Ukitaka kuishi vizuri Dar es Salaam ishi Kigamboni

Ukitaka kuishi vizuri Dar es Salaam ishi Kigamboni

Niliishi kigamboni toka 85-98 hapo maeneo ya feri kwa kadhia tulizopitia kipindi kile imenifanya nipachukie mpaka leo hi japo nimerudi tena kwa uwekezaji ila kwa kuishi mimi hapana labda litokee la kutokea,
 
Kipindi hicho theruthi ya wakazi wa maeneo ya ferry,kwa,urasa,mpaka tungi na midizini mpaka machava na maeneo ya tuamoyo tulikuwa tunajuana kwa majina mawili mpaka matatu,usafiri haukuwa changamoto bali ulikuwa ni shida haswaa,
 
Kuna wakati pantoon ilikosekana ikawa tunavukia kule TAFICO au kwa kutumia ngwanda ,maji yalikuwa ni tabu nyingine NUWA walitumia mtambo wao wa kule Mtoni Temeke,na ilikuwa tunakaa zaidi ya mwezi bila huduma ya maji Safi zaidi tukitegemea visima vya shimo
Usalama kwa maeneo yetu ulikuwa wa uhakika kwa asilimia zoote,ila kwa kadhia niliyopitia kumenitumbukia nyongo kuishi kigamboni ukijumlisha na gharama chakula kuwa juu
 
Kigamboni (sasa ni wilaya) ni sehemu ya jiji la Dar es Salaam ambayo tofauti na maeneo mengine ilichelewa kuendelezwa kimiundombinu mpaka kufika miaka ya 90. Watu walichelea kuishi huko kutokana na kupaona ni maporini palipostahili kuishi wanyama.

Hivi leo, mambo ni tofauti sana, mji unakua kwa kasi ya ajabu, barabara zinajengwa kutangulia makazi ya watu, ni sehemu pekee katika jiji la Dar es Salaam ambako ukiingia unasahau kuhusu foleni za barabarani, hali ya hewa ni nzuri kutokana kutokuwepo kwa ujenzi holela wa nyumba, ni karibu sana na city centre na kuna fursa nyingi za kuanzisha biashara.

Binafsi nilifika kwa mara ya kwanza na kuhamia Kigamboni mwaka 2015 kutoka Survey maeneo ya karibu na Mlimani city nilipoishi kwa takribani miaka minne ila mpaka kufikia leo sijawahi kujutia kuishi huku wala kuwaza kuhamia mahali pengine katika mji huu kutokana na sifa nilizozitaja hapo juu na kwa bahati nzuri Mungu amenijaalia kujenga kakibanda huku huku.

Kwa ambao hawajawahi kufika huku hudhani kwamba Kigamboni ni kisiwa na kwamba usafiri pekee wa kufika huku ni wa kuvuka maji kwa pantoni, la hasha! Kigamboni si kisiwa bali imetenganishwa na sehemu nyingine ya jiji kwa sehemu ya bahari iliyoingia nchi kavu (ghuba) ambayo ni bandari ya Dar es Salaam na Kwa sasa ukiachilia usafiri wa wa pantoni kuna daraja na barabara mbili ambazo unaweza kupita bila hata kuiona hiyo bahari.

Karibuni sana Kigamboni.
nina viwanja vinne kigambon nilinunua enz zile kikwete anasema unajengwa mji wa kisasa ila kiukweli cjawah kutaman kuish kigambon. napaona kumekaa kipemba sana aisee.
 
Una wasiwasi napo, dawa ni kwenda kununua kipindi cha masika, hapo ndio utajua km unauziwa bwawa la kambale ama kiwanja. [emoji23]

Sina wasi napo hata Kg napafahamu sana tangu enzi za 1980s to 1990s, sijaishi huko ila kila wiki nilikuwa naenda. Ofisi ya Mzee /Mshua ilikuwa huko.
 
Mmeshanichanganya Sasa, Mr anatafuta nyumba ya kupumzikia kipindi cha likizo na kwa hapo dar, kigamboni ameipa kipaumbele, ila kwa maelezo ya humu mh🙄
 
Mmeshanichanganya Sasa, Mr anatafuta nyumba ya kupumzikia kipindi cha likizo na kwa hapo dar, kigamboni ameipa kipaumbele, ila kwa maelezo ya humu mh[emoji849]
Usichanganyikiwe kwa kusikiliza maneno ya waropokaji wa humu,wengi wao wanajitia ujuaji kwa habari za kusikia na hawajui kama hawajui, njoo ujionee mwenyewe Kigamboni is safe and more secured compared to other places in Dar.Hakika utaenjoy likizo na mapumziko yako
 
Mmeshanichanganya Sasa, Mr anatafuta nyumba ya kupumzikia kipindi cha likizo na kwa hapo dar, kigamboni ameipa kipaumbele, ila kwa maelezo ya humu mh🙄
Kama yupo States au Europe, most likey hatotaka kujenga sehemu nyingine kama kibamba, tegeta, goba sijui mitaa ya kuelekea mlandizi huko kupo too disorganized.
Kigamboni is the future.
 
Usichanganyikiwe kwa kusikiliza maneno ya waropokaji wa humu,wengi wao wanajitia ujuaji kwa habari za kusikia na hawajui kama hawajui, njoo ujionee mwenyewe Kigamboni is safe and more secured compared to other places in Dar.Hakika utaenjoy likizo na mapumziko yako
Kwa dar mi sio mwenyeji kabisa, vipi Kuna mradi wa nyumba za serikali huko?
 
Kama yupo States au Europe, most likey hatotaka kujenga sehemu nyingine kama kibamba, tegeta, goba sijui mitaa ya kuelekea mlandizi huko kupo too disorganized.
Kigamboni is the future.
Shukrani sana mkuu, tutazingatia ushauri wako
 
Kuna wakati pantoon ilikosekana ikawa tunavukia kule TAFICO au kwa kutumia ngwanda ,maji yalikuwa ni tabu nyingine NUWA walitumia mtambo wao wa kule Mtoni Temeke,na ilikuwa tunakaa zaidi ya mwezi bila huduma ya maji Safi zaidi tukitegemea visima vya shimo
Usalama kwa maeneo yetu ulikuwa wa uhakika kwa asilimia zoote,ila kwa kadhia niliyopitia kumenitumbukia nyongo kuishi kigamboni ukijumlisha na gharama chakula kuwa juu
Pole sana kwa kadhia uliyopata ila fahamu sasa mambo yamebadilika na kila kukicha yanazidi kubadilika in a positive manner, usafiri si tabu tena , pantoon ni za uhakika zipo 3 na zinafanya kazi 24hrs
 
Vibaka vibaka, wezi na kaka zao majambazi wengi wameshapigwa vyuma [emoji379] na askari.. Ni watoto waliotoka mbagala, Kinondoni na maeneo memgine, ndio walianza kuleta usela mavi.

Nipo kigamboni toka 2000 mwishoni nikitokea kurasini.. Huku maisha yalikuwa shwaari kabisa unaanika hadi nguo na unazikuta asubuhi, walivyoanza kuja watu mbalimbali wakaanza kuharibu mji, ila sasa hali shwaari kabisa, mtaani si chini ya watoto 5 wamekula vyuma.. Kumepoa kinyama.

Hakuna sehemu kuna kosa kero..

Ila yoote kwa yoote kigamboni kuhama inataka moyo saana.
Ukome Kututukana Watoto wa Kinondoni sawa? Kinondoni ndiyo Tanzania na Mishahara yenu yote mnapata kwa 'cheques' zenu 'Kusainishwa' na Mabosi zenu ( Mataita wenu ) wanaokaa ( wanaoishi ) Kinondoni huku sawa? Washamba ( Mambwiga ) wakubwa nyie!!
 
Naam
wadaslam kuwaondolea kigamboni ni Temeke kichwani ni ngumu sana ila uzuri wake inakuzwa na middle income class na real estate projects, baada ya muda itakuwa ni habari nyingine maana vitu kama tatizo la usafiri si kitu permanent
 
Back
Top Bottom