msabillah
JF-Expert Member
- Dec 5, 2011
- 4,764
- 3,192
Castle,
Kwanza mpe pole sana. Mimi siyo Daktari ila ninajua dawa ya kienyeji ambayo niliwahi kuelekezwa kwa ajili ya my wife wangu, na alipoitumia akapona kabisa na ninatamani siku moja nimpate Daktari aliyebobea katika ugonjwa huu anielezee kwa undani.
Dawa yenyewe ni hivi, chukua kokwa la parachichi, likatekate vipande vidogovidogo kisha anika juani mpaka likauke. Baadae saga ili kupata unga laini. Chukua yai la kuku wa kienyeji, pasua utoe kile kiini chenye rangi ya njano, changanya na ule unga ambao umeandaa awali, koroga ili kupata mchanganyiko mzuri.
Kisha mpe mgonjwa wako anywe kijiko kimoja mara tatu, baada ya siku tatu atakuwa amepona.
Baada ya hapo akitaka kujua kama amepona au la, anaweza kufanya test ya kawaida kabisa kwa kula maharage, au chakula chenye pili*2 au akaenda kupima hospitali kabisa.
Ukifanikiwa ni PM.
sante lakini kwenye kula kiini cha yai mmmh! Wacha na mimi nijaribu.