Ugali unaopikwa kwa Unga wa mahindi (dona) hatari kwa afya ya binadamu

Ugali unaopikwa kwa Unga wa mahindi (dona) hatari kwa afya ya binadamu

unless uniambie kuna mahindi ya GMO labda unayoyajua wewe yenye viatilifu vya aina hiyo
kitu ambacho sijasikia Labda ndugu zetu wa TFDA NA Kilimo mtujuze.
Unauhakika kwamba hawajakujuza humu ndani
 
Watu wengi kwa sasa wamependelea kula ugali uliopikwa kwa unga wa mahindi usiokobilewa, maarufu 'dona'. Pamoja na kwamba mahindi uhifadhiwa kwa madawa ili yasiharibike (athari kwa fedha) kuna tatizo lingine kwa afya zetu yasemekana.

Tahadhali na unga wa dona, ni hatari kwa afya kwa sababu ya sumu inayoitwa 'aflatoxin" ambayo huwa ndani ya kiini cha mbegu ya mhindi. Ukikobolewa kiini uondolewa na kubaki unga mweupe (sembe).

Wengi sasa hawependi kula ugali wa sembe kwa sababu ya kukosa protini (iliyomo kwenye kiini). Lakini hasara ya kukosa hiyo protein ni ndogo sana kulinganisha na madhara ya "aflatoxin" itakayosababisha "cancer" mwilini mwa binadamu.

TAFAKARI CHUKUA HATUA
sipendagi kweli habari ambazo hazina ukweli ama zinazofikisha ujumbe ndivyo sivyo......
nani alikwambia kwamba aspergillas wanakaa kwenye kiini tu cha Indi??
nani alisema kwamba ukikoboa basi wewe utawaua hao aspergillas
 
kiukweli aspergillas ni fungus wanaotoa ama kutengeneza sumu ya aflatoxin ambayo husababisha cancer.
sfungus hawa hushambulia zaid mazao ya nafaka na karanga ama korosho. Nafaka zozote zile ambazo hazija limwa kwa kufuata taratibu za kilimo kwenye ukaushaj wa nafaka hupata fungus hawa kwan kawaida yake ni kuota kwenye nafaka zenye unyevunyevu.
mazao kama mihogo na ndizi za makopa na zenyewe pia huweza kupata laki pia hata mboga za majan za kukausha huweza kupata fungus hawa.
ili kujikinga na aspergilus hakkisha unatumia nafaka zilizo kavu na zilizofanyiwa sorting vizuri. changua nafaka vyema kisha osha anika na peleka kusaga huwez kuwapata.

ukitaka kujua kwamba nafaka imepata hawa fungus utaona imebadilika rangi kuwa kama nyeusi, darkblue ama kijan na ukila kama karanga itakereketa kwenye koo. mahind yote yaliyooza na hii ni hata kwenye nafaka zingine na karanga inabidi yasiliwe
 
Wewe endelea kula Ugali wa Sembe. Sisi tanaendelea kula Ugali wa DONA.
 
[emoji102] Siku hizi Kila chakula kina sumu

Sasa tutakula nini???[emoji12] [emoji12]
 
kazi kwelikweli mbona kila kitu sumu labda tule mawe sasa
 
Nadhani itakuwa ni kweli kwani ili mahindi yasioze si yanahifadhiwa kwa madawa...!
 
Ongezea na MAHINDI YA KUCHOMA NI HATARI KWA AFYA maana nayo yana kiini.

Hii sumu haiwauwi kuku, bata, ng'ombe na nguruwe wakila PUMBA?

JITAFAKARI UJICHUKULIE HATUA MWENYEWE.
 
Aflatoxin ni aina ya sumu inayotengenezwa na vimelea vya fangasi (hasa Aspergillus flavus na Aspergillus fumigatus) kwenye mazao hasa ya nafaka yakiwa bado shambani au baada ya kuvunwa na kuhifadhiwa katika mazingira mabovu. Nchi zinazoendelea ikiwemo zilizo kusini mwa jangwa la sahara zimeathirika zaidi kutokana na hali ya hewa ya joto na unyevunyevu ambavyo ni mazingira mazuri kwa hawa fangasi kuota kwenye mazao na kutengeneza hii sumu ya aflatoxin. Nafaka zinazotumiwa kwa wingi kwa chakula kama mahindi na karanga zinaathiriwa zaidi na hii sumu. Mbinu bora za kilimo ikiwemo kutifua ardhi kabla ya kupanda, matumizi ya mbolea na viwatilifu, na kumwagilia mazao huweza kusaidia mazao yasidumae hivyo yasishambuliwe kwa urahisi na hawa fangasi. Pia, kwa sababu kiwango kikubwa cha aflatoxin huzalishwa ikiwa nafaka hazikukauka na kuhifadhiwa vizuri, njia ya kukausha vizuri nafaka na kuzihifadhi katika mazingira yasiyoruhusu unyevu, au kuvunda na bila kuharibiwa na wadudu na panya inaweza kusaidia kupunguza sumu hii kwa kiwango kikubwa sana. Utafiti umehusisha utumiaji wa vyakula vilivyo na kiwango kikubwa cha aflatoxin na kansa ya ini (hepatocellular carcinoma) kwa watu wazima na kutokukua vizuri na kudumaa kwa watoto. Matumizi ya nafaka hasa mahindi zenye kiasi kikubwa cha aflatoxin huweza kupelekea kifo ndani ya muda mfupi baada ya hii sumu kuharibu ini (acute hepatotoxicity) kama ambavyo imekuwa ikitokea nchi jirani ya Kenya.
 
Watu wengi kwa sasa wamependelea kula ugali uliopikwa kwa unga wa mahindi usiokobilewa, maarufu 'dona'. Pamoja na kwamba mahindi uhifadhiwa kwa madawa ili yasiharibike (athari kwa fedha) kuna tatizo lingine kwa afya zetu yasemekana.

Tahadhali na unga wa dona, ni hatari kwa afya kwa sababu ya sumu inayoitwa 'aflatoxin" ambayo huwa ndani ya kiini cha mbegu ya mhindi. Ukikobolewa kiini uondolewa na kubaki unga mweupe (sembe).

Wengi sasa hawependi kula ugali wa sembe kwa sababu ya kukosa protini (iliyomo kwenye kiini). Lakini hasara ya kukosa hiyo protein ni ndogo sana kulinganisha na madhara ya "aflatoxin" itakayosababisha "cancer" mwilini mwa binadamu.

TAFAKARI CHUKUA HATUA
Nashukuru mkuu umeleta huu uzi..

Nimesoma baadhi ya comments na nimesikitika watu wengi hawajui kuhusu mycotoxins

1. Aflatoxin ni moja kati ya sumu nyingi sana zinazotokewa na fungus ambazo kwa ujumla huitwa mycotoxins.

2. Mojawapo ya nafaka ambapo aflatoxin huwepo sana ni mahindi hasa yanayolimwa maeneo ya kitropiki kama Tz

3. Tafiti kama 5 zimefanyika kwenye mahindi na kugundulika asilimia 30-50 ya mahindi yasiyokobolewa yameathirika na uwepo wa aflatoxin zaidi ya kiwango cha chini kinachoruhusiwa kitaifa na kimataifa

4. Kwa Tz kiwango cha chini kinachoruhusiwa ni 5 ppb (0.005 ppm) ingawa kwa mataifa mengi ni 10 ppb

5. Madhara yatokanayo na ulaji wa vyakula vyenye aflatoxin na kansa ya ini, ugonjwa wa figo, upungufu wa nguvu za kinga mwilini, matatizo kwq vichanga, kudumaa nk. (Kwa nchi nyingi ambazo chakula kina aflatoxin sana ikiwemo Tanzania watoto wengi wamedumaa)

6. Zaidi ya aflatoxin pia sumu nyingine za fungus kama fuminisins zipo sana kwenye mahindi

7. Hata uchemshe mahindi namna gani, aflatoxin haiwi deactivated.

8. Watu wanadhani mahindi yaliyooza au fungus zinaonekana kwa macho ndio yenye aflatoxin lakini ukweli ni kuwa hata mahindi masafi kabisa yanaweza kuwa na hiyo sumu

9. Aflatoxin na sumu nyingine za fungus hazina harufu, ladha wala rangi, hivyo sio rahisi kitambua chakula kilichaathirika

10. Mazao mengine ambayo yana aflatoxin kwa wingi ni karanga (zaidi hata ya mahindi), na mihogo ya kukausha.

11. Pamoja na kwamba madhara yanaweza kumpata yeyote lakini huwa na athari zaidi kwa watoto. Hivyo inashauriwa hata kama wewe unashindwa kuepuka basi walinde watoto wako. Usiwape vyakula vyenyr mahindi hayajakobolewa wala karanga
 
Hakuna kitu kama hicho duniani. Hiyo research imefanyika wapi? MKUU KAJIPANGE UPYA NDO UJE KUTOA UZI SIO KUKULUPUKA
 
Acheni hizo nimeula nanitazidi kuula
Sumu inatoka wapi wakati kabla ya kusonga unapika uji tena unaauacha unachemka kwa dk 15
 
Hii tetesi ina ukweli fulani
Hii sumu hutokezwa na aina ya fungus aitwaye Aspergillus flavus. Huyu fungus hushambulia nafaka kama karanga na wakati mwingine mahindi na nafaka zingine. Aflatoxin ni sumu, hata ukichemsha hii sumu haipungui makali na matokeo yake ni mabaya sana kama alivyogusia mleta mada. Kiukweli hili ni janga la karibuni sana kufahamika na huenda ikawa ndo "ukimwi" tuliohubiriwa kwa muda mrefu.

So far, hakuna antidot ya aflatoxin. Utafiti unaendelea kujua ni mlundikano wa sumu kiasi gani ya aflatoxin inaweza kusababisha madhara.

Wanaobeza hoja nadhani hawako sahihi.. wafuatilie na wachukuwe hatua za kujilinda dhidi ya hili janga
 
Hii tetesi ina ukweli fulani
Hii sumu hutokezwa na aina ya fungus aitwaye Aspergillus flavus. Huyu fungus hushambulia nafaka kama karanga na wakati mwingine mahindi na nafaka zingine. Aflatoxin ni sumu, hata ukichemsha hii sumu haipungui makali na matokeo yake ni mabaya sana kama alivyogusia mleta mada. Kiukweli hili ni janga la karibuni sana kufahamika na huenda ikawa ndo "ukimwi" tuliohubiriwa kwa muda mrefu.

So far, hakuna antidot ya aflatoxin. Utafiti unaendelea kujua ni mlundikano wa sumu kiasi gani ya aflatoxin inaweza kusababisha madhara.

Wanaobeza hoja nadhani hawako sahihi.. wafuatilie na wachukuwe hatua za kujilinda dhidi ya hili janga



  1. Aspergillus flavus
    Fungus
    Aspergillus flavus is a saprotrophic and pathogenic fungus with a cosmopolitan distribution. It is best known for its colonisation of cereal grains, legumes, and tree nuts. Postharvest rot typically develops during harvest, storage, and/or transit. Wikipedia

    Scientific name: Aspergillus flavus
    Higher classification: Aspergillus
    Rank: Species
hivi mpaka una kula mahindi yenye fungus utakua huwaoni mbona fungus wanaonekana by naked eyes
cha muhim ni kwamba tafuta mahindi safi osha kwa kadri utakavyoweza nenda kasage au nunua kutoka kwa reliable source.

kuna mdau aligusia unga wa mhogo kwa ufupi hakuna watu wanaoutumia sana kama watu wanaotoka kanda ya ziwa
lakini sijasikia canser cases za kutisha kiasi hicho mnachosema ,karanga pia yale yale jamani tusiwe washabiki kwanza topic yenyewe ukifuatilia imeandikwa tetesi ,wacha watu wale mbegu ndo mojawapo ya chakula alichoruhusu Mungu
usiwatishe kiasi hicho.
 

Attachments

  • download (6).jpg
    download (6).jpg
    4.1 KB · Views: 51
Nashukuru mkuu umeleta huu uzi..

Nimesoma baadhi ya comments na nimesikitika watu wengi hawajui kuhusu mycotoxins

1. Aflatoxin ni moja kati ya sumu nyingi sana zinazotokewa na fungus ambazo kwa ujumla huitwa mycotoxins.

2. Mojawapo ya nafaka ambapo aflatoxin huwepo sana ni mahindi hasa yanayolimwa maeneo ya kitropiki kama Tz

3. Tafiti kama 5 zimefanyika kwenye mahindi na kugundulika asilimia 30-50 ya mahindi yasiyokobolewa yameathirika na uwepo wa aflatoxin zaidi ya kiwango cha chini kinachoruhusiwa kitaifa na kimataifa

4. Kwa Tz kiwango cha chini kinachoruhusiwa ni 5 ppb (0.005 ppm) ingawa kwa mataifa mengi ni 10 ppb

5. Madhara yatokanayo na ulaji wa vyakula vyenye aflatoxin na kansa ya ini, ugonjwa wa figo, upungufu wa nguvu za kinga mwilini, matatizo kwq vichanga, kudumaa nk. (Kwa nchi nyingi ambazo chakula kina aflatoxin sana ikiwemo Tanzania watoto wengi wamedumaa)

6. Zaidi ya aflatoxin pia sumu nyingine za fungus kama fuminisins zipo sana kwenye mahindi

7. Hata uchemshe mahindi namna gani, aflatoxin haiwi deactivated.

8. Watu wanadhani mahindi yaliyooza au fungus zinaonekana kwa macho ndio yenye aflatoxin lakini ukweli ni kuwa hata mahindi masafi kabisa yanaweza kuwa na hiyo sumu

9. Aflatoxin na sumu nyingine za fungus hazina harufu, ladha wala rangi, hivyo sio rahisi kitambua chakula kilichaathirika

10. Mazao mengine ambayo yana aflatoxin kwa wingi ni karanga (zaidi hata ya mahindi), na mihogo ya kukausha.

11. Pamoja na kwamba madhara yanaweza kumpata yeyote lakini huwa na athari zaidi kwa watoto. Hivyo inashauriwa hata kama wewe unashindwa kuepuka basi walinde watoto wako. Usiwape vyakula vyenyr mahindi hayajakobolewa wala karanga
Mkuu laiti watu wengi wangekuwa na busara kama zako. Mimi bado nasisitiza kuwa elimu yetu ni majanga. Hii sumu iko dhahiri lakini kuna watu wanauliza mbona fulani kala dona mpaka kazeeka! Really? Mtu anayewaza namna hii elimu ilimsaidia? Wao wanataka kuona yale madhara ya tit for tat! Hawajui mambo ya probability...
 
Back
Top Bottom