Ukosefu wa maadili unatisha kwa kasi unayoporomoka Tanzania

Wapi tunakosea? Nini kifanyike?
 
Wazazi/Walezi/Walimu/Viongozi wa dini wajitambue na kulichukua jukumu la malezi serious,Serikali pia ihusike kwa namna moja ama nyingine.
Tumshauri nini waziri wetu wa ustawi wa jamii? Maana masikini ya Mungu, ndiyo kwanza plan ya wizara yake ipo kwenye kuandikwa. Wanayoiandika anafahamu mwenyewe ni akina nani.

Wajibu wetu tujadili na kushauri, wakiyapokea haya, wasipoyapokea haya.

Dkt. Gwajima D
 
Sasa watoto wadogo wanaona vibao kata huku mitaani unategemea nini
Wasaz wao wenyewe wanashiriki vibao kata huku wanajumuika na watoto zao
Baba mama mkononi wameshikilia smartgean

Ova
Hilo nalo neno.

Utakuta watoto wadogo wa kuanzia miaka 3 nyumbani wanachezeshwa kukata viuno, na watu wazima, wazazi wakiwemo ndiyo wanamsifia na video clips kuchukuwa na kutumiana kwenye jamii, kama vile kile wanachokishadidia ni chema sana.

Jamii inayaona, inayatazama na kuyachekelea tu. Inabidi kama jamii, unapotumiwa kitu kama hicho tukemee kwa ukali japo aliyekutumia aamke aelewe kuwa hilo si jema.
 
Ukitaka kujua maadili yamekua ya hovyo kwa vijana, tembelea Arusha, usikie kiswahili chao, uone mavazi yao, na namna wanavyo jifananisha ktk kitu wasicho nacho, unaona wazi kabisa tunakoelekea ni kubaya sana sana kwa vizazi, wakidhani kupokea watalii watakua ni kama hao watalii ktk maisha yao, kumbe wako Arusha ktk Africa, na mtalii atarejea kwao kuendelea na utamaduni wake

Mji huu unaongoza kwa maadili machafu hapa nchini
 
Ulitaka nieneze chuki za upagani?


Kama wewe huna dini unataka wote tusiwe na dini? Kukosa dini ndiyo chanzo kikuuu cha ukosefu wa maadili.

Kama huna dini hayo maadili utajifunza kutokea wapi?
Wewe unazungumzia maadili ya dini yako?
 
Umeainisha matatizo, hilo ni la kwanza. Linalofatia ni kila tatizo tulichukulie kulitatuwa kwa falsafa ya "Resilience", tuligeuze kuwa fursa.

Tuitafute fursa ya namna ya kuokoa jahazi na kurekebisha tulipokosea ili tusitatuwe kosa kwa kufanya makosa zaidi.

Suala muhimu linalotukabili, ni nini kifanyike kwa kila tatizo tulilonalo linalotuathiri kumomonyoka kwa maadili kijamii?
 
Wewe unazungumzia maadili ya dini yako?
Sielewi kama kuna "dini" ambayo haifundishi maadili mema. Ikiwepo hiyo itakuwa ni ya Kishetani, maana ushetani siku hizi umejaa.

Kabisa, tena kwa kujivunia dini yangu, mimi nazungumzia maadili niliyojifunza kwa mafunzo ya Kiislam.

Una wasiwasi na mafunzo ya Kiislam kimaadili?
 
Wewe ni kama unasema hakuna maadili ya kiafrika tofauti na hayo yaliyoletwa na wageni.

Kumbuka umesema “bila dini hakuna maadili”

Hilo siyo kweli.
 

Chakufanya ni kuwa kila mtu afanye wajibu na majukumu yake.
Mtoto hana wajibu wa kujilea wala kulea wazazi wake.

Unampa mtoto jukumu la kujilea unajiondolea haki na wajibu wake wa kukuheshimu.

Mtoto akutunze umeshafikisha miaka 60 kuendelea.
Lakini sio kuendekeza uvivu na kumpa majukumu mtoto huyo ni uhuni na Sisi tutausema siku zote. Hilo nimeliona sana.

Angalia watoto wengi waliokosa maadili utagundua asilimia 90% wazazi wao wamekimbia jukumu la malezi.
Nenda kaangalie Malaya, nenda Bara, angalia Wadada wa majumbani, nenda kwa machokoraa.

Vijana wanajitutumua kufanya kazi zozote ilimradi wawatumie WAZAZI (wabinafsi) pesa za kuwatunza.
Alafu huyo mzazi mwenyewe unakuta nguvu anazo, umri haujaenda, kuumwa haumwi. Hiyo ni akili au matope.

Acha mambo yaende jinsi yalivyo. Hiyo ndio namna ya kuisadia dunia. Acha mambo yaende vile yaendavyo.
Hiyo ndio maana ya kizazi cha nyoka.
Unazaa watoto, alafu watoto wanajilea wenyewe
 
Hao watalii wenyewe wanatushangaa sisi kuliko wanyama wanaokuja kuwaona.
 
Wewe ni kama unasema hakuna maadili ya kiafrika tofauti na hayo yaliyoletwa na wageni.

Kumbuka umesema “bila dini hakuna maadili”

Hilo siyo kweli.
Naam nimesema hivyo. Labda tunachotofautiana ni uelewa wa neno "dini".

Wewe ukisikia neno "dini" linamaanisha nini kwako?
 
Hayo majukumu ya wazazi ndiyo yepi? Tuwe specific, maadili huwezi kuya "generalize."

Ndipo niliposema, unaloliona wewe silo, mzazi mlezi mwengine analiona ndilo bora.
 
Hayo majukumu ya wazazi ndiyo yepi? Tuwe specific, maadili huwezi kuya "generalize."

Ndipo niliposema, unaloliona wewe silo, mzazi mlezi mwengine analiona ndilo bora.

Jukumu la mzazi ni kuhakikisha anamlea mtoto mpaka atakapojitegemea, kwani hao wazazi wanashindwa akili na wanyama?

Malezi ni pamoja na kumfundisha mtoto tabia njema, uadilifu, nidhamu, kazi na stadi za Maisha. Ili mtoto ajitegemee.

Na ili mtoto ajifunze hayo yote lazima wewe kama mzazi lazima uwe mfano kwake(Role model)
Kama mzazi mwenyewe huwezi kujitegemea utamfundishaje mtoto ajitegemee?
Hapo ndipo maadili yanapoanza kuyumba, kwenda alijeje.

Mtoto utamfundishaje aache aheshimu Watu ilhali anaona kila siku unawatukana, unawadhulumu, unatoka na waume/wake za Watu?

Au malezi ni hotuba za maneno zilizowashinda wazazi?

Nimeshakuambia Nyoka hazai jongoo.
 
Kizazi cha 2000+ kina laana...[emoji28]
 
Malezi, tunaiga sana ughaibuni.

Mtoto ana maamuzi, kipi afanye kipi asifanye. Mtoto ananyolewa/kusukwa mitindo ya kiutu uzima anayoona wasanii wavaa utupu wanasuka/kunyoa.

Mtoto anaveshwa hovyo kama kina zuchu na nandy. Mpaka anajitambua akiona mtu kavaa nguo ndefu anamshangaa coz yeye hawezi.

Mtoto anakua akiona tamthilia za mapenzi, makiss kama yote.

Na mbaya zaidi mtoto anakua haijui dini maana si baba wala mama wanaenda msikitini/kanisani wala kumpa nasaha zozote mtoto, zaidi ya kusherehekea kila sikukuu ya kidini.

Yaani madogo wanakua kingonongono tu. Wamedekezwa kiasi kwamba hawezi kuishi na mtu mwingine.

Hawa wa sasa ni cha mtoto subiri 2030.
 
Jukumu la mzazi ni kuhakikisha anamlea mtoto mpaka atakapojitegemea, kwani hao wazazi wanashindwa akili na wanyama?

Subiri niyakatekate majibu yako yajadilike vizuri.

Hilo swali lako umeliuliza kijazba sana, umekuwa "emotional" zaidi ya kujibu.

Nikufahamishe falsafa kidogo; Binaadam ni hatari kuliko mnyama yeyote unayemjuwa wewe duniani. Labda pia nikufahamishe kisayansi, sayansi inajitahidi kutuaminisha kuwa Mwanadamu ni mnyama.

Kidini (Uislam); Binadam siyo mnyama.

Sifahamu kiimani zingine.

Kama wewe ni mtu unayeiamini sayansi zaidi ya Uislam, jibu umeshalipata, kuwa binadam kama ni mnyama basi ni lazima atashindwa akili na wanyama wengine. Hapo hakuna utata.

Lakini Kiislam kama nilivyokwambia juu hapo, mwanaadam siyo mnyama na hawezi kushindwa akili na mnyama, mwanadam anatakiwa awe ni msimamizi (kwa wenzake) na kila kilichopo duniani, wakiwemo binadam wenzake.
 
Tatizo binadamu wa siku hizi ni wabishi sana...
 
Malezi, tunaiga sana ughaibuni.

Mtoto ana maamuzi, kipi afanye kipi asifanye. Mtoto ananyolewa/kusukwa mitindo ya kiutu uzima anayoona wasanii wavaa utupu wanasuka/kunyoa.

Mtoto anaveshwa hovyo kama kina zuchu na nandy. Mpaka anajitambua akiona mtu kavaa nguo ndefu anamshangaa coz yeye hawezi.

Mtoto anakua akiona tamthilia za mapenzi, makiss kama yote.

Na mbaya zaidi mtoto anakua haijui dini maana si baba wala mama wanaenda msikitini/kanisani wala kumpa nasaha zozote mtoto, zaidi ya kusherehekea kila sikukuu ya kidini.

Yaani madogo wanakua kingonongono tu. Wamedekezwa kiasi kwamba hawezi kuishi na mtu mwingine.

Hawa wa sasa ni cha mtoto subiri 2030.
 
Tatizo chama cha mambuzi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…