Ukitaka kuishi kwenye ndoa yenye furaha na amani fanya hivi kijana.....

Ukitaka kuishi kwenye ndoa yenye furaha na amani fanya hivi kijana.....

Habari za muda huu ndugu zanguni........

Wahenga wanasema kuishi kwingi ni kuyaona mengi.....katika hayo mengi kuna mabaya yanayoumiza na kutufunza na kuna mazuri yanayofurahisha.......

Suala la NDOA limekuwa mwiba mchungu sana linalotatiza akili za vijana wengi sana.......kiasi kwamba baadhi ya vijana wameshakata tamaa na masuala ya ndoa na kuamua kuachana nayo.......

Katika kuishi kwangu kwingi na katika mengi niliyoyaona pia yamo yanayohusu masuala ya ndoa......

Kwenye masuala ya ndoa nimejifunza mambo kadhaa ambayo ningependa kuyaweka hapa kwa vijana ili kila mmoja kuufurahia muunganiko wao...kama ifuatavyo......

1)Oa mwanamke anayekupenda.....
Sote tunajua kuwa kiumbe mwanamke akikukabidhi moyo wake jinsi anavyokuwa mjinga mbele yako..... mapenzi yakishaujaza moyo wa mwanamke basi wewe ndio utakuwa dira yake..... mwanamke akikupenda na akaamua kuishi na wewe basi jua yuko radhi muishi maisha yoyote yale na wewe ili tu uwe kando yake......hakika utayafurahia maisha.....

2)Hakikisha ndani hakukauki chakula.......
Hapa simaanishi ile misosi ya gharama au ya watu wazito kule masaki au oyster bay la hasha bali ni kile kinachoendana na mfuko kulingana na bajeti yako kwa wakati huo.......njaa haimpendezi mtu.....njaa inaweza kumfanya malaika kuwa shetani.....pambana Sana mtoto wa watu aisishinde njaa maana baada ya shibe ndio yanakuja mahaba......

3)MSHIBISHE KWENYE CHAKULA CHA USIKU.......
Hili halihitaji maelezo mengi maana ni suala pendwa na ndio tendo lilobeba maana nzima ya NDOA........hakikisha mdomo wa chini haulali njaaa......


Nawasilisha.......
Ajiri house girl anayejua kupika.
Mwenzenu wangu mzuri idara nyingi, Ila hii ya jikoni, sijui kwanini hataki kujifunza, halafu ikifika weekend akiwa nyumbani anataka apike yeye. Jamani hiki Ni Nini? Nyama so ndio mnasema Ni tamu, hamjaona inavyopikwa mpaka ladha yote ikapukutika. Mwambie una hamu ya chapati Sasa, utajuta mpaka uiite papati.
Kosea siku umwambie acha tu house gel apike, utasemwa mpaka usemeke.
Enewei, Bahati nzuri weekend Ina siku mbili tu.
Ingekua ndio mpishi kila siku......sinyaagile....
 
Humu jf waliooa ni wengi kuliko kataa ndoa,,sema kataa ndoa wana id zaid ya tano kila mmoja ionekane ni wengi........

Endeleeni tu kutupenda wake zenu😌
 
Ajiri house girl anayejua kupika.
Mwenzenu wangu mzuri idara nyingi, Ila hii ya jikoni, sijui kwanini hataki kujifunza, halafu ikifika weekend akiwa nyumbani anataka apike yeye. Jamani hiki Ni Nini? Nyama so ndio mnasema Ni tamu, hamjaona inavyopikwa mpaka ladha yote ikapukutika. Mwambie una hamu ya chapati Sasa, utajuta mpaka uiite papati.
Kosea siku umwambie acha tu house gel apike, utasemwa mpaka usemeke.
Enewei, Bahati nzuri weekend Ina siku mbili tu.
Ingekua ndio mpishi kila siku......sinyaagile....
Hahahaha!!!!.......mkuu kwa hiyo unagugumia chapati ngumu kama msasa kishingo upande
1002306758.jpg
 
Kuna Yule kijana anajiita Stamina muimba mziki
Asee iliteswa Na mke wake hadi kutoa wimbo
 
Suala la NDOA
Ni lazima mmoja asitumie akili hasa mwanaume, hapo mtafika mbali! Unajua hapa ni uongo wewe kubali tu! Utakubali kuiacha akili yako isifanye kazi??

Wazee wetu walitumia sana hii mbinu! Anajua kabisa yule siyo mwanangu na bado anaishi naye na kumlea!
 
Back
Top Bottom