Hivi, unafahamu kwamba kuna vyanzo vya uhakika vinasema kwamba abiria walokuwamo humo kwenye kivuko ni zaidi ya 200?
Na pia hakuna anaefahamu zaidi ikwamba inawezekena abiria wakawa zaidi ya 400 aana wengi walokuwa wakienda gulioni?
Sasa waziri wa uchukuzi anaingiaje hapo?
Cha msingi ni kwamba kivuko ni kizima na hakikuwa na kasoro yoyote ile kwani hivi karibuni kilipata injiini mbili mpya.
Suala linaanzia kwenye msimaizi wa hicho kivuko ambae anasimamia kwamba ni tiketi ngapi ziuzwe na abiria wangapi waruhusiwe kuingia kwenye kivuko.
Hivyo usimamizi kwamba kivuko kinabeba uzito upi, namba ya abiria, mizigo na korokoro zingine si jukumu la waziri.
Hilo ni jukumu la wasimamizi wa kivuko ambao ndo wanapaswa kuwajibishwa.