Ukabila ni jambo lisilo semwa sana nchini lakini lipo sana kazini/maofisini

Ukabila ni jambo lisilo semwa sana nchini lakini lipo sana kazini/maofisini

Binafsi nimeona kitu wakati najenga.

Ukipata fundi kabila fulani basi atakuwa akikushawishi vifaa mkanunue duka la mtu wa kabila lake kwa hoja ya bei nzuri au ubora wa bidhaa ila ukifuatilia hutoona utofauti wa bei/ubora na maduka mengine.

Ukienda Hardware moja ukakosa bidhaa husika hasa kama ni mzigo mkubwa eg tiles basi,muuzaji atakuunganisha na duka la mtu wa kabila lake hata kama duka jirani yake linauza bidhaa hiyohiyo.

Hizi jumuiya/vikundi vya watu wa kabila fulani wanaoishi mkoa/mji fulani vimefanya watu wa kabila moja watambuane na mambo ndiyo hayo.
Sambamba na hilo kuna magroup ya kikabila pia wanayo wasapu yaani mfano mimi msukuma nikienda lindi nitaunganishwa kwenye group la wasukuma wa lindi yaani ukikutana na msukuma wa kule atakuambia lakini pia tuna group letu mwenzetu akipatwa na tatizo tuna saidiana nitamwambia kiongozi akuunganishe!!(huu ni mfano tu) Unaona jinsi ukabila unavyopaliliwa sasa hapa nchini!!
 
Mdogo wangu yuko Arusha ila wilayani analia na ukabila ,mara wamtishe ...Kwa kweli siwezi kuondoka mkoa wangu mpaka kifo ,huko kwingine naenda sana na kurudi ila kuishi kwa makazi hapana kwa kweli.
 
Mdogo wangu yuko Arusha ila wilayani analia na ukabila ,mara wamtishe ...Kwa kweli siwezi kuondoka mkoa wangu mpaka kifo ,huko kwingine naenda sana na kurudi ila kuishi kwa makazi hapana kwa kweli.
Huu wimbo wa Tanzania hakuna ukabila unaimbwa nje tu ila ndani hapakaliki hata mimi dogo kaajiriwa hivi karibuni
siku3 tu akaniambia watu wa huku wana ukabila balaa nikamwambia hata huku sema umepazoea na kuona ni kawaida.
 
Sambamba na hilo kuna magroup ya kikabila pia wanayo wasapu yaani mfano mimi msukuma nikienda lindi nitaunganishwa kwenye group la wasukuma wa lindi yaani ukikutana na msukuma wa kule atakuambia lakini pia tuna group letu mwenzetu akipatwa na tatizo tuna saidiana nitamwambia kiongozi akuunganishe!!(huu ni mfano tu) Unaona jinsi ukabila unavyopaliliwa sasa hapa nchini!!
Kwa hiyo hutaki watu wasaidiane we jamaaa una matatizo ya akili
Na siku zote mtu anaye kusaidia ni yule anaye kufahamu period
 
Back
Top Bottom