Habari za mda huu wanajamvi, Kuna tetesi za kinywaji cha mzee wetu Bakhresa Azam energy kimefungiwa kwa kukutwa na viatarishi vya afya ya binadam. Sasa kama ni kweli baada ya miaka yote hii kuwepo sokon sijui imeshamaliza watu wangapi mpka sasa.
Utafiti ujikite huko kwenye energy drinks, maana watu wanazinywa kama maji, kuna siku niliwahi kunywa hiyo azam energy enzi hizo ndio zimeingia sokoni reaction niliyoipata ni mapigo ya moyo kwenda mbio na usiku kucha kuweweseka tu nikasema sitawahi kuja kunywa tena hizi energy drink hususani za Azam au Mo.
Hizo energy vijana hasa bodaboda zitawaua sana.
Kuna sehemu nina kaofisi kangu ka vinywaji,naweza nikaingiza mzigo wa vinywaji let's say carton 100 za energy drinks but ndani ya siku mbili zimeisha.