Uhamiaji tusaidieni kwanini passport haitumiki kama National Identification card katika baadhi ya ofisi nchini

Uhamiaji tusaidieni kwanini passport haitumiki kama National Identification card katika baadhi ya ofisi nchini

Ujuaji mwingi, fanya utafiti! Kila nchi na masuala yake. Sijawahi kuona nchi inayotumia passport kama Kitambulisho kwa raia isipokuwa kwa mhamiaji au Mgeni! Kwa uwanja wako wa kujidai -gesi na mafuta hatutii neno ila unapokuja tunapojua, ukiteleza tunakupa tu
Passport ndio ID, probably yenye taarifa sahihi kuliko hiyo NIDA
 
Lakini amekuuliza vizuri tu. Ulipaswa kumjibu kama inawezekana au haiwezekani. Na ukiingalia passport ina details zote ambazo zipo kwenye NIDA.
Yes, inautofauti ukienda mahali zamani hawataki passport maana sio kielelezo Cha mtanzania ni kielelezo Cha kujitambulisha wewe ni mtanzania ukiwa mahali nje ya Tanzania Sasa ukiwa ndani ya Tanzania huitaji passport Kwa sababu upo ndani ya Tanzania ndio maana wanahitaji vitambulisho vingine vikutambulishe wewe kama mtanzania mf. Cha kitambulisho ch mpiga kura , Cha nida basi
 
Yes, inautofauti ukienda mahali zamani hawataki passport maana sio kielelezo Cha mtanzania ni kielelezo Cha kujitambulisha wewe ni mtanzania ukiwa mahali nje ya Tanzania Sasa ukiwa ndani ya Tanzania huitaji passport Kwa sababu upo ndani ya Tanzania ndio maana wanahitaji vitambulisho vingine vikutambulishe wewe kama mtanzania mf. Cha kitambulisho ch mpiga kura , Cha nida basi
 
Unataka nikuoneshe sasa hivi nipo wapi dogo?
Wewe umesema hujawahi kuona Nchi zinatotumia Passport kama ID mimi nakwambia nimeona Nchi nyingi tu zinatumia Passport kama ID.
 
papsport ni idhini ya wewe kusafiri nje ys nchi ila sio kitambulisho kuwa na akili
 
Passport ya Tanzania anaweza kuipewa mtu asiye raia wa Tanzania ?
Ndio!... Passport ya Tanzania inaweza kutolewa kwa raia wa kigeni ili kumuwezesha kusafiri kwenda popote Duniani kama akipoteza au kuibiwa passport yake akiwa ugenini. Hii inakuwa rahisi zaidi kama huyo mgeni yuko kwenye jumuia kama ya Madola, SADEC au EAC.
Miaka ya 80/90 kulikuwa na idadi kubwa ya raia wa RSA, Malawi,Zimbabwe na Mozambique waliopewa passport za Tanzania ili waweze kusafiri kwende nchi za Ulaya kwa lengo la kupata Elimu.
Passport ya Tanzania inatolewa pia kwa raia wa kigeni ambaye yuko nchini na yuko kwenye mchakato wa kuukana uraia wa nchi nyingine ya kigeni. Mtu wa aina hiyo ni halali kujitambulisha kwa Passport ya Tanzania kwa sababu anakuwa hana kitambulisho cha uraia cha NIDA.
 
Duu single mother mna tabu ninyi
Wewendio single mother mie Sitegi wanaume kujitaki nuksi naunikome koma ukomae ndugu zako ndio watakuwa masingle mother na watatoa k ili wapat e matumizi ya watoto wako hawatapata kazi hata wafanyaje na Mungu atawapatiliza kizazi Cha tatu chakwako na Cha nne wamchukizao hawataoa Wala kuoa wote watakuwa masingle mother maasingle father
 
Kwani kuna tamko au sheria yoyote imeainisha aina ya vitambulisho vinavyotambulika kitaifa in a priority order?)
Kama hakuna basi tatizo linaanzia hapo.
Lakini pia nilishangaa Kuna kindi waziri Simbachawene alibishusha hadhi vibaya sana vitambulisho vya NIDA.
 
Sababu ni kuwa hakuna intergration kati ya Uhamiaji na hizo Ofisi.

Ofisi zote huchukua taarifa kutoka NIDA including Uhamiaji...

Afu usijipe umuhimu usio na lazima maana huwezi pata Passport bila kuwa na NIDA unless ni under 18
Si kweli
 
Passport ni hati inayotumika kumtambulisha mwenye hati kuwa ni mtanzania, pale anaposafiri nje ya nchi. Mtanzania awapo ndani ya nchi anapaswa kuwa na kitambulisho cha taifa pale anapohitaji kupata huduma tofauti na kusafiri.

Tangu zilipotoka passport hizi mpya, taarifa zilitolewa na idara ya uhamiaji kuwa passport za kuafiria za Tanzania hazitatumika kama kitambulisho zaidi ya kitambulisho cha taifa. Ofisi ulizotembelea ziko sahihi kabisa kukugomea maana kitambulisho cha taifa ndio kinachotumika ndani ya Tanzania na sio pasi ya kusafiria.

N.B. Naamini watalaam wa Idara ya uhamiaji watakuja kutoa somo humu kwa faida ya jukwaa hili.
Acha ushamba.

Passport ni ID inayotambulika kitaifa na kimataifa.

Nida inatambulika kitaifa tu.
 
Nimekwenda ofisi kama tatu za watu binafsi nimeshindwa kupata huduma kwa kutumia kitambulisho cha passport eti hakitambuliki. Yaani kitabu hakitambuliki?

Ni kweli karne ya 22 kuna baadhi ya ofisi hazitambui kama passport ya kusafiria ni kitambulisho.

Wananiambia hicho hakitambuliki sisi hapa tunahitaji NIDA na kitambulisho cha MPIGA kura.

Kweli nimeshangaa nimejisemea hiki sasa ni nini. Nimetamani kuutangazia uma palepale kuitambua passport kama kitambulisho kwenye ofisi zote za serikali na binafsi.

Passport na NIDA kipi ni kitambulisho.

Uhamiaji tusaidieni ni kwanini passport haitumiki kama National Identification card baadhi ya ofisi.

Tanzania hatuna kitambulisho cha mpiga kura bali tunayo kadi ya mpiga kura
 
Sema wewe nae unapenda ubishoo tu watu wajue na wewe unapassport. Ulishindwa nini kwenda na NIDA sababu lazima unayo.

Umenikumbusha miaka flani nyuma tuliitwa kwenye interview na taasisi flani hapa hapa bongo. Kuna sister mmoja alikuja na passport ya miaka miwili nyuma na hajawahi itumia hata kuingilia kenya. Ubishoo muache hasa nyinyi madada
 
Back
Top Bottom