Ukitaka kuishi vizuri Dar es Salaam ishi Kigamboni

Ukitaka kuishi vizuri Dar es Salaam ishi Kigamboni

Sijawahi kutamani kuishi huko,ila ni kuzuri kwa sasa hivi ukilinganisha na miaka ya nyuma.Ukitaka kuinjoy maisha ya kule uwe na ka usafiri kako na hela ya mafuta isiwe ya mawazo.Kuna hali flani hivi ya hewa tofauti na sehemu nyingi sana za Dar...
 
Kigamboni (sasa ni wilaya) ni sehemu ya jiji la Dar es Salaam ambayo tofauti na maeneo mengine ilichelewa kuendelezwa kimiundombinu mpaka kufika miaka ya 90. Watu walichelea kuishi huko kutokana na kupaona ni maporini palipostahili kuishi wanyama.

Hivi leo, mambo ni tofauti sana, mji unakua kwa kasi ya ajabu, barabara zinajengwa kutangulia makazi ya watu, ni sehemu pekee katika jiji la Dar es Salaam ambako ukiingia unasahau kuhusu foleni za barabarani, hali ya hewa ni nzuri kutokana kutokuwepo kwa ujenzi holela wa nyumba, ni karibu sana na city centre na kuna fursa nyingi za kuanzisha biashara.

Binafsi nilifika kwa mara ya kwanza na kuhamia Kigamboni mwaka 2015 kutoka Survey maeneo ya karibu na Mlimani city nilipoishi kwa takribani miaka minne ila mpaka kufikia leo sijawahi kujutia kuishi huku wala kuwaza kuhamia mahali pengine katika mji huu kutokana na sifa nilizozitaja hapo juu na kwa bahati nzuri Mungu amenijaalia kujenga kakibanda huku huku.

Kwa ambao hawajawahi kufika huku hudhani kwamba Kigamboni ni kisiwa na kwamba usafiri pekee wa kufika huku ni wa kuvuka maji kwa pantoni, la hasha! Kigamboni si kisiwa bali imetenganishwa na sehemu nyingine ya jiji kwa sehemu ya bahari iliyoingia nchi kavu (ghuba) ambayo ni bandari ya Dar es Salaam na Kwa sasa ukiachilia usafiri wa wa pantoni kuna daraja na barabara mbili ambazo unaweza kupita bila hata kuiona hiyo bahari.

Karibuni sana Kigamboni.
Mkuu mkadiriajimajenzi uliishi survey kwa miaka.minne na sasa unapata utelezi kuishi kigamboni toka 2015. Unaongea kama unazungumzia nafsi yangu,, maana na mimi niliishi survey pia nikahamia kigamboni ingawa nako nilihama na sasa niko mkoani Iringa.
Mkuu watu watakuoinga ingawa ukweli ndio huo, kigamboni inafunguka na inaendelea kufunguka, suala la malipo ya kuvuka darajani ni la muda na wimbi lake la upepo wa kisiasa linakuja pengine 2025 itakuwa mwisho, kwani ujio wa daraja la tanzanite unaondoa maana ya msingi kwanini kulipia juvuka kigamboni
 
Pameshangaa shangaa tu utasema mkoa wa wapi sijui!plus hayo makero ya vivuko na daraja nilijuta kupanga huko...
Ila kweli uko sahihi, maana ukizoweya sana Maisha ya Manzese,lazima Kigamboni utaiona Kama Mkoa, maana kuna greenish kwenye maeneo yake, wakati Manzese sizani Kama mti hata mmoja!!!
 
Ivi huwa kuna hospitali kubwa kule? Just in case kuna emergency ya ugonjwa usiku
Kwani hospitals kubwa Dar ziko ngapi? Si Muhimbili na Mlongazila tu? Kuna hospitali ya wilaya tu kama Mwananyamala/Temeke/Ilala. Hakuna kitu kama Aga Khan.
 
Upo kigamboni ipi? Yani beach zote zilizojaa kigamboni ndio upate uhaba wa wanyama?

Kwanza uelewe wanawake wengi sasa hivi wanauza ila hawaweki bango tu, kwahiyo usiangaike sana hata mtaani kwako huduma ipo, siku hizi hawauzi wala hawatowi bure, teguwa kitendawili hicho.
Kwani Kona bar alikua anawapata Bure?
 
SIPAPENDI KIGAMBONI.
Unatufokea?!! Sister du huwezi kukaa huko. Hakuna Kidimbwi,Samaki samaki. Wapangaji wengi wa Kigamboni ni wafanyakazi wa makampuni za mafuta,bandari,serikali kabla ya kuhamia Dodoma na wanafuzi wa IFM,TIA,Mwl Nyerere.
 
Hata Kiwanja Bure kigamboni sihitaji aisee!
1.Ni Risk hatari ni Kuvuko chetu mara Engine moja mara Matenegenezo,Kivuko,Nani anataka maisha ya Hofu Ivyo!
Uje Darajani Utatamani Ulie kwa foleni ile ya Malori pale Bandarini!
Yaani Kukaa Kigamboni ni Utumwa,
Hata Bure Kiwanja Sihitaji Over
Kweli aisee.Kila Ukitaka kwenda kwako unaanza kupata mawazo.Napitia darajani au Kwny kivuko.?
 
Unatufokea?!! Sister du huwezi kukaa huko. Hakuna Kidimbwi,Samaki samaki. Wapangaji wengi wa Kigamboni ni wafanyakazi wa makampuni za mafuta na wanafuzi wa IFM,TIA,Mwl Nyerere.
Wewe ni mfanyakazi wa kampuni ya mafuta au mwanafunzi wa IFM?
 
Back
Top Bottom