Ujinga ni tatizo kuu hapa Tanzania

Ujinga ni tatizo kuu hapa Tanzania

Acha kutusumbua hapa! Ingia hata YouTube uone hali ya China ilivyokuwa kabla ya mabadiliko ya Sera aliyofanya Den Xiapoing. Kwa kifupi ilikuwa hohehahe
Wewe utakuwa ni mpuuzi sana. Ninaijua vyema sana hali iliyokuwa nayo Marekani siyo miaka mingi iliyopita. Nimeishuhudia mwenyewe, sikuambiwa kama unavyofanya hapa.

Na bado najua utakuwa huelewi ninacholenga katika kukujibu hivi.

Kila ukiandika unazidi kujionyesha ni kiasi gani ulivyo mtupu kabisa.
 
Umezaliwa mwaka gani kwanza! Maana hapa tunaweza tukawa tunabishana na toto la mwaka 2000 ambalo halijui hata kipindi nchi yetu ilipita stage ya kufunga mkanda
Sina tena lolote la maana ninaloweza kutumaini kulisikia/kulisoma toka kwako.
 
Kuna wakati unaweza kujiuliza hivi ni kweli watu wote wanaopinga uwekezaji wa DP wameusoma mkataba wa makubaliano? Jibu ni jepesi sana, asilimia kubwa ya wanaopinga huenda hawausoma hata huo mkataba. Lakini kwanini watu wapinge tu hata bila kujua vizuri kilichopo kwenye mkataba? Jibu ni jepesi sana, historia ya mikata ya nyuma imewafundisha. Kama mikataba kama ya gas na kupitishwa kwa hati ya dharura Nini ilikuwa hatma yake, nenda kwenye migodi, turudi kwenye Reli na Muhindi, viwanda na wawekezaji tuliona viwanda vikifa. Hayo ndio yamewafanya ht wasiosoma mkata huo kujikuta wanaupinga tu.
 
Raisi wako amesema Serikali haifanyi Biashara hivyo mashirika yetu kuuzwa kwa state run foreign Governments, hiyo ndiyo irony yenyewe, Mashirika makubwa ya karibia nchi zote yako controlled na States na hii ni Dunia nzima, kwetu yanagawiwa kwa foreigners …
Kuingia ubia na uwekezaji sio kuuza.
 
Enzi za Mao, China ilikuwa nchi ya kikomunisisti iliyoamini katika Sera za Ukomunisti.

Pamoja na Ukomunisti wa China, Rais wa kwanza wa China, Mao aliamini kuwa ni lazima apeleke vijana nje ya China wakajifunze Dunia inaendaje na ikoje ili warudi kufanya mabadiliko China.

Moja ya vijana hao alikuwepo Den Xiapoing ambaye alikuja kuwa Rais wa China baada ya Mao. Den alipelekwa Ulaya na akajifunza sana namna uchumi wa Ulaya ulivyokuwa unaenda.

Alipokuja kurudi China, Den alianzisha mfumo wa Private Property na Uwekezaji wa Sekta binafsi katika mfumo wa Uchumi wa China. Kipindi chake ndo makampuni mengi ya Marekani yalienda kufungua viwanda na kufanya uwekezaji China.

Kwa wachina wengi walimuona Deng ni msaliti wa Mao kwa kuwa wengi walikuwa wanaamini kila kitu ni cha wachina na mwekezaji kutoka nje ni mwizi. Den aliwajibu haijalishi kama paka ni mweupe au ni mweusi ili mradi anakamata panya basi huyo anatufaa

Pamoja na wachina kupata shida kuelewa Sera za Den Xiapoing ila leo ndo wachina wanamsujudu kama The Father of Modern China.

Ukiacha China kuna nchi za Singapore na Umoja wa Falme za Kiarabu ambao Dubai ni nchi mojawapo za umoja huo.

Hizi nchi nazo miaka ya 1960 ilikuwa kama sisi! Ila watawala wao walipata akili kuwa kwa akili za kuwaza sisi ndo sisi hatutafika popote. Kupitia rasilimali ya mafuta Dubai walibadilisha Sera zao kuhamasisha uwekezaji wa sekta binafsi. Leo hii kila mtu Duniani anakwenda kutalii Dubai na si kwa sababu ya mafuta tu ila kutokana na namna ikivyojengwa , inavyopendeza na ilivyo na uchumi mkubwa na maendeleo makubwa.

Ukija Tanzania. Hapa ndo shida ilipo. Nchi hii ilianzishwa katika misingi ya kijamaa. Misingi hii iliwaaminisha watu kuwa kila kitu ni Serikali na Serikali ni kila kitu. Mfumo huu ambao unaamini katika state capture umedumaza akili za Watanzania wengi sana kiasi ambacho kuna Watanzania leo hawajifunzi hata dunia ikoje, inaenda wapi na itakuwa wapi miaka hata 50 mbele.

Akili hizi zinaamini kuwa Sera ya uwekezaji ni kuuza nchi, Uwekezaji ni uuzaji wa nchi. Sera hii imewafanya Watanzania kuwa nyuma sana. Nchi yetu kuwa nyuma sana, mifumo yetu ya huduma kuwa nyuma sana.

Leo hii Tanzania, unatoka Dar hadi Kigoma kwa masaa zaidi ya 15 kwenye treni ambayo muda wowote unaweza kuambiwa leo hakuna usafiri. Ndani ya hiyo treni vyoo vichafu, huduma ni mbovu ila mtanzania hana shida ili mradi tu inamilikiwa na Serikali

Leo hii nchi yetu ina bandari zinayoweza kuhudumia ipasavyo nchi hadi 8 zinazotuzunguka, ila meli zinakaa wiki 2 hadi 3 kushusha mizigo, wafanyabiashara wanapoteza mizigo yao, hakuna mapato makubwa nchi inaweza kupata na kufanya maendeleo makubwa ila watu wanaona sawa tu ili mradi iwe chini ya Serikali. Hawajali hata wakiambiwa meli zinakimbia zinaenda Bandari za nchi jirani ili mradi waone au wasikie Serikali ndo mmiliki. Huu ni ujinga uliotukuka sana.

Kibaya zaidi pamoja na ujinga huu wa Watanzania, nchi jirani zinazotuzunguka zinakimbia sana ili kukamata fursa za kiuchumi sisi tusiwe na kitu. Rwanda amejenga Bandari kavu kubwa sana ili mizigo ya Congo Mashariki ipite kwake . Bandari hii kawapa wawekezaji. Sasa Rwanda anajenga uwanja wa Ndege mkubwa zaidi Afrika Mashariki ambao utaendeshwa pia na Sekta binafsi.

Huku Kenya amejenga Bandari ya Lamu ambayo ataiendesha kwa sehemu kubwa kupitia sekta binafsi, Msumbiji kaomba vikosi vya Rwanda vilinde Bandari zake ili wawekezaji waweze kuwekeza na zifanye biashara. Hawa wakifanya haya Serikali ikichukua hatua kuboresha utendaji wa Bandari kuna watu wanaaza kusema nchi inauzwa.

Serikali ikiwasikiliiza hawa watu kuna hatari kubwa sana huko mbeleni nchi yetu kuja kuwa kituko cha mwisho zaidi kuliko hata sasa, kutokana na kusikiliza wajinga huku nchi ikitakuwa ikimbie iendane na mabadiliko ya Dunia ya sasa.

Kwa Dunia inavyokwenda sasa, Tanzania haipaswi kurudi nyuma tena! Ujinga usipewe tena nafasi Tanzania!
Wanaopiga makelele humu JF wengi wao hawajawahi hata kuitoa vespa pale bandarini wakajua ni milolongo ipi iliyopo kikazi.

Wengi ni makasuku wa wenye pesa zao, baadhi wanapewa pesa na wapigaji wa bandari waliozoea maisha ya ubwete ya kupata pesa chafu za mifumo isiyo rasmi.

Serikali ina mkono mrefu, na ikitaka kufanikisha jambo inaloona lina manufaa kwa taifa na itafanikisha tu iwe jua iwe mvua.

Tuna fukwe yenye urefu kilomita 1420, Kenya wanaionea wivu siku zote. Rais Kagame alisema wazi kabisa kwamba akipewa bandari ya Dar hii nchi inakwenda kuwa ya uchumi wa kiwango cha juu.

Samia kaamua kutembelea hoja kama hizi za kina Kagame za kunufaika na rasilimali tuliyopewa na Mungu, hawa wanaopiga hizi kelele upo mwisho wao unakuja.
 
Raisi wako amesema Serikali haifanyi Biashara hivyo mashirika yetu kuuzwa kwa state run foreign Governments, hiyo ndiyo irony yenyewe, Mashirika makubwa ya karibia nchi zote yako controlled na States na hii ni Dunia nzima, kwetu yanagawiwa kwa foreigners …
Kuwa controlled na state ndio kumeonyesha kila aina ya udhaifu wa uendeshaji.

Ufisadi na uzembe unaowapa wafanyakazi ile jeuri ya kujua kuwa wanafanyia kazi serikali yao hivyo hakuna baya litakalowakumba.
 
Issue sio umiliki wa serikali issue ni ufanisi, tatizo la serikali zetu hazina ufanisi kabisa embu niambie taasisi Gani ya serikali yetu Ina ufanisi? Zote zimeoza Sasa why ulazimishe tu umiliki wa serikali hata kama hakuna ufanisi?

TTCL na Vodacom ni mbingu na ardhi, ATCL na Precision ni mbingu na ardhi, kiufupi hakuna government entity inaizidi private sector kwa ufanisi. Hata kampuni kama Deloitte na PWC zinaizidi ufanisi TRA na NAO kwenye ukaguzi.

Nadhani mfumo wa uendeshaji taasisi za serikali ubadilike, ziwe za mikataba zenye KPI otherwise hawa mafisadi hawana uchungu na chochote sababu bandari iingize hasara au faida hawana Cha kupoteza na mishahara ipo pale pale.
Hilo suala la mishahara yao kuwa pale pale licha ya uvivu wao kazini na wizi wa mali ya umma ndio kichaka cha hawa wengi wanaopinga uwekezaji wa DP.

Wanakuja na sera za kijamaa za kumkumbuka Nyerere wakitaka kazi ifanyike kimazoea pale bandarini, hakuna atakaye kubaliana na upuuzi huo. Wanaletewa mwekezaji mpya mwenye teknolojia za kisasa na kama hawawezi kazi basi wapishe wengine.

Tusifuge umaskini kwa kigezo cha kukimbilia uzalendo na utaifa wetu. Sera za ujamaa za miaka iliyopita zisiendelee kutumika kutetea status quo pale TPA, ni muda wa mabadiliko kuwakumbuka wote wanaofanya kazi kimazoea.
 
Mkuu hata china na Hong Kong mbona Kuna bandari na terminal zipo chini ya Dp World.

Nadhani mjadala uwe mkataba uwe rafiki ila kubinafsisha hakukwepeki maana tumefeli kwa miaka 60. Hata JPM na ukali wote ule alishindwa bandari unadhani nani kwa serikali hii ataweza?

Mfano tu NIDA nmejisajili miaka 5 Sasa Sina NIDA mpaka Leo, hivi wakisema vitambulisho vichapwe na kampuni ya kizungu mtapinga? Tumeshindwa acha tusaidiwe maana hatuwezi.
Ukiona kila kitu tunashundwa maana yake ofis kuu ndo inashindwa ,na haina haja ya kwepo hapo juu
 
Watu kama wale uwezi kuwaelimisha tena; huko serikalini inatakiwa waseme inatosha. Ni muda wa kufunga huo ukurasa, wengi washaelewa inatosha, waliobaki awataki kuelewa.
Kila kitu kina muda wake, na hiyo kesi waliyofungua hao mawakili inakwenda kutupiliwa mbali huko mahakamani.

Huyo Mwabukusi awe mwangalifu sana na mwenendo wake, yanaweza kumkuta yale yale yaliyomkuta Ulimboka miaka ile ya JK.
 
Haya ndiyo mambo ya upotoshaji mnaotumia kuwafunga macho watu wasiokuwa na uelewa wa mambo.

1. Nani anahoji uwekezaji kwenye bandari kuongeza ufanisi? Kwa nini mnakimbilia huko badala ya kujadili masharti yanayohusiana na uwekezaji huo?
Hizo bandari za Marekani nao waliingia mikataba mibovu kama tunayotarajia sisi kuiingia?
Mazingira ya Marekani ni sawa na haya ya kwetu? Marekani wanazo bandari ngapi?

Hawa DPWorld ujuzi huu wao waliuokota wapi, au uliwashukia tu toka peponi?
Kwa hiyo nasi inatubidi tusubiri hadi hapo tutakaposhukiwa ndipo tuanze kujitutumua kuanza kufanya mambo yetu?
Hiyo itakuwa lini, na kama hao hao DPWorld wanataka tuwategemee wao milele!

Inakuwa mbaya zaidi, viongozi wanaposahau kabisa kushughulikia maswala ya kujenga uwezo wa wananchi wao, na badala yake wanakuwa watu wa kutembeza bakuli kutafuta wawekezaji hata katika mambo tunayoweza kuyamudu wenyewe.

Kwani hapa hatuna sekta binafsi. Wakulima wetu, siyo sektA BINAFSI HADI MTU ATOKE NJE? hUU NAO UTAUITA "uJAMAA"?

2. Hilo la Ujamaa, elewa tu kwamba hakuna nchi yoyote isiyokuwa na ujamaa.
Hii kasumba ya kukariri vitabuni na kuacha kuelewa hali halisi ni tatizo kabisa. Achana na mambo ya Ubepari/Usocialist, hakuna mahali popote mfumo mmoja ndio unaoendesha maisha ya nchi.

Ubepari ulishakufanyia kitu gani wewe binafsi?
Umeongea vitu vya msingi sana .sasa mtu kama samia anakula bure anavaa bure .anakula bure kwa kodi zetu , lakini kamwe hawwzi kuumiza kichwa kutatua hayo mambo yeye anapenda vitu virahisi sana
 
Kuna wakati unaweza kujiuliza hivi ni kweli watu wote wanaopinga uwekezaji wa DP wameusoma mkataba wa makubaliano? Jibu ni jepesi sana, asilimia kubwa ya wanaopinga huenda hawausoma hata huo mkataba. Lakini kwanini watu wapinge tu hata bila kujua vizuri kilichopo kwenye mkataba? Jibu ni jepesi sana, historia ya mikata ya nyuma imewafundisha. Kama mikataba kama ya gas na kupitishwa kwa hati ya dharura Nini ilikuwa hatma yake, nenda kwenye migodi, turudi kwenye Reli na Muhindi, viwanda na wawekezaji tuliona viwanda vikifa. Hayo ndio yamewafanya ht wasiosoma mkata huo kujikuta wanaupinga tu.
Saa100 hata sikumoja hatakaa aingie mkataba wenye maslahi kwetu ,kwa kuwa ni raisi mvivu kuumiza kichwaa chake ,yeye bora liende
 
Usilinganishe uwekezaji wa china na Tanzania. Unajua athari za devaluation kwenye uwekezaji unaofanyika Nchini? Hatunufaiki na uwekezaji ambao dola chache zinawekezwa kuvuna midola mingi kwa wageni huku sisi tunapata pesa kidogo ya kidogo kisa devaluation. Kama tunataka win win wasiwekeze kwa fedha zetu. Waajiri watanzania , walipe Kodi kwa dola, walipe waajiriwa wao kwa dola. Kuna migodi mingi Dhahabu zinabebwa na ndege usiku. Lakini watu wanapiga Cha juu. Mifumo ya uwekezaji kwetu haitulipi kama Nchi. Ni vizuri tuwe na mifumo dhabiti ambayo haitaruhusu ndege kupaa mgodini moja kwa moja kwenda nje. Ukaguzi uwe wakutosha na charging zifanyike kuhakikisha sent ya mtanzania inabaki.
 
Hilo suala la mishahara yao kuwa pale pale licha ya uvivu wao kazini na wizi wa mali ya umma ndio kichaka cha hawa wengi wanaopinga uwekezaji wa DP.

Wanakuja na sera za kijamaa za kumkumbuka Nyerere wakitaka kazi ifanyike kimazoea pale bandarini, hakuna atakaye kubaliana na upuuzi huo. Wanaletewa mwekezaji mpya mwenye teknolojia za kisasa na kama hawawezi kazi basi wapishe wengine.

Tusifuge umaskini kwa kigezo cha kukimbilia uzalendo na utaifa wetu. Sera za ujamaa za miaka iliyopita zisiendelee kutumika kutetea status quo pale TPA, ni muda wa mabadiliko kuwakumbuka wote wanaofanya kazi kimazoea.
Kanywe uji kwanza.
Sera za kijamaa ndizo sera gani hizo?
Nitajie sera mbili tu za Kijamaa Tanzania Ati za kumkumbuka Nyerere...toa peleka Upotoshaji wako sehemu nyingine.
 
Enzi za Mao, China ilikuwa nchi ya kikomunisisti iliyoamini katika Sera za Ukomunisti.

Pamoja na Ukomunisti wa China, Rais wa kwanza wa China, Mao aliamini kuwa ni lazima apeleke vijana nje ya China wakajifunze Dunia inaendaje na ikoje ili warudi kufanya mabadiliko China.

Moja ya vijana hao alikuwepo Den Xiapoing ambaye alikuja kuwa Rais wa China baada ya Mao. Den alipelekwa Ulaya na akajifunza sana namna uchumi wa Ulaya ulivyokuwa unaenda.

Alipokuja kurudi China, Den alianzisha mfumo wa Private Property na Uwekezaji wa Sekta binafsi katika mfumo wa Uchumi wa China. Kipindi chake ndo makampuni mengi ya Marekani yalienda kufungua viwanda na kufanya uwekezaji China.

Kwa wachina wengi walimuona Deng ni msaliti wa Mao kwa kuwa wengi walikuwa wanaamini kila kitu ni cha wachina na mwekezaji kutoka nje ni mwizi. Den aliwajibu haijalishi kama paka ni mweupe au ni mweusi ili mradi anakamata panya basi huyo anatufaa

Pamoja na wachina kupata shida kuelewa Sera za Den Xiapoing ila leo ndo wachina wanamsujudu kama The Father of Modern China.

Ukiacha China kuna nchi za Singapore na Umoja wa Falme za Kiarabu ambao Dubai ni nchi mojawapo za umoja huo.

Hizi nchi nazo miaka ya 1960 ilikuwa kama sisi! Ila watawala wao walipata akili kuwa kwa akili za kuwaza sisi ndo sisi hatutafika popote. Kupitia rasilimali ya mafuta Dubai walibadilisha Sera zao kuhamasisha uwekezaji wa sekta binafsi. Leo hii kila mtu Duniani anakwenda kutalii Dubai na si kwa sababu ya mafuta tu ila kutokana na namna ikivyojengwa , inavyopendeza na ilivyo na uchumi mkubwa na maendeleo makubwa.

Ukija Tanzania. Hapa ndo shida ilipo. Nchi hii ilianzishwa katika misingi ya kijamaa. Misingi hii iliwaaminisha watu kuwa kila kitu ni Serikali na Serikali ni kila kitu. Mfumo huu ambao unaamini katika state capture umedumaza akili za Watanzania wengi sana kiasi ambacho kuna Watanzania leo hawajifunzi hata dunia ikoje, inaenda wapi na itakuwa wapi miaka hata 50 mbele.

Akili hizi zinaamini kuwa Sera ya uwekezaji ni kuuza nchi, Uwekezaji ni uuzaji wa nchi. Sera hii imewafanya Watanzania kuwa nyuma sana. Nchi yetu kuwa nyuma sana, mifumo yetu ya huduma kuwa nyuma sana.

Leo hii Tanzania, unatoka Dar hadi Kigoma kwa masaa zaidi ya 15 kwenye treni ambayo muda wowote unaweza kuambiwa leo hakuna usafiri. Ndani ya hiyo treni vyoo vichafu, huduma ni mbovu ila mtanzania hana shida ili mradi tu inamilikiwa na Serikali

Leo hii nchi yetu ina bandari zinayoweza kuhudumia ipasavyo nchi hadi 8 zinazotuzunguka, ila meli zinakaa wiki 2 hadi 3 kushusha mizigo, wafanyabiashara wanapoteza mizigo yao, hakuna mapato makubwa nchi inaweza kupata na kufanya maendeleo makubwa ila watu wanaona sawa tu ili mradi iwe chini ya Serikali. Hawajali hata wakiambiwa meli zinakimbia zinaenda Bandari za nchi jirani ili mradi waone au wasikie Serikali ndo mmiliki. Huu ni ujinga uliotukuka sana.

Kibaya zaidi pamoja na ujinga huu wa Watanzania, nchi jirani zinazotuzunguka zinakimbia sana ili kukamata fursa za kiuchumi sisi tusiwe na kitu. Rwanda amejenga Bandari kavu kubwa sana ili mizigo ya Congo Mashariki ipite kwake . Bandari hii kawapa wawekezaji. Sasa Rwanda anajenga uwanja wa Ndege mkubwa zaidi Afrika Mashariki ambao utaendeshwa pia na Sekta binafsi.

Huku Kenya amejenga Bandari ya Lamu ambayo ataiendesha kwa sehemu kubwa kupitia sekta binafsi, Msumbiji kaomba vikosi vya Rwanda vilinde Bandari zake ili wawekezaji waweze kuwekeza na zifanye biashara. Hawa wakifanya haya Serikali ikichukua hatua kuboresha utendaji wa Bandari kuna watu wanaaza kusema nchi inauzwa.

Serikali ikiwasikiliiza hawa watu kuna hatari kubwa sana huko mbeleni nchi yetu kuja kuwa kituko cha mwisho zaidi kuliko hata sasa, kutokana na kusikiliza wajinga huku nchi ikitakuwa ikimbie iendane na mabadiliko ya Dunia ya sasa.

Kwa Dunia inavyokwenda sasa, Tanzania haipaswi kurudi nyuma tena! Ujinga usipewe tena nafasi Tanzania!
Hatujakataa wawekezaji tunakataa aina ya mkataba yaani haueleweki.
Mbaya zaidi mama anawapa wajomba zake urithi wa bara.
 
Kuna kitu muhimu katika uzi wako umekiacha tena kwa makusudi.

China hawakukaribisha Wawekezaji tu bila kuangalia Maslahi yao. Kitu cha kwanza walisomesha vijana wao na kwa hiyo Wawekezaji walipoenda China kulikuwa na sharti la kuajiri vijana wao. Vijana walioajiriwa walipopata mitaji wakaanzisha viwanda vidogo vidogo vya vipuri na ikawa progressive mpaka kuweza kutengeneza mitambo mikubwa. Na Serikali Ilikuwa inadhaibiti kwa manufaa ya Wananchi wake

Kwa hiyo China walikaribisha Wawekezaji wakiwa na nia ya kupata mtaji, ujuzi, exposure na teknolojia na matokeo yake China kwa sasa Wamewapita Sana Hao Wawekezaji na Wanashindana nao huko Duniani kwa mauzo ya bidhaa na huduma.

Kuhusu Falme za Kiarabu nayo iko hivyo, pamoja na Biashara ya Mafuta, Wawekezaji wote wa kigeni lazima wawe na Washirika wazawa hata kama hao wazawa hawana mitaji inabidi wapewe hisa za mkopo. Hali hiyo imepelekea Nchi hizo kushamiri kiuchumi.

Haya sasa Njoo kwenye nchi yetu. Ni mkakati gani umewekwa wa kufanya Uwekezaji wa Wageni kumnufaisha Mtanzania mmoja mmoja au Taifa kwa ujumla wake?
Wamechukuana na Kina kitenge wakaenda DUBAI alafu wakarudi hela zimejaa mifukoni then siri ikavuja ya mkataba wanatulazimisha tuwaelewe.
 
Back
Top Bottom