Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 28,722
- 20,610
Ndugu zangu Watanzania,
Ni lazima ifike wakati tukubaliane na ukweli mchungu ya kuwa CCM ndio Moyo wa Taifa letu,ndio Mapafu ya Taifa ,ndio damu ya Taifa na ndio OKSIJENI ya Taifa letu. Hakuna amani wala utulivu wala umoja wala mshikamano wala masikilizano wala upendo wala kuzungumza lugha moja pasipo uwepo wa CCM Madarakani.
Pasipo CCM hakuna amani wala utulivu ,hakuna mipango wala Dira kwa Taifa letu,hakuna kesho iliyo njema na yenye matumaini pasipo uwepo wa CCM Madarakani. Ni CCM pekee yenye uwezo wa kuliongoza na kulivusha Taifa letu katika nyakati ngumu,ni CCM pekee yenye uwezo wa kuwaunganisha watanzania wa Dini zote,rangi zote,jinsia zote,makabila yote na wa kanda zote.ni CCM pekee yenye uwezo wa kuwaletea pamoja watu wa rika zote.
Ndio maana ndani ya CCM na serikali yake utawakuta viongozi kutoka Dini zote, makabila yote,rika zote,makundi yote,jinsia zote na wenye kila aina ya Elimu. Kila mmoja ndani ya CCM anayo nafasi sawa na mwanachama mwingine.Ndio maana unaweza kuwa kiongozi ndani ya CCM hata kama wazazi wako hawakuwa viongozi.kwa sababu kinachoangaliwa ndani ya CCM ni uwezo wa mtu kiuongozi,sifa na uwezo wa kumudu majukumu na kukubalika kwa watu.
Ni CCM pekee yenye uchungu na Maisha ya watanzania na Taifa letu kwa ujumla wake. Ni CCM pekee yenye uwezo wa kumsikiliza kila mtu,kupokea maoni na mawazo ya kila mtu, kumvumilia kila mtu pasipo kumbagua mtu. Ndio maana wapo wengine ndani ya CCM unaweza kuhisi ni wapinzani au watahamia upinzani kesho ,lakini huwezi ukaona wakifukuzwa chamani.
Ni CCM pekee yenye kujiendesha kitaasisi .tofauti na vyama vingine kama CHADEMA. ambavyo vimewekwa mifukoni mwa mtu mmoja tu aliyeamua kujimilikisha chama Utafikiri kitega uchumi cha Familia .na kwamba ni yeye tu mwenye akili kuliko wanachama wengine wote na kwamba wengine hawana akili na ni mambumbumbu wa uongozi na hawana haki ya kuongoza chama.
Embu jaribu kuangalia Ingetokea CHADEMA ipo madarakani? Unafikiri nini kingetokea? Kwanza wangewagawa sana watanzania na kuwabagua.ndio sababu ya sera yao ya Majimbo,pili wangeleta ukabila sana hapa nchini nakuona makabila fulani kutoka ukanda fulani ni bora zaidi na yenye kupaswa kupewa nafasi za juu za uongozi. na kwamba makabila mengine kutoka kanda zingine ni washamba tu wanaopaswa kuongozwa na kuamuliwa kwa kila kitu.
Wangekuwa wamelipasua na kulisambaratisha kabisa Taifa. Kusingekuwa na habari za Muungano wala Umoja wa kitaifa. Ni muhimu sana watanzania kuendelea Kuiweka CCM madarakani na kuendelea kuiamini .kwa sababu imekuwa na usikivu, unyenyekevu na kujali Maisha ya watu pamoja na kutanguliza mbele masilahi ya Taifa letu na ustawi wa wananchi.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Ni lazima ifike wakati tukubaliane na ukweli mchungu ya kuwa CCM ndio Moyo wa Taifa letu,ndio Mapafu ya Taifa ,ndio damu ya Taifa na ndio OKSIJENI ya Taifa letu. Hakuna amani wala utulivu wala umoja wala mshikamano wala masikilizano wala upendo wala kuzungumza lugha moja pasipo uwepo wa CCM Madarakani.
Pasipo CCM hakuna amani wala utulivu ,hakuna mipango wala Dira kwa Taifa letu,hakuna kesho iliyo njema na yenye matumaini pasipo uwepo wa CCM Madarakani. Ni CCM pekee yenye uwezo wa kuliongoza na kulivusha Taifa letu katika nyakati ngumu,ni CCM pekee yenye uwezo wa kuwaunganisha watanzania wa Dini zote,rangi zote,jinsia zote,makabila yote na wa kanda zote.ni CCM pekee yenye uwezo wa kuwaletea pamoja watu wa rika zote.
Ndio maana ndani ya CCM na serikali yake utawakuta viongozi kutoka Dini zote, makabila yote,rika zote,makundi yote,jinsia zote na wenye kila aina ya Elimu. Kila mmoja ndani ya CCM anayo nafasi sawa na mwanachama mwingine.Ndio maana unaweza kuwa kiongozi ndani ya CCM hata kama wazazi wako hawakuwa viongozi.kwa sababu kinachoangaliwa ndani ya CCM ni uwezo wa mtu kiuongozi,sifa na uwezo wa kumudu majukumu na kukubalika kwa watu.
Ni CCM pekee yenye uchungu na Maisha ya watanzania na Taifa letu kwa ujumla wake. Ni CCM pekee yenye uwezo wa kumsikiliza kila mtu,kupokea maoni na mawazo ya kila mtu, kumvumilia kila mtu pasipo kumbagua mtu. Ndio maana wapo wengine ndani ya CCM unaweza kuhisi ni wapinzani au watahamia upinzani kesho ,lakini huwezi ukaona wakifukuzwa chamani.
Ni CCM pekee yenye kujiendesha kitaasisi .tofauti na vyama vingine kama CHADEMA. ambavyo vimewekwa mifukoni mwa mtu mmoja tu aliyeamua kujimilikisha chama Utafikiri kitega uchumi cha Familia .na kwamba ni yeye tu mwenye akili kuliko wanachama wengine wote na kwamba wengine hawana akili na ni mambumbumbu wa uongozi na hawana haki ya kuongoza chama.
Embu jaribu kuangalia Ingetokea CHADEMA ipo madarakani? Unafikiri nini kingetokea? Kwanza wangewagawa sana watanzania na kuwabagua.ndio sababu ya sera yao ya Majimbo,pili wangeleta ukabila sana hapa nchini nakuona makabila fulani kutoka ukanda fulani ni bora zaidi na yenye kupaswa kupewa nafasi za juu za uongozi. na kwamba makabila mengine kutoka kanda zingine ni washamba tu wanaopaswa kuongozwa na kuamuliwa kwa kila kitu.
Wangekuwa wamelipasua na kulisambaratisha kabisa Taifa. Kusingekuwa na habari za Muungano wala Umoja wa kitaifa. Ni muhimu sana watanzania kuendelea Kuiweka CCM madarakani na kuendelea kuiamini .kwa sababu imekuwa na usikivu, unyenyekevu na kujali Maisha ya watu pamoja na kutanguliza mbele masilahi ya Taifa letu na ustawi wa wananchi.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.