Hadithi ulizoweka haziko wazi kuonyesha siyo sahihi, sababu ya kwanza nilikuuliza kwani Mtume ameswali sala ya Khofu mara ngapi ?MKuu unazunguka ila Sijaona Kuhusu Jibu kuhusu Hadithi nilizokupa...maana Ziko wazi kabisa..
zijibu kwanza Hadithi hizo..
Maana nimeshakujibu Sanadi zao Hazina shaka ila matini ndo yana mashaka sasa hebu zijibu hizo matini acha Kuzunguka..
Je, Abu hurairah aliposema Mtume amesema na baadae watu walipomzonga kumuuliza Akiri mtu kasema na akabadilisha na kussma kassma yeye sio mtume hakudanganya?
Je, Abu hurarah aliposema aliswali swala ya Hofu na mtume mwaka wa 5 wa utume wakati Abu Huraira alikuwa hajasilimu kwa sababu alisilimu mwaka wa 7 wakati ilipotekwa ngome kuu ya Mayahudi Khaibar hakusema Uongo???
Au unaogopa Kusema Abu huraira Alisema uongo kwa sababu ndo anaongoza kwa isnad za Hadithi nyingi zaidi?
Lakini, uchambuzi wako wa hadithi sio sahihi sababu hujachambua sanadi tujue kweli maneno hayo ni ya swahaba Abuu Huraira au la. Lazima turudi kwenye asili kwanza.
Kwanza thibitisha ya kuwa hayo maneno aliyasema Abuu Huraira, ili iwe ameyasema chambua sanadi kwanza.
Kwenye hadithi haionyeshi ya kuwa alisema aliswali hiyo Sala mwaka wa 5. Ndio maana nikakuuliza je Mtume aliswali mara ngapi swala ya Khofu ? Hujajibu hili swali.
Siyo kwamba naogopa bali Abuu Huraira hawezi kusema uongo, ndio maana nataka uchambue sanadi kwanza kabla ya matini. Usiruke hatua za uhakiki wa habari.
Unachokifanya wewe uko nje ya misingi ya elimu ya Hadithi, na hizi tabia wanazo sana Mashia katika kuwatusi maswahaba wa Mtume.
Umejuaje kama hazina shaka na haujafuwekea uchambuzi wa sanadi hiyo, kwa kitabu ulichokuwa nacho, kimekata sanadi Sasa tafuta chenye sanadi utuchambulie kwa mujibu wa elimu ya Hadithi usahihi wa sanadi hiyo.