Ugonjwa wa Kuota Vinyama Sehemu za Siri (Bawasiri/ Hemorrhoids): Chanzo, Dalili, Tiba na Kinga

Ndugu...
Wanajamii Forum naomba msaada wa kujua nini kisababisha mtu anapata uvimbe kwenye njia ya haja kubwa na kupelekea kupata maumivu wakati wa kujisaidia na nini tiba ya huo ugonjwa?
picha please tuone
 
Hermorhoids aka Bawasiri, ni mishipa ya anus ikipata mshtuko inavimba au kupasuka. Kama ulibeba kitu kizito huku umebana pumzi kwa kutumua tumbo au umebadilisha namna ya kukaa/chutama ghafla ni mojawapo ya sababu, sio ugonjwa wala maambukizi.

Mara nyingi siku za mwanzo inakuwa na maumivu makali sana ukikaa au ukitaka kijisaidia ila baada ya cku chache inaisha na kuondoka yenyewe kwa dawa za maumivu na vyakula laini. Nlipataga hii kitu ilibidi nichukue leave ofisini mana kukaa ni vita.

Ukiona siku chache zimepita hakuna nafuu nenda kaone daktari, wengne wanafanya minor surgery kuondoa kile kinyama ila huwa sio wote unless imeshindikana kupona.
 
Weka hapa mkuu 2jue weng maana hili ni Janga kubwa s3ma vijana weng wajificha kusema
 
Habarini wanajamvi,

Naomba msaada wenu. Mama yangu anasumbuliwa na tatizo la bawasiri tangu mwaka 2008. Mwaka 2019 alienda hospital akafanyiwa matibabu na kukatwa kwa hizo nyama lakini baadae vikaota tena, mpaka sasa hana matumaini ya kwenda hospital.

Naomba mnisaidie kama kuna tiba sahihi ya hili tatizo.
 
Mkuu kwanza nikupe pole cha pili huo ugonjwa kufanyiwa upasuaji wa haraka huwa ni presha tu ya Madocta wengine huwafosi watu ili wapige hela

lakini huo ugonjwa ukitulia kwa kuzingatia dayati unaondoka wenyewe bila kisu, na wengi wanaita kinyama lakini sio nyama, ile ni sehem ya msuli wa kinyeo inavimba kwa sababu tofauti, so ukizingtia mlo, mazoezi ya kutembea, huwa vinarudi vyenyewe bila shida yoyote
 
Asante Sana mkuu kwa ushauri wako, ila hili tatizo lake nimekuwa hatarishi mpaka Sasa.
Hata kukaa hawezi tena anashinda amelala tu.
 
Unawaza au ulishawahi kuugua au una ushahidi wowote wa kuweza kumsadikisha mtoa mada ili afuate unachomuambia...?
 
Unawaza au ulishawahi kuugua au una ushahidi wowote wa kuweza kumsadikisha mtoa mada ili afuate unachomuambia...?
Mimi nliwahi kuumwa huo ugonjwa, nlitumia vyakula vyenye asili ya kamba... Viazi, mihogo na ndizi mbivu. Pia nilikunywa maji mara kwa mara na kuacha kula nyama nyekundu. Ilipona ndani ya wiki mbili.
 
Mimi nilipona baada ya kutumia dozi.
Na nikamwelekeza jamaa yangu naye akapona Ila inabidi uiwahi wiki hiyihiyo unapojitokeza.
Nilipewa dawa na Famasist juu ya kava pameandikwa hivi.

" Amoxillin & Clavulanate
Potassium Tablets USP
500mg 125mg
SPOTCLAV 625 "

Dozi, 2 × 7 kila siku vidonge viwili kwa siku saba.
Kau hadi Leo

Na Panadol za kutuliza maumivu
 
Kuna jamaa yangu alipona bila upasuaji alipata dawa hospitali ya Aga Khan na kuzingatia vyakula.

Nitext whatsapp 0745090905 nikupe namba yake akuelekeze.
 
Mkuu, with due respect!

Sio msuli, ni mishipa ya damu (blood vessels) ya maeneo hayo kutanuka (dilate).

Aende (hospitali yoyote yenye) Pharmacy kubwa wamtengenezee nifedipine 0.2% ointment.
 
Tumia karanda lugo chemsha na kunywa glass moja asubuhi na jioni kwa muda wa week 2 litaisha kabisa
 
Tumia dawa za kihaya karanda lugo mixed with akatashuba nyuma utarudi hapa kunishukuru week mbili tu utaona matokeo. Kuna mmoja humu humu ananishukuru sana
 
Mrejesho.

Nimetumia utomvu wa migomba. Nilikuwa napaka asubuhi na jion kila mara baada ya kuoga, nakausha na kitambaa laini na safi kisha napaka huo utomvu. Nimefanya hivyo kwa siku 5 hivi uvimbe ukaanza kutokomea, mara baada ukaanza kirudi tena. Niliendelea kupaka uvimbe ukaanza kutokomea hadi pamekuwa flat kabisa kama ilivyo kawaida.

Sihisi maumivu ya aina yoyote ile hadi naandika ujumbe huu nina zaidi ya wiki mbili sasa. Sema matatizo ya wabongo tu, sijapaka tena toka tatizo liishe.
Asante sana.
 
Mrejesho.

Nimetumia utomvu wa migomba. Nilikuwa napaka asubuhi na jion kila mara baada ya kuoga, nakausha na kitambaa laini na safi kisha napaka huo utomvu. Nimefanya hivyo kwa siku 5 hivi uvimbe ukaanza kutokomea, mara baada ukaanza kirudi tena. Niliendelea kupaka uvimbe ukaanza kutokomea hadi pamekuwa flat kabisa kama ilivyo kawaida.

Sihisi maumivu ya aina yoyote ile hadi naandika ujumbe huu nina zaidi ya wiki mbili sasa. Sema matatizo ya wabongo tu, sijapaka tena toka tatizo liishe.
Asante sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…