Ukitaka kujipima kama una upendo wa kweli na uvumilivu basi fuga mbuzi wa kienyeji

Ukitaka kujipima kama una upendo wa kweli na uvumilivu basi fuga mbuzi wa kienyeji

Nimechunga sana Mbuzi hasa enzi za udogoni(kabla sijaanza primary na kipindi niko primary, huu wakati ndio nimechunga sana pamoja na Ng'ombe, Kondoo, Punda)

Hata sasa nikienda kijijini kusalimia, lazima nichunge kuwasaidia na pia kitu ambacho nakipenda kutokana na kukifanya sana Udogoni.

Kati ya Wanyama wanaofungwa, Mbuzi ndiye anayesumbua wakati wa kuchunga.

Kero kubwa ni ulafi, wanavamia mazao yoyote yaliyopo mbele yao. Pia wana akili ya kukutega/kukuhadaa wewe mchungaji. Wanaweza kujifanya wameshiba na kulala chini huku wakicheu(wakitafuna majani waliyomeza kwa kuyatapika na kuyatafuna tena), ukizibaa kidogo utakuta washaamka na kukimbilia lilipo shamba na kuvamia mazao.

Wakifika lilipo shamba wanaingia ndani zaidi wakale mazao huko ndani, wengine wanajificha huko ndani ili waendelee kula mazao.

Wakivamia shamba la mtama uliokaribia kuiva, wanalaza/dondosha mabua ya mtama na wale punje za mtama.

Ukienda kuwatoa, walio wakorofi wataanza kukimbilia ndani ya shamba huku wakiendelea kula mtama wanaokutana nao mbele.

Muda huo ukiwa unakimbizana na mbuzi kama una ng'ombe nao wanaanza kuvamia shamba, inakuwa mtafaruku.

Hii adha imetukuta sana wachungaji na ilikuwa ni sababu kubwa ya kuchezea stick endapo mwenye shamba akinasa umelisha mazao yake.
 
Nimechunga sana Mbuzi hasa enzi za udogoni(kabla sijaanza primary na kipindi niko primary, huu wakati ndio nimechunga sana pamoja na Ng'ombe, Kondoo, Punda)

Hata sasa nikienda kijijini kusalimia, lazima nichunge kuwasaidia na pia kitu ambacho nakipenda kutokana na kukifanya sana Udogoni.

Kati ya Wanyama wanaofungwa, Mbuzi ndiye anayesumbua wakati wa kuchunga.

Kero kubwa ni ulafi, wanavamia mazao yoyote yaliyopo mbele yao. Pia wana akili ya kukutega/kukuhadaa wewe mchungaji. Wanaweza kujifanya wameshiba na kulala chini huku wakicheu(wakitafuna majani waliyomeza kwa kuyatapika na kuyatafuna tena), ukizibaa kidogo utakuta washaamka na kukimbilia lilipo shamba na kuvamia mazao.

Wakifika lilipo shamba wanaingia ndani zaidi wakale mazao huko ndani, wengine wanajificha huko ndani ili waendelee kula mazao.

Wakivamia shamba la mtama uliokaribia kuiva, wanalaza/dondosha mabua ya mtama na wale punje za mtama.

Ukienda kuwatoa, walio wakorofi wataanza kukimbilia ndani ya shamba huku wakiendelea kula mtama wanaokutana nao mbele.

Muda huo ukiwa unakimbizana na mbuzi kama una ng'ombe nao wanaanza kuvamia shamba, inakuwa mtafaruku.

Hii adha imetukuta sana wachungaji na ilikuwa ni sababu kubwa ya kuchezea stick endapo mwenye shamba akinasa umelisha mazao yake.
Dah!
Hawa wanyama kumbe pasua kichwa hivi?
 
Nikiwa mdogo, kuna kundi la vimbuzi saba nilikuwa nachunga. Kuna beberu mmoja alikuwa msumbufu sana hasa akiona majike. Huyu yeye machungani muda mwingi nilikuwa namfunga.

Siku moja jioni natoka kuchunga, amenisumbua njia nzima. Mara anatoka kundini anakwenda kulisha mazao ya watu. Namkimbiza nashika kamba namvuta anaresist na mamiguu yake yote manne, limenyanyua shingo limetoa ulimi kama linakara roho, nalichapa linatoka nduki linakwenda hovyo tuu kusiko julikana.

Alichokuja kuniudhi kabisa, nilikutana na dogo mwenzangu nae anatoka kuchunga mbuzi wa kwao. Tunafahamiana. Lile beberu acha lianze kuonesho umwamba kwa wale majike wa kundi la yule dogo. Linampanda huyu, linaacha linaenda kwa yule na yale makelele ya mabeberu yakiwa yanataka mbususu.

Nikijaribu kuliswaga lirudi kundini linakimbia hovyo. Yule dogo nae akaanza kunicheka. Nilipandisha hasira aisee. Nikatimua mbia kumfuata yule beberu. Akanyanyua miguu ya mbele tupigane sasa. Nikasimama. Nikaishika kamba nikaanza kumvuta anaresist huku mi namsogelea. Nilivomfikia nikamshika pembe nikampiga kichwa. Ile head to head yani. Hadi nikahisi kizunguzungu. Nikamuona nae ameanza kuruka ruka hovyo huku anatikisa kichwa. Alivyotulia akanyoosha njia hadi nyumbani. Yule beberu hakuwahi kunisumbua tena hadi alivyouzwa.
 
Mimi Hadi leo Nina kovu nilipigwa na pembe nilipokua mdogo.
Kuna kipindi nilimpanda mgongoni ,aisee akaanza kutimua mbio kuelekea kwenye miba, niliokotwa Kama Yesu vile alivyokuwa katoka kusulubiwa!!mwili una vidonda balaa!!

Ila nilikua napenda pale vitoto vidogo vilivyokuwa vikiingia kwenye shimo la choo halafu unaenda kuviokoa.
Unafunga kitanzi halfu unaingiza shimoni huku ukimulika na tochi
 
Nimechunga sana Mbuzi hasa enzi za udogoni(kabla sijaanza primary na kipindi niko primary, huu wakati ndio nimechunga sana pamoja na Ng'ombe, Kondoo, Punda)

Hata sasa nikienda kijijini kusalimia, lazima nichunge kuwasaidia na pia kitu ambacho nakipenda kutokana na kukifanya sana Udogoni.

Kati ya Wanyama wanaofungwa, Mbuzi ndiye anayesumbua wakati wa kuchunga.

Kero kubwa ni ulafi, wanavamia mazao yoyote yaliyopo mbele yao. Pia wana akili ya kukutega/kukuhadaa wewe mchungaji. Wanaweza kujifanya wameshiba na kulala chini huku wakicheu(wakitafuna majani waliyomeza kwa kuyatapika na kuyatafuna tena), ukizibaa kidogo utakuta washaamka na kukimbilia lilipo shamba na kuvamia mazao.

Wakifika lilipo shamba wanaingia ndani zaidi wakale mazao huko ndani, wengine wanajificha huko ndani ili waendelee kula mazao.

Wakivamia shamba la mtama uliokaribia kuiva, wanalaza/dondosha mabua ya mtama na wale punje za mtama.

Ukienda kuwatoa, walio wakorofi wataanza kukimbilia ndani ya shamba huku wakiendelea kula mtama wanaokutana nao mbele.

Muda huo ukiwa unakimbizana na mbuzi kama una ng'ombe nao wanaanza kuvamia shamba, inakuwa mtafaruku.

Hii adha imetukuta sana wachungaji na ilikuwa ni sababu kubwa ya kuchezea stick endapo mwenye shamba akinasa umelisha mazao yake.
Daaahh umenikumbusha, yaani mulemule😂😂
 
Back
Top Bottom