Afrika kisa tunaiga wazungu. Aaaaargh!


Sasa hivi mnaona Kuna milipuko ya kansa kwasababu mnaenda hospitali.... Zamani mlikuwa hamuendi hospitali mnaishia kusema wagonjwa wamelogwa.

Na pia hospitali zenyewe zilikuwa chache, vifaa vya uchunguzi vilikuwa hamna nk.
 
Sasa hivi mnaona Kuna milipuko ya kansa kwasababu mnaenda hospitali.... Zamani mlikuwa hamuendi hospitali mnaishia kusema wagonjwa wamelogwa.

Na pia hospitali zenyewe zilikuwa chache, vifaa vya uchunguzi vilikuwa hamna nk.
Mimi ni mfuatiliaji mzuri sana wa mambo haya na nina kabrasha zima limejaa research papers kuhusu ishu hii. Tatizo langu na wanasayansi hawa (wengi wao kutoka Ulaya) ni kutoa tafiti zinazokinzana halafu hawasemi watu wafanyeje. Leo utasoma kuhusu uzuri wa kunywa kahawa na kesho unasoma utafiti mwingine unasema kahawa ina madhara kibao. Juzi juzi hapa kulikuwa na mjadala mkubwa kuhusu utafiti mmoja uliosema kuwa "kuzamia chumvini" kunasaidia kupunguza baadhi ya kansa hasa za koo. Hapo hapo utafiti mwingine ukasema kuzamia chumvini ni chanzo kikubwa cha kansa za kinywa. Sasa hapo wanataka watu wafanyeje?

Mwaka juzi shirika la afya duniani (WHO) lilitoa ripoti ya kutisha kuhusu ueneaji wa kansa barani Afrika katika miaka ya karibuni. Sababu kubwa iliyotajwa ni kubadilika kwa mifumo ya maisha ikiwemo hasa utumiaji wa vyakula vilivyosindikwa viwandani na uhamiaji mijini ambako watu hudeka na hatimaye kunenepeana bila kufanya mazoezi wala shughuli za kuutaabisha mwili. Mengine ni unywaji wa pombe kali (viroba?) kuongezeka na uvutaji wa sigara.

Kama mdau mmoja alivyosema hapo juu mimi nadhani tatizo linaweza kuwa kwenye madawa yanayotumiwa kutunzia nafaka hizi ili zisiharibike. Hakuna anayejua viwango sahihi vinavyopaswa kutumiwa na unakuta mahindi yanachukuliwa kutoka ghalani yanapepetwa tu halafu yanakwenda kusagwa. Zamani watu walikuwa wanatumia majivu tu basi lakini sasa mambo yamebadilika.

Ushauri wangu ni ule ule. Kula ukipendacho lakini in moderation, badilisha badilisha, fanya mazoezi, epuka ulevi na sigara; na tumia common sense tu and you will be OK. Leo utakula hichi na kesho wataibuka tena na kusema nacho kinasababisha kansa.

Otherwise nakubaliana na point yako.
 
Mimi ni mfuatiliaji mzuri sana wa mambo haya na nina kabrasha zima limejaa research papers kuhusu ishu hii. Tatizo langu na wanasayansi hawa (wengi wao kutoka Ulaya) ni kutoa tafiti zinazokinzana halafu hawasemi watu wafanyeje. Leo utasoma kuhusu uzuri wa kunywa kahawa na kesho unasoma utafiti mwingine unasema kahawa ina madhara kibao. Juzi juzi hapa kulikuwa na mjadala mkubwa kuhusu utafiti mmoja uliosema kuwa "kuzamia chumvini" kunasaidia kupunguza baadhi ya kansa hasa za koo. Hapo hapo utafiti mwingine ukasema kuzamia chumvini ni chanzo kikubwa cha kansa za kinywa. Sasa hapo wanataka watu wafanyeje?

Mwaka juzi shirika la afya duniani (WHO) lilitoa ripoti ya kutisha kuhusu ueneaji wa kansa barani Afrika katika miaka ya karibuni. Sababu kubwa iliyotajwa ni kubadilika kwa mifumo ya maisha ikiwemo hasa utumiaji wa vyakula vilivyosindikwa viwandani na uhamiaji mijini ambako watu hudeka na hatimaye kunenepeana bila kufanya mazoezi wala shughuli za kuutaabisha mwili. Mengine ni unywaji wa pombe kali (viroba?) kuongezeka na uvutaji wa sigara.

Kama mdau mmoja alivyosema hapo juu mimi nadhani tatizo linaweza kuwa kwenye madawa yanayotumiwa kutunzia nafaka hizi ili zisiharibike. Hakuna anayejua viwango sahihi vinavyopaswa kutumiwa na unakuta mahindi yanachukuliwa kutoka ghalani yanapepetwa tu halafu yanakwenda kusagwa. Zamani watu walikuwa wanatumia majivu tu basi lakini sasa mambo yamebadilika.

Ushauri wangu ni ule ule. Kula ukipendacho lakini in moderation, badilisha badilisha, fanya mazoezi, epuka ulevi na sigara; na tumia common sense tu and you will be OK. Leo utakula hichi na kesho wataibuka tena na kusema nacho kinasababisha kansa.

Otherwise nakubaliana na point yako.


Sayansi, Research na ugunduzi ni dynamic haipo static.... Hivyo usitegemee ukipata jibu la jambo mara moja basi ndiyo hivyo hivyo
 
Watu wengi kwa sasa wamependelea kula ugali uliopikwa kwa unga wa mahindi usiokobilewa, maarufu 'dona'. Pamoja na kwamba mahindi uhifadhiwa kwa madawa ili yasiharibike (athari kwa fedha) kuna tatizo lingine kwa afya zetu yasemekana.

Tahadhali na unga wa dona, ni hatari kwa afya kwa sababu ya sumu inayoitwa 'aflatoxin" ambayo huwa ndani ya kiini cha mbegu ya mhindi. Ukikobolewa kiini uondolewa na kubaki unga mweupe (sembe).

Wengi sasa hawependi kula ugali wa sembe kwa sababu ya kukosa protini (iliyomo kwenye kiini). Lakini hasara ya kukosa hiyo protein ni ndogo sana kulinganisha na madhara ya "aflatoxin" itakayosababisha "cancer" mwilini mwa binadamu.

TAFAKARI CHUKUA HATUA

Wazee wetu zamani kulikuwa hakuna unga wa sembe walikuwa wanatwanga katika kinu au kusaga kwa mawe kisha wanapiga msosi. Tena walikuwa na afya nzuri kulinganisha na sisi wa kizazi cha digitali.

Walikuwa hawana maradhi kama ilivyo sasa tunaokula unga wa sembe.

Hivyo bado nina imani kubwa na unga wa dona katika afya ya binadamu.
 
Wazee wetu zamani kulikuwa hakuna unga wa sembe walikuwa wanatwanga katika kinu au kusaga kwa mawe kisha wanapiga msosi. Tena walikuwa na afya nzuri kulinganisha na sisi wa kizazi cha digitali.

Walikuwa hawana maradhi kama ilivyo sasa tunaokula unga wa sembe.

Hivyo bado nina imani kubwa na unga wa dona katika afya ya binadamu.
Kuna vituvingine vinahitaji akili iliyo lala ili uvielewee,tunaotoka kanda ya kati tunathamini dona kwea unyenyekevu usiohojika.naanzaje kuiletea madharau dona[emoji15]
 
Sayansi, Research na ugunduzi ni dynamic haipo static.... Hivyo usitegemee ukipata jibu la jambo mara moja basi ndiyo hivyo hivyo
You proved my point sir. That's what I was trying to say. Ni ku-adapt kulingana na mazingira mahali ulipo na siyo kufuata kila wanalosema hawa watafiti ambao mara nyingine tafiti zao zinakuwa contradictory!
 
Mbegu ikishaota imejichuuja na dawa za kuhifadhia haziingii ndani labda ukiloweka.

Kuweni makn wakt wa kusaga mahindi yaoshwe vzuri siyo na sabuni ila maji tu.
 
Mbona wazee wetu wa zamani ndo chakula walikuwa wanakula karne na karne na walikuwa hawaugui cancer?
 
Watu wengi kwa sasa wamependelea kula ugali uliopikwa kwa unga wa mahindi usiokobilewa, maarufu 'dona'. Pamoja na kwamba mahindi uhifadhiwa kwa madawa ili yasiharibike (athari kwa fedha) kuna tatizo lingine kwa afya zetu yasemekana.

Tahadhali na unga wa dona, ni hatari kwa afya kwa sababu ya sumu inayoitwa 'aflatoxin" ambayo huwa ndani ya kiini cha mbegu ya mhindi. Ukikobolewa kiini uondolewa na kubaki unga mweupe (sembe).

Wengi sasa hawependi kula ugali wa sembe kwa sababu ya kukosa protini (iliyomo kwenye kiini). Lakini hasara ya kukosa hiyo protein ni ndogo sana kulinganisha na madhara ya "aflatoxin" itakayosababisha "cancer" mwilini mwa binadamu.

TAFAKARI CHUKUA HATUA
hiyo *aflatoxin* inaingia kwenye kiini cha hindi muda gani... wa kupandaaaaa, kunyunyuziaaaa ama muda wa kuhifadhi mahindi....
 
Back
Top Bottom