Abdul-Aziz Ally Carter
New Member
- May 24, 2024
- 2
- 24
Habari,
Naitwa Abdul-Aziz Ally Carter, Mwanafunzi wa Mwaka wa 3 chuo kikuu cha Dar es salaam (UDSM) nasomea Historia na sayansi ya siasa, namba yangu ya usajili 2021-04-01016
Siku za karibuni nimekuwa active katika harakati za chuo hasa kupigania maslahi ya wanafunzi waliozuiliwa kuingia katika mitihani kwa kushindwa kulipia Ada na kucheleweshwa kwa malipo ya Boom.
Toka niwe active katika harakati hasa kipindi hiki, Maisha yangu yamekuwa magumu kitaaluma hasa katika Uwasilishaji (semina),
Katika semina ya leo, ya kozi ya "Public administration in Tanzania" yenye kozi code PS 341, Siku ya Jumanne Saa 8:00 mpaka 9:00 , inayofanyika Venue ya SR 5 na kusimamiwa na Kiongozi wa semina ( Seminar leader) aitwaye Moses Boaz,
Course instructor wa semina hii ni Prof E.Mallya, Ofisi yake ni namba 802 Jengo la COSS Tower.
Katika Uwasilishaji (presentation) ambapo kikundi cha watu watano (5) walifanya Uwasilishaji na Mimi nikiwemo,
Kiongozi wa semina (Moses Boaz) alisema nimekosea kutoa maana ya msamiati uitwao " Politicization"
UTATA
Kwanza, maana ya msamiati huo niliutoa kwenye vyanzo vya vinavyoaminika vilivyopo kwenye course outline iliyotolewa mwanzo wa semister,
Pili; Kiongozi wa semina ana wajibu wa kumrekebisha/ kumsahihisha mwanafunzi pale anapokosea katika semina kwa lengo la kumsaidia na kumjengea uwezo,
Tatu; Katika kikundi cha Uwasilishaji cha watu watano ( 5) ambacho kimekutana, Kikajadiliana na kukubaliana maudhui ya Uwasilishaji, ni mtu mmoja tu aliyekoselewa kwa vitisho ambaye ni Mimi ( Abdul-Aziz Ally Carter),
VITISHO
Kwanza; Kiongozi wa semina alitaka Mimi pekee yangu kati ya watu watano (5) Kulihama grupu hilo na kuamia grupu lingine kwa lazima,
Pili, Kiongozi wa semina alisema atanipatia "zero" kwenye kazi ya alama kumi (10),
Tatu, Kiongozi wa semina amesema nisipojiangalia nita rudia kozi mwakani (carryover),
Kiongozi wa Semina (Moses Boaz) alianza kuzitoa Kauli na lugha kali kama hizi juu yangu katika semina ya wiki iliyopita tukijianda kuhudhuria muadhara wa Uprofesa.
USHAHIDI
Kauli hii kaitoa kwenye chumba cha semina kikiwa na wanafunzi wote wa semina hiyo,
Wanafunzi ni mashahidi.
MTAZAMO WANGU
Kauli na Vitisho vya namna hii vimeanza baada ya harakati za kuwapigania wanafunzi waliozuiliwa kufanya mitihani kwa sababu ya kukosa Ada,
Kiongozi wa semina, Alihusisha maswali yangu ya kutaka kujua sababu za kauli alizotoa na harakati zangu kuanzia wiki mbili nyuma.
Kiongozi wa semina alizungumza kwa Hasira na Jazba, katika mazingira ambayo Jazba na Hasira haikupaswa kutumika,
Kwa mazingira hayo, nahitimisha kwamba sababu ya kilichotokea kati yangu na msimamizi wa semina (Moses Boaz) ni Harakati na siyo makosa ya Uwasilishaji.
WITO
Wito wangu, Naomba mamlaka zinazohusika, Ukiwemo Uongozi wa chuo, Wizara ya Elimu kufanya uchunguzi dhidi ya swala hili,
Ili niweze kusoma kwa Amani na Utulivu kwa kipindi chote nitakachokuwa chuoni.
Ahsante.
Naitwa Abdul-Aziz Ally Carter, Mwanafunzi wa Mwaka wa 3 chuo kikuu cha Dar es salaam (UDSM) nasomea Historia na sayansi ya siasa, namba yangu ya usajili 2021-04-01016
Siku za karibuni nimekuwa active katika harakati za chuo hasa kupigania maslahi ya wanafunzi waliozuiliwa kuingia katika mitihani kwa kushindwa kulipia Ada na kucheleweshwa kwa malipo ya Boom.
Toka niwe active katika harakati hasa kipindi hiki, Maisha yangu yamekuwa magumu kitaaluma hasa katika Uwasilishaji (semina),
Katika semina ya leo, ya kozi ya "Public administration in Tanzania" yenye kozi code PS 341, Siku ya Jumanne Saa 8:00 mpaka 9:00 , inayofanyika Venue ya SR 5 na kusimamiwa na Kiongozi wa semina ( Seminar leader) aitwaye Moses Boaz,
Course instructor wa semina hii ni Prof E.Mallya, Ofisi yake ni namba 802 Jengo la COSS Tower.
Katika Uwasilishaji (presentation) ambapo kikundi cha watu watano (5) walifanya Uwasilishaji na Mimi nikiwemo,
Kiongozi wa semina (Moses Boaz) alisema nimekosea kutoa maana ya msamiati uitwao " Politicization"
UTATA
Kwanza, maana ya msamiati huo niliutoa kwenye vyanzo vya vinavyoaminika vilivyopo kwenye course outline iliyotolewa mwanzo wa semister,
Pili; Kiongozi wa semina ana wajibu wa kumrekebisha/ kumsahihisha mwanafunzi pale anapokosea katika semina kwa lengo la kumsaidia na kumjengea uwezo,
Tatu; Katika kikundi cha Uwasilishaji cha watu watano ( 5) ambacho kimekutana, Kikajadiliana na kukubaliana maudhui ya Uwasilishaji, ni mtu mmoja tu aliyekoselewa kwa vitisho ambaye ni Mimi ( Abdul-Aziz Ally Carter),
VITISHO
Kwanza; Kiongozi wa semina alitaka Mimi pekee yangu kati ya watu watano (5) Kulihama grupu hilo na kuamia grupu lingine kwa lazima,
Pili, Kiongozi wa semina alisema atanipatia "zero" kwenye kazi ya alama kumi (10),
Tatu, Kiongozi wa semina amesema nisipojiangalia nita rudia kozi mwakani (carryover),
Kiongozi wa Semina (Moses Boaz) alianza kuzitoa Kauli na lugha kali kama hizi juu yangu katika semina ya wiki iliyopita tukijianda kuhudhuria muadhara wa Uprofesa.
USHAHIDI
Kauli hii kaitoa kwenye chumba cha semina kikiwa na wanafunzi wote wa semina hiyo,
Wanafunzi ni mashahidi.
MTAZAMO WANGU
Kauli na Vitisho vya namna hii vimeanza baada ya harakati za kuwapigania wanafunzi waliozuiliwa kufanya mitihani kwa sababu ya kukosa Ada,
Kiongozi wa semina, Alihusisha maswali yangu ya kutaka kujua sababu za kauli alizotoa na harakati zangu kuanzia wiki mbili nyuma.
Kiongozi wa semina alizungumza kwa Hasira na Jazba, katika mazingira ambayo Jazba na Hasira haikupaswa kutumika,
Kwa mazingira hayo, nahitimisha kwamba sababu ya kilichotokea kati yangu na msimamizi wa semina (Moses Boaz) ni Harakati na siyo makosa ya Uwasilishaji.
WITO
Wito wangu, Naomba mamlaka zinazohusika, Ukiwemo Uongozi wa chuo, Wizara ya Elimu kufanya uchunguzi dhidi ya swala hili,
Ili niweze kusoma kwa Amani na Utulivu kwa kipindi chote nitakachokuwa chuoni.
Ahsante.