Uganda imepiga marufuku michezo ya kamari na Kampuni za michezo hiyo hazitapewa tena kibali

Uganda imepiga marufuku michezo ya kamari na Kampuni za michezo hiyo hazitapewa tena kibali

Serikali ya Uganda imepiga marufuku michezo ya kubashiri maarufu kama betting kutokana na lundo kubwa la vijana nchini humo kujikita katika michezo hiyo huku wakishindwa kujishughulisha na kazi rasmi.

Kwa kuanzia, serikali imekataza utoaji wa vibali vipya kwa makampuni mapya ya betting, na yale makampuni ambayo leseni zao zimeisha, hawatapata vibali vipya kwa mwaka huu 2019.

My take:

Ni wakati muafaka kwa serikali yetu kulitazama pia suala hili la michezo ya kubahatisha kwa jicho la umakini.
Mbona Tanzania tunapiga marufu viroba lakin wao mbona hawatuigi,
Uwe unatumia akili

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hatimaye Rais wa Uganda Mwanamume ' Mwamba wa Mbarara ' au ' Mwamba wa Kinyankole ' Yoweri Kaguta Museveni amefuta rasmi na kuzuia kabisa michezo yote ya Kubahatisha ( Betting ) nchini humo kwa kusema kwamba imesababisha Waganda wengi wawe Wavivu na Kuirudisha nchi nyuma Kimaendeleo kwakuwa hawajitumi katika Kuwajibika na Kuijenga nchi hiyo.

Haya na wale Marais ' Watoto ' wengine igeni hili upesi ili nchi zetu nazo zipige hatua haraka.

Nawasilisha.
 
Hatimaye Rais wa Uganda Mwanamume ' Mwamba wa Mbarara ' au ' Mwamba wa Kinyankole ' Yoweri Kaguta Museveni amefuta rasmi na kuzuia kabisa michezo yote ya Kubahatisha ( Betting ) nchini humo kwa kusema kwamba imesababisha Waganda wengi wawe Wavivu na Kuirudisha nchi nyuma Kimaendeleo kwakuwa hawajitumi katika Kuwajibika na Kuijenga nchi hiyo.

Haya na wale Marais ' Watoto ' wengine igeni hili upesi ili nchi zetu nazo zipige hatua haraka.

Nawasilisha.


Hii ikitokea hapa Tanzania wananchi wataandamana na Zitto atawaunga mkono huku akiishambulia serikali kuwa haijali wananchi wake wababaishaji wa ku-bet kila kukicha ili tu apate kiki.
 
Kama hawafanyi kazi pesa ya kubetia wanapata wapi? Hii ni sawa na kusema watu hawafanyi kazi wanakunywa pombe tu. Je, hizo pombe wanagawa bure?!

Ujengaji wako wa ' Hoja ' ni wa ' Kitoto ' sana hivyo siwezi Kuishughulisha ' IQ ' yangu ama Kukuelekeza au Kujibizana nawe.
 
Hatimaye Rais wa Uganda Mwanamume ' Mwamba wa Mbarara ' au ' Mwamba wa Kinyankole ' Yoweri Kaguta Museveni amefuta rasmi na kuzuia kabisa michezo yote ya Kubahatisha ( Betting ) nchini humo kwa kusema kwamba imesababisha Waganda wengi wawe Wavivu na Kuirudisha nchi nyuma Kimaendeleo kwakuwa hawajitumi katika Kuwajibika na Kuijenga nchi hiyo.

Haya na wale Marais ' Watoto ' wengine igeni hili upesi ili nchi zetu nazo zipige hatua haraka.

Nawasilisha.
Hivi kweli kubeti kunazuia watu wasifanye kazi? Ujinga
 
Hahaha wakifanya tz italeta minong'ono maana ndio maisha ya watu hayo.
Ila kuna tatizo kubwa sana la watu kuwa addcted na betting

Sent using Jamii Forums mobile app

Binafsi naona hili la ' Betting ' hasa hapa Tanzania na kwa jinsi ninavyoona kama lisipoangaliwa kwa umakini au hata ' Kufutwa ' kabisa au kuwekwe ' Kanuni ' fulani kuna ' Hatari ' kubwa mno ya Kijamii na hata ya Kisaikolojia kwa ' Wanaobeti ' inakuja. Siamini kama Rais Museveni ' amekurupuka ' tu kuja na haya ' Maamuzi ' ila kuna aliloliona na ndiyo maana ameamua bora achukiwe au asemwe vibaya ila aiokoe Uganda na Vizazi vya Waganda.

Naungana nae Rais Museveni kwa 100% zote na nampongeza kwa hii hatua na nawaomba Marais wengine wamuige.
 
Kwa bongo hii....nadhani mapato yatapungua kwani 80% ya watu waliopo mjini wanabet....hivyo kufungia itakuwa ni kinyume na mikakati tuliyojiwekea ya ukusanyaji wa mapato hasa kodi.

Sent using Jamii Forums mobile app

Kimaendeleo hili likiachwa au lisipodhibitiwa ni ' Bomu ' kubwa ambalo likija ' Kulipuka ' huko baadae tutatafutana hapa Tanzania.
 
Back
Top Bottom