UKAWA wanavyobabaika: Historia ya 'juisi ya maembe' kujirudia?

UKAWA wanavyobabaika: Historia ya 'juisi ya maembe' kujirudia?

Mkandara,

Unapenda sana kutumia mfano wa mume na mke kujengea hoja aina ya muungano unaodhani unafaa. Naomba nikuulize - ndoa unayozungumziaga ni ya wake wangapi?


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mimi mgeni katika mjadala huu. Lakini nina jambo moja la kuuliza:

Wakati wa Mei Mosi mwaka huu nilisikia Rais wa JMT alitangaza ongezeko la mshahara kwa wafanyakazi wa Jamhuri. Baadaye tena, nikaja sikia kwamba Waziri wa Fedha, Zanzibar akitangaza kuwa mwaka hakutakuwa na ongezeko la mshahara kwa wafanyakazi wa Zanzibar.

Sasa,

1. Tangazo la Rais lilikuwa ni kwa ajili ya Jamhuri ambayo Zanzibar haimo?

2. Suala la Fedha siyo la Muungano?

3. Tangazo la Rais lilihusu wafanyakazi wa Tanganyika tu? Kwahiyo aliongea kama Rais wa Tanganyika ama?

Asante.
 
Mimi mgeni katika mjadala huu. Lakini nina jambo moja la kuuliza:

Wakati wa Mei Mosi mwaka huu nilisikia Rais wa JMT alitangaza ongezeko la mshahara kwa wafanyakazi wa Jamhuri. Baadaye tena, nikaja sikia kwamba Waziri wa Fedha, Zanzibar akitangaza kuwa mwaka hakutakuwa na ongezeko la mshahara kwa wafanyakazi wa Zanzibar.

Sasa,

1. Tangazo la Rais lilikuwa ni kwa ajili ya Jamhuri ambayo Zanzibar haimo?

2. Suala la Fedha siyo la Muungano?

3. Tangazo la Rais lilihusu wafanyakazi wa Tanganyika tu? Kwahiyo aliongea kama Rais wa Tanganyika ama?

Asante.
Nzi , hayo unayosema ni sehemu ya vitimbwi vya huu muungano. Nadhani umesoma katika mjadala unaohusu nchi kuwa na Amir Jeshi wakuu wawili, Kikwete na Sheni wakipokezana majukumu.

Hata mishahara unayosema inatofautiana sana. Wabunge watalii wa znz wanaokuja Dodoma wanalipwa tofauti na wajumbe wa BLW.

Hawa watalii kutoka nchi ya znz wanalipwa na JMT, dau lao ni nono sana ukilinganisha na baraza la wawakilishi.

Tangazo zililihusu Watanganyika kama JMT na siyo znz.

Waziri mkuu wa JMT hana nafasi, ni afadhali sheha wa znz anaweza kusikilizwa kuliko PM

Eti kuna watu wanatuaminisha tatizo ni znz kutopewa misaada, kuna watu wanasema tufunge bandari zetu, watu waache kufanya biashara na nchi za nje ili waende kuchukua bidhaa znz, tutakuwa na suluhu.

UKiwauliza watu hao mazonge zonge kama haya tunayoyaona, wanasema ahaa znz ni mke aachwe ale tu! ebo!
 
Mchambuzi,
Kwa hiyo muda woote tulokuwa tukilumbana hapa ulikuwa hujanipata sio? Mkuu wangu mimi nachoklsema S2 ktk mfano wangu ni ndoa ya Mume na Mke. Hii inasimamia NCHI zetu ambazo ktk kugawana mamlaka ya mambo ktk SERIKALI 2 yaani ile ya mke na mume. Hivyo ktk kukaa na kutazama hali ya maisha na nafasi ya mke, mwanamme anachukua jukumu kubwa zaidi ya kuhudumia Familia nzima kwa kila shida inayohusiana na fedha, mawasilio ya nje, mikopo na kadhalika kwa kuaminiwa na mkewe. Hivyo huwezi kusema ana wake wawili kwa sababu ajnajihudumia pia yeye ktk matakwa yake.

Kwa hiyo auankuwa na bajeti ya nyumbani na pia bajeti yake yeye ktk matumizi yake wakati mkewe fedha yake ya vitumbua sii lazima itumike ndnai ya familia ila anaponunua vitu vyake vya maswala ya kike inahesabika kama ni swala la familia sii lazima mama amuombe mume fedha za kununua Thong, lipstick na wanja. Hivyo basi jukumu la Mume halikomei tu kwake bali kwa familia nzima ila kwake yeye yapo mambo yake kama mume na yapo kama kiongozi mkuu mwenye kusimamia mabo yote ya familia.

Hivyo kwa ke ndnai ya nyumba kuwa na mamlaka zaidi ya Mume haimfanyi naye kuwa Amir jeshi mkuu hapana, Ila naye pia ana mamlaka makubwa ktk ndoa hiyo kama Mke, unless nyie mnataka kunambia mke ofisi yake ni jikoni tu akiinua kichwa kuonyesha usawa wake kwa mume huyo sii mke anataka kuwa baba wa Familia.

Kwetu sisi hatutakliwi kutofautisha baina ya Baba na Mama na tuwaheshimu kwa sabau huyu ni baba na huyu ni mama jhivyo mmoja akiingilia mamlaka ya mwenzake tunaanza kuulizanana. Nachosema mimi hakuna swala lolote linaloihusu familia hii sii la Familia. Hakuna shida wala raha ya mtu mmoja isomhusu mwenzi na hakuna watoto wa Mama ama watoto wa baba. Ila kuna kugawana mamlaka ya shughuli baina yao.

Hivyo basi, kama mke kazi yake iko jikoni haina maana haimhusu Mume na kama mume kazi yake ni shambani haina maana haimuhusu Mke.
 
Mimi mgeni katika mjadala huu. Lakini nina jambo moja la kuuliza:

Wakati wa Mei Mosi mwaka huu nilisikia Rais wa JMT alitangaza ongezeko la mshahara kwa wafanyakazi wa Jamhuri. Baadaye tena, nikaja sikia kwamba Waziri wa Fedha, Zanzibar akitangaza kuwa mwaka hakutakuwa na ongezeko la mshahara kwa wafanyakazi wa Zanzibar.

Sasa,

1. Tangazo la Rais lilikuwa ni kwa ajili ya Jamhuri ambayo Zanzibar haimo?

2. Suala la Fedha siyo la Muungano?

3. Tangazo la Rais lilihusu wafanyakazi wa Tanganyika tu? Kwahiyo aliongea kama Rais wa Tanganyika ama?

Asante.
Katika swala hili, mkuu wangu hata kama tungekuwa na serikali 3 bado mishahara ingekuwa vile vile Zanzibar wakitangaza yao na Bara tukitangaza yetu. Nachoweza kusema mimi ni kwamba Mishahara alotangaza JK ni kwa serikali ya JMT hivyo watumishi wote waloajiliwa kupitia serikali kuu JMT ndio wamelengwa hivyo serikali ya Zanzibar haihusiki na kwa maana ile ile viongozi wa Bara wametumia tena JMT kupandishwa mishahara. Na sidhani kama TUKTA wanahusika Zanzibar ama wanapodai mishahara huzungumzia pia watumishi wa Umma wa Zanzibar.

Katika mkanganyiko huu ndio huleta kero za Muungano na sidhani kama kuwepo kwa Tanganyika tunaweza kuondosha hili maana akitangaza JK kupanda kwa mishahara sijui atakuwa na maana gani ambayo leo hii haiwezi kutumika vile vile. Mnachotaka kusiia ni kwamba hata Zanmzibar nao mishahara imepanda sawa na bara. Lakini ukitazama huku majuu mishahara kati ya nchi za muungano huwa hazifanani na hii hutokana na mfumko wa bei (soko huria).

Unaweza kuta Ontario mshahara wa chini ni dollar 11, Quebec dollar 9, Alberta dollar 16 na kadhalika (mifano). Yote hii inatokana na ugumu wa maisha kwa sehemu husika. Hivyo yoote hayayanawachanganya ni kutokana na sisi kutobadilisha mfumo wa Utawala na kiuchumi ambao bado serikali kuu ndio hutangaza mishahara ya taifa wakati JUWATA imeshakufa kifo cha nyani ikilenga Bara kwenyea TUKTA. Badala ya kila nchi, kila jimbo hadi vijijini kuwa na mishahara yake kulingana na hali ya maisha ya sehemu izo.

Mtumishi wa Umma wa Lindi haiwezekani akapokea mshahara sawa na mtumishi wa Dar kwa sababu hali ya maisha baina ya mikoa hiyo hailingani kabisa. Uuwiano tunaozidi kuutumia ni asili ya mfumo wa Utawala wa Kisoshalist.
 
  • Thanks
Reactions: Nzi
Mchambuzi,
Kwa hiyo muda woote tulokuwa tukilumbana hapa ulikuwa hujanipata sio? Mkuu wangu mimi nachoklsema S2 ktk mfano wangu ni ndoa ya Mume na Mke. Hii inasimamia NCHI zetu ambazo ktk kugawana mamlaka ya mambo ktk SERIKALI 2 yaani ile ya mke na mume. Hivyo ktk kukaa na kutazama hali ya maisha na nafasi ya mke, mwanamme anachukua jukumu kubwa zaidi ya kuhudumia Familia nzima kwa kila shida inayohusiana na fedha, mawasilio ya nje, mikopo na kadhalika kwa kuaminiwa na mkewe. Hivyo huwezi kusema ana wake wawili kwa sababu ajnajihudumia pia yeye ktk matakwa yake.

Kwa hiyo auankuwa na bajeti ya nyumbani na pia bajeti yake yeye ktk matumizi yake wakati mkewe fedha yake ya vitumbua sii lazima itumike ndnai ya familia ila anaponunua vitu vyake vya maswala ya kike inahesabika kama ni swala la familia sii lazima mama amuombe mume fedha za kununua Thong, lipstick na wanja. Hivyo basi jukumu la Mume halikomei tu kwake bali kwa familia nzima ila kwake yeye yapo mambo yake kama mume na yapo kama kiongozi mkuu mwenye kusimamia mabo yote ya familia.

Hivyo kwa ke ndnai ya nyumba kuwa na mamlaka zaidi ya Mume haimfanyi naye kuwa Amir jeshi mkuu hapana, Ila naye pia ana mamlaka makubwa ktk ndoa hiyo kama Mke, unless nyie mnataka kunambia mke ofisi yake ni jikoni tu akiinua kichwa kuonyesha usawa wake kwa mume huyo sii mke anataka kuwa baba wa Familia.

Kwetu sisi hatutakliwi kutofautisha baina ya Baba na Mama na tuwaheshimu kwa sabau huyu ni baba na huyu ni mama jhivyo mmoja akiingilia mamlaka ya mwenzake tunaanza kuulizanana. Nachosema mimi hakuna swala lolote linaloihusu familia hii sii la Familia. Hakuna shida wala raha ya mtu mmoja isomhusu mwenzi na hakuna watoto wa Mama ama watoto wa baba. Ila kuna kugawana mamlaka ya shughuli baina yao.

Hivyo basi, kama mke kazi yake iko jikoni haina maana haimhusu Mume na kama mume kazi yake ni shambani haina maana haimuhusu Mke.

Basi ndio maana huwa unajichanganya kwani ndoa unayozungumzia wewe ni zile za zama za kale sana ambapo mwanamke alikuwa anaolewa kuwa ni mashine ya kumzalia mwanaume, kufanya kazi za ndani na kumpa usingizi. Unaishi zama za ndoa za ubabe ubabe, kutegeana na kunyonyana. Unaishi enzi za ndoa za wake magolikipa, wasio na elimu wala mchango wowote wa maana kiuchumi katika familia. Unaishi enzi zile ambapo prenuptual agreement wasn't an option.

Zama hizi ni za Gender Equity. Zama hizi ni za barrack na michelle, ni za Hillary na Bill, sio za Ali na Siti.

Isitoshe, katika ndoa ya mume na mke, kuna mamlaka tatu - ya kwanza ni ile ya mke na mume na watoto wao, ya pili ni ile ya wazazi na ukoo wa mume na ya tatu ni ile ya wazazi na ukoo wa mke. Siku ya harusi/muungano au siku ya kutafuta suluhu ya kero za muungano ndio utajua mipaka ya mamlaka hizi tatu.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Basi ndio maana huwa unajichanganya kwani ndoa unayozungumzia wewe ni zile za zama za kale sana ambapo mwanamke alikuwa anaolewa kuwa ni mashine ya kumzalia mwanaume, kufanya kazi za ndani na kumpa usingizi. Unaishi zama za ndoa za ubabe ubabe, kutegeana na kunyonyana. Unaishi enzi za ndoa za wake magolikipa, wasio na elimu wala mchango wowote wa maana kiuchumi katika familia. Unaishi enzi zile ambapo prenuptual agreement wasn't an option.

Zama hizi ni za Gender Equity. Zama hizi ni za barrack na michelle, ni za Hillary na Bill, sio za Ali na Siti.

Isitoshe, katika ndoa ya mume na mke, kuna mamlaka tatu - ya kwanza ni ile ya mke na mume na watoto wao, ya pili ni ile ya wazazi na ukoo wa mume na ya tatu ni ile ya wazazi na ukoo wa mke. Siku ya harusi/muungano au siku ya kutafuta suluhu ya kero za muungano ndio utajua mipaka ya mamlaka hizi tatu.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Mkuu wangu unajua unanichekesha sana maana ninachopinga mimi na ktk mifano yangu ni jinsi Tanganyika inavyowafanya Zanzibar kama mke wa kukaa ndani (housewife). Ni mfumo uu ninao ukemea kila wakati iwe ndani ya S1,S2 au S3 ila maadam hapa swla ni kuhusu S2 na S3, nyie mnafikiri naipinga S3, hivyo lazima naiunga mkono S2. Mkuu hizi serikali zote sioni tofauti yake , watu wale wale ikiwa mfumo wa Kiutawala utabakia vile vile..Ni hii tabia ya bwana ambayo inamweka chini mwanamke (msome Nguruvi3 vizuri utaona kila kosa ni upande wa pili). Bwana anayetaka ajulikane kuwa ndani ya nyumba bwana ni nani na mke hana mpango.. Hii tabia ndio tunatakiwa kuikemea na sii kuitazama upya ndoa yenyewe.

Ni nyie mnaoitunuku Tanganyika na CCM kwa ubabe wake kwa kutoamini kwamba wanayoyafanya sii kinyume ila ni haki yao kwa sababu Tanganyika ndio bwana anayeilisha Zanzibar, hao Zanzibar hawana kitu kazi yao kulalamika na kadhalika, haya ni sawa na matusi ya wanaume watindiga ambao hawajui umuhimu wa mke ndani ya nyumba na kwamba mke ni Partner ktk Ndoa sii Kijakazi. Malalamishi yenu makubwa ni pale mnapoona mke kachukua jukumu la bwana, hivyomnajiuliza bwana nani ndani ya nyumba? i majukumu yapio hay? oooh mke gani huyu amekaa kiti cha bwana!

Ni katika fikra hizi ndio mimi nasimamia ya kwamba tatizo ni jinsi Mume anavyo m treat mke wake na sii ndoa ya Mkeka ama ndoa ya kanisani hivyo tufuate maadili ya Kiislaam ruksa kuoa wake zaidi ya mmoja itaondoa kero na matatizo ya huyu mke mmoja na sii yake bwana maana hana tatizoAma kufikiri kusaini upya prenuptial Agreement ku define upya ndoa ili kila Mtu awe na mali zake na isomeke wazi kuwa hati ya nyumba ni ya Yussuph na sii Mr and Mrs. Ila wakutane kitandani kama mume na mke kwa mambo ya Kindoa maana mnaamini kuwa ndoa maana yake ni uzazi tu! hakuna jingine laa sivyo msingeoa abadan mkitishia mnaweza kuishi masela vile vile. Haya madini na gas inawazuzua sana Tanganyika.
 
Nzi , hayo unayosema ni sehemu ya vitimbwi vya huu muungano. Nadhani umesoma katika mjadala unaohusu nchi kuwa na Amir Jeshi wakuu wawili, Kikwete na Sheni wakipokezana majukumu.


Nimeusoma sana chifu. Na kwa kweli inakanganya!

Tangazo zililihusu Watanganyika kama JMT na siyo znz.

Sasa watanganyika si hawapo? Kwanini 'utanganyika' ujifiche ndani ya 'ujamhuri wa Muungano'? Ni heri Tanganyika iwe wazi, na kila upande ufanye mambo yake, ili kuondoa mikanganyiko kama hii.
 
Katika swala hili, mkuu wangu hata kama tungekuwa na serikali 3 bado mishahara ingekuwa vile vile Zanzibar wakitangaza yao na Bara tukitangaza yetu. Nachoweza kusema mimi ni kwamba Mishahara alotangaza JK ni kwa serikali ya JMT hivyo watumishi wote waloajiliwa kupitia serikali kuu JMT ndio wamelengwa hivyo serikali ya Zanzibar haihusiki na kwa maana ile ile viongozi wa Bara wametumia tena JMT kupandishwa mishahara. Na sidhani kama TUKTA wanahusika Zanzibar ama wanapodai mishahara huzungumzia pia watumishi wa Umma wa Zanzibar.

Nyekundu: Chifu, huoni kama ikiwa hivyo ulivyoandika, inakuwa heri na vyema? Hiyo itaondoa mikangayiko kama hiyo ya Rais wa JMT kutoa tangazo ambalo halina mashika katika mshirika wa Jamhuri!! La sivyo, ina maana Rais huyo wa JMT, pia kwa namna moja ama nyingine ni Rais wa mshirika mwanachama mwingine wa Jamhuri, mwanachama 'aliyejificha'.

Bluu:Chifu, unazidi kunichanganya!! Watumishi wote walioajiriwa kupitia serikali kuu ya JMT?!? Sasa, si nasikia suala la fedha ni la 'Muungano'? Kama ndivyo, basi suala la mishahara linapaswa kuwa la 'Muungano' ama sivyo? Vilevile, mtumishi wa wizara ya fedha pale Zanzibar, tamko lile la Rais wa JMT halitamhusu? Maana yeye kaajiriwa na SMZ na vile vile anahusika na suala la 'Muungano'!! Dang it! Viongozi gani tena wa Bara? Hiyo 'Bara' ndiyo mwanachama mwingine wa Jamhuri ama? Mbona nazidi kuchanganyikiwa!!

Katika mkanganyiko huu ndio huleta kero za Muungano na sidhani kama kuwepo kwa Tanganyika tunaweza kuondosha hili maana akitangaza JK kupanda kwa mishahara sijui atakuwa na maana gani ambayo leo hii haiwezi kutumika vile vile. Mnachotaka kusiia ni kwamba hata Zanmzibar nao mishahara imepanda sawa na bara. Lakini ukitazama huku majuu mishahara kati ya nchi za muungano huwa hazifanani na hii hutokana na mfumko wa bei (soko huria).

Nyekundu: Chifu, naamini kama kungekuwepo na Serikali ya Tanganyika na kiongozi wake, basi huu mkanganyiko husingetokea. Kwani, kiongozi huyo angesema wazi kabisa kwamba, wafanyakazi wote wa Tanganyika mishahara yao itapanda. Na ninaanza kuhisi kuwa pengine yule waziri wa fedha wa SMZ aliamua kusema kwamba hakutakuwa na ongezeko la mishahara Zanzibar ili kuweka jambo hilo wazi, pengine wafanyakazi wa SMZ (ambayo ni mwanachama wa JMT) walifurahia kauli ya Rais wao wa JMT!

Bluu:Chifu, huko majuu (Canada? US?), nchi zilizoungana si ziko wazi aisee? Sasa hapa nchi za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni SMZ na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania!! Sijui nimeandika sawa, maana nahisi nimeshachanganyikiwa tena!

Unaweza kuta Ontario mshahara wa chini ni dollar 11, Quebec dollar 9, Alberta dollar 16 na kadhalika (mifano). Yote hii inatokana na ugumu wa maisha kwa sehemu husika. Hivyo yoote hayayanawachanganya ni kutokana na sisi kutobadilisha mfumo wa Utawala na kiuchumi ambao bado serikali kuu ndio hutangaza mishahara ya taifa wakati JUWATA imeshakufa kifo cha nyani ikilenga Bara kwenyea TUKTA. Badala ya kila nchi, kila jimbo hadi vijijini kuwa na mishahara yake kulingana na hali ya maisha ya sehemu izo.

Chifu, hapo juu nadhani umezungumzia suala la kiutendaji ambalo linaweza kumalizika kama wanachama wa Muungano wetu huu wakitambulika na kujulikana bayana na kiuhalisia!! Vilevile, hayo uliyoyasema si ni majimbo yenye mamlaka kamili ama? Ina maana yana mamlaka ya kuamua mishahara kwa watumishi wake.. Kwa hali ya JMT, mwenye kuamua mishahara si Rais wa JMT ama? Sasa kama ndiyo, inakuwaje mwanachama wa JMT apingane na kiongozi wake mkuu?

Mtumishi wa Umma wa Lindi haiwezekani akapokea mshahara sawa na mtumishi wa Dar kwa sababu hali ya maisha baina ya mikoa hiyo hailingani kabisa. Uuwiano tunaozidi kuutumia ni asili ya mfumo wa Utawala wa Kisoshalist.

Chifu, naamini kuwa hata pale Texas (kama nchi mshirika wa USA), mtumishi wa umma aliyepo Houston, San Antonio na Dallas, mishahara yao haiwezi kutofautiana (naweza sahihishwa kama nimekosea). Si nchi moja bwana ama? Sasa ukitaka iwe unavyosema, ni kuamua Lindi, DSM n.k. ziwe na sehemu zenye mamlaka kamili kwa mfumo wa serikali za majimbo. Ziwe na serikali ambazo zinaweza kuamua mishahara ya watumishi wake. Jambo ambalo ndilo hilo nalisema kwamba, wanachama wa JMT watambulike bayana, ili kila mwanachama kupitia serikali yake, aamue mishahara ya watumishi wake.

Ama nimekosema chifu wangu?
 
Nyekundu: Chifu, huoni kama ikiwa hivyo ulivyoandika, inakuwa heri na vyema? Hiyo itaondoa mikangayiko kama hiyo ya Rais wa JMT kutoa tangazo ambalo halina mashika katika mshirika wa Jamhuri!! La sivyo, ina maana Rais huyo wa JMT, pia kwa namna moja ama nyingine ni Rais wa mshirika mwanachama mwingine wa Jamhuri, mwanachama 'aliyejificha'.

Bluu:Chifu, unazidi kunichanganya!! Watumishi wote walioajiriwa kupitia serikali kuu ya JMT?!? Sasa, si nasikia suala la fedha ni la 'Muungano'? Kama ndivyo, basi suala la mishahara linapaswa kuwa la 'Muungano' ama sivyo? Vilevile, mtumishi wa wizara ya fedha pale Zanzibar, tamko lile la Rais wa JMT halitamhusu? Maana yeye kaajiriwa na SMZ na vile vile anahusika na suala la 'Muungano'!! Dang it! Viongozi gani tena wa Bara? Hiyo 'Bara' ndiyo mwanachama mwingine wa Jamhuri ama? Mbona nazidi kuchanganyikiwa!!



Nyekundu: Chifu, naamini kama kungekuwepo na Serikali ya Tanganyika na kiongozi wake, basi huu mkanganyiko husingetokea. Kwani, kiongozi huyo angesema wazi kabisa kwamba, wafanyakazi wote wa Tanganyika mishahara yao itapanda. Na ninaanza kuhisi kuwa pengine yule waziri wa fedha wa SMZ aliamua kusema kwamba hakutakuwa na ongezeko la mishahara Zanzibar ili kuweka jambo hilo wazi, pengine wafanyakazi wa SMZ (ambayo ni mwanachama wa JMT) walifurahia kauli ya Rais wao wa JMT!

Bluu:Chifu, huko majuu (Canada? US?), nchi zilizoungana si ziko wazi aisee? Sasa hapa nchi za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni SMZ na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania!! Sijui nimeandika sawa, maana nahisi nimeshachanganyikiwa tena!



Chifu, hapo juu nadhani umezungumzia suala la kiutendaji ambalo linaweza kumalizika kama wanachama wa Muungano wetu huu wakitambulika na kujulikana bayana na kiuhalisia!! Vilevile, hayo uliyoyasema si ni majimbo yenye mamlaka kamili ama? Ina maana yana mamlaka ya kuamua mishahara kwa watumishi wake.. Kwa hali ya JMT, mwenye kuamua mishahara si Rais wa JMT ama? Sasa kama ndiyo, inakuwaje mwanachama wa JMT apingane na kiongozi wake mkuu?



Chifu, naamini kuwa hata pale Texas (kama nchi mshirika wa USA), mtumishi wa umma aliyepo Houston, San Antonio na Dallas, mishahara yao haiwezi kutofautiana (naweza sahihishwa kama nimekosea). Si nchi moja bwana ama? Sasa ukitaka iwe unavyosema, ni kuamua Lindi, DSM n.k. ziwe na sehemu zenye mamlaka kamili kwa mfumo wa serikali za majimbo. Ziwe na serikali ambazo zinaweza kuamua mishahara ya watumishi wake. Jambo ambalo ndilo hilo nalisema kwamba, wanachama wa JMT watambulike bayana, ili kila mwanachama kupitia serikali yake, aamue mishahara ya watumishi wake.

Ama nimekosema chifu wangu?
Hikanganyi kama utajaribu kuelewa kwamba Tanganyika ipo ndani ya JMT na hivyo ka kila jambo lisilokuwa la Muungano ina maana Rais atasimamia maslahi ya Bara. Hivyo badala ya kuwa na marais wawili wa bara na JMT tunae mmoja. Wakati wa Mwalimu Rais alipokea mshahara mdogo sana tofauti na huyu wa soko huria na utandawazi, na hata watumishi wa Umma walipewa mishahara midogo sana ukilinganisha na hawa wa leo hivyo kulikuwa na asilimia ndogo sana ya mapishano baina ya Kiongozi wa serikali na Mtumishi wa Umma.

Kusema kweli mimi nawashangaa nyie maana ikiwa unaelewa kwamba tunalo bunge la Taifa ambalo majadiliano mengi (@Nguruvi3 asema asilimia 95) yanahusu Tanganyika na huko Zanzibar wanalo bunge lao kwa asilimia 100 linalojadili maswala yake inakuwaje tunashangaa kuona haya wakati JK hufungua Bunge la JMT lakini sio la Zanzibar!.

Tuna wabunge wa kutoka Zanzibar ktk bunge la JMT wakati huo huo Zanzibar ina wabunge wake ktk baraza lao. Tuna mawaziri na manaibu Wazanzibar ktk serikali kuu mambo ya muunano, tunao watumishi wa Umma Wazanzibar ndani ya wizara mambo ya Muungano, wapo Watanganyika vile vile Zanzibar ktk serikali ya mambo ya Muungano. Na sidhani kama ipo siku mwanancjhi wa Zanzibar kawahi kushika madaraka ya mambo yasokuwa ya Muungano. Cha ajabu kipi hapa kama sii mfumo mbaya sana wa kuwa na haya mambo ya Muungano na yasiyokuwa na Muungano!

Nachosema mimi kuwepo kwa Tanganyika bado wizara zisizokuwa za muungano zitakuwepo na hiyo wizara ya fedha itakuwa ya Muunganpo lakini bado Tanganyika tutakuwa na mishahara yetu na Zanmzibar mishahara yao haijalishi nani katangaza. tatizo lenu kubwa ni Ubwana yaani mnataka kujua bwana hapa ni nani?Lakini Znz wameisha jitangazia kuwa wao ni nchi na watapanga mishahara yao kulingana na makali ya maisha (mfumko wa bei) hivyo swala hapa sio wizara ya Fedha bali mishahara ya watumishi wa Umma hutokana na kodi za wananchi. Hivyo la kujiuliza hapa ni kwamba zile kodi za wananchi wa Zanzibar hukusanywa na kupelekwa wapi?

Bado utagundua kwamba kinachofanyika hapa ni mfumo wa Kijamaa ambao tumeutumia kwa miaka 30 pasipo kuubadilisha ili uweze kwenda na wakati na sii serikali ngapi. Katika utekelezaji wa shughuli za serikali nchi za wenzetu, nchi huwa na mishahara yake, sio rais anayetangaza mishahara ila kiongozi wa nchi mwanachama. Na mara zote sii rahisi kwa Taifa zima kudai ongezeko la mishahara ila utayakuta ktk nchi za Kijamaa kama Cuba na Korea Kaskazini!

Jambo pekee linaloweza kuihusisha serikali kuu ktk ulimwengu huu ni pale kumekuwa na depression, uchumi umebwaya, ikatokea kukosekana ama mapungufu ya Ajira kwa wananchi wote na sii mishahara ya watumishi ambao wanategemea zaidi kodi kutoka private sectors. Hivyo kutangaza kwa JK mishahara ya wafanyakazi ni dalili nyingine ya kuwaonyesha kwamba bado tunafuata siasa ya Kijamaa utadhani JUWATA bado ipo kuwatetea wafanyakazi wote nchini. Hiyo TuKTA yenyewe ina wananchi watumishi wa Umma na wengine toka private sector, utadhani ni Union -Wapi na wapi?

Swala la kuwepo Tanganyika.
Hivi kweli kama wewe unaamini 2+3=5, lakini mtu akikupa 2+?=5 itakuwa kaficha jambo ili wewe usijue kilichofichwa ktk alama hiyo? Mimi sioni sababu kabsia ya mtu aandike 2+3 =5 ikiwa tunajua tunaweza kutoa 5-2 =3, hivyo hiyo alama ilofichwa ni sawa na 3 japo haikuandikwa kama 3 maana imeandikwa 5 na mshirika mwingine anachangia 2. Hivyo tatizo hapa sio kufichwa kwa 3 ila hizo jumla ya 5 zimetumikaje, na wanaozitumia vibaya watawajibikaje na zipi njia za kuwakomesha hao watu wasiendelee kumeza hizo 5 kwa jina la JMT. Hii ndio katiba ninayoiomba mimi ili tuachane kabisa na siasa za Ujamaa kama mwongozo wa Taifa, ibakie kuwa itikadi ya chama chao kisha wananchi wataweza kuwapima..

Sina uhakika na unachosema hapa maana Houston, San Antonio na Dallas ni miji tu ndani ya state moja kama vile Ilala, Temeke na Kinondoni kuwepo mkoa (jimbo) wa Dar, bora hata ungesema Mwanza na Dar japo zote bado ndani ya state yetu ya Bara. Nilichozungumzia ni kuwepo tufauti ya mishahara baina ya Texas na Ohio ama mtumishi wa umma wa serikali ya Texas (state) na mtumishi wa Umma wa Federal Government ya Obama.

Nachoelewa mimi
mtumishi wa Federal Government ana mshahara tofauti na mtumishi wa serikali ya State hata kama ni mji mmoja na sii kazi ya Obama kutangaza mishahara ya watumishi wa serikali ya Texas. Canada iko hivyo, na ndio nimekupa mifano ile maana hizo ni sawa na States zenye mamlaka ya nchi (republic) na hujipangia mishahara yao, bajeti zao na kadhalika.
 
Tuna wabunge wa kutoka Zanzibar ktk bunge la JMT wakati huo huo Zanzibar ina wabunge wake ktk baraza lao. Tuna mawaziri na manaibu Wazanzibar ktk serikali kuu mambo ya muunano, tunao watumishi wa Umma Wazanzibar ndani ya wizara mambo ya Muungano, wapo Watanganyika vile vile Zanzibar ktk serikali ya mambo ya Muungano. Na sidhani kama ipo siku mwanancjhi wa Zanzibar kawahi kushika madaraka ya mambo yasokuwa ya Muungano. Cha ajabu kipi hapa kama sii mfumo mbaya sana wa kuwa na haya mambo ya Muungano na yasiyokuwa na Muungano!
Mkuu Mkanadara suala la afya halipo katika yale 11 ya muungano wala yale ya kinymela.
Leo waziri wa Afya ni mzanzibar unataka kutuambia nini.

Leo bodi ya NECTA si ya muungano, wajumbe wa bodi ya NECTA nusu ni wznz.
Ndivyo ilivyo katika bodi zote
Hivi hawa wnajadili kitu gani kinachowahusu? Bodi zote na wizara kama afya haina masilahi kwao.

Hapa ndipo tunasema wznz wanataka muungano kwa jina ili wakitafuta ajira na manufaa mengine waingie kirahisi.
Sisi tunasema mambo 7 kama hawataki njia nyeyupee. Hatuwezi kubeba furushi la samadi tena.
 
Mkandara bwana, duh! Haijulikani anasimamia nini, anatetea nini, anapinga nini; mradi tu anajaza page after page kwa maandishi yasiyoeleweka. Lakini hapo hapo yeye ndiye anadai watu wameshindwa kumuelewa ingawa hakuna hata swali moja kati ya mengi tu aliyoulizwa ameweza kulijibu. Anataka asionekane anaunga mkono S2 lakini hapo hapo anadai S3 zitaua Muungano bila kusema katika hali ya sasa S2 zitadumishaje huo Muungano!

Akiulizwa kitu gani kifanyike kuondoa mkanganyiko uliopo baina ya hizi serikali mbili na kupunguza kama si kuondoa kabisa kero anarukia mambo ya ndoa. Akiulizwa nani wahusika wa hii ndoa anadai mume ni Tanzania na mke ni Zanzibar akisahau kwamba awali ndoa ilikuwa ni kati ya Tanganyika na Zanzibar! Kwa maana nyingine ni kwamba hawa wanandoa wawili, Tanganyika na Zanzibar, kwa pamoja wana mke, Zanzibar!...Te he he, Mkandara!

Kawaida ya ndoa, kama anavyodai Mkandara, ni mume kumtunza mke na hivyo kulazimika kumpatia huduma zote. Sasa kama ni hivyo tatizo liko wapi? Tatizo, Mkandara anatuambia, ni kwamba mume (Tanzania) aliamua kujihudumia na kusahau kuwa mkewe (Zanzibar) naye anayo mahitaji... itaendelea nikipata nafasi!
 
Mkuu wangu unajua unanichekesha sana maana ninachopinga mimi na ktk mifano yangu ni jinsi Tanganyika inavyowafanya Zanzibar kama mke wa kukaa ndani (housewife). Ni mfumo uu ninao ukemea kila wakati iwe ndani ya S1,S2 au S3 ila maadam hapa swla ni kuhusu S2 na S3, nyie mnafikiri naipinga S3, hivyo lazima naiunga mkono S2. Mkuu hizi serikali zote sioni tofauti yake , watu wale wale ikiwa mfumo wa Kiutawala utabakia vile vile..Ni hii tabia ya bwana ambayo inamweka chini mwanamke (msome
Nguruvi3 vizuri utaona kila kosa ni upande wa pili). Bwana anayetaka ajulikane kuwa ndani ya nyumba bwana ni nani na mke hana mpango.. Hii tabia ndio tunatakiwa kuikemea na sii kuitazama upya ndoa yenyewe.

Ni nyie mnaoitunuku Tanganyika na CCM kwa ubabe wake kwa kutoamini kwamba wanayoyafanya sii kinyume ila ni haki yao kwa sababu Tanganyika ndio bwana anayeilisha Zanzibar, hao Zanzibar hawana kitu kazi yao kulalamika na kadhalika, haya ni sawa na matusi ya wanaume watindiga ambao hawajui umuhimu wa mke ndani ya nyumba na kwamba mke ni Partner ktk Ndoa sii Kijakazi. Malalamishi yenu makubwa ni pale mnapoona mke kachukua jukumu la bwana, hivyomnajiuliza bwana nani ndani ya nyumba? i majukumu yapio hay? oooh mke gani huyu amekaa kiti cha bwana!

Ni katika fikra hizi ndio mimi nasimamia ya kwamba tatizo ni jinsi Mume anavyo m treat mke wake na sii ndoa ya Mkeka ama ndoa ya kanisani hivyo tufuate maadili ya Kiislaam ruksa kuoa wake zaidi ya mmoja itaondoa kero na matatizo ya huyu mke mmoja na sii yake bwana maana hana tatizoAma kufikiri kusaini upya prenuptial Agreement ku define upya ndoa ili kila Mtu awe na mali zake na isomeke wazi kuwa hati ya nyumba ni ya Yussuph na sii Mr and Mrs. Ila wakutane kitandani kama mume na mke kwa mambo ya Kindoa maana mnaamini kuwa ndoa maana yake ni uzazi tu! hakuna jingine laa sivyo msingeoa abadan mkitishia mnaweza kuishi masela vile vile. Haya madini na gas inawazuzua sana Tanganyika.
Hapanaaa! Ninaangalia pande zote.

Nimeonyesha wznz hawapati misaada na mikopo kutoka Washington, wanapata kutoka Dar es Salaam.

Nimeonyesha wazi kila jambo la muungano ni kuwaonea wznz kwasababu wana yao. Njia muafaka ni kuondoa na tubaki na 7 na kama hayo hawaridhiki nayo Njia nyeupee waondoke zao.

Nimeonyesha kuwa kodi za TRA za Zanzibar zinabaki huko, nikaonyesha upande wa pili unapeleka kodi Unguja na Pemba.

Nimeonyesha wznz wanavyonufaika na jina Tanzania, nikaonyesha Watanganyika wanavyo nyanyaswa kwa jina la znz.

Hivi mkuu unataka tuongelee pande mbili zipi? Pande mbili za hadithi au uchumi. Mmoja atoe 100 na mwingine achangie maneno halafu tuseme tunacha kuongelea hapo.

Tuongelee nini wakati watoto wetu wanamnyimwa nafasi kwasababu tu kuna mznz ana qualification za uznz na Div IV.

Tuongelee nini wakati kuna watalii 81 wanakuja Dodoma kupiga soka ili hali hakuna mtalii anyekwenda BLW kuzogoa.

Tuongelee nini ili hali kuna mtu na wajukuu hajui bei ya umeme, ili hali deni lake anatwisha mluguru asiyejua hata znz ipo upande gani.

Mkandara, hata ujenge hoja namna gani ukweli unabaki kuwa Tanganyika imeibeba znz na mzigo huo ni kodi ya mvuvi, mfanyakazi na mkulima wa Tanganyika.
Je, investment hiyo inalipa nini? Mkandara hana jibu.

Ukweli utabaki kuwa choyo, ubinafsi na kiburi cha hovyo cha wznz ndio kero za muungano.
Hivi kweli watu 50 wanaweza kukaa mahali na kuamua tujenge wodi Muhimbili au la!
kuna akili hapo.

Si hawa walisikia kuna mapipa 200 ya mafuta, wakakimbia kuondoa katika mambo ya muungano. Leo unataka uniambie mznz akichanua kiuchumi atamjali Mtanganyika kweli.
Hawa wznz na ubinafsi wao.

Tuwaeleze ukweli tusiwaogope jamani, wanatuhitaji na hivyo wanapaswa kuwa na discipline.Period.

Mkandara, tunahitaji Tanganyika tuachane na ugomvi usio na maana.
Hili tatizo lipo miaka 50 na halina jibu.

Huo mfumo wa S2 unaopendekeza hauna majibu.
CCM wamesambaa nchi nzima, hakuna hata mmoja anayeeleza suluhu ya kero na anatatua vipi Kero.
Haiwezekani chama chenye majibu kizunguke nchini kumjadili Lissu.
Hizo ni dalili za kutokuwa na majibu.

Mimi nasema ni vema mambo yakaishia mezani, yakilazimishwa huko mtaani hakufai.
Wananchi wamechoka kuona wanalipa kodi zinakwenda nchi jirani ya znz.

Tunataka Tanganyika ili tupange mipango yetu. Hii habari ya kutaka kujenga vyoo vya shule zetu eti twende tukaulize watu 50 wa BLW kama wanakubali au la ni kuuza uhuru. Ni utumwa huu na wendawazimu

Habari ya kubeba gharama za muungano kwa ujira wa matusi na kashfa sasa basi, tugawane kwa kila mmoja kuchangia alicho nacho, haiwezekani tuvunje jahazi.

Hii habari ya kulipa watu 81 bilioni 9.6 kwa mwaka sawa na pesa za maendeleo za mkoa wa K'njaro basi. Watalii wanaleta pesa, hawa wznz wanachukua.

Tunasema kodi zetu ziamue hatima yetu na ni dhalili watu 50 wa BLW kukaa na kuamua tufanye nini na kodi zetu.
 
Mkuu Mkanadara suala la afya halipo katika yale 11 ya muungano wala yale ya kinymela.
Leo waziri wa Afya ni mzanzibar unataka kutuambia nini.

Leo bodi ya NECTA si ya muungano, wajumbe wa bodi ya NECTA nusu ni wznz.
Ndivyo ilivyo katika bodi zote
Hivi hawa wnajadili kitu gani kinachowahusu? Bodi zote na wizara kama afya haina masilahi kwao.

Hapa ndipo tunasema wznz wanataka muungano kwa jina ili wakitafuta ajira na manufaa mengine waingie kirahisi.
Sisi tunasema mambo 7 kama hawataki njia nyeyupee. Hatuwezi kubeba furushi la samadi tena.
Sasa hii ndio hofu yangu kubwa sana ya Muungano huu na mtazamo wa Mranganyika kama wewe mwenye kuelewa taffsiri moja tu ya Ukabila. Ebu nifahamishe vizuri, huyu hivi Rashid ni mkazi wa wapi na mbunge wa jimbo gani kwanza! Sasa kweli nyie mnaotaka serikali 3, kesho mkipewa sii mtanfukuza mbunge huyu na kina Baklhresa wataitwa Wazanzibar warudi kwao ama!

Ebu jifunze kwanza kitu kimoja, tazama huko USA au Canada hakuna watu wenye asili ya jimbo jingine wanaoitumikia serikali kama watumishi wa Umma? Hivi sisi tumeungana kwa sababu zipi haswa maana unatisha kuanza kuitafuta asili badala ya Ukazi wa mtu.

Mkuu napotumia hili neno Mzanzibar ktk mjadala huu ni muhimu uelewe tunazungumzia watu wanaoishi sehemu (nchi) hiyo kama tulivyopendekeza ktk katiba hii mpya kuwa kila Mbunge lazima awe mkazi wa jimbo analogombea, hii haina maana mtu huo lazima awe ni wa makabila ya pale. Mkuu wangu hata hiyo serikali ya Zanzibar, wapo wengi wenye asili ya Bara ila sii wakazi tena wa Bara. Tukianza kutazama mjadala huu kwa fikra za kusema Mzanzibar ni mzawa wa Zanzibar ama mwenye asili ya Zanzibar badala ya Mkazi basi tutakuwa tunapoteza tena maana ya hata kuwepo kwa serikali 2 ama 3.

Labda nikuulize hivi Kwa nini watu kama sisi Diaspora mnatuita sio Raia wa Tanzania japo tuna asili ya hapa? Na inakuwaje sisi mnatuita Wa Canadian..Mimi nilikuwa nikiishi Montreal, Quebec na nikapewa karatasi za kuihsi Quebec nikaitwa Mquebec. Nikafanya kazi nalipa kodi za Quebec, ktk hali hiyo Quebec walifaidika na asilimia 5 ya kodi yangu wakati huo huo Canada wakifaidika na asilimia 7. Nilipohamia Toronto, Ontario kama mkazi na raia nilianza kulipa kodi kwa serikali ya Ontario kama mkazi wa Ontario na hivyo Ontario Kufaidika na kodi yangu sio Quebec tena. record zangu zote zikahamishiwa Ontario. Kwao wao haijalishi wewe una asili ya wapi isipokuwa wewe unatumikia serikali gani? na hivyo unakuta Mchina, Mspanish Mghana na Mimi sote tunaitwa Wana Ontario na tunajivunia kuwa kitu kimoja.

Mkuu unaizidisha hofu yangu ktk swala la serikali 3 na ndio maana naomba saana swala hili liondolewe ktk mjadala wa katiba mpya kwa sababu watu wengi wanafikiria kama wewe. Kesho mimi Mkerewe nitaambiwa nirudi kwetu Dar sii mahala pangu na siruhusiwi kuitumikia manispaa ya Dar.
 
Sasa hii ndio hofu yangu kubwa sana ya Muungano huu na mtazamo wa Mranganyika kama wewe mwenye kuelewa taffsiri moja tu ya Ukabila. Ebu nifahamishe vizuri, huyu hivi Rashid ni mkazi wa wapi na mbunge wa jimbo gani kwanza! Sasa kweli nyie mnaotaka serikali 3, kesho mkipewa sii mtanfukuza mbunge huyu na kina Baklhresa wataitwa Wazanzibar warudi kwao ama!

Ebu jifunze kwanza kitu kimoja, tazama huko USA au Canada hakuna watu wenye asili ya jimbo jingine wanaoitumikia serikali kama watumishi wa Umma? Hivi sisi tumeungana kwa sababu zipi haswa maana unatisha kuanza kuitafuta asili badala ya Ukazi wa mtu.

Mkuu napotumia hili neno Mzanzibar ktk mjadala huu ni muhimu uelewe tunazungumzia watu wanaoishi sehemu (nchi) hiyo kama tulivyopendekeza ktk katiba hii mpya kuwa kila Mbunge lazima awe mkazi wa jimbo analogombea, hii haina maana mtu huo lazima awe ni wa makabila ya pale. Mkuu wangu hata hiyo serikali ya Zanzibar, wapo wengi wenye asili ya Bara ila sii wakazi tena wa Bara. Tukianza kutazama mjadala huu kwa fikra za kusema Mzanzibar ni mzawa wa Zanzibar ama mwenye asili ya Zanzibar badala ya Mkazi basi tutakuwa tunapoteza tena maana ya hata kuwepo kwa serikali 2 ama 3.

Labda nikuulize hivi Kwa nini watu kama sisi Diaspora mnatuita sio Raia wa Tanzania japo tuna asili ya hapa? Na inakuwaje sisi mnatuita Wa Canadian..Mimi nilikuwa nikiishi Montreal, Quebec na nikapewa karatasi za kuihsi Quebec nikaitwa Mquebec. Nikafanya kazi nalipa kodi za Quebec, ktk hali hiyo Quebec walifaidika na asilimia 5 ya kodi yangu wakati huo huo Canada wakifaidika na asilimia 7. Nilipohamia Toronto, Ontario kama mkazi na raia nilianza kulipa kodi kwa serikali ya Ontario kama mkazi wa Ontario na hivyo Ontario Kufaidika na kodi yangu sio Quebec tena. record zangu zote zikahamishiwa Ontario. Kwao wao haijalishi wewe una asili ya wapi isipokuwa wewe unatumikia serikali gani? na hivyo unakuta Mchina, Mspanish Mghana na Mimi sote tunaitwa Wana Ontario na tunajivunia kuwa kitu kimoja.

Mkuu unaizidisha hofu yangu ktk swala la serikali 3 na ndio maana naomba saana swala hili liondolewe ktk mjadala wa katiba mpya kwa sababu watu wengi wanafikiria kama wewe. Kesho mimi Mkerewe nitaambiwa nirudi kwetu Dar sii mahala pangu na siruhusiwi kuitumikia manispaa ya Dar.
Mkuu unazungumzia Canada watu wa TAIFA moja. Sisi si watu wa taifa moja, narudia sisi si taifa moja.

Pili, ukienda Quebec unagombea uongozi, ukienda znz huna nafasi wewe ni Mtanganyika.

Tatu, mznz akija Tanzania kama waziri wa afya ni Mtazanzani, yupi waziri mtanganyika znz. Kama hata kuishi unahitaji kibali kuna muungano hapo.

Wewe unaleta hoja halfu unapiga kona. Hoja kubwa ilikuwa kama yupo mznz mwenye madaraka Tanganyika. Tukakwambia waziri afya isiyo mhusu mznz sasa unaleta habari za kuhama n.k.

Katiba ya znz 2010 inambagua Mtanganyika, imeshavunja muungano hili lazima ukubali hata kama unagoma.
Hakuna muungano kwa kuanzia kuna kitu kama muungano.

Ndiyo maan tunasema we don't need usumbufu wa znz, kama hawataki kuishi kwa amani na adabu njia nyeupe.
Mezani tutajadiliana mambo 7, mtaaniitakuwa hadithi nyingine kabisa.

Hakuna muungano na wala znz haina manufaa yoyote kwa Mtanganyika.Period.
S2 zimeshindwa kulinda muungano JK akivunja katiba halafu leo unalinganisha na Canada.

Mkuu ukileta hoja uwe na mahali pa kuismamia, sio ulete hoja halafu ukate kona bila indicator.
 
Mkuu unazungumzia Canada watu wa TAIFA moja. Sisi si watu wa taifa moja, narudia sisi si taifa moja.

Pili, ukienda Quebec unagombea uongozi, ukienda znz huna nafasi wewe ni Mtanganyika.

Tatu, mznz akija Tanzania kama waziri wa afya ni Mtazanzani, yupi waziri mtanganyika znz. Kama hata kuishi unahitaji kibali kuna muungano hapo.

Wewe unaleta hoja halfu unapiga kona. Hoja kubwa ilikuwa kama yupo mznz mwenye madaraka Tanganyika. Tukakwambia waziri afya isiyo mhusu mznz sasa unaleta habari za kuhama n.k.

Katiba ya znz 2010 inambagua Mtanganyika, imeshavunja muungano hili lazima ukubali hata kama unagoma.
Hakuna muungano kwa kuanzia kuna kitu kama muungano.

Ndiyo maan tunasema we don't need usumbufu wa znz, kama hawataki kuishi kwa amani na adabu njia nyeupe.
Mezani tutajadiliana mambo 7, mtaaniitakuwa hadithi nyingine kabisa.

Hakuna muungano na wala znz haina manufaa yoyote kwa Mtanganyika.Period.
S2 zimeshindwa kulinda muungano JK akivunja katiba halafu leo unalinganisha na Canada.

Mkuu ukileta hoja uwe na mahali pa kuismamia, sio ulete hoja halafu ukate kona bila indicator.
Huwezi kwenda Quebec kugombea Uongozi wa serikali ya Quebec kama wewe sii Mkazi wa Quebec. Vivyo hivyo ktk majimbo mengine ila unaweza kuwa kiongozi ktk serikali kuu inayounganisha majimbo yote na kwa mambo yote ni ya Muungano, isipokuwa kila mmoja wenu atakuwa ktk nafasi yake ya kazi, mahala pake na kadhalika. Mkuu ndio maana nasema nyie mnataka muundo wa S3 wakati hamjui muundo huo ni utawala wa aina gani na unaendeshaje shughuli zake ili wapate kufanikiwa.

Ndani ya serikali ya Zanzibar kuna viongozi kibao wenye asili ya Bara yaani Watanganyika lakini maadam ni wakati wa Zanzibar wanahesabuiwa kama Wazanzibar. Na huku bara wapo Wazanzibar wanaoishi Bara na wanahesabiwa kama Watanganyika kwani muungano wetu umetokana na WATU na sii Karume au Nyerere hawa wamewezesha tu kuwepo kwa Muungano wa nchi. Udugu wetu umekuwepo toka karne ya kwanza..

Na ndio sababu kubwa mimi napingana na rasimu kwa sababu inachofanya ni kugawa nchi sehemu 3 lakini bado inaendeleza ya S2. Kama vile mkoa wa Arusha unaugawa na kuwa Kuunda Manyara. Hatua hiyo haibaidlishi kitu zaidi ya kuongeza wakuu wa mkoa, wilaya na kadhalika! pia kuwapa nafasi viongozi mafisadi nafasi zaidi ya kufisadi.
 
Huwezi kwenda Quebec kugombea Uongozi wa serikali ya Quebec kama wewe sii Mkazi wa Quebec. Vivyo hivyo ktk majimbo mengine ila unaweza kuwa kiongozi ktk serikali kuu inayounganisha majimbo yote na kwa mambo yote ni ya Muungano, isipokuwa kila mmoja wenu atakuwa ktk nafasi yake ya kazi, mahala pake na kadhalika. Mkuu ndio maana nasema nyie mnataka muundo wa S3 wakati hamjui muundo huo ni utawala wa aina gani na unaendeshaje shughuli zake ili wapate kufanikiwa.

Ndani ya serikali ya Zanzibar kuna viongozi kibao wenye asili ya Bara yaani Watanganyika lakini maadam ni wakati wa Zanzibar wanahesabuiwa kama Wazanzibar. Na huku bara wapo Wazanzibar wanaoishi Bara na wanahesabiwa kama Watanganyika kwani muungano wetu umetokana na WATU na sii Karume au Nyerere hawa wamewezesha tu kuwepo kwa Muungano wa nchi. Udugu wetu umekuwepo toka karne ya kwanza..

Na ndio sababu kubwa mimi napingana na rasimu kwa sababu inachofanya ni kugawa nchi sehemu 3 lakini bado inaendeleza ya S2. Kama vile mkoa wa Arusha unaugawa na kuwa Kuunda Manyara. Hatua hiyo haibaidlishi kitu zaidi ya kuongeza wakuu wa mkoa, wilaya na kadhalika! pia kuwapa nafasi viongozi mafisadi nafasi zaidi ya kufisadi.
Nkaubaliana na Mag3 hapo juu kuwa Mkandara haeleweki ingawa anashangaa kwanini hatumwelewi.

Mkuu kwanza ukaazi wa Quebec au majimbo mengine sijui unazungumziaje kisiasa.
Unaweza kuhama kutoka Ontari ukaenda Alberta na kupiga kura kama ulivyo na haki ya kuchaguliwa. Ukaazi umewekwa kwasababu za mambo kama health care, haina maana ukienda Quebec unakosa haki kama raia wa Canada.

Nadhani unajaribu sana kutumia mifano ya huko uliko pengine ukidhani hatuna ufahamu huo.

Pili, unajichanganya sana unaposema undugu wetu ni wa karne. Undugu huo upo kwa Kenya, Msumbiji na Malawi kwa uchache. Hatuna muungano lakini tunaishi vema tu bila shaka.

Zanzibar hawapaswi kumwekea Mtanganyika kitambulisho cha ukazi. Wala hawapaswi kutangaza kuwa wao ni TAIFA nje ya hili tulilo nalo. Sasa wametangaza kuwa ni nchi ikiwa na kila kitu.

Hadi hapo mkuu muungano hakuna, unachotetea ni masilahi ya znz tu.

Nikupe mfano wa juzi. ZNZ wamepewa bilioni 15 zaidi mwaka huu kwasababu ya kodi ya wafanyakazi wa muungano wanaoishi Zanzibar. Wafanyakazi hao wanalipwa na Tanganyika kwasababu znz haina mchango na wala haijachangia takribai miaka 20 sasa.

Kwa maneno mengine, fursa za wznz kuishi Tanganyika ni pamoja na ajira za mambo yasiyowahusu. Na bado tunalipa mishahara hadi mawaziri wao wasiotuhusu.
Sasa tunawazawadia pesa za ili kuwatengenezea ajira.

Wale wabunge 81 wanaolipwa na Tanganyika, znz ina mchango gani.

Labda ueleze umma, hivi Mtanganyika anafaidika na nini na muungano huu zaidi ya mzigo wa gharama. Huenda kuna kitu hatuelewi.

Znz hawataki mambo yote yawe ya muungano ndiyo maana wanayanyofoa.
Wanachotaka ni jina ili wakija wadai kwa mgongo wa Tanzania.
Unapolaumu Tanganyika hutendi haki hata kidogo.

Mambo yote unayosema ni ya muungano huko nyuma umesema ni ya kinyemela na kuwaumiza wznz. Leo unasema yote ni ya muungano!

Hapa ndipo naungana na Mag3 kuhoji kama kweli mkuu unamahali pa kusimamia au ni shoot any moving object.

Kama wznz wameondoa mambo mengi, sisi tunasema basi 7 yawe yetu.
Kama hawataki hatuna sababu za kuwazuia, tunawaacha waendelee na mipango ya TAIFA lao.

Kwani mkuu, tukivunja jahazi na kugawana mbao kuna tatizo gani kwa Tanganyika, na pili, kwa znz?
 
Last edited by a moderator:
Huwezi kwenda Quebec kugombea Uongozi wa serikali ya Quebec kama wewe sii Mkazi wa Quebec. Vivyo hivyo ktk majimbo mengine ila unaweza kuwa kiongozi ktk serikali kuu inayounganisha majimbo yote na kwa mambo yote ni ya Muungano, isipokuwa kila mmoja wenu atakuwa ktk nafasi yake ya kazi, mahala pake na kadhalika. Mkuu ndio maana nasema nyie mnataka muundo wa S3 wakati hamjui muundo huo ni utawala wa aina gani na unaendeshaje shughuli zake ili wapate kufanikiwa.

Ndani ya serikali ya Zanzibar kuna viongozi kibao wenye asili ya Bara yaani Watanganyika lakini maadam ni wakati wa Zanzibar wanahesabuiwa kama Wazanzibar. Na huku bara wapo Wazanzibar wanaoishi Bara na wanahesabiwa kama Watanganyika kwani muungano wetu umetokana na WATU na sii Karume au Nyerere hawa wamewezesha tu kuwepo kwa Muungano wa nchi. Udugu wetu umekuwepo toka karne ya kwanza..

Na ndio sababu kubwa mimi napingana na rasimu kwa sababu inachofanya ni kugawa nchi sehemu 3 lakini bado inaendeleza ya S2. Kama vile mkoa wa Arusha unaugawa na kuwa Kuunda Manyara. Hatua hiyo haibaidlishi kitu zaidi ya kuongeza wakuu wa mkoa, wilaya na kadhalika! pia kuwapa nafasi viongozi mafisadi nafasi zaidi ya kufisadi.
Mkuu kwani huo ukaazi unapatikanaje huko ? Maana huwezi kusema ukaazi bila kuwa na muda. Hebu tupe habari kidogo.
 
KIWEWE CHA RASIMU CHAZIDI KUITESA SERIKALI NA RAIS

UKAWA WAFIKIWA NA SERIKALI ILI WARUDI BUNGENI

WAJUMBE WATUMWA KUONANA NA LIPUMBA, MBOWE NA MBATIA

UKAWA WAANZA KUBABAIKA, WAFIKIRIA KURUDI KUNYWA JUISI TENA.


Wanaduru
'Taarifa zilizopo' Rais kuwafikia viongozi wa UKAWA ili kupata mufaka wa kurudi bungeni.
Jitihada za kuwatuma akina Nape ili kupotosha, ukweli ni kuwa bila wapianzani rasimu ni ya CCM na ingeweza kuandikwa Lumumba.

Taswira nje ya nchi inapoteza ung'avu wananchi wakionekana kuunga mkono UKAWA.
Wasomi na wenye weledi na ushawishi wameonekana kutoridhishwa na uhuni wa bunge.

Hali hiyo imeongeza pressure kwa serikali ambayo si tu itaonekana kushindwa kuendesha mambo ya taifa, bali pia kulitia taifa gaharama nyingi.Bajeti ya bunge la katiba haipo,'waliotoa' wanafuatilia mchakato mzima.

Serikali ilidhani ilikuwa ni tisha toto na UKAWA wangerejea baada ya muda.
Hali haionekani kutotengamaa na hilo linazidi kumweka serikali katika wakati mgumu.

Kuna taarifa za viongozi wa UKAWA kufikiwa kwenda kunya Juisi pale magogoni.
Ni mazungumzo yale yale ya kunywa juisi na kuwafariji kama ilivyozoeleka

Tunarudia ,wapinzani walipokwenda IKULU hawakuambulia chochote zaidi ya kunywa juisi ya maembe. Kuna nyakati Rais aliwapiga makofi kwa kujadiliana mamboili hali alishasaini kile walichokipinga.

Mbowe anafahamu, jumatatu akiahirisha maandamano ya kupinga ubabe ili kuonana na JK, jumatatu hiyo hiyo JK akasiani mswada uliopitishwa na wabunge 100. Mbowe aliambulia Juisi tamu sana

Kuna habari pia kuwa Mh Profesa Lipumba amekataa kuonana na rais,anaweza kufanya hivyo kupitia wawakilishi.

Duru za siasa tunapenda kuwashuri UKAWA kama ifuatavyo

1. Mbinu za kuwagawa zinaendelea hivyo lazima muwe macho.
Kitendo cha kuonana na viongozi tofauti ni dalili za kuendelea kuwagawa.
Msimamo wa uongozi ukitofautiana,ndio mwisho wa UKAWA.


2. Rais Kikwete alisema 'UKAWA' wapo likizo na ni suala la muda tu watarudi

3. Akina Nape wanapita kuwashambulia kwa kuchukua posho , kumezuka kundi la washabiki wanaotaka muende mahakamani. Kundi hili linajenga hoja dhaifu ili kumkingia kifua Rais ambaye:
a. Amewadhalilisha ninyi kuwepo likizo
b. Ameleta mtafaruku kuhusu jeshi letu
c. Ametuma mawaziri kwenda maeneo ya dini kuchoche vurugu

3. Historia haionyeshi kukutana na Rais kumewahi kubadilisha hali yoyote zaidi ya glass za juisi

4. Kitendo cha kukataa kuonana na Rais, mkitaka muonane na wawakilishi ni cha kushangaza na kutisha.

Rais atatumia mwanya kuwananga siku za baadaye akitumia wawakilishi. Hapa mtakuwa mnajikaanga kwa mafuta yenu.


NNI MKIFANYE KAMA MNGEOMBA USHAURI

1. Kwanza ni serikali na rais kuomba radhi kwa dhalili, uchochezi wa kidini na kuliingiza jeshi pasipohusika
2. Kwamba, mtarejea katika bunge la katiba kwa masharti haya
a) Rasimu ya tume ijadiliwe kama ilivyoletwa na kusainiwa na rais.
b) Maboresho ya rasimu yazingatie framework ya rasimu original
c. Uwepo usawa katika mijadala na uendeshaji wa bunge kwa kufuata kanuni na sheria
d. Kuzuia aina yoyote ya rasimu nje ya ile ya Warioba.

UKAWA wakiurudi mezani kabla ya madai,watambue wameuza ghala la silaha.
Umma utawaelewa kwa kuongea na Rais aliyesema muundo ni S2, akatishia nchi kupinduliwa na kutuma mawaziri katika makanisa kushindilia hoja za uchochezi.


UKAWA, mkienda kama mnakwenda kwenye ngoma ya mkole kumnema bibi harusi mumekwisha.
Dalili za kuanza kubabaika ni pamoja na hili la kukubali wawakilishi.

Jiandaeni kwa juisi ya maembe, kuna kila dalili mumeshaanza kubabaika.

Tusemezane

Mwigulu Nchemba Kobello Nape Nnauye Mkandara EMT Mchambuzi Alinda Ngongo Bongolander Kichuguu @J.Mnyika Anna Tibaijuka Mzee Mwanakijiji Alinda gfsonwin Mkuu wa chuo Tumaini Makene mohamed mohamed Mtoi Paul Makonda Ezekiel Maige Mag3
 
KIWEWE CHA RASIMU CHAZIDI KUITESA SERIKALI NA RAIS

UKAWA WAFIKIWA NA SERIKALI ILI WARUDI BUNGENI

WAJUMBE WATUMWA KUONANA NA lLIPUMBA, MBOWE NA MBATIA

UKAWA WAANZA KUBABAIKA, WAFIKIRIA KURUDI KUNYWA JUISI TENA.


Wanaduru
Taarifa zilizopo Rais kuwafikia viongozi wa UKAWA ili kupata mufaka wa kurudi bungeni.
Pamoja na jitihada za kuwatuma akina Nape ili kupotosha, ukweli ni kuwa bila wapianzani rasimu itakuwa ya CCM na ingeweza kuandikwa Lumumba.

Taswira nje ya nchi inapoteza ung'avu wananchi wakionekana kuunga mkono UKAWA.
Wasomi na wenye weledi na ushawishi wameonekana kutoridhishwa na uhuni wa bunge.

Hali hiyo imeongeza pressure kwa serikali ambayo si tu itaonekana kushindwa kuendesha mambo ya taifa, bali pia kulitia taifa gaharama nyingi.Bajeti ya bunge la katiba haipo na 'waliotoa' wanafuatilia mchakato mzima.

Serikali alidhani ilikuwa ni tisha toto na UKAWA wangerejea baada ya muda.
Hali haionekani kutengamaa na hilo linazidi kumweka serikali katika wakati mgumu.

Kuna taarifa za viongozi wa UKAWA kufikiwa kwenda kunya Juisi pale magogoni.
Ni mazungumzo yale yale ya kunywa juisi na kuwafariji kama ilivyozoeleka

Tunarudia , mara zote wapinzani walipokwenda IKULU hawakuambulia chochote zaidi ya kunywa juisi ya maembe. Kuna nyakati Rais aliwapiga makofi kwa kujadiliana mamboili hali alishasaini kile walichokipinga.

Mbowe anafahamu, jumatatu akiahirisha maandamano ya kupinga ubabe ili kuonana na JK, jumatatu hiyo hiyo JK akasiani mswada uliopitishwa na wabunge 100. Mbowe aliambulia Juisi tamu sana

Kuna habari pia kuwa Mh Profesa Lipumba amekataa kuonana na rais isipokuwa anaweza kufanya hivyo kupitia wawakilishi.

Duru za siasa tunapenda kuwashuri UKAWA kama ifuatavyo

1. Mbinu za kuwagawa zinaendelea hivyo lazima muwe macho.
Kitendo cha kuonana na viongozi tofauti ni dalili za kuendelea kuwagawa.
Msimamo wa Lipumba utakapotofautiana na Mbowe au Mbati, huo ndio mwisho wa UKAWA.


2. Rais Kikwete alisema 'UKAWA' wapo likizo na ni suala la muda tu watarudi

3. Akina Nape wanapita kuwashambulia kwa kuchukua posho , kumezuka kundi la washabiki wanaotaka muende mahakamani. Kundi hili linajenga hoja dhaifu ili kumkingia kifua Rais ambaye:
a. Amewadhalilisha ninyi kuwepo likizo
b. Ameleta mtafaruku kuhusu jeshi letu
c. Ametuma mawaziri kwenda maeneo ya dini kuchoche vurugu

3. Historia haionyeshi kuwa kukutana na Rais kumewahi kubadilisha hali yoyote zaidi ya glass za juisi

4. Kitendo cha ninyi kukataa kuonana na Rais lakini mkitaka muonane na wawakilishi wake ni cha kushangaza na kutisha.

Rais atatumia mwanya huo kuwananga siku za baadaye akitumia wawakilishi mlio onana nao.
Hapa mtakuwa mnajikaanga kwa mafuta yenu.


NNI MKIFANYE KAMA MNEOMBA USHAURI

1. Kwanza ni serikali na rais kuomba radhi kwa dhalili, uchochezi wa kidini na kuliingiza jeshi pasipohusika
2. Kwamba, mtarejea katika bunge la katiba kwa masharti haya
a) Rasimu ya tume ijadiliwe kama ilivyoletwa na kusainiwa na rais.
b) Maboresho ya rasimu yazingatie framework ya rasimu original
c. Uwepo usawa katika mijadala na uendeshaji wa bunge kwa kufuata kanuni na sheria
d. Kuzuia aina yoyote ya rasimu nje ya ile ya Warioba.

UKAWA wakiurudi mezani kabla ya madai,watambue wameuza ghala la silaha.
Hakuna namna umma utawaelewa kwa kuongea na Rais yule yule aliyesema muundo wa muungano ni S2. akatishia nchi kupinduliwa na jeshi na kutuma mawaziri katika makanisa kushindilia hoja za uchochezi.


UKAWA, mkienda kama mnakwenda kwenye ngoma ya mkole kumnema bibi harusi mumekwisha.
Dalili za kuanza kubabaika ni pamoja na hili la kukubali wawakilishi.

Jiandaeni kwa juisi ya maembe, kuna kila dalili mumeshaanza kubabaika.

Tusemezane

Mwigulu Nchemba Kobello Nape Nnauye Mkandara EMT Mchambuzi Alinda Ngongo Bongolander Kichuguu @J.Mnyika Anna Tibaijuka Mzee Mwanakijiji Alinda gfsonwin Mkuu wa chuo Tumaini Makene mohamed mohamed Mtoi Paul Makonda Ezekiel Maige @
Source please!
Ila siyo mbaya kama itatokea.
 
Back
Top Bottom