Uhusiano uliopo kati ya wasukuma na wanyamwezi

Uhusiano uliopo kati ya wasukuma na wanyamwezi

Acha kukariri stori za wanafiki wachache waliopotosha ukweli. Angalia hata uhusiano wa hizi jamii Bantu, Nubian na wasukuma; nani yukokaribu zaidi na wasukuma katika lugha za asili-mbantu au mnairoti?
We ndo umekariri nitakupa mfano mmoja Wahima/Ankole wanafuga ng'ombe wenye mapembe na Usukumani ndo wanapatikana kwa wingi. Kuna kitu kinaitwa "evolution" so usishangae. Tatizo tafiti nyingi zimefanywa na wazungu kabla ya baadhi ya makabila kujitambua kuandika historia zao wenyewe na hii bado changamoto kubwa.
 
Habari zenu wanajukwaa ninaomba kufahamishwa vizuri juu ya haya makabila makubwa mawili ya Tanzania wasukuma na wanyamwezi yanauhusiano gani kihistoria , nawasilisha .
Kama wamasai na waarusha, wabarbaig na wairaq, wachaga na wapare, warangi na wanyanturu nk nk
 
We ndo umekariri nitakupa mfano mmoja Wahima/Ankole wanafuga ng'ombe kwenye mapembe na Usukumani ndo wanapatikana kwa wingi. Kuna kitu kinaitwa "evolution" so usishangae. Tatizo tafiti nyingi zimefanywa na wazungu kabla ya baadhi ya makabila kujitambua kuandika historia yao wenyewe na hii bado changamoto kubwa.[/QUOTE]

Nashauri kwa suala zima la LUGHA za Tanzania, soma ATLASI YA LUGHA ZA TANZANIA (2009), kilichochapishwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Ni matokeo ya utafiti uliofanywa na Wataalamu wa KITANZANIA!
 
Nashauri kwa suala zima la LUGHA za Tanzania, soma ATLASI YA LUGHA ZA TANZANIA (2009), kilichochapishwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Ni matokeo ya utafiti uliofanywa na Wataalamu wa KITANZANIA!
Elewa mtu anaposema kwamba "bado changamoto".
 
Elewa mtu anaposema kwamba "bado changamoto".
Nimekuelewa vema Ndugu yangu. Changamoto hiyo/hizo zinapatiwa ufumbuzi na Tafiti Mpya na zinazofanywa na wananchi wenyewe! Bado nashauri, tena kwa dhati kabisa, ISOME hii Atlasi ya Lugha za Tanzania.
 
Nimekuelewa vema Ndugu yangu. Changamoto hiyo/hizo zinapatiwa ufumbuzi na Tafiti Mpya na zinazofanywa na wananchi wenyewe! Bado nashauri, tena kwa dhati kabisa, ISOME hii Atlasi ya Lugha za Tanzania.
Funguka na kuwa muwazi tu
 
Unachosema kinaweza kuwa sahihi kwa sababu kuna watu wako maeneo fulani hawajielewi kama ni wasukuma, wadakama, wanyamwezi au ntuzu people hii inatokana na wao kujiita kabila fulani wakati majirani zao wakiwaita na kuwatambua tofauti. Kwa mfano msukuma wa Shinyanga mjini akienda Bariadi ataitwa mdakama/mnyamwezi hali yeye anajiita msukuma. Uyu huyu wa Shinyanga mjini anamwita mwenzake wa kahama mnamweli hali watu wa kahama wakijua mnamweli ni yule wa magharibi ya Kahama yaani Lunzewe, Ushirombo na viunga vyake.
Hii inatokana na pande kuu za dunia kama nilivyosema awali na "magharibi yako wewe ina magharibi yake pia" hivyo aliye magharibi yako utamwita mnamweli wakati huyu unayemwita mnamweli anakataa kwa sababu yeye anachojua mnamweli ni yule aliye magharibi yake zaidi.
Wasukuma raha jamani a nice tribe itz. kuanzia Mwanza, Shinyanga, Tabora, Geita, na hata kwa wajukuu zetu akina mbwane, mihanyanyi ni uroda mtupu.
Yaani kwa ufupi ni kuwa, Mnyamwezi na Msukuma ni jamii moja tu. Tofauti ya ndimi inatokana na upande walipo. Mimi nilibahatika kukaa kwenye mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu, nikagundua kuwa jamii zote hizi hazina tofauti
 
Wengi humu nimeona mnasema wasukuma wametokana na wanyamwezi.

Swali: Je ni kwa nini wasukuma wapo wengi kuliko wanyamezi.?
 
Wengi humu nimeona mnasema wasukuma wametokana na wanyamwezi.

Swali: Je ni kwa nini wasukuma wapo wengi kuliko wanyamezi.?
Mimi sikubaliani na hili la kusema wasukuma wametokana na wanyamwezi bila kujali wingi wa wasukuma au uchache wa wanyamwezi.
 
Yaani kwa ufupi ni kuwa, Mnyamwezi na Msukuma ni jamii moja tu. Tofauti ya ndimi inatokana na upande walipo. Mimi nilibahatika kukaa kwenye mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu, nikagundua kuwa jamii zote hizi hazina tofauti
Sikukatalii lakini sisi tunajuana tena vizuri sana iwe kwa matamshi au tofauti ya baadhi ya maneno. Pia kama umepitia argument zangu humu nimelizungumzia sana hili la pande ambazo zinatugawanya: mashariki, kaskazini, magharibi na hata kusini kwa ndugu zetu (wanyamwezi).
 
Origin yao ni moja toka huko west Africa, walipofika pwani ya Afrika Mashariki walitapakaa maeneo ya kaskazini magharibi mwa Tanganyika(Kwasasa Mwanza,Shinyanga,Simiyu,Geita na Tabora). Jamii hii ilikuwa ni ya wafugaji kama shughuli kubwa ya uchumi lakini pia miongoni mwao walikuwepo wakulima. Nyamwezi empire chini ya mtemi Milambo na wenzake waliomtangulia ndiyo iliyokuja kutenganisha wasukuma na wanyamwezi kwa maana ya waliokuwa chini ya himaya ya Milambo walikuwa wanyamwezi.

Hivyo ndiyo nilivyosimuliwa na marehemu babu yangu.

Mwisho na declare interest kuwa mimi ni Mnyamwezi.

Eeeh kaka wamilemoo. ...wangaluka iiigh bamishakola kaka..... nahenee kaka Ngosha.
 
Mkuu kifupi kabila la wanyamwezi ni watu waliotoka magharibi mwa afrika,Niger-Congo,kabila mama ni Wanyamwezi,wasukuma ni tabaka lilikotoka kwenye kabila kubwa la wanyamwezi.Katika kabila kubwa la wanyamwezi kuna mashina(makabila matano) yametoka humo,na yanafanana kitabia,asili,lugha,desturi nk.Mashina hayo ni kabila la Wanyamwezi,wakonongo,wakimbu,wasumbwa na wasukuma.Wanyamwezi walipotoka magharibi mwa afrika waliweka makazi Tabora kabla ya kuanza kusambaa kuelekea kaskazini magharibi(ukanda wa ziwa).Hivyo mpaka sasa Tanzania kabila linaloongoza kuwa na watu wengi ni Wasukuma,wakifuatiwa na kabila la pili kwa ukubwa ni wanyamwezi.Makabila haya kwa kifupi yanaongoza kwa kuchapa kazi na ukarimu..ndio maana toka Enzi wanasema 'mzigo mzito mpe mnyamwezi',na hata marekani(ambayo inasifika kwa watu wake ukarimu wa kusaidia watu wengine inaitwa 'unyamwezini',hela yao ya dola inaitwa 'mnyamwezi', au mtu akiwa anamzungumzia rafiki yake wa ukweli utasikia akisema 'mnyamwezi wangu'. Lakini pia ndio makabila yanaongoza kwa ushujaa na mapambano,ndio maana machifu wao ni maarufu zaidi kuliko wa makabila mengine kama chifu mirambo na jeshi lake la wavuta bangi 'maarufu kama warugaruga',chifu Isike,chifu Mihayo,chifu Fundikira nk. Makabila haya yanasifika kwa kilimo na ufugaji,pia kwa ukarimu wa hali ya juu hususani wasukuma.Hakuna kabila wakarimu kama wasukuma,labda ndio maana Mungu nae amewazidishia katika ardhi yao kuna kila aina ya neema,chakula cha kutosha,masamaki,madhahabu,mapamba,mang'ombe,maasali,mahela... nk. Ila pia hawako nyuma kwenye uchawi na mizimu hasa kama umewaonea au umewaibia.Inawezekana ni mauchawi waliyotoka nayo huko afrika magharibi na njiani walipopitia congo kuingia Tanzania.So take care
Kwakweli tumetisha
 
Hapa ndo mtu anatakiwa aelewe kabila la wasukuma ni kubwa kuliko mtu anavyoweza dhania na lina vijikabila vingi sana ndani yake ambavyo vina tabia za kwake tu tofauti na zile za wasukuma wanaopigiwa chapuo kila siku.
Kwa mfano ni hawa wanyantuzu huwezi wafananisha na wasukuma licha ya kupatikana kanda ile ile na hata kutokufautiana sana katika lugha (kisukuma). Wanyantuzi katika case ya mapenzi ni wafanyabiashara sawa na biashara zingine tu. Mnyantuzu akiona maisha yamempiga yuko ladhi kuhamia dakama (kusini kwa wanyamwezi/wadakama) na mkewe na akifika huko kila mmoja kivyake japokuwa mawasiliano ni kama kawaida. Ataishi huko huku mkewe akijilengesha kwa wanaume wamtongoze na hakatai, ole wako umtongoze atakubali fasta na kukukaribisha kwake ukalale. Ile unaingia tu na kuvua nguo zote mmewe anaibuka na watu wake wanakukamata ugoni na mke akihojiwa anakiri kulala na wewe hapo unagongwa faini ya nguvu ya ng'ombe lukuki. Ukishatoa tu ng'ombe jamaa anarudi kwao na mifugo "okwabha ushinhu".
Vile vile kwa asili ni wagawaji wazuri tu kama wahaya.
NB. Wasukuma original hawako kama wanyantuzu na wako poa sana katika mahusiano, ni wapole na wakarimu sijawahi ona katika nchi hii.

Asante kwa kuwadadavua vizuri, nimedaka pointi hapo.
 
Mimi Msukuma Original ndiye baba yenu nyie Wanyamwezi!!

Duuh....

Fuata historia bana ote dugu moja bana.....
Sawa na mtu na binamu yake hawanyimani wala hawadhuriani maana ni nyama ya hamu looh.
 
Wote ni wamoja sema kuwa scattered ndo yakazuka haya matabaka!
Atakachoongea mnyamwezi na msukumu ni 99.99 equal. Tamaduni na mila ni zilezile...
Au kwa maana nyingine hakuna kabila la wasukuma bali wote ni wanyamwezi isipokuwa wao hujibagua wa dakama(tabora-nyamwezi), wa sukuma, wa ng'hweli, wa kiya etc etc
Watakuja wengine kukuelewesha hapa..
Ni wale wale ila wanawake wa kinyamwezi kwa kuzungusha buno hadi utasema bhashi.
 
Sikukatalii lakini sisi tunajuana tena vizuri sana iwe kwa matamshi au tofauti ya baadhi ya maneno. Pia kama umepitia argument zangu humu nimelizungumzia sana hili la pande ambazo zinatugawanya: mashariki, kaskazini, magharibi na hata kusini kwa ndugu zetu (wanyamwezi).
Mkuu ulikuwa kitengo gani hapo Bulyanhulu?
 
Nimeona watu wengi wameelezea wasukuma na wanyamwezi hapa na makabila yanayoambatana nayo.
Kuua mziki wa fitina wale wenzangu na mie eanyamwezi na binamu zetu wasukuma na viunga vyake tuanze kuongea kisukuma na kinyamwezi ili tuwahakikishie kuwa makabila haya makuu tunasikilizana au hata lugha zetu ni tofauti.

Haya mwendo kasi.... tuanze....

Wangaluka wosee, mlimhola?
 
Back
Top Bottom