Ujue uchaguzi wa Marekani (USA) na jinsi rais wake anavyochaguliwa

Ujue uchaguzi wa Marekani (USA) na jinsi rais wake anavyochaguliwa

Narudia kuandika hapa, State popular votes (ambayo ndio msingi wa kumpata rais wa USA) ni tofauti kabisa general popular votes (ambayo haitumiki kabisa kumpata rais wa USA). Mara zote general popular votes hutumika kuchambua umaarufu wa mgombea kiujumla jumla mbele ya wamarekani wote kuliko kuelezea ushindi katika uchaguzi wa USA. Wagombea na vyama vyote wanalijua sana hilo, na wakati wote hulizingatia sana katika kampeni zao. Kushinda urais wa USA kunahitaji hesabu za kisayansi katika siasa za kidemokrasia na wala sio umaarufu wa kiujumla jumla wa kisiasa.
Umeamua kung'ang'ana na usichokijua muda si mrefu utaumbuka hongera lakini kwa kuonyesha msimamo wa kusimamia kile usichojua
 
Nadhani mleta mada kuna nanna haufahamu uchaguzi wa USA kiuhalisia, ni kama umekaririshwa fulani au ameandika kinadharia mnoo hata kama alichokiandika kuna chembechembe za ukweli.

Kwa kifupi sana, mfumo wa uchaguzi wa USA kumpata raisi wake huamuliwa na wamerekani wenyewe kwa wingi wao na wala sio kweli kuwa mshindi huamuliwa na wajumbe wa Electoral college! Ukishinda Popular votes katika majimbo mengi na muhimu zaidi basi wewe tayari ni mshindi. Kura za wajumbe wa Electoral college ni hitimisho la mchakato wa kura za Popular vote za kila jimbo. Kwanini nasema hivyo, waza haya.

1. Uchaguzi wa USA rasmi (ambapo Popular votes hupigwa) utafanyika siku ya jumanne (5/November) na katika hali ya kawaida kufikia jioni ya siku ya jumatano (6/November) tayari mshindi wa kiti cha urais wa USA atakuwa tayari amejulikana kwa kila mtu dunia nzima, wakati upigaji wa kura za wajumbe wa Electoral college zitakuja kufanyika wiki kadhaa huko baadaye. Kama wajumbe wa Electoral college (independently) huamia mshindi wa urais wa USA, kwanini mshindi ajulikane kabla ya kura zao kupigwa?

2. Hakuna mgombea yoyote wala chama chochote katika USA kinachoweza kupoteza hata dakika moja kuwafuata hao wajumbe wa Electoral college kikiomba kura zao. Yaani hakunaga kampeni za kuwashawishi hao wajumbe wa electoral college. Sio kwamba inakatazwa bali kimsingi hakuna mantiki ya kufanya hivyo.
Sasa Kama hao wajumbe ndio huamua nani awe rais, kwanini wagombea na vyama vyao wasitumie kila resource kuwashawishi hao wajumbe kuliko kutumia hizo resource kusaka popular votes ambazo 'haziamui' nani awe rais?


HITIMISHO LANGU.
Mchakato wa uchaguzi wa USA kumpata mshindi hauna tofauti yoyote ya kimsingi na chaguzi zingine za nchi nyingi za kidemokrasia ya moja kwa moja, tofauti chache zinazoelezwa zipo katika sayansi ya kutafsiri walio wengi ni kina nani au wamepatikanaje. Kwa mfano, katika uchaguzi wa Tz, mshindi wa kiti cha urais ni lazima apate zaidi ya 50% ya kura zote halali, na mshindi wa kiti cha ubunge au udiwani ni yule mwenye kura nyingi zaidi ya wagombea wengine (hata kama mshindi amepata chini ya 9% ya kura zote).
Kwa Tanzania umekosea, mshindi wa rais ni yule anayepata kura nyingi bila kujali amepata asilimia ngapi hii ni baada ya kipengele Cha asilimia 50+ kuondolewa
 
Lakini Electoral College imeshatoa Marais watano walioshindwa Popular vote wa karibuni wakiwa George Bush na Trump.
Kuna kitu hakjakiweka sawa katika maelezo yake ndio maana hata wewe umeingia wasiwasi ukauliza swali lako. Kwa ninavyofaham mimi raisi hupatikana kwa kura 270+ za delegates ambao yeye kawaita mabwanyenye. Lakini hizi kura hupatikanaje? Kila Jimbo la marekani Kati ya hayo 50 Lina Idadi ya delagates wake. Mgombea akishinda popular votes za Jimbo husika, anapewa kura zote za delegates kwa Idadi yao kwenye hilo jimbo. Na kwa sababu majimbo yanatofautiana winginwa delegates mgombea anaweza kushinda kwa gepu dog tu kwenye majimbo yenye delagates wengi na akashindwa mbali mno kwenye majimbo yenye delagates wachache kiasinkwamba ukijumlisha popular votes mgombea huyo anakuwa amepata kura nyingi lakini delegates wachache Hivyo anakuwa ameshindwa na mtu mwenye popular votes chache

Mfano majimbo A, B na C. Jimbo A linawapiga kura 13 na delegates 2, Jimbo B wapiga kura 20 delegates 3 na Jimbo C Lina wapiga kura 50 na delegates 6. Mgombea X akapata kura 11 za Jimbo A, kura 16 za Jimbo B na kura 23 za Jimbo C. Mgombea huyu atakuwa amepata popular vote 50. Wakati huo huo mgombea Y kapata kura 2 za Jimbo A, kura 4 za Jimbo B na kura 27 za Jimbo C, Hivyo atakuwa na jumla ya popular votes 33.

Kwa kigezo cha popular votes, mgombea X atakuwa na kura 50 wakati mgombea Y ana kura 33.

Tukirudi kwenye delagates, mgombea X kashinda majimbo A na B na Hivyo kujipatia Kura 2 za delegates wore wa Jimbo A na kapata kura zote 3 za delegates wa Jimbo B, Hivyo anakuwa na jumla ya kura 5 za mabwanyenye.

Kwa upande wa mgombea Y, kashinda Jimbo A na B hivyo Hana kura youote huko ila kashinda Jimbo C lenye delegates 6. Hivyo kwakuwa Katina ya marekani inamtambua mshindi kuwa ni yule mwenye kura nyingi za delegates basi mgombea Y ndio atakuwa mshindi
 
Kuna kitu hakjakiweka sawa katika maelezo yake ndio maana hata wewe umeingia wasiwasi ukauliza swali lako. Kwa ninavyofaham mimi raisi hupatikana kwa kura 270+ za delegates ambao yeye kawaita mabwanyenye. Lakini hizi kura hupatikanaje? Kila Jimbo la marekani Kati ya hayo 50 Lina Idadi ya delagates wake. Mgombea akishinda popular votes za Jimbo husika, anapewa kura zote za delegates kwa Idadi yao kwenye hilo jimbo. Na kwa sababu majimbo yanatofautiana winginwa delegates mgombea anaweza kushinda kwa gepu dog tu kwenye majimbo yenye delagates wengi na akashindwa mbali mno kwenye majimbo yenye delagates wachache kiasinkwamba ukijumlisha popular votes mgombea huyo anakuwa amepata kura nyingi lakini delegates wachache Hivyo anakuwa ameshindwa na mtu mwenye popular votes chache

Mfano majimbo A, B na C. Jimbo A linawapiga kura 13 na delegates 2, Jimbo B wapiga kura 20 delegates 3 na Jimbo C Lina wapiga kura 50 na delegates 6. Mgombea X akapata kura 11 za Jimbo A, kura 16 za Jimbo B na kura 23 za Jimbo C. Mgombea huyu atakuwa amepata popular vote 50. Wakati huo huo mgombea Y kapata kura 2 za Jimbo A, kura 4 za Jimbo B na kura 27 za Jimbo C, Hivyo atakuwa na jumla ya popular votes 33.

Kwa kigezo cha popular votes, mgombea X atakuwa na kura 50 wakati mgombea Y ana kura 33.

Tukirudi kwenye delagates, mgombea X kashinda majimbo A na B na Hivyo kujipatia Kura 2 za delegates wore wa Jimbo A na kapata kura zote 3 za delegates wa Jimbo B, Hivyo anakuwa na jumla ya kura 5 za mabwanyenye.

Kwa upande wa mgombea Y, kashinda Jimbo A na B hivyo Hana kura youote huko ila kashinda Jimbo C lenye delegates 6. Hivyo kwakuwa Katina ya marekani inamtambua mshindi kuwa ni yule mwenye kura nyingi za delegates basi mgombea Y ndio atakuwa mshindi
Asante kwa ufafanuzi mzuri Sima70
 
Electoral college votes zinapatikanaje?

Kwa nini, kwa mfano, electoral college votes za Florida ni nyingi kuliko za South Carolina?

Nani huamua kwamba hizi electoral college votes za Florida apewe Dr. Cornell West na si Dr. Jill Stein wala Donald Trump?
Electoral college votes zinapatikana baada ya mgombea kushinda popular votes nyingi kwenye uchaguzi hivyo kila jimbo linatoa mgombea wa chama chama ambacho mgombea husika amepata kura nyingi

Kuna majimbo makubwa yana watu wengi kama Frorida ukisha huko popular votes unapata idadi kubwa ya wajumbe watakao kupigia kura ya electoral college votes
 
Kila chama kinachagua wajumbe wake kwa kanuni zake kinawasilisha listi katika serikali ya jimbo, baada ya matokeo ya popular vote kuhesabiwa yote na mshindi wa kura kujulikana katika jimbo wajumbe wa chama kilichoshinda wanaapishwa na kupiga kura za electoral college.
Very thank you
 
Lakini Electoral College imeshatoa Marais watano walioshindwa Popular vote wa karibuni wakiwa George Bush na Trump.
Kweli tupu unaweza shinda popular votes ukashindwa kwenye electoral college votes ukapoteza nafasi
 
Kuna kitu hakjakiweka sawa katika maelezo yake ndio maana hata wewe umeingia wasiwasi ukauliza swali lako. Kwa ninavyofaham mimi raisi hupatikana kwa kura 270+ za delegates ambao yeye kawaita mabwanyenye. Lakini hizi kura hupatikanaje? Kila Jimbo la marekani Kati ya hayo 50 Lina Idadi ya delagates wake. Mgombea akishinda popular votes za Jimbo husika, anapewa kura zote za delegates kwa Idadi yao kwenye hilo jimbo. Na kwa sababu majimbo yanatofautiana winginwa delegates mgombea anaweza kushinda kwa gepu dog tu kwenye majimbo yenye delagates wengi na akashindwa mbali mno kwenye majimbo yenye delagates wachache kiasinkwamba ukijumlisha popular votes mgombea huyo anakuwa amepata kura nyingi lakini delegates wachache Hivyo anakuwa ameshindwa na mtu mwenye popular votes chache

Mfano majimbo A, B na C. Jimbo A linawapiga kura 13 na delegates 2, Jimbo B wapiga kura 20 delegates 3 na Jimbo C Lina wapiga kura 50 na delegates 6. Mgombea X akapata kura 11 za Jimbo A, kura 16 za Jimbo B na kura 23 za Jimbo C. Mgombea huyu atakuwa amepata popular vote 50. Wakati huo huo mgombea Y kapata kura 2 za Jimbo A, kura 4 za Jimbo B na kura 27 za Jimbo C, Hivyo atakuwa na jumla ya popular votes 33.

Kwa kigezo cha popular votes, mgombea X atakuwa na kura 50 wakati mgombea Y ana kura 33.

Tukirudi kwenye delagates, mgombea X kashinda majimbo A na B na Hivyo kujipatia Kura 2 za delegates wore wa Jimbo A na kapata kura zote 3 za delegates wa Jimbo B, Hivyo anakuwa na jumla ya kura 5 za mabwanyenye.

Kwa upande wa mgombea Y, kashinda Jimbo A na B hivyo Hana kura youote huko ila kashinda Jimbo C lenye delegates 6. Hivyo kwakuwa Katina ya marekani inamtambua mshindi kuwa ni yule mwenye kura nyingi za delegates basi mgombea Y ndio atakuwa mshindi
Uko vizuri wewe jamaa hongera kwa ufafanuzi mzuri
 
naomba jawabu kati ya donard trump na hilal Clinton nani alipata kura nyingi kimajimbo usemavyo na akatangazwa RAIS wa marekani?
Hilal Clinton alipata kura nyingi za wananchi Donald Trump akapata kura nyingi za majimbo kwa kuwa yeye alishinda yale majimbo nyeti yanayotoa wajumbe wengi wa electrol Votes ndio maana alitangazwa mshindi kipindi hicho
 
District of Columbia ina wajumbe watatu [3], siyo wawili.

535+3=538.




Maelezo mazuri.

Inafurahisha kuona walau wapo watu humu ambao kidogo wana uelewa wa mfumo wa uchaguzi mkuu wa urais ulivyo nchini Marekani.

Maana kuna watu wengine humu hawajui, na mbaya zaidi, hawajui kama hawajui.

Ukiwaeleza kuwa wanavyoelewa ni makosa, wanashupaza shingo na kuleta ubishi.

Hawajui tofauti ya national popular votes na state popular votes.

Hawajui ni votes zipi ndizo zinazoamua mgombea apate EV za jimbo.

Ukiwaeleza kwamba demokrasia ya Marekani siyo ‘direct democracy’, bali ni ‘representative democracy’, ndo unazidi kuwachanganya.

Ukienda ndani zaidi na kuwaeleza kwamba, Marekani siyo demokrasia [America is not a democracy] bali ni constitutional federal republic, ndo unawapoteza kabisa na watakubatiza majina yote!

Nyongeza: electoral college votes za jimbo huongezeka na/au hupungua kuendana na idadi ya watu/ wakazi waliopo jimboni.

Mfano, jimbo la California, Abraham Lincoln alipata kura 4 mwaka 1860. Kwenye uchaguzi wa 1864 akapata kura 5.

Mwaka 1980, Ronald Reagan alipata kura 45. Mwaka 1984 akapata kura 47.

Mwaka 2000 Al Gore alipata kura 54.

Hillary Clinton 2016 na Joe Biden 2020, walipata kura 55.

2024, California ina electoral votes 54.

Hapo utaona zimepungua. Hiyo ni kutokana na jimbo kupungukiwa wakazi na hivyo kupoteza kiti kimoja cha bunge la wawakilishi.

Kuongezeka au kupungua kwake, kunafuatia matokeo ya sensa.

Sensa ya mwisho Marekani ilikuwa 2020. Matokeo ya sensa hiyo yalitolewa 2021.

Ndo maana Joe Biden 2020 alipata EV 55. Lakini mwaka huu 2024, zimepungua na kuwa 54.
Uko vizuri mdogo wangu
 
kwa kuwa yeye alishinda yale majimbo nyeti yanayotoa wajumbe wengi wa electrol Votes ndio maana alitangazwa mshindi kipindi hicho
Majimbo hayo siyo nyeti au muhimu eti kwa vile yana wajumbe wengi. Umuhimu wake ni kwamba yana wapiga-kura shindani kwa vyamba vyote; mgombea fulani akizubaa kidogo tu basi inakula kwake.

Nevada ina electoral votes 6 na Wisconsin 11. Haya mawili ni majimbo ya ushindani. Kwa upande mwingine New York (28) na California (54) hayamo kwenye kundi hilo la majimbo nyeti, licha ya wingi wa electoral votes.
 
Majimbo hayo siyo nyeti au muhimu eti kwa vile yana wajumbe wengi. Umuhimu wake ni kwamba yana wapiga-kura shindani kwa vyamba vyote; mgombea fulani akizubaa kidogo tu basi inakula kwake.

Nevada ina electoral votes 6 na Wisconsin 11. Haya mawili ni majimbo ya ushindani. Kwa upande mwingine New York (28) na California (54) hayamo kwenye kundi hilo la majimbo nyeti, licha ya wingi wa electoral votes.
Kwa nini sasa New York na California hapo kwenye ushindani?
 
Kwa nini sasa New York na California hapo kwenye ushindani?
Kwa sababu ni ngome ya chama cha Democrats. Wapiga-kura wengi ni wa huo mrengo wa kushoto.

Lakini yale majimbo saba (Arizona, Georgia, Michigan, Nevada, North Carolina, Pennsylvania na Wisconsin), yenyewe yana takriban idadi sawa ya wapiga-kura kwa vyama vikuu shindani.

Au kwamba wapiga-kura wake hawafungamani na chama chochote - wanazingatia maslahi mapana ya taifa lao. Kwa hiyo jinsi wanavyoshawishiwa kisera ndivyo wanavyopiga kura. Ndiyo maana Trump kakomba hayo yote awamu hii.

Hii ni tofauti na majimbo ambayo ni ngome (ama ya Democrats au Republicans), ambapo hata sera ziwe mbaya mbovu kiasi gani, wao wataimba ngonjera ileile: ^sisi tumeipenda wenyewe; na wavimbe wapasuke...!^
 
Kwa sababu ni ngome ya chama cha Democrats. Wapiga-kura wengi ni wa huo mrengo wa kushoto.

Lakini yale majimbo saba (Arizona, Georgia, Michigan, Nevada, North Carolina, Pennsylvania na Wisconsin), yenyewe yana takriban idadi sawa ya wapiga-kura kwa vyama vikuu shindani.

Au kwamba wapiga-kura wake hawafungamani na chama chochote - wanazingatia maslahi mapana ya taifa lao. Kwa hiyo jinsi wanavyoshawishiwa kisera ndivyo wanavyopiga kura.

Hii ni tofauti na majimbo ambayo ni ngome (ama ya Democrats au Republicans), ambapo hata sera ziwe mbaya mbovu kiasi gani, wao wataimba ngonjera ileile: ^sisi tumeipenda wenyewe; na wavimbe wapasuke...!^
Asante mkuu kwa darasa lakini sasa kama majimbo hayo yanatoa wajumbe wengi wa electrol votes si zingembeba mgombea huyo wa Democrats akishinda popular votes?
 
Asante mkuu kwa darasa lakini sasa kama majimbo hayo yanatoa wajumbe wengi wa electrol votes si zingembeba mgombea huyo wa Democrats akishinda popular votes?
Ndiyo zimembeba sana. Kwani huoni Kamala alipiga hadi 226?

Angeshinda pia majimbo mengine matatu tu (North Carolina-16, Pennsylvania-19 na Wisconsin-10) katika yale 7 ya ushindani, angefikisha electoral votes 271. Hivyo angetangazwa kuwa mshindi wa urais.
 
Back
Top Bottom