Ugumu anaoupitia Harmonize ni kielelezo tosha kwanini sanaa yetu haikui. WCB inaua wasanii nje ya lable yao

Ugumu anaoupitia Harmonize ni kielelezo tosha kwanini sanaa yetu haikui. WCB inaua wasanii nje ya lable yao

Diamond anakusaidia ukiwa sio threat kwake
ukishakua tishio wa himaya yake lazima mgombane anajua team yake yote itamsapoti na watakushusha.
Shetta /Ommy dimpoz /Konde boy nk
yoyote anaetishia himaya ya Diamond[emoji724]
Diamond alivyokua anamsifia konde,Wakina shetta /ommy anaenda nao kila mahala kama chawa sio wa kuishia ivi leo.Kama sio fitna ni nini[emoji2]
Hizo fitna anazofanya ni Kama zipi tujue?
 
Diamond anakusaidia ukiwa sio threat kwake
ukishakua tishio wa himaya yake lazima mgombane anajua team yake yote itamsapoti na watakushusha.
Shetta /Ommy dimpoz /Konde boy nk
yoyote anaetishia himaya ya Diamond[emoji724]
Diamond alivyokua anamsifia konde,Wakina shetta /ommy anaenda nao kila mahala kama chawa sio wa kuishia ivi leo.Kama sio fitna ni nini[emoji2]
Chunguza vizuri hao wote ulowataja nani anaanzaga kumzingua mwenzake.... Isijekuwa unachuki zako jombaa.
 
Nimefatilia kwa undani mikiki anayopitia kondeboy toka ajiengue WCB. Kiukweli hajashuka Kama tunavyolazimishwa tuamini. Kwanza official songs katoa UNO na KUSHOTO KULIA na zote zimefanya vyema you tube. Hainshtui na Hujanikomoa ni bonus track wakati anajiandaa kuachia album Yake. Inashangaza sana kuwa nchi yenye watu million 50 tunataka msanii awe DIAMOND PLATINUMZ TU.

Wenzetu Nigeria international artist ni wengi kwa sababu wanaachiana nafasi. Huku Tz tunapambana kushushana yaani mpaka media za YouTube hazipost show za harmonize ili tu akose mvuto. Wenzetu wamefanikiwa kwa kuachiana nafasi.

Sasa hivi wamemwachia nafasi BURNABO.Hata hapa watu watakavyojibu ni kwa kumkatisha tamaa kondeboy.
Tatizo mna bonga Sana , Harmonize akifanikiwa mnamrushia dongo Diamond na kumcheka , wakat 80% ya watu wenye uelewa na mambo ya mtandao na Wana passion na mziki wa bongo ni fan kidanki danki wa mond ....na konde boy anategemea hao hao ndo wamtoe , aendelee Tu kucheza twist , wanigeria hawana unafiki huo....
 
Umeongea kitu kikubwa sana Mzee ila team Wcb watakuponda na watakukebei sana

Kama Diamond angebaniwa wakati anatoka sidhani kama angefika hapo alipo, Team ina meneja anajisifu kwa kujiita kamati ya Fitina
Diamond alibaniwa Sana na hao mawingu wako na wahuni kibao waliokuwa wanajifanya bongo fleva ni yao, ikabid atobokee Nigeria chini ya kamanda Sallam Sk , kitu kikawaka MTV , kila mmoja apambane kivyake endeleeni kumsuport konde boy mwacheni mond na fans wake
 
Mbona diamond kawasaidia wasanii wengi amempa connection shetta kufanya collabo na kcee, chege na run town, amemlipia video ya dully Sykes inde, kamsaidia dj ommy kumpa connection mpaka kumwezesha kufanya vizuri medani za kimataifa.Pia angekuwa ni mbinafsi Kama unavyosema harmo asingekuwa msanii wa kimataifa, Asingemtoa Rayvanny, Lavalava na mbosso
Tatizo kila msanii anataka afanane na Mond , asipomfikia anachukia anaona anabaniwa , diamond ni Baba Yao , Ni Mungu wao ndo aliwaumba , ?? Wapambane kivyao
 
Japo mimi sio shabiki wa Diamond lakini huwa nashangaa sana mtu anaposema sijui Diamond mbinafsi,anataka kuwa juu peke yake,anatengeneza beef na wasanii wengine nk,Msanii anabaniwa vipi na Diamond kama yeye mwenyewe hajitumi,hana uthubutu,hajui kuutangaza mziki wake,hatafuti angalau collabo na wasanii wakubwa wa nje ambapo watamtangaza zaidi au muziki wake kuvuka border,muziki ni biashara kila mtu anahangaikia upande wake unabaniwa vipi na msanii mwingine?, Harmonize kuondoka WCB binafsi hata mimi nilipongeza nikijua ataleta changamoto kubwa ktk mziki wa bongo,sasa iweje aonekane anabaniwa wakati lebo aliyokuwepo mwanzo ndio inaongoza kubaniwa na media nyingi?,wakati yupo WCB anatoa hit songs haikua clouds media,East Africa radio/tv,efm,millard ayo ambazo zilikua zikimsampoti,leo hii media hizo zinamsapoti harmonize hapa anabaniwa vipi?, tayari wakati yupo WCB alishafanya international collabo nyingi ambazo zimeshafanya atambulike zaidi Africa hapa napo nini kinamzuia asiwe mkubwa zaidi ya Diamond?,pengine hii ndio ingekuwa fursa kwake kutoa hit songs nyingi na kujiongezea fan base kwasababu yupo huru,hebu nielewesheni labda sielewi wakuu maana ya msanii kubaniwa..

Sent using Jamii Forums mobile app
Yaan kinacholalamikiwa hapa ni kuwa fans wa WCB wanambania konde boy Kwa influence ya Mond , inadaiwa wamemkimbia kisa katoka WCB na lawama zote zinamwangukia Diamond
 
WCB ni Diamond peke yake, ukiwa katika Lebal hiyo mashabiki wake ndio watakua wako, ukiondoka unabakia na mashabiki wa Muziki pekee, wale wenhine wanabaki nae na kukuchukia wewe.

Naamini hivi kwasababu, wanaojitoa WCB sio member wa kundi au Band kusema tuwaone peke yao watafanyaje?

Na kama Nyimbo alizozitoa nje ya WCB angezitoa akiwa hajajitoa amini zingekua habari nyingine, mfano UNO na ingekua na Collable ya Mond ndani yake.

Sisi wabongo ni wavivu so inapotokea mtu kufanikiwa huchukia wengine kuwa juu yake ili kutokana na uvivu wake asije kuanza kutumwa.

Hali hii inasababisha Tasnia nzima kukosa uwazi na yote ni woga wakushuhudia wengine wakipata mafanikio.

Mfano. Thamani ya msanii mmoja mmoja hajulikani, malipo wanayoyapata katika tour, social media au shows hawayaweki wazi. Maisha yao tuu ni siri wengi hatujui wanaishi vp...

kwa vile ni kibongo bongo utaambiwa unafuatilia mambo ya watu ambao wengi wao hawana maisha ya majina yao. Lakini maisha yakina jigga tunayajua hadi mtaa anaoishi na kwa mwaka kaingiza shing ngapi na ni mmoja wa mabilionea.

Kwahiyo naamini katika uwazi kama chachu yakuchochea wengine wapambane zaidi na hatimae kupatikana wasanii wengi wenye mafanikio. Kuliko hivi sasa wenhi wanaogopana kutokana na njaa.




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo ninaloliona ni kuwa konde boy anataka ajilinganishe na mond kitu ambacho kwa namna moja ama nyingine hakiwezekani kama ataamua afanye music bila kushindana na mtu atatoboa ila akiendelea hivi na mafumbo kwenye music atapotea kingine sie mashabiki hatuwambii ukweli wasanii wetu tunawapa sifa zilizo nje ya uwezo wao
Na haya yote ni matokeo ya wimbo wa kwangwaruu , hamna kingine
 
Afanye mziki wake aache majungu,kaanza Hainishtui watu kimya,kaja Hujanikomoa WCB wamekaa kimya ,sababu wameona ujumbe umekaa kimafumbo labda hauwahusu wao.

Juzi tena kapost video kuna kiemoro kinakunywa,huku kinacheza kakifananisha na meneja wake wa zamani ambaye anapenda bata (Sallam ) naona wenzake nao wamereact,sasa hivi anatafuta huruma.

Yy afanye mziki wake kama ameamua kumove on,akina Kiss Daniel,Lil Kesh,Tiwa Savage,Wizkid wametoka kwenye label zao za zamani lakini hawana madongo wala mafumbo kutoka kwenye label zao zilizo watoa na kuwasaidia.

Nigeria hamna mziki wa kuachiana nafasi haupo,ila wenzetu wanabebana sana,Burna boy kaachia nyimbo imehit kuliko wenzake,lkn mwaka jana Wizkid kaachia nyimbo,Olamide kaachia nyimbo,Davido kaachia nyimbo,Naira Marley,Zlatan,Patoranking,Simi,Adenkule gold,Rekardo Bank,Joeboy,Fireboy wote wameachia nyimbo.

Na kwa mwaka jana msanii alifanya vizuri Nigeria ni Naira Marley,akifuatiwa na Zlatan.Burnaboy alifanya vizuri 2018 na ndio maana mwaka jana alikusanya tuzo nyingi sana.
Hapo kwa BurnaBoy mtoa tafadhali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Me sipo kwa Diamond wala Harmonize, me nipo tu kama mchambuz wa mziki , nachojiuliza ni kwamba mfano USA yan Chriss Brown amwachie nafasi August Alsina aachie ngoma ili nae ashine ? Mbona Marekan kila mtu kwa Muda wake anaachia ngoma zake anaacha jamii ichague, Yan Cardi B asubir Nicky Minaji avumee ye ndio aachie ngoma ? Nope thats not true, ila hata hivyo Bongo kuna tatizo, kama uchawi upo kweli(which i dont believe) watakuwa wanarogana sana, Kitu kibaya kwenye mziki wa Tanzania ni kwamba Diamond ambae ndio mkubwa hataki wenzake wafanikiwe sasa huwa simwelewi kwakweli, we angalia jambo moja mtu alijitoa lebo ukataka alipe hela ili awe na copyright ya ngoma zake kalipa me nlidhan after payment they were supposed to be good, Yan bado kuna kwere tu ? Nakumbuka Birdman, Lil wayne alivyojitoa cash money alidemand hela na alipolipwa wakawa wako poa tu na birdman na kuna ngoma wamefanya pamoja na ndio birdman alikubali kuachia the carter IV.

SOMO LA KUJIFUNZA

Kwenye maisha hapa duniani tusiwe watu wa roho ya kwanini, hata tukiwa successful hatuwez kuwa na baraka, kuna leo na kesho jitahidini kuwa humble one way or the other...BE HUMBLE....


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Mbona diamond kawasaidia wasanii wengi amempa connection shetta kufanya collabo na kcee, chege na run town, amemlipia video ya dully Sykes inde, kamsaidia dj ommy kumpa connection mpaka kumwezesha kufanya vizuri medani za kimataifa.Pia angekuwa ni mbinafsi Kama unavyosema harmo asingekuwa msanii wa kimataifa, Asingemtoa Rayvanny, Lavalava na mbosso
Watu kwa lawama!

kelphin kepph
 
Harmonize aache kulalamika, kwa namna alivyojiondoa WCB amemnufaisha Diamond, mashabiki wamekuwa na huruma zaidi kwa Diamond wakidhani ndie alitendwa, kinyume chake mashabiki wamekuwa na chuku juu yake wakiamini ni mshenzi asiye na fadhila.

Imekuwa mapema sana kwake kuungana na maadui wa Diamond, hii inaendelea kuwafanya mashabiki wamuone yeye against Diamond, matokeo yake wameamua kumuadhibu.

Binafsi naona atazidi kushuka vile yuko peke yake ni vigumu kukaa midomoni na machoni mwa watu siku zote. Pole yake ila namuombea mazuri.
Screenshot_20200221-130719.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hio video nimepost bila kuquote mtu wala kuandika caption mbona unajishtukia kama umetiwa doko?
Hata tukija kwenye Hiyo video niambie video ipi hapa bongo ambayo maudhui yake au scenes zake hazifanani na video yoyote duniani?
 
Nimefatilia kwa undani mikiki anayopitia kondeboy toka ajiengue WCB. Kiukweli hajashuka Kama tunavyolazimishwa tuamini. Kwanza official songs katoa UNO na KUSHOTO KULIA na zote zimefanya vyema you tube. Hainshtui na Hujanikomoa ni bonus track wakati anajiandaa kuachia album Yake. Inashangaza sana kuwa nchi yenye watu million 50 tunataka msanii awe DIAMOND PLATINUMZ TU.

Wenzetu Nigeria international artist ni wengi kwa sababu wanaachiana nafasi. Huku Tz tunapambana kushushana yaani mpaka media za YouTube hazipost show za harmonize ili tu akose mvuto. Wenzetu wamefanikiwa kwa kuachiana nafasi.

Sasa hivi wamemwachia nafasi BURNABO.Hata hapa watu watakavyojibu ni kwa kumkatisha tamaa kondeboy.
Lack of originality.

Mmakonde 98% anamuiga Diamond , hana ubunifu ndio maana anazidi kufeli kila kukicha.

Na bado [emoji23]
 
Kwani kabla Diamond hajakua kimziki mziki ulikuaje? Ulikua umekua?
ulikua mzuri sana kila mtu alipewa nafasi yake kwa ukali wake.
Ndo mana unaona hata diamond amefika alipofika
kwa sasa kuna namna mziki umetengenezwa haupendezi tena
 
Back
Top Bottom