Ukitaka kujipima kama una upendo wa kweli na uvumilivu basi fuga mbuzi wa kienyeji

Ukitaka kujipima kama una upendo wa kweli na uvumilivu basi fuga mbuzi wa kienyeji

Kuwafuga hawa wanyama inahitaji uvumilivu wa Hali ya juu na upendo uliotukuka vinginevyo utakuwa unavunja mguu wa mbuzi kila sku ,

Wana visirani na viburi sijawahi ona ,

Picha linaanza akikata kamba aisee atakupigisha tizi moja sio ya nchi hii , na ukimkamata ukaanza kumvuta na kamba yake anaamua kuzingua tuu yaani , anagoma kabisa na anaamua kukaa huku amenyanyua kichwa juu na amekuangalia Kwa kibri kana Kwanza huna la kumfanya

Humo kwenye Banda usiku wanaweza amua kuanza kuzichapa Tu yaan , ni mnyukano na makelele usku mzima , usishangae kuwakuta wote wamejifunga kamba kama wanataka kujinyonga ,
, kama unaamini Una huruma Sana na upendo basi fuga hawa wanyama , vinginevyo unatutania

View attachment 2612275
Ulivyoandika na nilivyousoma huu uzi asee kweli hawa viumbe wanatesa...

Wakiamua kula mahindi yako sasa uliyoyaanika yapigwe na jua...afu unatoka shambani njaa kali 😂😂😂😂 asee utasema walikuwa wanakusubiri ndio wale mahindi yako.
 
Ao wajinga wanakuaga na kiongoz wao mjinga kuliko wako wao, yani ukiwafungua tu ye anaongoza to njia kwa speed kwenda kula mazao ya watu, dawa yao kamba asa iyo kamba ukute wako wa 3 ndo shughuli inakua ngumu mara wakuvute uku mara uku wakikushinda ujue kesi iyo, mazao ya watu washakula,

Basi nilikua nkiwatuliza kimbelembele na mfunga kamba kwenye lisho alafu namtia fimbo nyingi hadi asira yangu ipoe.... Kuna wakati kimbelembele alikua beberu mkorofi ukimchapa anageuka anaruka anataka akupige, basi nkawa nampa kolabo mwanangu mmoja, nafimbo zetu ndefu mmoja mbele mwingine nyuma akigeuka akupige fimbo akigeuka uku fimbo.....

Ila mikoa mingine noma Mbuzi 50 walipikutika mwezi mmoja, yani mbuzi anapatwa na kichaa, ukimpasua unakuta hadi irizi,

Pia kuna watu noma, waroho ata mbuzi kajifia hadi anaanza kuaribika ila wanakula tu....
 
Nimewavunja sana hao miguu, mbuzi na ng'ombe nimechunga sana.
Bora ufuge kondoo kuliko hao vicheche.

Wakishazoea kulisha shamba fulani, ukiwa njiani unawaswaga wanatimua mbio hata kama ni umbali wa kilometa 3 mbele. Inabidi ukimbizane nao na lazima utakuta wameshaharibu tu.

Raha ya kufuga hao ni nyama, baba alikuwa akichinja kila wiki mbuzi.

Nb: ukitaka kuwa mfugaji wa hutu "tushenzi" basi uwe na eneo kubwa vinginevyo kila siku utaitwa kwa mwenyekiti au mtendaji kujibu mashitaka ya kuharibu mazao ya watu.😂😂😂
 
Wanapenda mazao ya watu utasema wanajua kulima. Niliwahi kumpiga mmoja ñusura nimuue baada ya kuwaongoza wenzake kula mazao nikapigwa halafu ile nimekaa nasikilizia maumivu kakaja kakanipigia chafya usoni
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] pole mkuuu

Sent from my Infinix X665 using JamiiForums mobile app
 
IMG_20220713_230946.jpg

Mbuzi akiangalia vijana wa JF wakiwajadili
 
Huku mbagala Kuna mbuzi kibao wanazurura tu Kama hawana mwenyewe. Wanakula chochote Hata andazi.
Wezi wanaogopa kuwaiba eti wanadai ukliba ukachinja na kula, unaanza kulia Kama mbuzi😂😂😂😂
 
Samahani:
Hivi ushawahi funga KONDOO?

Ushawahi wakuta ule ukiburi wao waki inamisha vichwa chini?

Kati ya mbuzi na Kondoo, basi kondoo ni mchafu zaidi, ni anakiburi zaidi alafu kiburi cha kimya kimya.

Alafu akili zao wanazijua wenyewe wakiamua jambo lao.

Nawashangaa sana wanakubaligi kuitwa MAKONDOO kanisani.
 
Nikiwa mdogo, kuna kundi la vimbuzi saba nilikuwa nachunga. Kuna beberu mmoja alikuwa msumbufu sana hasa akiona majike. Huyu yeye machungani muda mwingi nilikuwa namfunga.

Siku moja jioni natoka kuchunga, amenisumbua njia nzima. Mara anatoka kundini anakwenda kulisha mazao ya watu. Namkimbiza nashika kamba namvuta anaresist na mamiguu yake yote manne, limenyanyua shingo limetoa ulimi kama linakara roho, nalichapa linatoka nduki linakwenda hovyo tuu kusiko julikana.

Alichokuja kuniudhi kabisa, nilikutana na dogo mwenzangu nae anatoka kuchunga mbuzi wa kwao. Tunafahamiana. Lile beberu acha lianze kuonesho umwamba kwa wale majike wa kundi la yule dogo. Linampanda huyu, linaacha linaenda kwa yule na yale makelele ya mabeberu yakiwa yanataka mbususu.

Nikijaribu kuliswaga lirudi kundini linakimbia hovyo. Yule dogo nae akaanza kunicheka. Nilipandisha hasira aisee. Nikatimua mbia kumfuata yule beberu. Akanyanyua miguu ya mbele tupigane sasa. Nikasimama. Nikaishika kamba nikaanza kumvuta anaresist huku mi namsogelea. Nilivomfikia nikamshika pembe nikampiga kichwa. Ile head to head yani. Hadi nikahisi kizunguzungu. Nikamuona nae ameanza kuruka ruka hovyo huku anatikisa kichwa. Alivyotulia akanyoosha njia hadi nyumbani. Yule beberu hakuwahi kunisumbua tena hadi alivyouzwa.
Mbuzi we Acha tuu , ukifuga hawa lazima ukumbane na kesi za mazao Kula miti ya watu , ni swala la mwez mmoja tuu majirani wote hamuongeleshani
 
Nikiwa mdogo, kuna kundi la vimbuzi saba nilikuwa nachunga. Kuna beberu mmoja alikuwa msumbufu sana hasa akiona majike. Huyu yeye machungani muda mwingi nilikuwa namfunga.

Siku moja jioni natoka kuchunga, amenisumbua njia nzima. Mara anatoka kundini anakwenda kulisha mazao ya watu. Namkimbiza nashika kamba namvuta anaresist na mamiguu yake yote manne, limenyanyua shingo limetoa ulimi kama linakara roho, nalichapa linatoka nduki linakwenda hovyo tuu kusiko julikana.

Alichokuja kuniudhi kabisa, nilikutana na dogo mwenzangu nae anatoka kuchunga mbuzi wa kwao. Tunafahamiana. Lile beberu acha lianze kuonesho umwamba kwa wale majike wa kundi la yule dogo. Linampanda huyu, linaacha linaenda kwa yule na yale makelele ya mabeberu yakiwa yanataka mbususu.

Nikijaribu kuliswaga lirudi kundini linakimbia hovyo. Yule dogo nae akaanza kunicheka. Nilipandisha hasira aisee. Nikatimua mbia kumfuata yule beberu. Akanyanyua miguu ya mbele tupigane sasa. Nikasimama. Nikaishika kamba nikaanza kumvuta anaresist huku mi namsogelea. Nilivomfikia nikamshika pembe nikampiga kichwa. Ile head to head yani. Hadi nikahisi kizunguzungu. Nikamuona nae ameanza kuruka ruka hovyo huku anatikisa kichwa. Alivyotulia akanyoosha njia hadi nyumbani. Yule beberu hakuwahi kunisumbua tena hadi alivyouzwa.
Sipatii picha kiko kichwa chako 😂😂😂
 
Back
Top Bottom