Ukweli hausemwi. Kilimo cha Parachichi ni kigumu sana na pesa yake ni ndogo

Ukweli hausemwi. Kilimo cha Parachichi ni kigumu sana na pesa yake ni ndogo

Jipe moyo tu mzee baba ila nikwambie ukweli tu kwamba kilimo cha kibongo walanguzi na madalali ndio wanaopiga hela 😂
Na huu ndo ukweli nakumbuka kuna mtu alipeleka maembe kiwanda fulani cha juice, kufika tu pale madalali hao kumbe pale kiwandani kuna madalali ambao wao ndo wana connection za kuuza maembe mle kiwandani basi jamaa akagoma kuwapa madalali mzigo wakamwambia utaona, jamaa kuongea na afisa manunuz afisa akamwambia malori ya matunda yana foleni zake hivyo asubiri wiki nzima ndo na yeye atapewa kuingiza maembe yake auze jamaa akasubiri aisee wiki imeisha na embe zimeanza kuiva kupitiliza muda huo woote madalali wanazengea jamaa alegeze msimamo jamaa kumcheki tena afisa manunuzi afisa akamwambia asubirie tu dah jamaa ilibid alegee tu mwenyewe akawapa madalali tena kwa bei ya kutupa tu na ndo ikawa mwisho wa kilimo cha embe
 
Leo njombe parachichi bei kilo Moja madalali wanasema ni shillingi 500 na wanapakia lumbesa utaki unaacha . Na parachichi ikiwa over matured awanunui
Kuna siku niliona video clip inasambaa watsup ya RC wa huko Njombe akiwashawishi wale diaspora sijui wanaishi marikani wale kwamba ndani ya mkoa wake Kuna fursa kubwa sana ikiwemo ya kilimo cha parachichi pia viwanda ambavyo vinanunua kwa bei nzuri mno. Sasa sijui wale diaspora walishannua maeneo kwa ajili ya kilimo cha hizo Hass, dah Sema yule RC ukimsikiliza ni pure joy to listen he's talented ana power ya ushawishi, maana alivyouongelea mkoa ni kama wana land use planning nzuri sana hopefully hii ya kg 1 kwa 500 haitawapata diaspora wetu.
 
Katika Mazao yote Ya Matunda yanayolimwa Tanzania, Wakulima wa Machungwa wanapiga hela kama Mkulima atakua Mtulivu, kilimo hiki Hakina siasa, Mtu mwenye heka Moja ya michungwa aina ya Valencia imbayo imechanganya kuzaa, kupata kuanzia milioni 6 ni mambo la kawaida, tunachoomba Mungu siasa isije ikaingia huku ,Tukaanza kuundiwa bodi,
Watu wanauza mpaka Tsh 100 kwa chungwa Moja bei ya Shamba kama unakua na Uvumilivu na unauza huku unaringa
N kweli lakn nao wanalalamika sahz Bei imekuwa changamoto
 
Mkuu wa mkoa njombe anajitahidi sana kufanya uhamasishaji wa mazao mengi yanayositawi katika mkoa wake mfano Ngano, parachichi, chai , pareto, kahawa, pamoja na miti changamoto ni mifumo jumuishi ya masoko na mikataba ya kuaminika Kwa wakulima wake Kwa baadhi ya mazao
 
Kuna watu kibao wametelekeza mashamba. Usipokua na hela usilime parachichi
 
Leo njombe parachichi bei kilo Moja madalali wanasema ni shillingi 500 na wanapakia lumbesa utaki unaacha . Na parachichi ikiwa over matured awanunui
Wakuu wa Mkoa na halmashauri wanajua mchezo wanaofanya. Wanunuzi toka Kenya wanahonga sana.

Umaskini wa Mtanzania ni watawala
Wakulima wekeni umoja mtashinda achaneni na vikao vya halmashauri vya kuwadanganya.

Wanajua mchezo mchafu
Kila anayepelekwa Njombe akiondoka anaondoka millionea.

Watawala acheni kuumiza Watanzania mkawatajirisha WaKenya

Waziri hili linakuhusu ingilia kati

Mfikishieni ujumbe Waziri wa Kilimo

Mnacheza na akili za WaTanzania vile mnataka

Parachichi linauzwa China Europe lina label ya Kenya kumbe ni zao na Tanzania

Wakenya acheni mchezo wenu mchafu.

Njombe fukuzeni wanunuzi wooooote tangazeni kama tenda wakulima woooote bei iwe moja elfu 3 kilo hutaki sogea
 
Tatizo ni aidha Tanzania haina soko la kimataifa kuuzia au maparachichi ya Tanzania hayakidhi viwango.
Sababu haiwezekani Mexico inaelemewa na mahitaji ya soko la parachichi kutoka Canada na US kwa kushindwa kukidhi mahitaji na mpaka Drug Cartels wameaanza kujihusisha na hii biashara ya parachichi kwa jinsi ilivyokuwa na faida.
Halafu huku kwetu tunalima na kulamimika ni zao halina faida
 
Wakuu wa Mkoa na halmashauri wanajua mchezo wanaofanya. Wanunuzi toka Kenya wanahonga sana.

Umaskini wa Mtanzania ni watawala
Wakulima wekeni umoja mtashinda achaneni na vikao vya halmashauri vya kuwadanganya.

Wanajua mchezo mchafu
Kila anayepelekwa Njombe akiondoka anaondoka millionea.

Watawala acheni kuumiza Watanzania mkawatajirisha WaKenya

Waziri hili linakuhusu ingilia kati

Mfikishieni ujumbe Waziri wa Kilimo

Mnacheza na akili za WaTanzania vile mnataka

Parachichi linauzwa China Europe lina label ya Kenya kumbe ni zao na Tanzania

Wakenya acheni mchezo wenu mchafu.

Njombe fukuzeni wanunuzi wooooote tangazeni kama tenda wakulima woooote bei iwe moja elfu 3 kilo hutaki sogea
Wakigomea kununua hayo maparachichi,wakulima watayapeleka wapi?
 
20240615_162158.jpg
 
Tangantika atakwambia yeye ana mbinu. Mimi niliwaonya nikaondoka zangu
Nipo hapa nimerudi jukwaani nilikiwa likizo. Wabena waache wapigwe za USO. Mwaka jana wameniibia miti yangu kama ishirini yenye umri mkubwa pumbabu zao. Mwaka huu wameuza parachichi sh. 200 naomba mungu waendelee kupigwa mpaka waisome namba waache wizi. Wanapata laana ya wizi. Wanatabia ya kuchoma moto hovyo.
Mimi mtoto wa mjini husler sintauza AVOCADO SH 200! Yaani mimi mtoto wa uswazi nikalime BUSH avocado halafu niiuze kwa 200 ! Mimi nina plani yangu, parachichi zangu bado haziijaanza labda mwakani nipo eneo la barafu napambana nakujaribu kufanya innovation mbali mbali kuepusha barafu isiue miti.
By now siwazi kuhusu bei wenye parachichi watajiju. Wakulima waache waendelee kupigwa tu ili wakate tamaa.
Mimi nina PLAN.
 
Nimefanya kilimo cha parachichi kwa miaka nane sasa, nilichokiona ni haya;

1. Kilimo kina mzunguko wake ni mdogo parachichi huzaa kidogo kidogo kadri miaka inavyoenda, unatumia million 10 unapata million mbili.
2. Bei hazijadiliki anayeamua ni mnunuzi unless uwe na mtaji mkubwa ambayo unakuruhusu ku export mwenyewe, na uwe na uwezo wa kuwa na cold room Ili zikikomaa uchume uzihifadhi kama bei hueilewi kwa kipindi hicho (hii mitaji watanzania wengi hatuna). 3. Management ya parachichi ni ngumu sana linahitaji maji kidogo (hapa unaweza manage kumwagilia) linahitaji mbolea za chumvi na mbolea za majani, sumu. Kila nk kwa kiasi kidogo, linahitaji muda Kwa wingi, upatikanaji wa Samadi ni mtihani sana (wengi wamejikuta parachichi zimedumaa na wengine wanazalisha reject kwa wingi) kisa tu wameshindwa kuwa na Samadi, udhibiti wa nyasi (ukweli ni kuwa Ili miti iwe Bora unahitaji kulima badala ya kufyeka nyasi)

Nimefanya observation shambani kwangu panapolimwa pana matokeo kuliko panapofyekwa, distance kati ya mti na mti inamua sana miti iliyokaribu inasumbua sana na mingi huwa haizai vizuri. Hizi issue zimefanya watu tukimbie mashamba yetu, hata kiwango cha pesa kinachotajwa wengi hawapati ni figure za uwongo Ili kujifariji, njoo na hoja zako kupinga zangu hapo juu, zangu ni hizo.

Nashauri kama una pesa zako kidogo lima mazao ya chakula tu viazi, mpunga, mahindi nk hivi vinalipa. Huku pesa ipo na kama location ulipo ni nzuri lima mazao yanayohifadhika like kahawa, miaka miwili inazaa, management yake rahisi. Nalima kahawa makete pia ni mwaka wa tatu tayari nimeanza kuvuna.

NB: Mazao ya chakula ndio kila kitu hizi nyingine tabu umezitafuta.
Ogo tata pole sana .
 
Nopo hapa nimeridi jukwaani nilikiwa lokizo. Wabena waavue wapigwe za USO. Mwaka kana wameniibia miti yangu kama ishirini uenye umri mkubwa pumbabu zao. Mwaka huu wameuza parachichi sh. 200 naomba mungu qaendeoee kupigwa mpaka waisome namba waache wizi. Wanapata kaana ya wizi. Wznatabia ya kuchoma moyo hovyo.
Mimi mtoto wa mjini husler sintauza AVOCADO SH 200! Yaani mimi mtoto wa uswazi nikalime BUSH avocado halafu niiuze kwa 200 ! Mimi nina plani yangu, parachichi zangu bado haziijaanza labda mwakani nipo eneo la barafu napambana nakujaribu kufanya innovation mbali mbali kuepusha barafu isiue miti.
By now siwazi kuhusu bei wenye parachichi watajiju. Wakulima waache waendelee kupigwa tu ili wakate tamaa.
Mimi nina PLAN.
Shamba liko wapi mkuu nifike kukutembelea
 
Nimefanya kilimo cha parachichi kwa miaka nane sasa, nilichokiona ni haya;

1. Kilimo kina mzunguko wake ni mdogo parachichi huzaa kidogo kidogo kadri miaka inavyoenda, unatumia million 10 unapata million mbili.
2. Bei hazijadiliki anayeamua ni mnunuzi unless uwe na mtaji mkubwa ambayo unakuruhusu ku export mwenyewe, na uwe na uwezo wa kuwa na cold room Ili zikikomaa uchume uzihifadhi kama bei hueilewi kwa kipindi hicho (hii mitaji watanzania wengi hatuna). 3. Management ya parachichi ni ngumu sana linahitaji maji kidogo (hapa unaweza manage kumwagilia) linahitaji mbolea za chumvi na mbolea za majani, sumu. Kila nk kwa kiasi kidogo, linahitaji muda Kwa wingi, upatikanaji wa Samadi ni mtihani sana (wengi wamejikuta parachichi zimedumaa na wengine wanazalisha reject kwa wingi) kisa tu wameshindwa kuwa na Samadi, udhibiti wa nyasi (ukweli ni kuwa Ili miti iwe Bora unahitaji kulima badala ya kufyeka nyasi)

Nimefanya observation shambani kwangu panapolimwa pana matokeo kuliko panapofyekwa, distance kati ya mti na mti inamua sana miti iliyokaribu inasumbua sana na mingi huwa haizai vizuri. Hizi issue zimefanya watu tukimbie mashamba yetu, hata kiwango cha pesa kinachotajwa wengi hawapati ni figure za uwongo Ili kujifariji, njoo na hoja zako kupinga zangu hapo juu, zangu ni hizo.

Nashauri kama una pesa zako kidogo lima mazao ya chakula tu viazi, mpunga, mahindi nk hivi vinalipa. Huku pesa ipo na kama location ulipo ni nzuri lima mazao yanayohifadhika like kahawa, miaka miwili inazaa, management yake rahisi. Nalima kahawa makete pia ni mwaka wa tatu tayari nimeanza kuvuna.

NB: Mazao ya chakula ndio kila kitu hizi nyingine tabu umezitafuta.
Sisi wakulima wa mjini tuliaminishwa eti miaka mitatu tu umeshatajirika, tukaambiwa na vanilla sijui aise
 
Shamba liko wapi mkuu nifike kukutembelea
Mkuuu shamba bado. Nipo kwenye ZONE ya barafu na vijana niliwaachia ni wajinga wasio na vision. Lipo Njombe.
Kununua ardhi njombe ni kamali unaweza pata "frost zone" ukaisoma namba. Shamba lilikuwa la PILOT project ili nipate uzoefu nikapande kubwa. Nafikiria kubadili project sitaki mambo ya AVO yanachangamoto nyingi. Mimi bei sioni kuwa ni changamoto kubwa ila kupata matunda ndio mziki. Kuna jirani yangu yeye imekula kwake zaidi ya miti 500 kupigwa barafu, kijana alileta ubishi wa kufunikia barafu, maua yote na majani yameungua.

20240613_131144.jpg


Hapa barafu ni 500%.
 
Nimekuele
Ukitumia akili kwenye jambo lolote unalofanya utakwepa mishale kama hii. Nimesoma na kufuatilia sana parachichi kwa China na nimekubali ni biashara ngumu sana.
1. Soko lake kubwa hasa hizo Hass ni China ambapo wao soko lao linapanda na kushuka kutokana na supply wanayopata kutoka Mexico, Kenya, Australia na zaidi ya nusu kutoka Peru. Ikitokea ni msimu wa Peru huko kwingineko bei inashuka sana, muda wa kupiga hela ni pale nchi nyingine zinapokuwa sio msimu.
China iko busy kujitosheleza kwenye parachichi kwahiyo soko litazidi kupungua, na uzuri wa China ni nchi kubwa yenye usawa wa bahari tofauti sana kila eneo hivyo kila upande unaweza zalisha kwa msimu wake na zikawa sokoni mwaka mzima.

2. Teknolojia hatuna. Unavuna parachichi unapakia kwenye fuso utamuuzia nani uko nje? Hamna cold rooms, hamna grading, hakuna refrigerated trucks, hamna kupima quality, water content, protein, texture, ile nyama ya ndani, mbolea haipimwi, ardhi wanatifua tu hata hawajui ardhi gani ina nini na inakosa nini. Tunaenda kienyeji.

3. Serikali inasubiri kutoza ushuru na kodi, yenyewe hata haijui hiyo biashara na kilimo chake inafanyikaje. Hakuna support kabisa sababu parachichi zikiachwa nchi haitokufa njaa.

4. Ni zao lenye usumbufu na linataka mtaji mkubwa. Wakati huo haliuziki ndani, ukikosa soko la nje ukauza ndani unakula hasara kutokana na gharama kubwa za uendeshaji.

5. Ni zao gumu sana kuuzwa, yani hawa walanguzi wetu wakienda nje uko wanapigwa za uso kirahisi sana. Unatafuta certifications za ubora na kila kitu unapeleka msimu huu, msimu ujao unaweka mtaji wote then Wachina wanapima wanakuta water content kubwa kisa mvua zilizidi uko Niombe. Zinamwagwa, huyo mfanyabiashara atarudi?
Mwaka juzi Wakenya walizuiwa na TFDA ya China kwamba kuna mlipuko wa fruit flies parachichi zao zinaenda na mayai yake. Wakaambiwa ukitaka kuuza menya uuze ile nyama ya ndani. Sasa process ya kumenya na kuuza nyama ya ndani alafu hiyo nyama isiwe nyeusi hata kidogo sio kazi ya kitoto.

Haya yote nimeyajua nikiwa sina mpango wa kulima, ningetaka kulima ningejua mengi zaidi. Sasa mkulima yeye akisikia kwenye redio anaamka na kufyeka eneo atengeneze shamba. Content creators ile ndio kazi yao, kuongea. Usikubali kushikwa masikio
Nimekuelewa sana aisee parachichi tuko nayo hapa makambako ila mh sijaielewa sana hii tunda
 
Back
Top Bottom