Ujumbe wa Dr. John Karugia: Watanzania lindeni sana rasilimali zenu

Ujumbe wa Dr. John Karugia: Watanzania lindeni sana rasilimali zenu

Daah!

Umeandika kwa uchungu sana mkuu!

Naapa! Kama hakutatokea mwafaka mzuri kwenye hili, Sasa niko tayari kwa maandamano ya kupinga uuzwaji wa bandari zetu yenye kukutana na usalama wangu na ama vinginevyo,

Hii inaitwa, kufa na kupona ili kupinga kutawaliwa na warabu kwa mara ya pili

Nasubiri kuiongozi yeyete atamke ni lini maandamano
Hakika tuko pamoja.
 
Kweli nyani haoni kundule, unachukia matusi na papo hapo unaita wenzio wapumbavu wengine! Oke, mpumbavu ni yule anajua madhara ya jambo ila anaendelea kulifanya hivyo hivyo akiitegemea matokeo tofauti. Je, wasemao tumekuwa tunaleta uwekezaji kwa ujanja ujanja hivi hivi tukuamibishwa tutaimarika ila mambo yanakuwa hola. Sasa wapumbavu ni wepi kati ya wale wasemao hapana kwa namna hii, tubadilishe mambo fulani au wale wasemao twende hivi hivi tuwaamini viongozi wetu (wale wale waliotudanganya hapo nyuma)?
Rais ni nembo ya Nchi, mpumbavu mmja hawezi mdahalilisha
 
Kama swala la kuwekeza unaunga mkono Sasa inakuaje Lisu na wapumbavu wengine wa Chadema wanaotukana na kudhalilisha Mamlaka ya Rais? Kwani inahitaji kudhalilisha Ili kufikisha ujumbe? Na Serikali imeshasema itazingatia hayo maoni na Wasiwasi wa Wananchi then why Wapuuzi waache kuendelea kupotosha Kwa kueneza Chuki?
Mkuu., punguzeni JAZIBA maana kama watawala hawatauelewa UMMA, nina uhakika Taifa litaingia hatua ngum sana. Huwa hamuoni maandamano yenye nguvu naamini mtayaona, nayanaweza kumtoa mtawala kwenye kiti.
 
Mkristo huyu lazima apinge waarabu kuwekeza bandarini, anajua magari na vifaa vyao havitapita bure tena kwa msamaha wa kanisa.
Kwa hiyo hata kazi ya kukusanya mapato ya kodi ya forodha (TRA) mtawapa hao DPW!!
Maana wanaotoa msamaha ni TRA na si TPA.
Rudi ukasome elimu dunia japo kidogo ili usiitie aibu familia yako na taifa jwa ujumla kwa kuwekeza nguvu nyingi kwenye elimu ahera ambayo ni utapeli mtupu.
 
Mkuu., punguzeni JAZIBA maana kama watawala hawatauelewa UMMA, nina uhakika Taifa litaingia hatua ngum sana. Huwa hamuoni maandamano yenye nguvu naamini mtayaona, nayanaweza kumtoa mtawala kwenye kiti.
Yaleteni au mnadanganyana humu mitandaoni? Na wewe utakuwepo au Kuna mtu unasubiria aende Kwa niaba Yako?
 
Rais ni nembo ya Nchi, mpumbavu mmja hawezi mdahalilisha
Hata mimi sipendi kudhalilishana, sio Rais tu hata mtu mwingine si vema kudhalilishana. Shida yangu ni pale unapondhalilisha yule unayeamini anadhalilisha wengine. Please, tuwe kind ila hasira zetu zionekane wazi katika yale tusiyoyapenda. Mimi naamini asiyekosea ni MUNGU tu! Wengine wote pasi na kujali ni kina nani, tunakosea na kwa mtazamo wangu hata katika hili Rais AMEKOSEA.... Kwanza kasema amezima masikio... (Maana yake hayupo tayari kusikiliza) hiki ni KIBURI! (viongozi wengi wa kiafrika wapo hivi), hata kama hutaki kusikiliza wengine ila si busara kusema NIMEZIBA MASIKIO! Sasa tumuambie nani ili hali NCHI tumempa yeye!
 
Yaleteni au mnadanganyana humu mitandaoni?
Sawa., kama hujuwi kaa ukijuwa hata hilo Jeshi mnalojivunia litakaa pembeni nakusikiliza amri ya Jeshi la Wananchi linasemaje, msione limekaa kimya mkajuwa halioni na linafurahia hayo madudu yanayofanyika.
 
Taasisi zipo ili kutoa ufafanuzi katika hili jambo, wanaweza kulikataa ama kulikubali; kama ziko 'inactive', wewe kama 'individual' unataka nini cha zaidi; pambania familia yako tu, maisha ni mafupi haya.​
Wizi na ufisadi ndio chanzo cha huduma mbovu shule hazijengwi wanafunzi wanasomea chini ya mti, wajawazito kujifungulia chini mahospitalini hakuna dawa tatizo kwa sababu ya walafi wachache kuingia mikataba mibofu kwa lengo la kujinufaisha wao na familia zao na ndugu jamaa na marafiki.
 
Rais ni nembo ya Nchi, mpumbavu mmja hawezi mdahalilisha
Mtazamo wako kuhusu hili ni wa hovyo kipumbavu na kijinga na kichonganishi

Wanancho 90% ukiondoa wale tunaodhani wamekula cha mwarabu, wanahoji kuhusu ubovu wa mkataba, na katika hili viongozi wengi wameanza kuwasikiliza wananchi, wewe unaita udhalirishaji kwa Rais mambo ambayo ni hatima ya nchi yetu kikiwepo na kiti hicho?

Kwa nini ccm wengi akili hamnazo?
 
Watanzania wapendwa,

China ilipokuwa na nia ya kuwekeza 35% katika bandari ya Hamburg ambayo ni bandari kubwa kabisa Ujerumani, bunge la Ujerumani, wizara sita za Serikali ya Ujerumani na Usalama wa Taifa (yaani Foreign Intelligence Service) ya Ujerumani na European Commission wote walikataa na kusema kwamba ni lazima kujihadhari sana na uwekezaji wa mwekezaji yeyote atokaye Ulaya katika sehemu kama bandari kwa sababu ni sehemu muhimu sana kwa usalama wa taifa - yaani: Strategic national security area.

Baraza la Mawaziri lilifanya kikao maalum na Usalama wa Taifa wa Ujerumani wakanyafanya utafiti.

Wanasiasa na wananchi wakapaza sauti sana. Nia ya wote ilikuwa kuchunguza kama ni sawa kuiruhusu China kuwekeza katika bandari la Hamburg.

Baada ya Utafiti na baada ya mazungumzo marefu, mapna na makali kama pilipili uamuzi ulitangazwa kwamba China haitaruhusiwa kuwekeza zaidi ya 25% katika bandari ya Hamburg. Nia ya China ilikuwa 35%.

Mwezi wa tano mwaka huu wa 2023, kampuni ya COSCO ya China ilitia sahihi mkataba wa uwekezaji wa 24.9 % katika bandari ile ya Hamburg.

Kwa nini 10% iliondolewa?

Ili kuondoa kabisa uwezo wa COSCO kuwa na nguvu za kupinga maamuzi yoyote yanayohusu uendeshaji wa bandari la Hamburg (yaani Veto power).Nguvu za uamuzi wa uendeshaji wa bandari na mambo yote yanayohusu bandari zimebaki na serikali la Jimbo la Hamburg na serikali ya Ujerumani.

Sio kitu kigeni kuwa na mwekezaji kutoka nje ya nchi katika bandari, ila lazima kujitahadhari kwa sababu bandari kubwa kama bandari ya Dar es Salaam ni sehemu - very strategic kwa national security.

China haijawekeza katika bandari la Hamburg tu. Imewekeza katika bandari la Rotterdam kule Netherlands, bandari la Piraeus kule Greece na pia Ubelgiji, Uispania na Italia.

Naunga mkono Mama Rais Samia Suluhu na Serikali ya Tanzania na Usalama wa Taifa wa Tanzania katika uamuzi wa kutafuta mwekezaji wa bandari la Dar es Salama. Pia, nawaunga Watanzania wote mkono wanaoomba kwamba Tanzania ijitahadhari na ihakikishe mikataba yote ya wawekezaji kutoka nje inalinda matakwa (yaani interests) za Tanzania kwanza, kwamba mikataba inaipa Tanzania nguvu zaidi ya mwekezaji yeyote kutoka nje na pia inahakikisha kwamba Tanzania inabaki na nguvu za maamuzi ya mwisho, (yaani veto power) katika bandari kama walivyofanya Wajerumani.

Dubai haiwezi kumpa mwekezaji yeyote kutoka Tanzania nguvu zaidi ya Emirati ya Dubai. China haiwezi kumpa mwekezaji yeyote kutoka Ujerumani nguvu zaidi ya China katika uwekezaji bandarini China. Waarabu wanalinda mali yao sana. Wachina wanalinda mali yao sana. Wajerumani wanalinda mali yao sana sana sana sana. Waafrika lazima tulinde mali yetu pia sana sana sana sana sana sana sana sana.


Bana e. Kiswahili changu ni cha Kenya jamani ndugu zangu nawaomba munisamehe kama nimekosea hapa na pale ila natumai mumeliewa kwa umbali jambo nililotaka kuwaambia.

Ni wajibu wetu kuilinda Afrika Mashariki pamoja. Nyie ni ndugu zangu na ninawapenda sana.

Maana nimewaandikia baruapepe hii. Nawaomba nisalimie Mama Suluhu na nawaombea awaletee suluhu na suluhu ile iwe yenye baraka. Nawaombea kher ya mwenyezi Mungu.

Mnisamehe kama nimeingilia mambo ya ndani nchi yenu, ila rafiki mwema ni yule akwambiaye ukweli kwa kukutizama machoni. Rafiki wa kweli hakusemi kichinichini hata mwenyezi Mungu hapendi hivyo.

Salamu nyingi kutoka Berlin.
Ni mie wenu awapendaye,Mwalimu John Njenga Karugia
Na wajerumani huwa wanapiga sana pesa za umma ??!!
 
Kama swala la kuwekeza unaunga mkono Sasa inakuaje Lisu na wapumbavu wengine wa Chadema wanaotukana na kudhalilisha Mamlaka ya Rais? Kwani inahitaji kudhalilisha Ili kufikisha ujumbe? Na Serikali imeshasema itazingatia hayo maoni na Wasiwasi wa Wananchi then why Wapuuzi waache kuendelea kupotosha Kwa kueneza Chuki?
Sheria zipo kwa yeyote anayezivunja nendeni mahakamani kama una ushahidi wa hayo matusi, kinyume na hilo ni malalamiko.
 
Taifa letu tuna bahati mbaya sana, tulipata uhuru wa kisiasa tukiwa hatuna wasomi wa kutosha, ikitegemewa kwamba, baada ya kupata uhuru, ndio tungeenda kuwekeza ili kuwaondoa wale maadui watatu ikiwemo ujinga.

Bahati mbaya sana, licha ya kuongeza idadi ya wasomi, lakini bado tumejikuta tuna tatizo kubwa zaidi, kubwa zaidi ya kutafuta ule uhuru wa kisiasa, wasomi waliotegemewa waje kuikomboa nchi kifikra, wamegeuka wajinga wanaopenda kuishi kwa kujipendekeza kwa watawala, huku wakichekelea bila aibu kwa vyeo wanavyopewa.

Matokeo yake sasa, wasomi hao toka idara mbalimbali za serikali ambao wangetegemewa walisimamie taifa kwenye kulinda rasilimali zake, ikiwemo TISS, wamegeuka chawa wa mtawala wanaofanya kila wanaloamriwa bila kuzingatia kama lina maslahi kwa taifa ama hapana.

Sasa tumegeuka taifa la wajinga tusio na mwelekeo, kila mmoja anajitazama binafsi hajali jirani yake ana shida gani, wabunge wamegeuka walafi licha ya mishahara mikubwa na posho, lakini bado wanadanganyika kwa rushwa, tena mbaya zaidi, rushwa inayozitoa sadaka rasilimali za nchi yetu, hii kwangu ni laana.

Hapa tumekaa tunasubiri maamuzi ya mahakama kwenye kesi zilizofunguliwa kupinga ule uwekezaji wa kihuni, tuone kama wasomi kwenye mahakama zetu wataona umuhimu wa kulinda rasilimali zetu, au nao watageuka kama wasomi wa bungeni na serikalini waliotusaliti, ili mwisho wa siku, umma wa Tanganyika ujiamulie kulinda rasilimali zao, tena kwa nguvu zao wenyewe, wasomi tuliowategemea, wamegeuka hasara kwa taifa, wasomi wasiojua hata kuhoji!.

Ndg yetu jiran yetu Mkenya, tunashukuru nawe kuchangia katika suala la Bandari zetu za Tanganyika. Hila kuna wale Chawa wabwatukaji watakwambia wewe hayakuhusu, wewe ni Sukuma gengi na mengi mengineyo. Huku kwetu tumeamua sio kumpa kwa 100% ila tumempa kila kitu, uhuru wetu na mamlaka ya kufanya chochote akitakacho pasipo kuhingiliwa na yeyote hata serikali. Na hata hivyo anachukua maeneo yote yanye kuzungukwa na maji kwa maisha yote labda Bahari, Maziwa na Mito vikauke ndo ataondoka lah mpk akirudi mkombozi wetu YESU KRISTO siku ya kiyama. Sijui ni uMangungo wa kihasi gani sijui kwa kweli.
 
Kama swala la kuwekeza unaunga mkono Sasa inakuaje Lisu na wapumbavu wengine wa Chadema wanaotukana na kudhalilisha Mamlaka ya Rais? Kwani inahitaji kudhalilisha Ili kufikisha ujumbe? Na Serikali imeshasema itazingatia hayo maoni na Wasiwasi wa Wananchi then why Wapuuzi waache kuendelea kupotosha Kwa kueneza Chuki?
Lini Serikali ilianza kuchukua maoni ya wananchi juu ya sakata hili?! Bunge ambapo ni jicho la wananchi nalo limekuwa tepetepe mbele ya Mwarabu hayo maoni yalichukuliwa kwa njia gani?! Acheni kudanganya wananchi kama watoto wadogo. Kwanza utachukuaje maoni baada ya kusaini mkataba?
 
Watanzania wapendwa,

China ilipokuwa na nia ya kuwekeza 35% katika bandari ya Hamburg ambayo ni bandari kubwa kabisa Ujerumani, bunge la Ujerumani, wizara sita za Serikali ya Ujerumani na Usalama wa Taifa (yaani Foreign Intelligence Service) ya Ujerumani na European Commission wote walikataa na kusema kwamba ni lazima kujihadhari sana na uwekezaji wa mwekezaji yeyote atokaye Ulaya katika sehemu kama bandari kwa sababu ni sehemu muhimu sana kwa usalama wa taifa - yaani: Strategic national security area.

Baraza la Mawaziri lilifanya kikao maalum na Usalama wa Taifa wa Ujerumani wakanyafanya utafiti.

Wanasiasa na wananchi wakapaza sauti sana. Nia ya wote ilikuwa kuchunguza kama ni sawa kuiruhusu China kuwekeza katika bandari la Hamburg.

Baada ya Utafiti na baada ya mazungumzo marefu, mapna na makali kama pilipili uamuzi ulitangazwa kwamba China haitaruhusiwa kuwekeza zaidi ya 25% katika bandari ya Hamburg. Nia ya China ilikuwa 35%.

Mwezi wa tano mwaka huu wa 2023, kampuni ya COSCO ya China ilitia sahihi mkataba wa uwekezaji wa 24.9 % katika bandari ile ya Hamburg.

Kwa nini 10% iliondolewa?

Ili kuondoa kabisa uwezo wa COSCO kuwa na nguvu za kupinga maamuzi yoyote yanayohusu uendeshaji wa bandari la Hamburg (yaani Veto power).Nguvu za uamuzi wa uendeshaji wa bandari na mambo yote yanayohusu bandari zimebaki na serikali la Jimbo la Hamburg na serikali ya Ujerumani.

Sio kitu kigeni kuwa na mwekezaji kutoka nje ya nchi katika bandari, ila lazima kujitahadhari kwa sababu bandari kubwa kama bandari ya Dar es Salaam ni sehemu - very strategic kwa national security.

China haijawekeza katika bandari la Hamburg tu. Imewekeza katika bandari la Rotterdam kule Netherlands, bandari la Piraeus kule Greece na pia Ubelgiji, Uispania na Italia.

Naunga mkono Mama Rais Samia Suluhu na Serikali ya Tanzania na Usalama wa Taifa wa Tanzania katika uamuzi wa kutafuta mwekezaji wa bandari la Dar es Salama. Pia, nawaunga Watanzania wote mkono wanaoomba kwamba Tanzania ijitahadhari na ihakikishe mikataba yote ya wawekezaji kutoka nje inalinda matakwa (yaani interests) za Tanzania kwanza, kwamba mikataba inaipa Tanzania nguvu zaidi ya mwekezaji yeyote kutoka nje na pia inahakikisha kwamba Tanzania inabaki na nguvu za maamuzi ya mwisho, (yaani veto power) katika bandari kama walivyofanya Wajerumani.

Dubai haiwezi kumpa mwekezaji yeyote kutoka Tanzania nguvu zaidi ya Emirati ya Dubai. China haiwezi kumpa mwekezaji yeyote kutoka Ujerumani nguvu zaidi ya China katika uwekezaji bandarini China. Waarabu wanalinda mali yao sana. Wachina wanalinda mali yao sana. Wajerumani wanalinda mali yao sana sana sana sana. Waafrika lazima tulinde mali yetu pia sana sana sana sana sana sana sana sana.


Bana e. Kiswahili changu ni cha Kenya jamani ndugu zangu nawaomba munisamehe kama nimekosea hapa na pale ila natumai mumeliewa kwa umbali jambo nililotaka kuwaambia.

Ni wajibu wetu kuilinda Afrika Mashariki pamoja. Nyie ni ndugu zangu na ninawapenda sana.

Maana nimewaandikia baruapepe hii. Nawaomba nisalimie Mama Suluhu na nawaombea awaletee suluhu na suluhu ile iwe yenye baraka. Nawaombea kher ya mwenyezi Mungu.

Mnisamehe kama nimeingilia mambo ya ndani nchi yenu, ila rafiki mwema ni yule akwambiaye ukweli kwa kukutizama machoni. Rafiki wa kweli hakusemi kichinichini hata mwenyezi Mungu hapendi hivyo.

Salamu nyingi kutoka Berlin.
Ni mie wenu awapendaye,Mwalimu John Njenga Karugia
We jamaa umeamua kuwasigina ccm wenzako😆😆😆
 
Back
Top Bottom