Ukabila Ikulu, Ujenzi, Mambo ya nje, Mipango, TRA, BoT + Ofisi nyeti za serikali

Ukabila Ikulu, Ujenzi, Mambo ya nje, Mipango, TRA, BoT + Ofisi nyeti za serikali

TUSIWE WATU WA KUKURUPUKA TU MIDHALI STUDY IMEFANYIKA TUNASEMA NI SAHIHI. TUMEONA STUDY NYINGI TU AMBAZO NI BOGUS - WHO KNOWS TRA BETTER THAN WALE WANAOFANYA KAZI PALE NA AMBAO WANANYANYASWA NA UKABILA. JE NI STUDY GANI YA UHAKIKA YA WATANZANIA AU WAGENI KUTOKA NJE. LAZIMA TUWE MAKINI NA HIZI STUDIES.

well said Dua,
 
Mkandara et al,

mtu mmoja mmoja anaweza kuwa na hisia ya kutukuza kabila lake na hivyo kuwadharau wafanyakazi wa makabila mengine kazini. Mtu mwenye ukabila wa aina hiyo, hahitaji mtu mwingine kuwa na ukabila. Mwenye ukabila kazini, atapendelea kuwapa watu nafasi watu wa kabila lake, huku watu wa makabila mengine wakinyimwa nafasi hizo. Mwenye ukabila kazini anapoangalia nani wa kumpandisha cheo anaangalia watu wa kabila lake kwanza.

Sasa kama ukabila wa aina hii upo Tanzania basi siyo himaya ya Wachagga peke yake! Sitashangaa ukamkuta Mzaramo ambaye akijua mtu fulani kazini ni mzaramo mwenzake basi akampa nafasi zaidi n.k Lakini hilo haliwafanyi Wazaramo wote mahali pa kazi kuwa na ukabila hata kama wapo kwenye kitengo kimoja na huyo mtu mwenye ukabila.

Wote wenye ukabila mahali pa kazi ni rahisi kuwagundua. Hukutana kwenye vikao vya watu "wao", mwenzao akikosea huchukuliw hatua nyepesi za kinidhamu ukilinganisha na mtu wa kabila jingine. Lengo la watu wenye ukabila ni kujinufaisha na kunufaishana. Watu hawa wanapoajiri mtu hawaangalii kitu kingine ila kabila la huyo mtu hata kama hawamfahamu. Lengo lao ni kukusanya nguvu zaidi kwenye kabila lao. Ili kufikia lengo hilo basi watawafukuza kazi watu wa makabila mengine, watawanyima vyeo watu wa makabila mengine, watawanyanyasa kwa kuwaona duni na wengine wanaweza hata kuthubutu "kuwaita majina" watu wa makabila mengine.

Mtu mwenye ukabila kazini hawezi kufanya kazi na kukubali kuwa na mahusiano ya kazini na watu wa makabila mengine kwani hakuna ulazima huo. Na hata ikimlazimu kufanya kazi na watu wa makabila mengine basi utaona anavyojitenga na watu hao!! Huo ndio ukabila!!!

Hivyo ukabila katika ajira siyo wingi wa majina ya kabila moja kwenye kitengo fulani bali ni muunganiko wa tabia na matendo unaoongozwa na hisia ya ukuu, upekee, na kustahili unaowafanya watu wa kabila moja kutumia nafasi zao za kikazi kujinufaisha au kuwanufaisha watu wa kabila lao.

Hoja yangu ni kuwa ukabila wa aina hiyo Haupo. Hoja ya pili ni kuwa hakuna ushahidi wowote kuwa Wachagga TRA wanao ukabila huo, tatu wenye kutetea uwepo wa ukabila wa aina hiyo wanaongozwa na hisia ya chuki ya kikabila. Mawazoni mwao wameshawahukumu wachagga na hivyi kuwabandikiza neno "Ukabila" siyo vigumu kwao hata kama wataoneshwa kuwa hakuna ushahidi wa kitu hicho.

Nieleweke vizuri, sijakataa kuwa mtu mmoja mmoja anaweza kuwa na ukabila na kama nilivyosema hisia hizo si za kipekee kwa wachagga, bali watumbatu,makua, wanyakyusa, wavinza n.k wanaweza kuwa na watu wenye hisia hizo kwenye makabila yao.

Batizeni jina la "kupendeleana" au "kufahamiana" kama ndilo tatizo la ajira na hilo halichagui kabila. Mkikubali kuondoa neno na maana ya "Ukabila" mnapozungumzia TRA hapo ndipo angalau tutakuwa kwenye ukurasa mmoja. Neno "ukabila" halina ushahidi hata chembe na ni kejeli kwa jamii ya Watanzania, ni kama tusi kwa ndugu zetu! Kunyoshea kidole kabila moja na kulia "ukabila" wakati sote tunajua kuwa ajira watu wanapeana kwa kujuana zaidi ya kwa ukabila ni mwanzo wa ubaguzi usio na msingi.

Binafsi sitarajii kuwashawishi wale wenye kuuona ukabila kubadili mawazo hayo kwani mawazo ya namna hiyo hayawi ndani ya mtu kwa siku moja ni mawazo ambayo yanamsingi wa malezi ya mtu na mtu alikokulia. Niliposoma Arusha miaka hiyo katika mojawapo ya shule kulikuwa na affirmative action ya kuhakikisha watu wa maeneo hayo wanapatiwa nafasi kwanza kwenye shule hizo kabla ya sisi "wakuja" kukubaliwa. Lakini tulipokuwa shuleni licha ya kuwa wao walikuwa ni wengi, hakukuwa na ubaguzi wa aina yoyote na hata ilipotokea mitihani tulishandana sawa. Walimu wote ukiondoa Mwl. Munisi walikuwa ni kabila la huko. Lakini waliposahihisha mitihani hakukuwa na wazo la ukabila, ingawa mtu mwingine angeona walimu wa kabila moja, wanafunzi wengi wa kabila moja angeweza kulia "ukabila"!!

Ndugu zangu tukwepe jaribu hili la kunyoshea kidole Watanzania wenzetu na kuwabatiza jina wakabila "genge la Kilimanjaro", n.k Inaweza kutupa furaha ya kihisia kuwa "watatukoma" lakini madhara zaidi yanakuwa kwetu kwani ni sisi ndio tunaohangaika na "ukabila" wao.
 
MSWAHILI SIJATAJA MESSENGER HAPA.....TUTAJIE BASI RRO,PRO I/C WA MIKOA YOTE TUONE...HATA HAYO MAJINA ULIYOYARUDIA HAYAASHIRII UKABILA HATA CHEMBE....

KIMSINGI HII MADA SASA INABOA KWA SABABU KINA MSWAHILI INAONEKANA WANA SPECIAL MISSION...YOU JUST TAKING PEOPLE FOR A RIDE WITH YOUR SYNDICATE AMBAYO INAANZIA DEEP TRA and culprits for this in TRA are known already,..teknelojia si mchezo bwana,HUKU NI KUTISHIA USALAMA WA TAIFA LETU ,WATU WAPO HAPO JIRANI NA WAMEONA.. ndio maana mtaona hapa wanaongelea TRA tu hoja ya BOT na BANYAMULENGE ilipokuja humu ndani kina mswahili kimya ,kwa mswahili bora kazi afanye mtu wa nchi ya jirani kuliko MCHAGGA,sasa HII NI HATARI.
SIJASHANGAA mshiriki mmoja huku alipofananisha hoja za chuki dhidi ya wachagga na lile gazeti na redio huko RWANDA...
KWA nini naogopa KUENDELEA NA HII MADA ,jibu rahisi naona aibu hata majirani zetu wanaopita huku watasema ,NA WATANZANIA WAMO???? NDIO MAANA NAHISI HAWA KINA MSWAHILI WANATUMIWA NA WATU WA NDANI Na nje...lakini mkumbuke maneno ya mwalimu.kuwa "dhambi ya ukabila ni akma kula nyama ya mtu,mkimaliza wachagga ,mtaendelea na wahaya,,...mwisho mtajeukiana wenyewe..."nilikuwepo!!!!!!!!!! later
 
Mwanakijiji,

Post yako hapo juu, ukiangalia para 1, 3, 5 zote hizo zapatikana TRA!! Ukisoma vizuri maelezo ya Mmanda na kama unamjua mtu mwenyewe utakubali kuwa Mmanda kawakilisha kundi la wakubwa "wachagga" pale TRA kujibu tuhuma.
Yes nakubali Historia ni kioo, However, huwezi kuwa unafanya 1, 3 and 5 (paragraph zako) eti kwa kisingizio cha kuhalalish historia wakati history ni dynamic.
Nakubaliana na wewe tusi-generalize kuwa Wachagga wote ni wakabila, kwa hapa tunaweza sema wachagga wa TRA wana ukabila!!, nafikiri tutakuwa tumehitimisha majibishano, na sasa tufikirie dawa yake.

Duuh Mswahili wee ni moto!!
niliambiwa pale TRA kuna kitu chaitwa "FAMILY" (similar to Mtandao ndani ya CCM) hebu tumegee ni kitu gani hicho, and why kina-exist. Na je ni kweli mapato yanayotangazwa yana reflect hali halisi?
 
Tatizo 1, 3, 5 (ref last post ya MKJJ) lipo.
Kukwepa/kukimbia/kuficha tatizo ni mwanzo wa failures. I don't think JF are ready for failures.
JF, lets tackle it and not otherwise.
 
phillemon mikael

Hakuna mwanabodi anayebisha kwamba kuna wachaga TRA ambao ni wachapakazi na hakuna mwanabodi aliyesema hawa sio watanzania. Hiyo link ya kazi ndio kwenye maneno huko angalia kichwa cha habari.
 
IFUATAYO NDIO BODI YA WAURUGENZI YA TRA AMBAYO MSWAHILI ANASEMA IMEJAA "WACHAGGA"

http://www.tra.go.tz/board.htm


na HII NI MANAGEMENT TEAM [WAENDESHAJI WA SHUGHULI ZA SIKU HATA SIKU] WA TRA AMBAO KWA MACHO YA KINA MSWAHILI WANASEMA NI "WACHAGGA" TUPU

http://www.tra.go.tz/team.htm

BAADA ya hapa napendekeza mjadala uishe tu,sidhani hivyo vichwa vyote hapo juu vinaweza kukumbatia ukabila ,kwanza woote wametoka sehemu zote za nchi hii...ni uzandiki kuendelea kuwapaka matope TRA bila ushahidi zaidi ya majungu...sasa kama mswahili ana viongozi wengine zaidi ya hawa na awataje ..tuache majungu jamani...nafikiri hata TRA Kuna section ya wafanyakazi wasiokuwa waaminifu waliokalia majungu na kuwatupia kina mswahili....
hizi taarifa ninazokupa mimi sio majungu wala siri it is for public consumption.,,hata kwenye mtandao utazipata ...na kama hujaridhika peleka manunguniko yako...

info@tra.go.tz

au peleka IKULU nao pia wanayo website au yumia ole ya ..kikweteshein..


mada closed ,,isn"t it????
 
dua nimetumia fasihi tu kusema "wachagga" kama umeangalia hizo link utagundua hiyo management ya TRA ina wachagga wachache tu kama makabila mengine pia, sasa na hapo bado hutaki!!!!!!!

kwaherini...later!!!
 
samahani wazee, hii ilinipita

jokakuu wrote..........

.............Jamboforums imekuwa kama gazeti la kihutu kangura lilokuwa likihamisha chuki dhidi ya watutsi...............

Please watch your language na usituletee UNAZI hapa JF, kama huna la kuandika kaa pembeni

This is where we are heading!
JF is losing sight of its agendas; badala ya kujenga sasa tunabomoa...this is Kangura indeed! and we can clearly see the extremists here.
Admn:, can we put an end to this? afterall its not serving any purpose...
the conclusion should be: WE HAVE AGREED TO DISAGREE
 
phillemon mikael

Jibu hoja kwa hoja, majina aliyotoa Mswahili ni ya uongo?

Hakuna mahali popote ulimwenguni ambapo watatangaza sera za ukabila, udini etc. kwani wanafahamu moto wake. wanaofanya ukabila sio wajinga eti.

Majungu unayafahamu wewe na huwezi kusema hii mada sasa imekwisha umeona kichwa cha habari bado hatujaingia IKULU, UJENZI, MAMBO YA NJE, MIPANGO, BENKI KUU na OFISI NYETI ZA SERIKALI. Na wewe mara unataka kufunga mjadala. VIPI MZEE UNAPATA CHOCHOTE HUKO KWENYE UKABILA? acha jazba. Hii ngoma bado mbichi kabisa. Mficha maradhi kifo humfichua, huu ukabila kokote uliko ni lazima ukomeshwe.
 
Kwa wanabodi,
Ikiwa swala la TRA limekataliwa kujadiliwa basi toka leo naamini kabisa kuwa Tanzania kuna UKABILA!...
Mnaweza sema wanaokataa sio kabila la mhusika wa TRA, lakini hiyo sii hoja kwa sababu kuna wahindi South Afrika walikataa kuwepo kwa Apertheid, just because wao walijipendekeza kwa maslahi yao.
Haya ndiyo Maswala ya Bosnia ambapo Serbia wanakataa kuwa mauaji yale hayakuwa Genocide. Utawala wa Sudan Unakataa mauaji ya Darfur kuwa genocide. Na Wayahudi wanakataa kabisa kuwa mauaji ya Serbia, Rwanda na Sudan are worth kuitwa genocide isipokuwa mauaji yao chini ya Hitler.
Na laukama Ulimwengu wangekaa kimya kwa kufuata hizi tafsiri sijui kama tungeweza kupata suluhu ya matatizo hayo. Inashangaza sana Wana JF wenye elimu za juu wamekazania neno moja UKABILA kuwa sababu kubwa ya kutotazama tatizo la Ajira nchini.

Na hii yote inathibitisha mtazamo wangu ktk kutazama matokeo mabaya ya sera kama za Majimbo!
Tutashindwa kabisa ku deal na tatizo hilo pindi likitokea na yawezekana linasukumwa na watu wenye Mtazamo kama wa TRA.
Mtanisamehe!...that's me!
 
Mkandara, can you listen to urself talking? yaani suala la "ukabila" wa wachagga TRA na vitengo vingine mmeanza kulifananisha na Serbia, Sudan, Rwanda n.k... keep breaking the principle, and principle will find a way of breaking you. !

Ndugu zangu mnaomini wachagga wa TRA ni wakabili (tribalists) tafadhali endeeleni maana imani ni imani huhitaji ushahidi! Binafsi nimekubali kuna watu wanafanya mambo ya kikabila, but haijafikia kujumlisha ofisi nzima, idara nzima, kuwa ni wakabila!
 
nadhani mjadla ni mzuri na unaonyesha jinsigani watu walivyokuwa tayari kutetea hoja zao regardless

sasa kukubaliana au kutokubaliana ni lingine lakini ni mambo mengi sana ya kujifunza humu
 
Mzee Mwanakijiji,
Unajua wewe mzito sana kuelewa watu wanazungumzia kitu gani?..
Hapa nachozungumzia ni DENIAL!..
Tafsiri yake hii hapa:-

Denial is a defence machanism in which a person is faced with a fact that is too painful to accept and rejects it instead, insisting that it is not true despite what may be overwhelming evidence. The subject may deny the reality of the unpleasant fact altogether (simple denial), admit the fact but deny its seriousness (minimisation) or admit both the fact and seriousness but deny responsibility (transference). The concept of denial is particularly important to the study of addiction.

Karagabaho!
 
mswahili wrote:
MKASA WA FOY KUMBAMBIKIA KESI benny lusege aliyekuwa officer incharge bandarini na kumfukuzisha kazi kwa maksudi kisa yeye ni RRO na alikuwa anapitisha mabomu yake kwa jina la benny lusege hakujua kama lusege kaenda shule kwa maana ya shule.Foy KWA kushirikiana na kittlya na wachagga wenzao wakamtimua kazi benny akaenda kujitetea kwenye bodi na kila ushahidi hatimaye benny akarudishwa kazini lakini wachagga wote wamekuwa na chuki naye hadi kuchoma moto nyumba yake na akapelekwa porini na hii kesi ilifika hadi kwa Meghji.
jamani msitete kitu msichokijua huenda mnazuia haki za watu kwa kujifurahisha akina lusege wametaka kuuliwa TRA KUNA genge la majambazi.

mswahili,
kwanini unaona ni ukabila tu ndiyo unawasukuma hao jamaa kumdhuru mr.lusege? kwanini isiwe RUSHWA au WIZI? je, huyo jamaa angekuwa ni mchaga mwenzao hivi unaamini wangemstahi kama angetakaa kupitisha hayo magendo?

Ogah wrote:
TUSIWE WATU WA KUKURUPUKA TU MIDHALI STUDY IMEFANYIKA TUNASEMA NI SAHIHI. TUMEONA STUDY NYINGI TU AMBAZO NI BOGUS - WHO KNOWS TRA BETTER THAN WALE WANAOFANYA KAZI PALE NA AMBAO WANANYANYASWA NA UKABILA.[red] JE NI STUDY GANI YA UHAKIKA YA WATANZANIA AU WAGENI KUTOKA NJE.[/red] LAZIMA TUWE MAKINI NA HIZI STUDIES.

well said Dua,

Ogah,
kama umefuatilia postings za Dua basi ataona kwamba tayari ana-conclusions zake. study yoyote ile itakayoleta conclusions tofauti yeye ataiponda. Kama ameikataa study hiyo hapo juu, nini kitamzuia kuiponda study nyingine itakayofuatia?

Dua huyo huyo, yalipoletwa majina hapa na Phillemon akazua kisingizio kwamba uko uwezekano kwamba wapo waliobadili majina!!

Mwanakijiji,Philemon,Mkandara,
1.Mwanzo mwa hoja hii tulikubaliana kwamba kuna uwezekano wachaga wako kwa wingi ktk posti kubwakubwa kutokana na ukweli kwamba kabila hilo lilikwenda shule mwanzoni. Hali hiyo unaweza kuiona hata ktk mashirika mengine. Suala hilo lingekuwa TRA tu, basi tungesema kuna ukabila. Suala hilo lipo accross the board.

2.Malalamiko yakageuka kwamba: kama ni suala la wachaga kusoma zaidi mbona hata UMESENJA na UKARANI makabila mengine hayaajiriwi? Philemon akaleta a random list, ndefu kidogo, ambayo inaonyesha kwamba hakuna monopoly ya wachaga at all.

3.Baada ya Phillemon kuleta listi hiyo Mswahili akadai listi hiyo ni ya MAKARANI,MGAMBO, MESENJA,na MADEREVA wa TRA!! Zaidi katika kuichambua listi hiyo Mswahili ameonyesha wote siyo wasomi. Mswahili alipaswa kutetea hoja yake ya awali kwa kutuonyesha kwamba wachaga wamehodhi hata ukarani, na umesenja.

4.Mwanakijiji ameleta copy ya utafiti ambao umefikia conclusion kwamba tatizo la ukabila lipo URA, na siyo TRA. Kwanini watu wameidismiss ripoti hiyo outrightly? Badala yake watu wanataka another independent investigation.

5.Mwanzo wa mada kulikuwa na hata malalamiko kwamba ukabila wa wachaga unakuwa facilitated na mawaziri toka kilimanjaro. Waziri anateua wajumbe wanne kati ya 10 wa board ya TRA. Mwenyekiti huteuliwa na Raisi, na wengine watano huingia kutokana na sheria ya TRA. Ukiangalia wajumbe walioteuliwa na Waziri utaona hakuna ukabila.

6.Management kuu ya TRA imeonyesha a reasonable tribal balance. Hata meneja utumishi na uajiri siyo mchaga, bali ni mpare. Katika suala linalohusisha wapare basi Mswahili hubadilika na kusema kuna "genge la wakilimanjaro." Naelewa kwamba haya makabila ni watani wa jadi, lakini hivi wanaweza kuwa na mkakati wa pamoja kuyakandamiza makabila mengine? Mimi ningemwamini mswahili kama angedai lipo genge lingine independent--"genge la wapare." Hii hoja ya "wakilimanjaro" hainiingii akilini.
 
Jokakuu,
Bahati mbaya Benny sio mchagga!.. na pengine kama angekuwa Mchagga lisingetumiwa jina lake.. who knows!. Hizi zote ni dhana sasa hivi kwani kitendo kilichotendeka ndio issue hapa!..Deny! deny! deny!. Tutafika kweli?

Hawa jamaa ni wakabila na haina maana Wachagga wote ni Wakabila!.. msipoelewa hilo itakuwa kazi nyingine kuutambua Ukabila ni kitu gani.
 
#329 Yesterday, 12:23 AM
phillemon mikael
Senior Member Join Date: Sun Nov 2006
Posts: 373
Rep Power: 21




--------------------------------------------------------------------------------

wanabodi nimemaliza kuipitia list ndefu ya wafanyakazi wa TRA wapatao 1,000...ninachoweza kusema MSWAHILI ni mzushi mkubwa ,sijaona ukabila wowote katika hizo kada anazosema mswahili..kama ni wachagga,wahya na wanyakyusa labda kidogo kwenye senior position pale makao makuu...ambao tena wengi ni wa uteuzi..i wish hii copy ingekuwa electronic ,hata hivyo kama unataka distribution ya kituo chochote bara na visiwani ,niulize....

nimepitia list za idara zifuaTazo,EXAMINATION OFFICERS,CUSTOM OFFICERS,PREVENTIVE OFFICERS,CUSTOM GUARDS,MESSENGERS,DRIVERS,...
 
MKJJ Binafsi nimekubali kuna watu wanafanya mambo ya kikabila, but haijafikia kujumlisha ofisi nzima, idara nzima, kuwa ni wakabila!

Kwenye idara kuna watu wachache tu wenye uwezo wa kuajiri na kufukuza, tunapoongelea ukabila tunaongelea watu hao wenye nyadhifa za kuajiri na kufukuza hatuongelei akina Tom, Dick and Harry. Hapo ndipo pana shida na ukikuta kuna watu wa kabila moja wanafanya hivyo kama TRA basi ni hatari sana.

Mkandara
Naona hukutaka kumalizia hiyo definition of denial naongeza kidogo i.e. ........................as a mechanism of the immature mind, because it conflicts with the ability to learn from and cope with reality.
 
Nimejaribu pia kufuatilia kama kuna watu ambao majina yao yanafanana na majina ya juu ya watu kama lauwo na luoga ,..nikakuta wawili ambao wapo dar es salaam ...long room/warf mmoja wao anaitwa humphrey ,lakini kufanana kwa majina ya ubini si lazima wawe ndugu wa damu inawezekana ni kabila moja...na kila mtu anaweza kua ameingia kwa muda wake....

sasa angalia list ya EXAMINATION OFFICERS waliopo dar uangalie mwenyewe kama kweli kuna harufu ya ukabila....hoja yangu hapo ni kuwa hata kama watu wamesaidiana humo si ukabila bali tukubaliane ni URAFIKI/KUJUANA ets

hawa ni wa kituo cha dar[wharf/long room/DIA]
1 BENS MWENDA
2.MOHAMED NGAIRI.
3.THOMAS KOKO
4.SALIM NAPUNDAR
5.HERMES KUWETA
6.HEAVEN MINJA
7.SEKELA MWASAMBUNGU
8.ANNA RAGWITABA
9.KOMBO L.
10GLAD NYANGE
11.MPANGILE L.
12.EDANA ROBERT
13.ANDREW Y.
14.LAUWO...
15.A.RWEYENDERA
16.M.MSANGI
17.M.NYAMANGA
18.KALUMUNA N.
19.NSHEMIYE K.
20. MAJI F.
21.NYAMANGA M.
22.MAKUNDI L.
23.JUMA K.
24.ZAINABU B.
25.NGANDAKU B
26.AZIZI S.
 
Back
Top Bottom