Uganda yapitisha sheria mpya kukataza wanawake kuvaa nguo fupi

Uganda yapitisha sheria mpya kukataza wanawake kuvaa nguo fupi

Sisi ma-air hostess itakuwaje sasa
Na wafanyakazi wa banks na kwenye mahotel ya kitalii, manake ndo mavazi yetu sie
 
Sisi ma-air hostess itakuwaje sasa
Na wafanyakazi wa banks na kwenye mahotel ya kitalii, manake ndo mavazi yetu sie

Mh..hakuna sheria kama hiyo.airhostess ni zamani ram sasa hivi wanaitwa(cabin crew or flight attendant)kuvaa nguo fupi ram ni mtu mwenyewe anahamua maana sehemu nyingi ni chini ya goti..watu ndio wanavunja sheria wanavaa nusu uchi..
 
Hata mimi naongelea mini sketi au gauni zinazoishia katikati ya goti au chini kidogo ya goti, sio mini za akina wema sepetu na akina aunt ezekiel, hata mimi sikubaliani na mini za hao wanaojiita mastaa. Vipi hawa vijana wanaovaa suruali chini ya makalio, sheria haijawatambua?


Mh..hakuna sheria kama hiyo.airhostess ni zamani ram sasa hivi wanaitwa(cabin crew or flight attendant)kuvaa nguo fupi ram ni mtu mwenyewe anahamua maana sehemu nyingi ni chini ya goti..watu ndio wanavunja sheria wanavaa nusu uchi..
 
Screen-Shot-2014-02-19-at-8.03.41-AM.png


Taarifa ikufikie kwamba imepigwa marufuku kwa jinsia ya kike kuvaa nguo fupi (ki-mini) nchini Uganda na tayari Rais wa nchi hiyo Yoweri Museveni amesaini rasmi sheria hii.
Japokua baadhi ya Wabunge walipinga kwamba marufuku hii inaingilia uhuru wa mtu kuvaa, wabunge wengi wameunga mkono uamuzi huu.
Unaambiwa marufuku hii ambayo imelenga kuepusha vitendo vya ubakaji na ngono zembe kutokana na ushawishi unaotokana na uvaaji huu, inahusisha pia nguo nyingine fupi ambazo zinaacha sehemu kubwa ya mwili wazi kama vile kifuani.

Wanawake/Wasichana wataruhusiwa kuvaa mavazi mafupi kwenye matukio maalum tu yanayohusisha uvaaji huu kama vile michezo ambapo Waziri husika
Sheria hii pia inawabana Wanamuziki wa kike ambao wamekua wakivaa nguo fupi kwenye show zao pamoja na video ambapo Waziri Lokodo amesema ‘hatutaki uhusike kufanya watu wakutamani au watamani kufanya ngono, hatutaki ushawishi chochote kwa jinsia ya kiume, kuwa na tabia njema kwa kuvaa kiheshima’


Vilevile vyombo vya habari yakiwemo Magazeti na TV, vimepigwa marufuku kuonyesha picha za watu wakipigana busu au picha zozote za Wanawake wakiwa nusu uchi.


Natamani na Hapa Tz ije hii sheria

Chanzo Hapa



Mkuu ya mambo yanategemea na interest ya mkuu wa kaya ndio maana Mswati anapenda kuangalia mabinti wakiwa uchu na hapa duniani kuna waswati wengi wanao shabikia kimya kimya.
 
140219081848_africa_miniskirt_304x171_bbc_nocredit.jpg


Maandamano ya kkupinga agizo la wanawake kutovalia sketi fupi


Rais wa Uganda, Yoweri Museveni, ametia saini sheria mpya inayotoa adhabu kali kwa wanaopatikana na hatia ya kutembea nusu uchi au kuhusika na vitendo vinavyohusisha picha zenye watu uchi.
Wanawake pia wamezuiwa kabisa kuvalia sketi fupi sana au 'Mini Skirt' kama zinavyojulikana au blausi ambazo zinaonyesha kifua chao hadharani na kusababisha hisia za kingono .
Vimini.JPG





Sheria hiyo inasema kuwa nguo kama hizo zitakubalika tu ikiwa zinatumika kwa ajili ya mafunzo au wakati wa michezo na hafla za kitamaduni.
Akihutubia waandishi wa habari, mjini Kapmala, waziri wa maadili na utawala bora, Reverend Simon Lokodo alisema kuwa Rais Museveni alipitisha sheria hiyo tarehe 6 mwezi huu, miezi mwili bada ya bunge kuipitisha.
Kwa mujibu wa sheria hiyo kamati dhidi ya vitendo hivyo itabuniwa ili iweze kutekeleza sheria hiyo kwa kuhakikisha kuwa picha, au video zenye watu uchi zinanaswa na kuharibiwa.
Kamati hiyo, itajumuisha watu kutoka katika sekta mbali mbali ikiwemo ya habari na utumbuizaji.
Sheria hiyo inasema kuwa mtu yeyote atakayepatikana akijihusisha na vitendo cya watu kuwa uchi, kuvalia nusu uchi , kuona sinema za watu wakiwa uchi au kuchapisha picha za watu walio uchi kwa lengo la kuleta hisia tofauti utachukuliwa hatua kali za kisheria.
Waziri alisema kuwa serikali haitaki watu kuvalia nguo zisizo na heshima na kuzua hisia zisizofaa miongoni mwa watu.
Watakaopatikana wakivunja sheria na kuvalia visivyo watafungwa hadi miak 10 na wale watakaopatiokana na hatia ya kuhusisha watoto katika biashara ya ngono watafungwa hadi miaka 15.



14476-1.jpg%3Fw%3D470


source; BBC
 
Hata mimi naongelea mini sketi au gauni zinazoishia katikati ya goti au chini kidogo ya goti, sio mini za akina wema sepetu na akina aunt ezekiel, hata mimi sikubaliani na mini za hao wanaojiita mastaa. Vipi hawa vijana wanaovaa suruali chini ya makalio, sheria haijawatambua?

hapo mi mwenyewe nawaza inakuwaje..alieiona sheria yenyewe au mwenye jibu sahihi anifumbue
 
Habari zenu wana jf
raisi wa Uganda amepitisha sheria inayokataza uvaaji wa vimini na adhabu yake itakuwa kifungo cha miaka kumi jela
SOURCE BBC facebook page
 
Huko vimini vitakua vinarudisha maendeleo nyuma...maana naskia uganda kwa starehe ni balaa
 
Back
Top Bottom