Uhamiaji Tanzania: Bila dhumuni la safari hakuna kupewa pasi ya kusafiria (Passport)

Uhamiaji Tanzania: Bila dhumuni la safari hakuna kupewa pasi ya kusafiria (Passport)

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Hii ndio taarifa mpya kutoka Uhamiaji iliyotolewa leo na Msemaji wake Paul Mselle.
Passport.png

Paul Mselle amesema haya...

Pasi ya kusafiria ni 'document' ya kiusalama na ni haki ya kiusalama na ni mali ya Serikali, pale ambapo mtu ataitumia vibaya basi anaweza akanyang’anywa

Pasi ya kusafiria sio kitambulisho kusema mtu achukue abaki nayo ndani ni lazima kuwe na dhumuni la safari, kama hauna safari hatuwezi kukupa pasi ya kusafiria

Mtu atakayepoteza Pasi yake ya kusafiria (Passport), itamlazimu kutoa taarifa Polisi pamoja na kutangaza kwenye gazeti na kwamba ni lazima atoe kiasi cha shilingi Laki tano kwa kupoteza Passport hiyo, na ili aweze kupata nyingine.

Kumekuwa na changamoto ya kuchelewa kwa pasi ya kusafiria sababu unakuta mtu hajakamilisha vigezo vya kupata pasi ya kusafiria. Kuna wengine wanawasilisha vyeti vya kuzaliwa ambavyo haviko kwenye mfumo wa RITA na ukimuuliza alikipataje anasema alimtuma mtu kwa maana ya vishoka na hawa unakuta wengine ni raia wa Tanzania na wengine sio raia wa Tanzania

Wengine nao unakuta taarifa za cheti cha kuzaliwa zinatofautiana na taarifa za vitambulisho vya Taifa, unakuta kwenye Kitambulisho cha TAIFA(NIDA) kazaliwa Temeke kwenye cheti kazaliwa Morogoro.

Passport.png
 
kwani ukimpa mtu passport akakaa nayo unapungukiwa na nini? Kwani unampa bure?

tanzania pekee ndo tunaona passport NI MALI. Nchi nyingi haya mambo hayapo.
Sasa utaombaje passport kama huna matumizi nayo?

Si unakua na mpango wa safari ndio unatafuta passport!? Au nakosea ndugu zangu[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2]
 
Hii ndio taarifa mpya kutoka Uhamiaji iliyotolewa leo .

View attachment 1727134
Man!!!!!!!!! Jamani mbona kila kukicha kila aliepewa madaraka anajifanya kuwa mbabe na kutoa amri za ajabu sana?

Hivi alitoa uamuzi huu hata alifikiri kwanza? Mtu tuseme anataka kwenda kusoma au kutembea nchi fulani, inabidi uombe visa, utaombaje visa bila ya kuwa passport. Mtu hatoki tu akaenda kununua tiketi ya kusafiri bila ya kuwa na uhakika wa kupata visa ya huko anakotaka kwenda.

Hawa jamaa hivi kweli wao wenyewe walishajaribu hata kusafiri nje ya nchi? Mfumo mzima wa kusafiri kwanza ni kuwa na lengo na uwezo wa kusafiri, unapata passport kisha unaomba visa. Unapoomba visa ndio unapoonyesha kwa ubalozi husika uwezo wako wa kununu ticket, lengo la safari yako, mdhamini wako, unapofikia n.k. Unapokubaliwa na kupewa visa ndio unanunua ticket ya kuondoka nchini.

Sasa hawa wanaotaka mtu anunue ticket ya safari ilhali hujui lini utaipata passport au hata akama utaipata si wana vichaa. infacts, mashirika mengi duniani siku hizi unaponunua ticket za ndege unatakiwa ujaze details zako na za passport yake, sasa mtu atajaza nini ikiwa hana passport?
 
Sasa utaombaje passport kama huna matumizi nayo?

Si unakua na mpango wa safari ndio unatafuta passport!? Au nakosea ndugu zangu[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2]
Passport ni haki ya kila Mtanzania.

Unafikiri unaweza ukafanya application

Ya mmb ya scholarship au kwenda kusoma chuo nje. Ajira nchi za nje bila kuwa pport taatifa zake

Ova
 
Back
Top Bottom