Ukitaka kujua hii nchi ina wajinga wengi tembelea @bambalivetz

Jamaa alikua anauliza watu swali

Unawazungumziaje watu wanao muworship mungu bila uoga wowote?

Majibu ya wa Tz
1. Wanao muworship Mungu bila uoga wowote wanakosea sana Mungu siyo wa kumfanyia mchezo.
2. Mimi nawashauri wanao muworship Mungu watubu dhambi zao na waache kumuworship.
3. Kama umewahi kumuworship Mungu tubu mapema na uache tabia hiyo kabla hujafa.

Shida yetu wa Tz huwa hatupendagi kuuliza kitu kama hatujaelewa ndo maana hata shule mwalimu anafundisha hatuelewi na akiuliza nani hajaelewa hatunyooshi mkono kuonyesha kuwa hatujaelewa matokeo yake tunajibu kibishi huku hatuelewi tunajibu nini
 
Na ni watu wazima hawa na ndio wanarudisha nyuma juhudi za waelevu wachache, ila wabishi balaa huko vijiweni.
 
Huyu jamaa anaiumbua sana Serkali, anaonyesha ni kwa namna gani hizi Fofoho zinazopambaniwa sana ni vichwa wazi na ndizo zinaongoza baadhi ya majimbo, majeshini na ndio wapiga kura hawa hawajui hata Oxygen ni nini watu kama hawa hatawezaje kudai Gas ya Mtwara.
 
Ahsante sana Mkuu hii ndo point yangu sasa kwa wale ambao walikua hawajaelewa kwa kusema napiga promo.
 
Barakoa na bara la afrika lipi ni bara kubwa, mwamba alijibu barakoa. 😂
 
Kama umefuatilia vizuri Mtanzania kuliko kusema sijui ni bora akupe jibu lolote lile.
 
Naunga mkono hoja
 
Kumbuka hawa wanataka hivo clip za kipumbavu ambazo wewe ndio utafurahia zote za wajanja wanakata
 
Burudani tu hizi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…