Ukuaji wa lugha ya Kiswahili: Neno Mbashara

Ukuaji wa lugha ya Kiswahili: Neno Mbashara

Hii yako ulitakiwa useme naangalia mpira wa miguu matangazo " mubashara" huku nikiwa tufaa na sharubati mkononi.
Angesema "naangalia mpira wa miguu mubashara huku nikinywa sharubati ya tufani".

Sent from my TECNO-W3 using JamiiForums mobile app
 
Mpulukio=>ushoroba katika uwanja wa ndege ambapo ndege hupuluka
 
Sikuwahi kufahamu kuwa katika kiswahili kuna neno linaitwa mubashara, likimaanisha "matangazo ya moja kwa moja yaani live".

Jana kwa mara ya kwanza nilivyoona hilo neno chini ya nembo ya ITV nilidhani ni kifupisho cha maneno fulani.

Hivyo tuendelee kujifunza lugha yetu adhimu:

Mbashara (si mubashara) = Live
Sharubati = Juice
Tufaa = Apple
Nywila = Password

View attachment 467982

Hapo neno jipya ni "nywila" tu. Kwa Waswahili hayo mengine tumeyakuta na yapo enzi na enzi.

Hujasikia, mbashiri? Basi hata kina Bashiri? Au kubashiri? Yote hayo yanahusiana na neno mbashara.

Sharubati halina upya wala tofaha halina upya ni upunguani wako tu.
 
Neno "mubashara" ni jina la kiarabu la msichana likimaanisha "mleta habari njema". Matangazo ya moja kwa moja kwa kiingereza ni "live broadcast" ambapo ukifasiri kwa kiswahili ingefaa kuwa "matangazo hai".
Wewe ndio miongoni mwa watu mliotafsiri Central Police kama Kituo cha kati cha polisi badala ya Kituo Kikuu cha Polisi
 
Wikipedia wanasema Mubashara na sio Mbashara, yupi yupo sahihi!?
 

Attachments

  • Mubashara - Wikipedia, kamusi elezo_ - https___sw.wikipedia.org_wiki_Mubashara.png
    Mubashara - Wikipedia, kamusi elezo_ - https___sw.wikipedia.org_wiki_Mubashara.png
    34.5 KB · Views: 60
Sikuwahi kufahamu kuwa katika kiswahili kuna neno linaitwa mubashara, likimaanisha "matangazo ya moja kwa moja yaani live".

Jana kwa mara ya kwanza nilivyoona hilo neno chini ya nembo ya ITV nilidhani ni kifupisho cha maneno fulani.

Hivyo tuendelee kujifunza lugha yetu adhimu:

Mbashara (si mubashara) = Live
Sharubati = Juice
Tufaa = Apple
Nywila = Password

View attachment 467982
Msimbo=code

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo lako ni kwamba unajizuia kufikiri ndio maana umekimbilia kutia maneno kinywani mwangu.
Sorry mkuu kama nimekukwaza au nimeandika kwa lugha ambayo imekuumiza lakini kusudio langu lilikuwa ni kwamba sio lazima neno litafsiriwe kwa neno kama yaani "live broadcast" iwe matangazo hai ndo nikatoa mfano wa wale waliotafsiri Central police kuwa kituo cha kati badala ya kituo kikuu...otherwise ni majadiliano tu mkuu na sifa yetu wanadamu ni kutofautiana mawazo lakini mwisho wa siku kinapatikana kilicho bora..samahani kwa mara nyingine tena
 
Back
Top Bottom