Uhamiaji hawaoni aibu kutoa passport laki mbili kwenye nchi yenye watu milioni 55?

Uhamiaji hawaoni aibu kutoa passport laki mbili kwenye nchi yenye watu milioni 55?

Uleanzisha uzi kichwa chako kibovu, hivi unajua unyeti na gharama yakutengeneza passport1? Ishu za passport si za kukurupuka! Na hakuna nchi duniani inayotegemea pesa kwenye miradi kama ya passport, passport ukitaka kuifanya biashara yataibuka mengi haswa swala la rushwa na urasimu, nawapa kongole kwa wanachokifanya uhamiaji, mnataka passport zipatkane hovyo alafu mkafanye matukio nchi za watu!?

Sent using Jamii Forums mobile app
Nadhani wao wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanaempatia passport ni Mtanzania halisi tu... Wanatakiwa ku focus kwenye uraia maana ni hatari sana mtu ambaye sio raia wa nchi X kuwa na pass ya nchi X
 
Watakudai uthibitisho wa safari kama utawaambia unaenda kufanya shughuli maalumu - invitation ya mkutano, admission letter ya shule, medical treatment etc. Sina uhakika sana kama kukudai hivyo vitu is to your advantage ili wakupatie passport haraka ama la. Lakini ukiwaambia ninajiandaa kwa mfano kwenda safari binafsi tu hapo Uganda hawatakudai chochote kuhusu safari zaidi ya those other key supporting documents. Nina uhakika 200% na hiki ninachokisema.

All in all, passport hi haki ya kila raia na hakuna evidence kuwa kuna Mtanzania yeyote amewahi kunyimwa passport kwa kushindwa tu kuelezea vizuri madhumuni ya safari yake. Kimsingi Uhamiaji wala hawaconcentrate saaana kwenye madhumuni ya safari, zaidi huwa wanataka uthibitisho wa uraia na mara nyingi wale wanaotokea mipakani (Kigoma, Ngara etc) usumbufu wake huwa ni mkubwa zaidi.
Madhumuni ya safari yanawahusu nini?
 
Nadhani wao wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanaempatia passport ni Mtanzania halisi tu... Wanatakiwa ku focus kwenye uraia maana ni hatari sana mtu ambaye sio raia wa nchi X kuwa na pass ya nchi X
Hawana mechanism ya kujua mtanzania halisi na hasio halisi zaidi ya usumbufu kwa raia kweli mtu anakuomba vyeti vya wazazi wako walio zaliwa kabla ya uhuru wa Tanzania kweli vitapatikana manaake mtu ambaye hana wazazi/au walezi, hana haki ya kupata passport? Ni usumbufu tu hi nchi inaongozwa kisiasa kila jambo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi ni sahihi Uhamiaji kutoa Passport mpya laki mbili kwenye nchi yenye watu milioni 55?

Nchi za wenzetu mfano Marekani passport na visa ni chanzo kikubwa cha mapato ya serikali.

Mfano uhamiaji wangepewa lengo mfano la kutoa Passport milioni moja tu kwa mwezi kwa bei ya Passport ya shilingi laki moja na nusu serikali ingeingiza pato la shilingi bilioni 150 ambazo zingesaidia mno nchi.

Kikwazo kikubwa cha watu kupata Passport ni kuwa Afisa Passport hatakiwi kumuuliza mtu anaenda wapi kufanya nini akitaka kumpa. Hilo atapambana nalo Ofisi ya Ubalozi anakoenda akienda kuomba Visa. Wewe kila Mtanzania mpe passport mengine mwachie akapambane na hali yake mbele kwa mbele

Passport ni kitambulisho tu cha kawaida kama cha NIDA tofaiti iliyopo ni kuwa cha NIDA kinatambuliwa ndani ya nchi wakati passport ni kitambulisho cha raia cha Kimataifa .Mtu ruksa kuwa na passport hata kama hasafiri ni kitambulisho chake cha kimataifa.

Mtu anakiwa kuwa na vitambulisho viwili cha NIDA na passport

Uhamiaji wanaona passport kama kitu kikuubwa!

Asante kwa hii mada. Naomba nifafanulie; tunajaza nini pale walipouliza unaenda nchi gani na kufanya nini.. wakati me nahitaji tu passpoti niwe nayo.
 
Is that number really true?.
No wonder when you get a trip abroad people feel like ur going to a semi-heaven
 
Uleanzisha uzi kichwa chako kibovu, hivi unajua unyeti na gharama yakutengeneza passport1? Ishu za passport si za kukurupuka! Na hakuna nchi duniani inayotegemea pesa kwenye miradi kama ya passport, passport ukitaka kuifanya biashara yataibuka mengi haswa swala la rushwa na urasimu, nawapa kongole kwa wanachokifanya uhamiaji, mnataka passport zipatkane hovyo alafu mkafanye matukio nchi za watu!?

Sent using Jamii Forums mobile app

Mkuu wanaposema hati ya kusafiria ni haki yako wana maanisha nini.....na kwann si kila mtu hatakiwi kuipata ukinijibu haya maswali ntashukuru sana


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Sema mimi kuna jambo limenitisha kidogo; Nilipata passport yangu miaka 12 iliyopita. Na by that time nilikuwa under 18, so mlezi wangu ndiye aliyefanya process zote. Tulikuwa na safari ya nje ya nchi then baada ya ile safari sikuwahi kutumia tena ile passport na apparently ilikuja kupotea mwaka 2016. Unfortunately, sikukariri namba ya ile passport (uzembe ofcoz😉) - wala mlezi wangu. Nilitoa taarifa polisi kama kawaida, na taratibu zinataka mtu apeleke tangazo kwenye gazeti la serikali kabla hajapewa nyingine.

Now here comes the issue; mimi nilisahau namba ya passport yangu iliyopotea. Kwa hiyo haiwezekani kutangaza gazetini mpaka niipate namba ya passport. Sehemu pekee ninayoweza kuipata namba ni uhamiaji. Kilichonitisha ni kuwa, uhamiaji pia hawana records zangu kabisa - as if sijawahi kupewa passport at all. Sababu inayotolewa ni moja; mabadiliko ya mfumo, kutoka zile 'za mkono' kuja hizi mpya 'mashine readable'.

Nilipopewa jibu hilo ofisi za uhamiaji mkoani, sikushangaa sana - maana wao walishauri nifike Dar nitasaidiwa. Ishu ni kuwa hata nilipoenda pale mambo ya ndani hawana records zangu!!! I was like,.. WTF 😳🙄😡 Nilicho-notice ni kuwa, mfumo huu mpya hauna taarifa za wamiliki wa passport zile za zamani otherwise uwe ume-upgrade personally.

Mimi ni mzembe bila shaka, lakini kwa hili uhamiaji nao dizaini ni wazembe zaidi yangu!😎
*I stand to be corrected*

Dah kumbe ndo maana ukitaka kubadili kupata mpya yaani process ni kama kuanza upya


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Hawana mechanism ya kujua mtanzania halisi na hasio halisi zaidi ya usumbufu kwa raia kweli mtu anakuomba vyeti vya wazazi wako walio zaliwa kabla ya uhuru wa Tanzania kweli vitapatikana manaake mtu ambaye hana wazazi/au walezi, hana haki ya kupata passport? Ni usumbufu tu hi nchi inaongozwa kisiasa kila jambo

Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa kwa sababu hawana hiyo mechanism, mtu akienda na nationa ID tu inatosha kumpa pass... Mambo mengine wawaachie vyombo vingine!
 
Maelezo yafuatayo yapo kwenye pasipoti. "Hii ni kuwaomba na kuwasihi, kwa jina la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wote wanaohusika, kwa kusudi la kumruhusu mwenye pasipoti hii kupita bila kizuizi ama kipingamizi chochote na vile vile kumpa msaada na ulinzi wowote ambao utaonekana kuwa wa lazima"
Pasipoti ni hati ya kusafiria nje ya nchi na siyo kitambulisho.
 
Hayakuhusu naweza kuitaka hata for prestige tu kuwa Nina passport wewe kinakuuma Nini? It is non of your bussiness.Wewe nipe passport mengine niachie mwenyewe

If everyone angekua anataka maisha yaende ivo kama unavotaka wewe, this world would have been a big mess
 
Hayakuhusu naweza kuitaka hata for prestige tu kuwa Nina passport wewe kinakuuma Nini? It is non of your bussiness.Wewe nipe passport mengine niachie mwenyewe

Hata terrorists wanataka sana passport ndo maaana wanahangaika na passport feki, you think leading people is an easy thing as you just say nipe! Afterall skushangai something is still missing kichwan kwako
 
Maswaali meengi " unaenda wapi, kufanya nini, nani kakupa mwaliko, je ni ndugu yako, utakaa siku ngapi, tuone akaunti ya benki una tsh ngapi, ulishawahi kwenda huko, unafanya kazi gani/wapi,? "
kifupi wanakuintarogeti pale... Kaaazi kweli kweli
 
Hata terrorists wanataka sana passport ndo maaana wanahangaika na passport feki, you think leading people is an easy thing as you just say nipe! Afterall skushangai something is still missing kichwan kwako
kwa hiyo nchi zinazotoa passport chap chap ndani ya saa tatu kama rwanda zimejaa terrorists?
 
Maswaali meengi " unaenda wapi, kufanya nini, nani kakupa mwaliko, je ni ndugu yako, utakaa siku ngapi, tuone akaunti ya benki una tsh ngapi, ulishawahi kwenda huko, unafanya kazi gani/wapi,? "
kifupi wanakuintarogeti pale... Kaaazi kweli kweli
wanataka waonekane wako busy while they are busy for nothing kwa kuuliza maswali kama hayo

hayo maswali ni ya ubalozi unapoomba viza sio yao.Yaani mtu anafika jioni anasema leo nimechoka nimefanya kazi kweli kweli kwa kushinda akiuliza maswali ya ubalozini?

Akienda mtaalamu consultant afanye work study uhamiaji kuna watu kibao watapewa retrenchment au redundancy
 
kwa hiyo nchi zinazotoa passport chap chap ndani ya saa tatu kama rwanda zimejaa terrorists?

Unajua passport zinategemeana right? Mfano passport ya afrika mashariki ukiachana na lile likitabu ni few hours unapata? Passport gan hio ingine unapewa ya 3 hours nje ya afrika? Electronicr passport ama? Na unajua Rwanda ni kama singida tu kuwahudumia wananchi ni rahisi, na watu wengi wamestarabika hata ujenzi wa taifa lao wanalichukulia kwa makini sana, mfano wanayo event flan wanafanya usafi kwa pamoja nchi nzima na biashara zote znafungwa? Na pia wanawajengenea watu nyumba kipindi cha huo usafi na mengine mengi


Ni tafauti na sisi ambao gari LA taka likipita unasubiri lianze kuondoka ndo ukimbize takataka na bado unataka kutema mate juu
 
wanataka waonekane wako busy while they are busy for nothing kwa kuuliza maswali kama hayo

hayo maswali ni ya ubalozi unapoomba viza sio yao.Yaani mtu anafika jioni anasema leo nimechoka nimefanya kazi kweli kweli kwa kushinda akiuliza maswali ya ubalozini?

Akienda mtaalamu consultant afanye work study uhamiaji kuna watu kibao watapewa retrenchment au redundancy
Kweli kabisa
 
Back
Top Bottom