Ukiangalia jinsi Rais Ruto alivyopokelewa kwa heshima Marekani utashangaa

Ukiangalia jinsi Rais Ruto alivyopokelewa kwa heshima Marekani utashangaa

Hapo wanamtongoza ili akubali waweke kambi hapo Kenya. Mzungu ukiona anajifanya anamheshimu kiongozi wa kiafrika jua anawindwa. Umesahau bwana Membe alivyotumiwa farasi maalum wamkokote UK.

Marekani naona anatafuta mahali pa kuweka uwepo wake akapambane na influience ya Warusi na Wachina Afrika.
Marekani,uingereza wote wana kambi Kenya.
 
Hapo wanamtongoza ili akubali waweke kambi hapo Kenya. Mzungu ukiona anajifanya anamheshimu kiongozi wa kiafrika jua anawindwa. Umesahau bwana Membe alivyotumiwa farasi maalum wamkokote UK.

Marekani naona anatafuta mahali pa kuweka uwepo wake akapambane na influience ya Warusi na Wachina Afrika.
Nimeona wameideclare kenya kama ally wao, wachambuzi inakuaje hii
 
Ni kweli kuna uelewa mdogo, lakini watu wote hawawezi kuwa na uelewa mkubwa, ukitaka iwe hivyo na wewe utakuwa na uelewa mdogo. Kuna watu wanajifunza, wengine wadogo, sasa watajuaje mambo bila kujifunza?

Jana niliandika tofauti ya state visit na visits nyingine, nikaitaja hii ziara ya Nyerere, lakini sikuona haja ya kubeza watu.

Zaidi, swali la msingi liko palepale, kwa nini Kenya inashamiri sana kinataifa zaidi ya Tanzania? Kwa nini Kenya imekuwa nchi ya kwanza Afrika kupata State Visit Marekani tangu mwaka 2008, na Tanzania haipati nafasi hizi?

Kuna jibu refu la historia ya Kenya kama koloni proper la Waingereza ambalo halijapitia Ujamaa kama sisi, geopolitics, Wakenya walivyojipanga ku lobby, business culture ya Kenya, masuala ya Kenya kwenda kulinda amani Haiti, siasa za Umagufuli kujifungia zilivyoharibu mahusiano ya kimataifa ya Tanzania, Samia kutojua anataka kufanya nini, Tanzania kuji align zaidi na China, yote haya yanahusika.
Katika mambo yote uliyoandika hoja ya msingi ni moja tu kwa nini Tanzania hatutoboi kimataifa?

Na si lazima taifa liwe na uhusiano wa karibu na Marekani au wanachama wa NATO ili liwe na uchumi mzuri.

Tanzania ni taifa lisilofungamana na upande wowote linaweza kuwa na ushirika na taifa lolote duniani iwe ni China au Marekani
 
Umejitahidi sana kujieleza, na yote uliyoeleza yanajulikana. Ila bila kusita kabisa nabaki palepale. Ziara ya Ruto haikuwa ya kustukiza hata kidogo; hii imepangwa kiutaratibu tokea mwanzo kwa nia ile ile ya Marekani kuwa na eneo lake katika ukanda huu. Kenya haikuanza jana chini ya Ruto kuwa chini ya 'influence' ya Marekani. Kidogo Mwai Kibaki aliwastua sana wakubwa, alipogeukia Mashariki. Na kutokana na kuingia kwa China, Marekani anaona maslahi yake yanalegalega; kwa hiyo sasa ana'catch up'.
Siyo mara ya kwanza Ruto kuingia Jumba Jeupe tokea ashike madaraka. Mipango hii ilianzia hata kabla Uhuru hajaachia madaraka. Huu ni mpango endelevu, siyo wa kustukiza.
Haikupangwa siku nyingi sana; mwaliko ulikuja mwezi wa pili ikiwa ni muda mfupi sana baada ya Mahakama Kuu ya Kenya kuzuia polisi wa Kenya kwenda Haiti. Hata kama kulikuwa na mipango hiyo ya kumwalika, jambo ambalo Marekani inataka kufanya kwa kiongozi mmoja mmoja wa Afrika, huenda ziara hii ya Rutto isingekuwa mwezi huu.
 
Katika mambo yote uliyoandika hoja ya msingi ni moja tu kwa nini Tanzania hatutoboi kimataifa?

Na si lazima taifa liwe na uhusiano wa karibu na Marekani au wanachama wa NATO ili liwe na uchumi mzuri.

Tanzania ni taifa lisilofungamana na upande wowote linaweza kuwa na ushirika na taifa lolote duniani iwe ni China au Marekani
Inawezekana hiyo point ya kwa nini Tanzania haitoboi ndiyo ya msingi, lakini hizo point zote zina umuhimu.

Mfano, huwezi kuongelea Ruto kupata state visit Marekani bila kuongelea business culture ya Kenya iliyomtengeneza Ruto, the Hustler in Chief. Inayoweka watu wa kumu inform Ruto nini cha kufanya, .

Huwezi kuongelea business culture ya Kenya bila colonial influence ya Waingereza na siasa zilizofuatia uhuru za Kenya ambazo hazijapitia distractions za Ujamaa.

Angalia mashirika makubwa ya kimataifa yaliyo na ofisi Nairobi, halafu angalia mashirika ya hivyo yaliyo na Ofisi Dar/Dodoma. Utaona Wakenya wametuzidi sana hapo.

Tanzania tumeshindwa hata kumu accommodate Benjamin Fernandez, wa NALA, aliyepata ahadi mpaka za rais Samia kusaidiwa, akaishia kuzinguliwa na kwenda kufungua ofisi Nairobi.

Kutofungamana na upande wowote kwenyewe tunakufanya kisiasa bila kuzingatia uchumi.

Kenya rais wao Ruto anaongoza kampeni ya kimataifa ya nchi za Afrika kujinasua kutoka kwenye US dollar dependency, ukimuangalia kwa juujuu unaweza kuona anapinga American hegemony. Lakini hapo hapo Ruto ndiye amekuwa rais wa kwanza wa Africa kupata State Visit US tangu 2008, anaingia kwenye alliance na US mpaka amepewa hadhi ya first sub-Saharan Africa non-NATO ally wa US.

Kajua kuuma na kupuliza anapata faida kwa kuibana US na kwa kuungana kupiga deal na US. Ruto mwenyewe kasema yeye si anti US, anawapigania Wakenya tu.

Tanzania Rais Samia kaonekana mwanamke, watu wakampa deal aongoze mazungumzo ya Africa kupewa hela za climate change (carbon credit and climate justice), wakifikiri huyu mwanamke anaweza kuchukua attention ya dunia. Samia kaenda Misri hajajiandaa kabisa, yani kashindwa kusimamia hiyo hoja si tu kimataifa, karudi Tanzania mpaka kwenye press conference hoja hajaipa kipaumbele. Sasa sijui ndiyo wamepiga deal na Rostam wakaona waifiche isijulikane sana?

Yani Wazambia ambao hawakupewa pande la kuongoza hii ajenda wamejipanga vizuri, wamechukua mabilioni ya US dollar, sisi tuliopeea kuongoza ajenda hatujapata kitu.

Kifupi wanasiasa wa Tanzania ni washamba, hawaijui dunia, hawajui lobbying, hawajui wanataka nini, hawajui siasa za kimataifa, wamezoea kukimbizana na Waswahili wetu japo ndani tukija kwenye geopolitics wanapwaya sana.
 
Mfano, huwezi kuongelea Ruto kupata state visit Marekani bila kuongelea business culture ya Kenya iliyomtengeneza Ruto, the Hustler in Chief. Inayoweka watu wa kumu inform Ruto nini cha kufanya, .
Mshirika mkubwa wa kibiashara wa Kenya ni China. Ushawishi wa China kupitia BRI na BRICS ndio unafanya Marekani aimarishe ushawishi wake Africa.

Imeanza kuonekana mataifa ya Africa yameanza kuwa na nia ya kujiunga na BRICS

Hii state visit ya Ruto pale Marekani ni issue ya ki-geopolitics
 
Huwezi kuongelea business culture ya Kenya bila colonial influence ya Waingereza na siasa zilizofuatia uhuru za Kenya ambazo hazijapitia distractions za Ujamaa.
Vietnam imekuwa na siasa za ujamaa lakini ni mshirikia mkubwa wa kibiashara wa Marekani kuliko Kenya

Sijaona point yako ya maana hapa?

Vipi kuhusu China mshirika mkubwa wa kibiashara wa Marekani. Vipi siasa za China?
 
Mshirika mkubwa wa kibiashara wa Kenya ni China. Ushawishi wa China kupitia BRI na BRICS ndio unafanya Marekani aimarishe ushawishi wake Africa.

Imeanza kuonekana mataifa ya Africa yameanza kuwa na nia ya kujiunga na BRICS

Hii state visit ya Ruto pale Marekani ni issue ya ki-geopolitics
Bado inaiweka Kenya juu na Ruto anakuwa strategic geopolitical player.

Ruto akisema hafungamani na upande wowote nitamuelewa, kwa sababu anacheza na Wachina, halafu anacheza na Wamarekani.

Sisi tunasema hatufungamani na upande wowote halafu hata exports za ku exploit fursa za AGOA tu hatuna.

Sasa Samia apewe State Visit US aende kuongea deal gani?

Kwenye geopolitics za kusaidia Haiti hayupo.

Kwenye deals kubwa za kudhibiti ugaidi horn of Africa hayupo.

Kwenye mtifuano wa kupingana na Marekani kwenye dollar dependency hayupo.

Kwenye kuongoza mazungumzo ya climate change na climate justice kapewa uongozi kashindwa kuongoza.

Kwenye biashara kubwa za export za AGOA hayupo.

Samia mwenyewe ukimwambia ukikutana na Biden utampa agenda gani, hajui atasema nini.

Sasa mtu kama huyo apewe State Visit Marekani ya nini?
 
wangemuacha yule mama Mulamula labda angemsaidia raisi sasa kawaweka ma failure waliouwa tanesco kawahamishia huko nje, hata huko wanaharibu pia, wanapanga safari za kimaslahi binafsi na siyo states visit, cha ajabu hata hapewi respect kama first female president huko nje ni jambo la ajabu sana, akina Sirleaf wa liberia mpaka walihutubia Bunge la USA na full standing ovations, hata Banda tu alikuwa respected kama female president, mimi naamini tatizo anaweka watu incompetent na failure kwenye big decisions.

Nixon aliwahi kusema „little people in big jobs“ , tatizo likohapo kwa maoni yangu …
 
Vietnam imekuwa na siasa za ujamaa lakini ni mshirikia mkubwa wa kibiashara wa Marekani kuliko Kenya

Sijaona point yako ya maana hapa?

Vipi kuhusu China mshirika mkubwa wa kibiashara wa Marekani. Vipi siasa za China?
Vietnam imeondoka kwenye Ujamaa tangu mageuzi ya Doi Moi ya miaka ya 1980. Pia Vietnam imejua kujipanga kutumia historia ya vita na US kujenga biashara.

Sisi hata hatujui tunaenda wapi.

Ujamaa umeua private sector na uchumi kiujumla, hatujawa na uninterrupted private sector kama Kenya.

China tangu mageuzi ya Deng Xiaoping inafuata siasa za uchumi wa viwanda kupata exports. Sisi hatuna hata hizo exports.

Utaenda kuongea nini na Mmarekani wakati huna exports, hutaki majeshi yake, madini unagawa tu kwa makampuni bila shida, huna hata influence regionally, utaenda kuongea deal gani na Wamarekani wakati huna exports?
 
Vietnam imeondoka kwenye Ujamaa tangu mageuzi ya Doi Moi ya miaka ya 1980. Pia Vietnam imejua kujipanga kutumia historia ya vita na US kujenga biashara.

Sisi hata hatujui tunaenda wapi.

China tangu mageuzi ya Deng Xiaoping inafuata siasa za uchumi wa viwanda kupata exports. Sisi hatuna hata hizo exports.

Utaenda kuongea nini na Mmarekani wakati huna exports, hutaki majeshi yake, madini unagawa tu kwa makampuni bila shida, huna hata influence regionally, utaenda kuongea deal gani na Wamarekani wakati huna exports?
Kwani Tanzania ni nchi ya kijamaa mpaka sasa? Umeona hoja zako jinsi hazina mashiko.

Why kwa Tz uangalie political historical backgroundna sio kwa Vietnam?

Deng Xiaoping alifanya mageuzi ya kibiashara na siyo ya kisiasa
 
Kwani Tanzania ni nchi ya kijamaa mpaka sasa? Umeona hoja zako jinsi hazina mashiko.

Why kwa Tz uangalie political historical backgroundna sio kwa Vietnam?

Deng Xiaoping alifanya mageuzi ya kibiashara na siyo ya kisiasa
Tanzania haijui hata inafuata mfumo gani.

Vietnam wana viwanda, wana export processed goods, wanatengeneza nguo, viatu etc.

Sasa unaifananishaje Tanzania isiyo export processed goods na Vietnam?

Unasema Deng Xiaoping alifanya mageuzi ya biashara, si siasa. Ukisoma historia ya class struggle ni historia ya biashara, means of productions.

Biashara ni siasa, ndiyo maana mpaka sasa tunaongelea "diplomasia ya uchumi", usichoelewa nini?
 
Tanzania haijui hata inafuata mfumo gani.

Vietnam wana viwanda, wana export processed goods, wanatengeneza nguo, viatu etc.

Sasa unaifananishaje Tanzania isiyo export processed goods na Vietnam?

Unasema Deng Xiaoping alifanya mageuzi ya biashara, si siasa. Ukisoma historia ya class struggle ni historia ya biashara, means of productions.

Biashara ni siasa, ndiyo maana mpaka sasa tunaongelea "diplomasia ya uchumi", usichoelewa nini?
Ni lini China walibadilisha siasa zao wakati wa Deng Xiaoping mkuu?

Kwa hiyo point yako ya nchi kupitia siasa za ujamaa kutokuwa na ushirika na Marekani haina uhalisia, si ndio?

Leo Marekani wana uwekezaji mkubwa Vietnam kuliko Kenya. Imekaaje hapo?
 
Mbona Kenya ni taifa lisilofungamana na upande wowote mkuu
Kwani wapi nimesema si taifa lisilofungamana na upande wowote?

Kenya wanaelewa kutofungamana na upande wowote katika zama hizi za diplomasia ya uchumi. Tanzania hawajui.

Ndiyo maana Ruto anawabana US kwenye dollar dependency, halafu hapo hapo anaingia alliance nao.

Sisi tunapiga kelele za kutofungamana na upande wowote kisiasa katika ulimwengu wa diplomasia ya kisiasa, bila ya kuwa na mkakati.

Tulikuwa na rais aliyepiga sana kelele kuwasema vibaya mabeberu, kisiasa, wakati agenda kubwa kabisa ya kuwabana Wamarekani ni kuwapiga hapo kwenye dollar dependency anapowapiga Ruto. Ruto anapiga kotekote. Huyo anajua kutofungamana na upande wowote.

Na Wamarekani wamemjua Ruto ndiye threat, kwa sababu mjanja, anaongea issues muhimu za kiuchumi, si kupiga kelele za kisiasa na kufungua kesi za makinika ambazo haziendi popote kama Magufuli.

Ndiyo maana Wamarekani wanamuweka karibu Ruto kwa state visit, Tanzania tunaonekana hatuna uzito.
 
Back
Top Bottom