Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Kwani rambirambi ni kiasi gani hasa mbona naona mapovu..ndio maana baadhi ya misiba utakuta jamaa furani haendi mbali na sahani na daftari…na huku akiwa na sura ya mbuzi…na hakawii kurusha ngumi ukitaka kumfuatilia…jamani rambirambi ni yatokanayo tu huhitaji kuitegemea saaana!

Kabla hujaandika ujinga wako, fikiria kuwa wewe ulipokuwa na miaka mitatu ama minne, una wadogo zako wawili hapo, baba na mama yako ndio wamebeba vimizigo wameelekea sokoni. Unasubiri giza linaingia, hujala, akili za kujitambua zaidi ya kulia huna, hujui ndugu, unawafahamu baba na mama pekee, unalia, watoto wanalia hadi sauti hazitoki tena, hakuna wa kwenda kuwatambua wazazi wako ambao huenda wameshahesabiwa kuwa ni wale ambao hawajatambulliwa, na wamezikwa tayari......
JUST IMAGINE, KISHA ANDIKA TENA ULICHOANDIKA.
 
Haya ndio tulikuwa tunayasema na sasa yanaanza kutimia!

Kwahiyo watu wasipochanga hayo hayatafanyika?

Hivi nani ni mshauri wa hawa watu?!

Nini wajibu wa serikali katika matukio ya aina hii?

Bajeti ya kitengo cha maafa chini ya waziri mkuu inafanya kazi gani?

Ndio maana wengine tunawafurahia sana watu kama Zitto na Lissu kwa jinsi wanavyowasema wenye mamlaka.

Watanzania amkeni hasa wale wanaodhani wapinzani wana chuki tu na hii serikali.

Kweli kama ni serikakali ya wanyonge, basi watanzania Mungu katupendelea!
Hivi unyonge ni kitu cha kujivunia? Hivi baada ya zaidi ya miaka 50 ya uhuru bado kuna watu wanajisifu kuwa wanyonge na hata akatokea mtu na kujisifu dunia nzima imsikie kuwa yeye ni kiongozi wa wanyonge?!
 
Inavyojulikana ni kuwa rambirambi ni kwa ajili ya wafiwa ili kuwapunguzia machungu na kuwafuta machozi!
Haya mengine inabidi serikali iyabebe na kuyafanyia kazi!View attachment 875701
Sawa sawa.. Mijitu haikomi kutoa rambirambi na kuwapa wasio stahili... Mtu aliyeguswa na tukio hili wawapelekee wafiwa mkononi na sio hawa mchwa
 
Serikali imeelekeza matumizi ya rambirambi wewe unabeza sasa mlitaka inunulie pombe?
Wee ni pumbafu sana, hivi rambi rambi ni kodi ndio mpaka serikali ielekeze matumizi yake?
Zipo familia zimepoteza wapendwa wao tena zaidi ya mmoja na hao ndio pengine walikuwa tegemeo! Hizo familia zinahitaji faraja na kuwezeshwa kupata mahitaji muhimu n.k hawana shida na hiyo minara, tuache ushabiki wa kijinga na kipuuzi pale panapokuwa na masuala yanahusu maisha ya watu!
Kauli za viongozi wetu na hata maamuzi yao hayawezi kuwa sahihi nyakati zote, huwa wanakosea pia! Wakubali ushauri, hata kama unayoka kwa mwananchi wa kawaida sana...
Kwenye hili la rambirambi kama serikali itabadilisha matumizi itakuwa haikawatendea haki wananchi wake...
 
Mlitarajia kupata tender ya kutengeneza majeneza?
Nyie mnaotumia mamilioni ya shilingi kununua bombadier kwa manufaa ya wachache wenye chapaa na kuacha majority kutumia vivuko vibovu ndio mnaotafuta tender.. Blood sucker
 
Naomba niulize swali, rambi rambi kwa upeo wako unajua ni nini? Je kazi yake ni ipi?
kufa ni kufa ila bora hata wale waliofia macca mwaka juzi kwa kukanyagana kila familia ikala kama milioni 300!!si afadhari angalau waliobakia wanajifutia machozi na wakizichanga fresh umasikini ndio basi tena !!kuliko kufia kwa watu ambao pesa za kuwafariji ndio tena zitumike kwa vitu ambavyo ni wajibu wao!!!daaaa indekuwa mtu unachagua pa kufia bora ukafie macca tu!!!
 
Nadhan mnara unetafutiwa chanzo kingine cha fedha kuujenga kwan kiuhalisia hakuna mfiwa hata mmoja aneuhitaji nadhan wawasiliane na makampuni ya cm kama wao wanaweza Ku..........................
 
Concept yako imekaa kisiasa na imepoteza maana. Janga hili haliko kisiasa wala halina hata chembe za siasa ndani yake; chuki binafsi hizo.

R.i.p wote waliofikwa na mauti katika ajali hiyo.
 
Back
Top Bottom