Ukiona Mwembe umejaa Maembe yaliyoiva kwenye Nyumba yenye Watoto watukutu basi kuna mawili

Ukiona Mwembe umejaa Maembe yaliyoiva kwenye Nyumba yenye Watoto watukutu basi kuna mawili

Ukiona muembe umejaa maembe yaliyoiva na kuning'inia kiasi cha kuvutia kwenye nyumba ya watoto watukutuku au shule basi tambua kuna haya mawili;

1. Huenda Mzee mwenye muembe ni mkali sana au Mchawi
2. Maembe ni machungu balaa yasiyolika hata kwa chumvi!

Kwa mfano ule ule utumie pia unapoona Mrembo/Mkaka wa makamo Ambaye hajaolewa/oa Usikurupuke kuingia kichwa kichwa lipo jambo!

Vuta subira!

Tambua kwamba kama kwa jirani maembe kama hayo yanaliwa na chumvi yakiwa machanga! Iweje Hayo yakomae yakiwa mtini?
Huenda Mzee mwenye muembe ni mkali sana au Mchawi[emoji23]
 
Ukiona muembe umejaa maembe yaliyoiva na kuning'inia kiasi cha kuvutia kwenye nyumba ya watoto watukutuku au shule basi tambua kuna haya mawili;

1. Huenda Mzee mwenye muembe ni mkali sana au Mchawi
2. Maembe ni machungu balaa yasiyolika hata kwa chumvi!

Kwa mfano ule ule utumie pia unapoona Mrembo/Mkaka wa makamo Ambaye hajaolewa/oa Usikurupuke kuingia kichwa kichwa lipo jambo!

Vuta subira!

Tambua kwamba kama kwa jirani maembe kama hayo yanaliwa na chumvi yakiwa machanga! Iweje Hayo yakomae yakiwa mtini?
3. Au manyigu yamejenga humu mtini.
 
Kwahiyo tuliofika age ya juu kama 30 nakuendelea tusiolewe? Acha hizo wewe usitubanie.
 
Hiyo ni justification ya kukinga udhaifu!

Ndiyo maana tunakumbushwa kutafakali! Mfano!

Anaweza akawa anajipanga lakini huko mtaani akazalisha wanawake kibao! Then anakuja kuoa nyuma analea mitoto kibao!
Au anaweza akawa mwanadada anajipanga lakini katoa mimba kama 800!

Au anaweza kuwa anajipanga kumbe anangoma!

Au anaweza kuwa anajipanga kumbe ni mwezi mchanga (waruwaru) lakini huwezi kujua hadi awe mpenzi wako!

NDIYO MAANA NIKASEMA UKIONA KINANG'AA single KIICHUNGUZE KWANZA LAZIMA KUNA JAMBO!
Ha ha ukiwa naye ndo utajua kwann umemkuta single [emoji1][emoji1]
 
Mwaka fulani nilirudi mtaani baada ya miaka kadhaa ya kupambania kombe ughaibuni, pale mtaani kulikuwa na zigo hilo balaa,, zigo zigo kweli, la kuvunja chaga la makamo hivi, nilipoulizia kali nikaambia halina mtu,, wakati najipanga ili nitupe karata yangu kuna mwana mmoja wa kuheshimika pale kitaa akanisanua ya kuwa lile zigo kumbe ni TSS na lipo pale mtaani kwa misheni maalum,, basi nyeg^#e zote zikanishuka
 
We ndio hujui,sisi tulikuwa tunakula yale ya ndani,unapanda unakula hukohuko juu,mengine unang'atia mtini baada ya siku kadhaa linaiva
 
Watu wengi sana wameangamia kwa kuingia kichwa kichwa! Wewe unaona kabisa watu wamesimama nyomi pembeni kuna kiti kiko wazi!

Wewe unafika pasipo kutafakali unabandika makalio.....hakika kuna mawili! Either kiti kibovu au ni cha kiongozi/dereva! Jiandae kunyanyuliwa
Una point nzuri.

BTW,: nilitaka nikupe dada yangu sema nae ni mtu wa makamo Mkuu.
 
Mimi mwembe wangu unaisha maembe yakiwa machanga nimechoka kukemea na kufukuza watoto watukutu wasiyapopoe, mwaka wa pili sasa maembe hayakomai na kuivia mtini yanaliwa hivyo hivyo na uchanga wake.
 
Hivi na yale mapapai na mapera yanayoivia mtini na kuliwa na ndege tu wakati wapangaji wapo wanaogopa nini kuyala? Au wanamuogopa mwenye nyumba wakiyala watapandishiwa kodi? Inatia huruma sana matunda kuivia mtini hakuna mtu wa kuyala ni ndege tu wanayafaidi.
 
Labda huyo mtu wa makamo ina misimamo migumu
 
Back
Top Bottom