Ukiangalia jinsi Rais Ruto alivyopokelewa kwa heshima Marekani utashangaa

Ukiangalia jinsi Rais Ruto alivyopokelewa kwa heshima Marekani utashangaa

Tunaweza kutumia muda mwingi kuongelea hili lakini ileweke tena kuwa swala la Haiti ndiyo limesababisha uratibu wa safari hii kwa haraka haraa hivyo.
Kwanza hii siyo "safari ya haraka" kama unavyo sema wewe. Imepangwa muda kitambo sana.
Kama ulivyosema hapo, kwa upande wangu la Haiti halina uzito mkubwa katika ziara hii. Hata hili limekuwepo muda mrefu wa kutosha, lisingehitaji uharaka wa ziara.
Kama yale mazungumzo ya mkataba wa kiuchumi/biashara yangekuwa yamekamilika, labda hapo ningesema hapo ni jambo muhimu zaidi; lakini siyo Haiti.
Inashangaza kidogo jambo linalohusu swala hilo wala haligusiwi katika ziara hii. Naona AGOA mpya imeyazika hayo.
 
Mbona Nyerere alishawahi kupokelewa hivyo na nyimbo za taifa la Marekani na Tanzania zikapigwa kipindi John F. Kennedy akiwa raisi wa Marekani

Ni kawaida kupokelewa hivyo ikiwa ni mwaliko rasmi (state visit)

Vijana wengi wa bongo mna uelewa mdogo sana inapohusu diplomatic issues na geopolitcs. Mnaongozwa sana na mihemko

View attachment 2997720

View attachment 2997723
Utapeli waliotakiwa kutapeliwa wamarekani walipoushitukia , hata vazi sutico,linakataliwa nchini ikabidi kaundasuti ziaze kuvaliwa

Tazara yenyewe imechoka kuliko mchoko wenyewe
 
Subirini Yanga nayo imealikwa. Mabingwa wa ball wa mara zote Tanzania wanaenda unyamwezini kukaa kwenye kiti cha mzee baba
 
Sasa hili la (d) linaonekana dogo sana kwenye geopolitical policies za Marekani kwa Afrika, lakini kwa bahati mbaya ndilo kubwa lililosababisha ziara hii kuratibiwa haraka haraka hivyo. Biden angependa huu mgogoro wa haiti uishea hata kabla ya September. Hili la wakimbizi, ujue kuwa siyo idadi wa wakimbizi wa Haiti wanaoisumbua Marekani, bali ni ile ripple effect ya wakimbizi wanaotoka Haiti kupitia Central America. Kwa wakimbizi kumi watakaovuka bahari kutoka Haiti hadi central America huvuta wakimbizi wengine wengi kutoka central Amefrica na kuwa na Caravan kubwa kuelekea Marekani.
Umejitahidi sana kujieleza, na yote uliyoeleza yanajulikana. Ila bila kusita kabisa nabaki palepale. Ziara ya Ruto haikuwa ya kustukiza hata kidogo; hii imepangwa kiutaratibu tokea mwanzo kwa nia ile ile ya Marekani kuwa na eneo lake katika ukanda huu. Kenya haikuanza jana chini ya Ruto kuwa chini ya 'influence' ya Marekani. Kidogo Mwai Kibaki aliwastua sana wakubwa, alipogeukia Mashariki. Na kutokana na kuingia kwa China, Marekani anaona maslahi yake yanalegalega; kwa hiyo sasa ana'catch up'.
Siyo mara ya kwanza Ruto kuingia Jumba Jeupe tokea ashike madaraka. Mipango hii ilianzia hata kabla Uhuru hajaachia madaraka. Huu ni mpango endelevu, siyo wa kustukiza.
 
Mbona Nyerere alishawahi kupokelewa hivyo na nyimbo za taifa la Marekani na Tanzania zikapigwa kipindi John F. Kennedy akiwa raisi wa Marekani

Ni kawaida kupokelewa hivyo ikiwa ni mwaliko rasmi (state visit)

Vijana wengi wa bongo mna uelewa mdogo sana inapohusu diplomatic issues na geopolitcs. Mnaongozwa sana na mihemko

View attachment 2997720

View attachment 2997723
Ni kweli kuna uelewa mdogo, lakini watu wote hawawezi kuwa na uelewa mkubwa, ukitaka iwe hivyo na wewe utakuwa na uelewa mdogo. Kuna watu wanajifunza, wengine wadogo, sasa watajuaje mambo bila kujifunza?

Jana niliandika tofauti ya state visit na visits nyingine, nikaitaja hii ziara ya Nyerere, lakini sikuona haja ya kubeza watu.

Zaidi, swali la msingi liko palepale, kwa nini Kenya inashamiri sana kinataifa zaidi ya Tanzania? Kwa nini Kenya imekuwa nchi ya kwanza Afrika kupata State Visit Marekani tangu mwaka 2008, na Tanzania haipati nafasi hizi?

Kuna jibu refu la historia ya Kenya kama koloni proper la Waingereza ambalo halijapitia Ujamaa kama sisi, geopolitics, Wakenya walivyojipanga ku lobby, business culture ya Kenya, masuala ya Kenya kwenda kulinda amani Haiti, siasa za Umagufuli kujifungia zilivyoharibu mahusiano ya kimataifa ya Tanzania, Samia kutojua anataka kufanya nini, Tanzania kuji align zaidi na China, yote haya yanahusika.
 
Back
Top Bottom