Ukishuka Airport Dar ukapita barabara kuu unaona jinsi nchi na watu wake walivyochoka. Viongozi mnafeli wapi?

Sahihi hiyo barabara huwa inajengwa tu miaka yote, Itakuwa kuna namna mkandarasi na watu wake wanafaidika na huo ucheleweshwaji,
 
Huu uzi ungekua unaambatana na picha ingependeza zaidi,
Huenda wahusika wangeona na kuchukua hatua kwa baadhi ya issue.
 
Ndio hali yenyewe laana inaisumbua nchi.
 
Kanchi kamechoka Mbaya.

Sijui watawala wanajisikiaje wanavyotumbua mikodi ya wabongo huku Kanchi kakiwa hoi
Kule Arusha kitovu cha utalii wageni na wenyeji wanasongamana kwenye barabara inayopita soko la Kilombero.
Pananuka harufu ya vinyesi na siku ukiwa na bahati unaviona live kwenye mitaro kushoto na kulia!
Dar harufu ya uozo na vinyesi kwenye mitaro iliyoziba ni kawaida maeneo mengi! Sasa ongezea hilo joto na mijasho ya watu.. .. Unapigwa uvundo mmoja matata ukirudi room unaugua!

Aibu sana!
 
Mimi hayo mabati yenye kutu tu!

Dar es salaam ingekuwa na nyumba za maghorofa ya ghorofa 4 mpaka 5 kwa sehemu kubwa, ingechukua sehemu kama robo ya mji wa sasa.
Yes, they are eyesores.

But, what are people to do? Hali ya uchumi ni mbaya siku zote halafu inakuwa compounded na jamii kwa ujumla kutokupenda vitu vizuri.

Kuna mambo mengi tu ambayo hayahitaji hela nyingi lakini utashangaa kwa nini hayafanyiki!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…