Elections 2015 UKAWA na Lowassa unganeni mchukue nchi, wakati ndio huu, mkipuuzia huu ushauri basi tena!

Elections 2015 UKAWA na Lowassa unganeni mchukue nchi, wakati ndio huu, mkipuuzia huu ushauri basi tena!

Napenda kutoa maoni yangu kama raia wa Tanzania hii ya sasa kwa UKAWA kama wao wanapenda kututumikia wananchi nawasihi sana waungane na Mhe. Lowassa ili kuiondoa CCM madarakani na UKAWA tukachukua nchi.

Ikumbukwe UKAWA sio chama cha siasa ila ni umoja wa muunganiko.

Asanteni..


Na inavyoonekana lowassa ana lake la kumoyon kama richmond mzigo alitupiwa aubebe wao wamemwaga mboga yeye amwage ugali kama mbwai na iwe mbwai.
 
Kwani Lowasa naye alitoka nje ya Bunge la Katiba?.... Kwa nini sasa asimame kwa tiketi ya Ukawa?
 
fuvu la paka

Kama lengo ni kuiondoa CCM nakubaliana na wewe. Lakini kama ni kuwatumikia wananchi kuna mambo mengi sana ya kuyachunguza kabla ya kufikia hapo.....kumbuka Lowasa ana marafiki akina Karamagi, Rostam, na mafisadi underdogs wengi mno ambao sidhani kama Ukawa wanaweza kukubali kuungana nao.....labda Lowasa atangaze kuachana nao kitu ambacho hana ubavu nacho.
Kumpokea Lowasa kwenu haita jalisha hata CUF mlio wadhihaki leo mmeungana nao, CUF mlikuwa mnawaita majina yote yasiofaa leo mmeungana nao, haita shangaza kwenye kusaka maslahi mnakula matapishi yenu.
 
naomba kwa mungu teamlowassa waungane na ukawa alafu jina la kundi libadilishwe kuwa 'ukawa-na-waliokatwa' yaani ccm wajue kuwa kukata na kujifanya kuruka zile sarakasi bungeni siyo hoja, hii nchi sio yao na hawana mamlaka wakutupeleka kama punda.

Chadema wamefanya kazi kubwa sana kujenga upinzani na kuiinyesha ccm vya kutosha

Cuf nayo kule zanznibar ndo usiseme

CCM kwa kutokujua na kujifanya wababe zaidi wamesababisha cuf,cdm, nk kuungana na sasa tuna 'ukawa', upinzani unazidi kukua na kuimarika zaidi.

Sasa kwa wale walio umizwa kwa kukatwa, tunawaomba mfanye maamuzi magumu ili ccm ijue kuwa hii nch siyo ya baba yao na sisi sio punda wao. jiungeni na umoja huu ili watu tutoe hasira zetu kwenye sanduku la kura.

....hii ni evolution siyo revolution ........to be continued
 
Kumpokea Lowasa kwenu haita jalisha hata CUF mlio wadhihaki leo mmeungana nao, CUF mlikuwa mnawaita majina yote yasiofaa leo mmeungana nao, haita shangaza kwenye kusaka maslahi mnakula matapishi yenu.

kwetu wapi...we chizi nini? naona unawewezeka fisadi wako kupigwa chini
 
Mimi ni mmoja wa watu niliyekuwa nikipinga Lowassa asichaguliwe CCM sababu ni moja tu alikuwa threat kubwa kwa UKAWA. Angepitishwa Lowassa UKAWA ingebaki historia siasa haina rafiki wa kudumu wala adui hata Slaa alivyokatwa CCM alihamia CHADEMA.

Nawaomba CHADEMA na UKAWA msipoteze hii turufu huyu mtu bado yupo vinywani mwa watu wengi.Bado ana influency kubwa kwenye media ambacho ni kitu muhimu wanaomkataa asipokelewe hawaijui siasa.

Kama Lowassa akipokelewa akapeperusha bendera ya UKAWA mtauona mtikisiko wa hii nchi.UKAWA watabeba kila kitu kuanzia Ubunge hadi urais. Lowassa anatakiwa atoke hadharani aeleze uhusika wake wa Richmond naamini akiwa CHADEMA atakua huru kusema.

Ni bora ushirikiane hata na shetani ili mradi uitoe CCM madarakani nyuma ya Lowassa kuna watu wengi sana.Narudia tena kwa wanachadema wenzangu siasa haina rafiki wala adui wa kudumu.

Kama lengo kushika dola shirikiana hata na shetani umalize mchezo, kama lengo ni kupinga ufisadi tutabaki hivi hivi tunapinga ufisadi huku tukiwa wapinzani, vita ni vita tu.
 
Atakayebisha hili atakua hana jicho la tatu.Naungana na wewe kwamba kama UKAWA wanataka wabaki kama chama cha upinzani kwa miaka 10 ijayo na waikatae hii golden chance ya Lowassa.
Hata hivyo nasikia mzee wa maamuzi magumu yuko chini ya ulinzi mkali wa TISS sasa sijui itakuwaje.
CCM hawatokubali kirahisi kumuachia Lowassa aje upinzani.
 
Hatuhitaji kuhamisha ufisadi from ccm to ukawa. Na kama wanampitisha Lowasa kugombea maana yake hakutakuwa na mabadiliko tunayoyataka na ni kubadili CHaDEMA kuwa ccm.


Ninachoshauri, Lowasa kama watanzania wengine, akiomba kujiunga na CHaDEMA akaribishwe lakini asipewe uongozi. Anatakiwa asihame na mashart yake ya kugombania uraisi. ahame na mtazamo mpya wa uzalendo kwamba anataka sasa kujenga nchi kwa mtazamo sahihi kwa taifa si ule wa kifirauni ccm.

CHADEMA haiwezi kuzuia mtu kujiunga kwa sababu lengo lake ni kuhakikisha inakua na inabadilisha mitazamo ya Watanzania wenye mawazo ya kifisadi, rushwa na uhayawani wa ccm kuwa Watanzania wazalendo wajenzi wa taifa, Lowasa akiwa mmoja wao. Na baada ya October, Watanzania wote watatakiwa kuwa na uwajibikaji kwa taifa katika m isingi ya UKaWA lowasa akiwe mmoja wao awe ndani ama nje ya ccm.

Suala la uongozi hattutampigia kura kwa kuwa hatutaikomboa nchi kwa kuongozwa na fisadi. Lakini uanachama sidhani kama kuna mtu anamzuia kwa kuwa Milango ya kujiunga nadhani iko wazi kwa Watanzania wote ili kukuza chama na kuondoa itikadi za kifisadi za ccm kwakuwafanya wapya.

Ahsanteni,
 
Hili jambo siyo geni hasa siasa za Kenya. Mfano Raila alijivua uanachama
KANU na kutamka Kibaki tosha. Pamoja walichukua dola. Hivi karibuni Ruto alijiengua CORD na kuungana na Uhuru again pamoja walichukua dola.
 
Hatuhitaji kuhamisha ufisadi from ccm to ukawa. Na kama wanampitisha Lowasa kugombea maana yake hakutakuwa na mabadiliko tunayoyataka na ni kubadili CHaDEMA kuwa ccm.


Ninachoshauri, Lowasa kama watanzania wengine, akiomba kujiunga na CHaDEMA akaribishwe lakini asipewe uongozi. Anatakiwa asihame na mashart yake ya kugombania uraisi. ahame na mtazamo mpya wa uzalendo kwamba anataka sasa kujenga nchi kwa mtazamo sahihi kwa taifa si ule wa kifirauni ccm.

CHADEMA haiwezi kuzuia mtu kujiunga kwa sababu lengo lake ni kuhakikisha inakua na inabadilisha mitazamo ya Watanzania wenye mawazo ya kifisadi, rushwa na uhayawani wa ccm kuwa Watanzania wazalendo wajenzi wa taifa, Lowasa akiwa mmoja wao. Na baada ya October, Watanzania wote watatakiwa kuwa na uwajibikaji kwa taifa katika m isingi ya UKaWA lowasa akiwe mmoja wao awe ndani ama nje ya ccm.

Suala la uongozi hattutampigia kura kwa kuwa hatutaikomboa nchi kwa kuongozwa na fisadi. Lakini uanachama sidhani kama kuna mtu anamzuia kwa kuwa Milango ya kujiunga nadhani iko wazi kwa Watanzania wote ili kukuza chama na kuondoa itikadi za kifisadi za ccm kwakuwafanya wapya.

Ahsanteni,

Mkuu hutompigia wewe Lowassa akija Ukawa na kugombea Urais lakini sisi tutampigia tena kwa ushawish na nguvu zote, Karibu sana Lowassa Ukawa ujisafishe tukupe mikoba.
 
Wewe siyo UKaWA. Unampa uraisi kwa misingi gani? Kwamba kwa kuhama ccm ufisadi wake umekwisha? Fikiria twice.



Mkuu hutompigia wewe Lowassa akija Ukawa na kugombea Urais lakini sisi tutampigia tena kwa ushawish na nguvu zote, Karibu sana Lowassa Ukawa ujisafishe tukupe mikoba.
 
Mkuu hutompigia wewe Lowassa akija Ukawa na kugombea Urais lakini sisi tutampigia tena kwa ushawish na nguvu zote, Karibu sana Lowassa Ukawa ujisafishe tukupe mikoba.
Magamba in action.

Kwa kuwa tunajua nchi yetu tunayo TISS ambayo moja ya jukumu lake kubwa ni kuhakikisha kuwa Sisiemu inatawala daima.

Inaelekea hii hoja ambayo imeibuka kwa nguvu sana katika siku 2 hizi humu JF kabla Ukawa hawajamtaja mgombea wao itakuwa ime-originate kutoka huko.

Hivi inawezekanaje Chadema ambayo imejipambanua na agenda yao kuu ya kupambana na ufisadi wa CCM kwa nguvu zote sasa impokee mtu kutoka CCM ambaye anafahamika kama fisadi papa?

Hivi inawezekanaje mtu ambaye hata Chama chake mwenyewe kilimuita kuwa ni fisadi papa na chama hicho kikampa jukumu Nape ambaye alizunguka nchi nzima kuwatangazia wananchi kuwa mafisadi papa watatu (akiwemo Lowassa) wamepewa siku 90 na chama chao ili wajivue gamba sasa ndiyo Chadema kimpokee kama shujaa wao anayetakiwa kuwapeleka Ikulu?

Kwa hiyo huku kupigiwa debe kupita kiasi humu JF siku 2 hizi ili Chadema impokee fisadi Lowassa kwenye chama chao ni mpango madhubuti ulioandaliwa na Sisiemu kupitia kitengo 'chao' cha usalama wa Sisiemu.

Huyo jamaa mahali pekee panapomfaa kama kweli atataka kuondoka CCM si pengine bali ni kwenda kwenye chama cha 'swaiba' wake, chama cha AKTI.
 
mchambuzixx

It's true kwani kikubwa ni Upinzani kuchukua dola na kubadilisha mfumo. Hata kama ni kwa miaka mitano lkn ccm nzima ya CCM itakuwa imebadilika. Na Watanzania watakombolewa
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom