Ukabila Ikulu, Ujenzi, Mambo ya nje, Mipango, TRA, BoT + Ofisi nyeti za serikali

nakuambia!! yaani hawa jamaa wakipewa mapanga na kuambiwa "fyeka" sitashangaa watadhania wameambiwa wawafyeke Wachagga!!
 

Tukiangia EAF, tutaanza wakenya wakenya, wakenya. Kwa mtanzania kama alivyosema MKJJ some where, kila kifo kina mchawi!


Nafikiri mchawi anafikirika kwa wale wanaoamini wakati mkabila yupo na wengine wanajisifia na kuuendekeza kama vile Bongo ni mali yao. Ukweli ni lazima usemwe na usipindishwe hata kama unaingiliana na maslahi ya mchangiaji.
 
mwanasiasa, kama tumeshahitimisha kuwa ukabila upo kuna haja gani ya kufanya uchunguzi? Haiwezekani kimantiki kutafuta ushahidi wa kitu ambacho unajua tayari kipo. Kama swali ni "Je kuna ukabila Tanzania?" Hebu tuchunguze, mimi ningekubali, lakini mmeshatuambia kuna ukabila na wameshatajwa ni kina nani wakabila, uchunguzi wa nini? Endapo uchunguzi ukija na kuonesha hakuna ukabila na kabila linalotajwa halina ukabila hivi wewe na wengine mnaoona ukabila sasa hivi mtakubali kweli au mtasema "ni hao hao wakabila waliofanya uchunguzi"?

Haya ndio aliyoyasema "mswahili" kwangu:


nilipomjibu na kutaka aandike hicho hadharani akanijibu na kuniambia:

mswahili said:
Nadhani wale wayahudi walikuwa milioni 6 jee wachagga wanafika milioni 6? NAOMBA USHAURI WAKO? HAKUNA TATIZO KWANI HAWA WATU SI WATANZANIA ASILI YAO ETHIOPIA.
NIPE JIBU LAKO

Sasa huyu ndiye nyinyi mnamuunga mkono!! Nikisema kati ya wachagga na mswahili nani mkabila.. of course nyinyi mtasema "wachagga"!!
 
kuna mtu humu ndani alishawahi kusema ,mtu kama mswahili angefaa kuwa mmoja wa wanapropaganda kama wale waliopelekea mauaji ya rwanda..AHSANTE MJJ KWA KUMUONYESHA ALIVYO WATU WAPATE KUJUA NA KUMJUA ..na nashauri kuwa wale waliokuwa wakimuunga mswahili kwenye hii mada WAJITOKEZE WASEME KAMA NA KWENYE HILI[likiwemo option ya kutumia mbinu iliyomaliza wayahudi milioni 6]..WANAMUUNGA MKONO..WAPINGE NA KULAANI AU WAKAE KIMYA TUJUE WAKO NAE KWENYE HILI !!!!!
Allah akhbar!!!! Mungu ni mkubwa!!!! amemuumbua mnafiki....kelele zote hizi kumbe ni chuki mbaya kabisa,MODERATOR VIPI ???? UTAKAA KIMYA KWA HILI NA KUSEMA NI TUSI LA KAWAIDA!!!!!!!!!!! WATANZANIA TUNAELEKEA WAPI..WE ARE OBSERVING WITH MUCH INTEREST utamchukulia hatua gani separatist ..a serial HOLOUCAST kama huyu mswahili!!!!!!
mwisho nakumbusha nilipata kumwambia mswahili asiwapigie sana debe baadhi ya watu ...tusije tukaamini kuwa hao pia wanaamini kama yeye!!!!
 
Phil, inahitaji ujasiri mtu kukiri makosa na kupotea. Wakati mwingine ukimya unatoa jibu la ndio!!
 
Mwalimu alitukumbusha tukianza na tabia ya kubagua kabila moja hatutaishia hapo.Leo ni wachagga, kesho wameru, keshokutwa wasukuma.
Ukabila ni cancer ambayo lazima ikatwe mizizi yake pale inapoanza kujitokeza.
 
Jasusi, watu wamechelewa! tulipata nafasi ya kukataa ukabila huu mada hii ilipoanza lakini kwa vile ilikuwa "yametajwa na majina" ya ukabila wa watu wengine, ukabila wa baadhi ya wanachama wenzetu ukafumbiwa macho! Watu wakatoa pongezi kwa mtu ati "amekata issue" na "amemwaga data". Watu wakasifia na kusema ni wa wakati wa "kumkoma nyani geledi"! Kila tulipojaribu kuonesha upotofu wa mawazo hayo tukaambiwa "kwanini tunawatetea wachagga? tuna maslahi gani na wachagga" Wengine tumeulizwa kama tumechumbia uchaggani (jambo ambalo silithibitishi wala kukanusha)!

Hata sasa kuna ndugu zetu hapa bado wanakubali kuna ukabila. Lakini ukabila wanaozungumzia wao ni wa wachagga kwa vile mtu ambaye hana ukabila kasema hivyo!!! Maneno anayoyasema mwanachama huyo mwenzetu kama yangewekwa kwenye TV yangemfukuzisha kazi kama Imus!! Lakini kwa vile tumeonekana tumeshapepewa na kufukizwa moshi huu wa chuki ya kikabila, baadhi tumeanza kuamini na kuwashuku Wachagga!! Tumeanza TRA, inabidi tuendelee kuwatafuta, twende Hazina, twende Ikulu, twende Benki Kuu, popote tutakapowakuta wachagga tujue ni ukabila umewaweka hapo.

Tangu nilipoweka aliyoyasema mwanachama huyo kwangu hadharani nilitarajia wanachama wengi ambao wamesoma kutokea kulaani na kuyakana mawazo hayo na kuonesha mshikamano na ndugu zetu Wachagga. Anyway watu wanaogopa, kwa sababu wataonekana "wanawapenda wachagga" au "wananufaika na ukabila"!

Maneno ya mwanachama huyo kuhusu wachagga ni ya kichochezi, kibaguzi, na yaliyojaa sumu ya ukabila. Ni maneno ya hatari ambayo licha ya kuwa ana haki ya kuyasema hadharani ili tujue kilichomo ndani yake, hayana nafasi katika Tanzania yetu, hayavumiliki, na hisia zake ni za kupiga vita kwa nguvu moja! Niko tayari kusimama peke yangu kutamka hivyo.

Ninachoomba ni kuwa asichukuliwe hatua yoyote ile hapa JF bali tujue ni kitu gani kinamuongoza na tuwe tayari kugundua sumu yake hiyo anapoandika juu ya Wachagga! Haki yake ya kutoa maoni, isitishiwe kwa namna yoyote ile kwani ni vizuri kujua mtu anasema nini kwani inatuonesha anachofikiri, kuliko mtu atutendee kitu ambacho hatukujua amewahi kufikiri!!
 
Mzee Mwanakijiji naona wewe umemaliza yote yanayotakiwa kujadiliwa kwenye hii hoja. Mimi nataka kuongezea kidogo kwakutumia statistic. Kutokana na historia ya Tanzania, kama ulivyosema wamissionary waliwapatia elimu watu wa maeneo haya. Hii iliendelea hata baada ya Uhuru kwani wazazi wa maeneo haya walikuwa wameshapata mwamko waelimu na ndio maana nao waliendelea kujenga shule nyingi za kata za wazazi kwaajili ya watoto wao. Kwamfano Mwaka 1992 shule za sekondari zilizokuwa mkoa wa Kilimanjaro zilikuwa zaidi ya asilimia 18 ya shule zote. Mikoa kama Lindi na Kigoma zilikuwa na shule chini ya 5 kwa mkoa mzima Je mikoa hii iwiane kwa wahitimu wa sekondari?.

Mwaka 2004 kati ya wanafunzi 28 waliomaliza Mlimani degree ya uchumi wanafunzi 21 walikuwa wachaga, 5 walikuwa wanyakyusa na 3 walitoka makabila mengine. Je kama TRA, Hazina wanataka watumishi hawa jamaa wasiajiriwe kwasababu ni wamakabila haya? Mimi naona kama ulivyosema Nyerere Alimaliza kila kitu. Cha msingi sisi makabila mengine Tuangalie ni vipi tutawasaidia vijana wetu wapate elimu kwa wingi na elimu Bora ili baadae waweze kuwa na uwiano katika soko la ajira.

Turudi kwenye Uongozi wa ngazi za juu serikalini. Ni wachaga wangapia wamekuwa mawaziri kwa awamu hizi tatu za mwisho? Kwa awamu hii ya Kikwete Ambayo inabaraza kubwa sana la mawaziri Kuna Mramba, Chami kama naibu waziri, Megji sina uhakika kama ni mchaga. Je kwa hili tusema kwenye siasa kuna ubaguzi wa kikabila? Mikoa ya kusini kama Mtwara na lindi mbona imekuwa ikitoa mawaziri wengi sana.

Tukirudi kwenye nyanja za biashara ukichukulia mfano mdogo wa Kariakoo, zaidi ya 50% ni wachaga na wafipa, Je tusema nako kuna ukabila?

Mimi kwa maoni yangu naona hii issue haina mjadala tupe ushawishi wa kueleweka ili tuamini kweli ukabila upoo.
MWANAKIJIJI KULA TANO MKUU.
 
Mkjj,

Duh!! mkulima Mkjj umeleta mtoto wako ili akusaidie (joke)

Mtoto wa Mkulima,

Karibu sana katika ukumbi wa JF, natumai utakuwa kama baba yako Mkjj (joke) mzee wa "hoja hujibiwa kwa hoja"
 
Kuna mtu anajaribu kung'ang'aniza kwamba, kwasababu mtu kaleta hii topiki na washabiki wake...basi huyo mtu na washabiki ni wakabila. Mambo ya kuongea kimafumbo, yanafanywa na wanawake.
Ok, kama hiyo ndiyo logic ya famous quote yake 'Hoja hujibiwa kwa hoja'.....mimi nina swali lenye hoja, ina maana; mtu anaye-mislead watu kuwachangisha hela kwaajili ya mtanzania wetu, akificha facts, wakati kila mtu anajua, na yuko convinced, na watu bado tunajua ukweli....je, kwa bidii yake hii iliyopotosha wengi..........je ni haki kumwiita mtu huyu muuza madawa ya kulevya???

Mtu huwezi kutengeneza facts zikae kivyako tu, when it suits you. Mtu hufanyi research yako. Ndio maana mheshimiwa hana time na interview na mtu ambaye hakusanyi facts vizuri.

On that account. I sign out, personally got mad love for ma Chagga peeps.
 
mwelekeo wa hii mada ulianza kupotea tangu baadhi ya watu walipoanza biased attacks!

hamna kitu kibaya kama kuhisi mtu,kitu,n.k....hii inakufanya ufanye vitu kama kipofu!kwa mfano ukihisi mwanao mchawi[anakuloga]...unamuua sio?

halafu watu kusahau historia yao....tulipotoka,n.k.....sijasikia mtu akisema wangoni warudi kwao south africa! ila kuna mtu anajua mpaka asili ya baadhi ya wachagga[sio wote wana asili moja]ambayo bado haijawa proved with historical facts!

watu wanafumbia macho mambo ya kikabila yanayofanywa na makabila mengine na kuwashtumu wachagga kwa kitu kisichowahusu....

kwa mfano,jk sio mchagga...lakini mbona ana wachagga kadhaa kwenye baraza la mawaziri? je,huo ni ukabila au ni safu ya watendaji kazi wake?

unajua,wakati mwingine mtu unajiuliza hivi elimu imetusaidia kung'amua mambo?je tumeelimika kwa kwenda shule?je,kwa hilo tutasaidia katika maendeleo ya nchi yetu?au tutakuwa mzigo,tatizo,na kikwazo?
 

http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=1747&page=3

Sasa Mzee Mwanakijiji hiyo quote ya Mswahili ilitolewa katika mazingira gani? Wote tunafahamu mwamba ngozi huvutia kwake. Je unataka tukuamini kwa kauli zako kama hiyo hapo juu? Kama utaweka details zetu in confidence?

Kwa kweli naanza kuona jinsi uchangiaji unavyokuwa kwa mleta hoja ni nani na siyo hoja ndio yenye nguvu.
 

Well spotted Dua. Kama hayo maneno kweli amesema Mswahili, sikubaliani nae, and its wrong, those are not the values Nyerere laid for us Tanzanians. Lakini on that note, its takes a big backstabber to put someone's message which they have been in contact through PM (thats why its called Private Message), and expose it here without their permission. For all we know, he could have doctored that message.
Huyu ni mtu mwenye 'Radio' where if someone has information, they can pass on in 'confidence'!! Ndio mambo ya ku-abuse DATA PROTECTION haya. And the words coming from his mouth about 'mapanga kufyeka fyeee'......hayo ni maneno yake. Yeye ndio anang'ang'aniza kucreate chuki.
Two wrongs dont make it right. It says a lot about the person who actually pasted that message. Now that is low!!
 

PM, my reply to this issue is above. My request to you is, dont force everyone to be mkabila when they are not.
 
mimi nilianza kumshtukia huyu bwana tangu hajaanzisha hii topic. lakini jambo la kushangaza zaidi ni jinsi watu walivyo-COMFORTABLE na "TONE" ya postings zake.

huyu bwana amejibiwa kwa data. karibu kila dai aliloleta bila data zozote limejibiwa kwa data. alileta madai kwamba serikali inapendelea barabara mkoani kilimanjaro tu, bajeti ya serikali niliyoileta inaonyesha kinyume cha hivyo. zaidi taarifa ya matumizi ya Tanroads ilionyesha kwamba madai yake hayakuwa ya kweli.

inasikitisha, lakini i am leaning into believing Watanzania tunapenda mambo ya uvumi-uvumi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…