Ukiwa Dar es Salaam unaweza kudhani maisha umeyapatia, kumbe umechelewa sana bila kujua

Dar hakuna maisha mazuri kwa watafutaji ila kuna mzunguuko mkubwa wa pesa kwa watafutaji

Nawahakikishia vijana wa dar pesa wanapata tena nyingi tu ila hawafanyi malengo sawa na vijana wa mkoani kwa sababu ya sketi yani pesa zinarudi zilikotoka chap kwa haraka
 
Hongereni kwanza mliochangia huu Uzi maoni yenu nimeyapenda Ila naona hisia zimetawala kuliko akili .


Naomba nidokezee jambo ambalo linaweza kutofautisha maisha ya dar na mikoani .

Mindset - mtazamo wa mtu mmoja mmoja .

Ukija DSM ukata kuishi Kama ukivyokuwa unaishi kijijini haitakuchukua round uta-lost haraka

Mfano zile mentality za kijijini za kuamini kuwa mafanikio ni Nyumba ,Gari na wanawake basi haitakuchukua round utakaa nje ya mchezo.

Miji mikubwa yote duniani inahitaji utumie akili Sana kuliko nguvu na uishi kwa kufatisha mifumo ya watu waliofanikiwa na sio kuiga mediocre life.


Mfano mjini utajiri wa kwanza ni ule wa watu network , mjini ukiwa na network tayari kwako swala linalohusu pesa unakuwa umeshaliweka sawa.


Na Kwa kijijini utajiri mkubw ni hayo mashamba na mifugo.


Sasa kinachotokea kuna ambao wanaishi mjini Ila wana akili Kama za mtu aliyepo kijijini hawa ndo utawakuta wanalalamika kuwa maisha ya dar ni magumu Sana. Kitu ambacho sio kweli .

Na kuna amabao wanaishi kijijini Ila wanaishi kijijini Kwa akili Kama za mtu aliyepo mjini mfano unakuta mtu yupo kijijini Ila hana shamba wala mifugo inayoeleweka zaidi ya kutegemea michongo ya kulimia watu mashamba Kama kibarua na kuwatengezea watu gongo.


So hakuna sehemu ambayo mtu hawezi Ku-beat odds iwe kijijini au mjini

pia katika uchumi inategemea na mtu anachukuliaje mfano wahindi hawana Nyumba Ila wanamiliki cash flow sasa hawa hauwezi kuwafananisha na waswahili ambao wamejenga Ila pesa hawana.

So ikiwa ilishundwa kutoboa sehemu fulani usiseme kuwa hiyo sehemu watu wengine hawawezi Ku-beat the odds.
 
Ukweli mtupu, Dar kama huna konekisheni bora uwe Chilwa kuna maeneo ukipanda mkonge 15ml kwa mwaka unazo
 
Sasa hayo maisha mbona hawayapati..wanaishi kama wanyama. Mtu anakimbizana na magari kwenye jua kali kwenye barabara anauza maji au karanga ni mateso tu.
Huko mikoani kwenu wote mna maisha ya juu? Last time I checked huko ndio kuna umaskini kuliko Dar. Chances za kutoboa Dar ni kubwa kuliko sehemu yoyote hapa Tz.
 
Huko mikoani kwenu wote mna maisha ya juu? Last time I checked huko ndio kuna umaskini kuliko Dar. Chances za kutoboa Dar ni kubwa kuliko sehemu yoyote hapa Tz.
Nilimjibu mwenzako hapo juu mimi mzaliwa wa Dar. Nimejenga Dar na nilirithi nyumba Dar tena prime area. Hivyo Dar ni my domicile yaani nazikwa Kisutu. Hapa tunajadili uchumi na kufanikiwa kimaisha, wengi wa mnaokuja mjini mnaishia umachinga na sasa hivi bodaboda au mnaishia kukata viuno kwenye bar ili kujikimu hayo si maisha.
 
Umenikumbusha nilikuwa zangu maeneo ya kimara temboni miaka kazaa imepita jamaa zangu nikawaaga kuwa naenda zangu mikoani nikasalimie ndugu nikakuta watu wanaishi DUNIA YAO NYINGINE nafika nikiwa najiona mjanja mjanja kumbe ni mjanja wa maneno na mipango ya badae Mjomba alikuwa mlimaji na kipindi hiko alikuwa anauza miti Eka 5 ilikuwa Ina miaka 7 akapewa M 35, Mwanae Nina umri naye sawa alikuwa ana miti Eka 3 Zina miaka 3 na analima mpunga akatokea jamaa mjini GEITA alikula hasara baada ya kununua marudio ya Dhahabu jamaa alikuwa na gari ndogo TOYOTA IST,,,, akawa anaiuza MILION 7 namba D mtoto wa Mjomba akampa Akamwambia mzee anataka ainunue Mjomba hakuwa na hiana kwa mwanae Akamwambia ww umekuwa miaka 28 Unaweza kununua Mimi Mjomba na binamu tukaenda Mashine wanapokobolea mpunga ndio wanapotunzia nikakuta Binamu anajunia 100 akatoa Junia 70 akakoboa na kuuza papo papo tukaifata chuma ya ujanani.... Da nilishangaa jamaa MILION kazaa anacheza Nazo basi bana ikanivutia na Mimi kuanza kulima mpunga nikajifunza safi safi nikapata kamtaji maisha yanaendelea Leo huku junia 110000 kwenu huko shingapi
 
Wewe huna hata Banda dar acha uongo humu
 
At least You Got a lesson. Hukukaza Fuvu
 
Ni Ushauri tu we kama unaona ni Chuki kuukubali au kuukataa ni juu yako.
 
Dar imejaa Waajiriwa hata wafanya biashara ni wachache.
 
Ni kweli ni muhimu Mtu kujiangalia Yeye kama Yeye, sio kujichanganya na waliofanikiwa na wewe ukajiita umo.
 
Ni Ushauri tu we kama unaona ni Chuki kuukubali au kuukataa ni juu yako.
Ushauri uliojaa manung'uniko๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚ Daslam yenyew haihitaji VISA kwenda na bado mnalalamika.Ingekuwa ukifika Mbezi Luis unaombwa passport mbona mngepasuka sana.

Asiwadanganye mtu hata matajiri wa mikoani huwa hawakauki Daslam.Hizo ngebe za kumiki sijui vitu gani vya huko kolomije haifikii hadhi ya Kiwanja cha 20ร—20 kwenye jiji la Chalamila.

Daslam ndio mji wenye hadhi Tz yote, huko kwingine kunahesabika kama nchi jirani na Tz( Daslam).
 
๐Ÿ˜…๐Ÿ˜…
 
๐Ÿ˜…๐Ÿ˜…
Uza mali zako huko mkoani kwako nenda Magomeni au Kinondoni kuna watu wananyumba za urithi zinauzwa tafuta mwanasheria, nunua vunja shusha kasri lako hapo mjini๐Ÿคuishi kifalme kama umezaliwa hapo.

Daslam bado haijapata mpinzani tusijifariji mikoani huku tupo tu kwasababu ya hali za kimaisha ila kila mtu katika nchi hii anapenda akae mjini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ