Ukiwa kama abiria unasafiri safari ya mbali ni vizuri ule nini njiani na uepuke kula nini

Ukiwa kama abiria unasafiri safari ya mbali ni vizuri ule nini njiani na uepuke kula nini

Tlaatlaah

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2023
Posts
24,665
Reaction score
25,388
Safari ni hatua, Safiri salama.

Mpendwa,

Mthalani abiria anasafiri kwa basi kutoka mkoa moja kuelekea mkoa mwingine.

Ni aina gani nzuri ya vyakula avitumie njiani na aina gani ya vyakula abiria huyu msafiri aviepuke kula njiani, ili hatimae safari yake iwe tulivu, huru, nzuri na salama kiafya?
 
Kuna vile Viepe hua unakuta wameweka kwenye kimfuko tayari, chukua hiyo na zile Juisi za Avocado (Wanatengenezeaga nyumbani) hua kwenye chupa za soda za take away, kula kabisa

Ukiwa ndani ya gari, utanishukuru baadae.
Hivyo kila stendi lazima upate mkuu.
 
Kwa safari, pata zaidi vinavyokaangwa
kuliko vinavyochemshwa

Mfano kula zako
Chips
Kuku
Yale mapande ya mbuzi na ng'ombe
Biskuti
Yai la kuchemsha lafaa maana lipo sealed
Pata maji kiasi tu
Eeh, wataongezea
 
Kuna vile Viepe hua unakuta wameweka kwenye kimfuko tayari, chukua hiyo na zile Juisi za Avocado (Wanatengenezeaga nyumbani) hua kwenye chupa za soda za take away, kula kabisa

Ukiwa ndani ya gari, utanishukuru baadae.
Hivyo kila stendi lazima upate mkuu.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] naona unataka ampe Dereva kazi yakusimama Kila baada ya dkk 5
 
Tafuta Biscuits mfano; Digestive kabox kakubwa, juice, maji, peremende mchanganyiko, hivi ni vya kuanzia safari hadi unafika, maana safarini siyo sehemu ya kushindilia tumbo.

Njiani sasa mle mnaambiwa 'kuchimba dawa dakika 10, shuka kanywe chai moto ya rangi na bites kidogo, achana na kubeba machips au maubwabwa.

Binafsi safarini huwa nanunua mapema Brown bread, mix jam juice na maji hadi nafika, bila kusahau peremende.
 
Tafuta Biscuits mfano; Digestive kabox kakubwa, juice, maji, peremende mchanganyiko, hivi ni vya kuanzia safari hadi unafika, maana safarini siyo sehemu ya kushindilia tumbo.

Njiani sasa mle mnaambiwa 'kuchimba dawa dakika 10, shuka kanywe chai moto ya rangi na bites kidogo, achana na kubeba machips au maubwabwa.

Binafsi safarini huwa nanunua mapema Brown bread, mix jam juice na maji hadi nafika, bila kusahau peremende.
hii muzuri zaidi 👌💪
 
Classic vip wanakula short cakes,juisi au vinyama kidogo vya kukaanga!

Changanyikeni utakua wanakula miwa, mahindi, supu mara mtoto ananyonyeshwa ziwa lote nje, abiria wamepakata virushi vya mabegi na mifuko mapajani!!
 
Safari ni hatua, Safiri salama.

Mpendwa,
Mthalani abiria anasafiri kwa basi kutoka mkoa moja kuelekea mkoa mwingine.
Ni aina gani nzuri ya vyakula avitumie njiani na aina gani ya vyakula abiria huyu msafiri aviepuke kula njiani, ili hatimae safari yake iwe tulivu, huru, nzuri na salama kiafya?
karanga za kukaanga ama korosho na kama ni nyama iwe ya kukaanga
 
Katika stadi za Kazi tulifundishwa Kula vyakula vikavu....mfano ndizi /viazi Choma au vya kukaanga.
Nyama Choma au za kukaanga.....usipendelee vyakula vilivyotengenezwa Kwa kutumia mayai au nyama za mchuzi hasa zilizolala utajuta.
 
Kula mahindi ya kuchemsha, mayai ya kuchemsha, mtindi uliochachuka sana na karanga. Hakika safari yako itakuwa nzuri na tulivu.
Kama utapata na juisi ya maembe ile ya kutengeneza au juisi ya miwa pia ni nzuri upande wa kinywaji yaani safari itakuwa taaam!
 
Ni vizuri usile.

Aibu ya kusumbuliwa tumbo njiani ni mbaya sana....

Usile kabisa, au kunywa chai asubuhi tu...
actually ndio chimbuko la bandiko langu, nimesafiri hivi leo akatokea abiria moja kwa utambulisho wa mavazi na lafudhi alikua mmasai,
Na alipandia basi letu njian na basi halikua na choo cha ndani na abiria huyo hakua amepata siti alisimama...

Ndugu yangu ,
kwa bahati nadhani tumbo likamvuruga na kufurukuta, akatoa sauti kubwa simamisha gariiiiiii, abiria wakawa wanamshangaa......

Akashauti tena mara ya pili simamisha gariiiiiii nichimbe dawa tumbo imefurugaaaaa tumbo yangu maskini abiria yule mpaka akakaa chini.......

Abiria wakashtuka na kuona kwamba sasa huyu anaporomosha muharo sasaivi...

Ndipo kelele za abiria zikasaidia dereva wa basi akasimamisha, abiria yule hakua amevaa chochotete ndani zaidi ya shuka alizokua amejifnga, na aliposhusha mguu njee ya mlango wa basi tu, palepale akafanye yake pwraaaaaaaaaaa akashusha muharo wa nguvu sana....

alipomaliza akakusanya kitita cha majani makavu akajichamba nayo mara mbili akawa anaingia kwenye basi, abiria wakashauti wakagoma hadi ajichambe na maji....

wakamrushia chupa za maji akajichamba vizur ndipo akaingia kwenye basi tukaendelea na safari....

So,
milo ni muhimu izingatiwe kabla, wakati na baada ya safari...
 
Back
Top Bottom