Ukweli kuhusu Israel, Waarabu, na Ibrahim

Ukweli kuhusu Israel, Waarabu, na Ibrahim

Sijakuelewa hapo unaposema ismail ni baba wa waarabu kwa kuwa mama yake alikua mwarabu .inamaana waarabu wanafata koo zao kupitia kwa mama na si baba?? Kwanini ismael aendeleze ukoo wa waarabu wakati baba yake hakua mwarabu?? Kwanini asiendeleze ukoo wa kizazi chake cha babaake??

Sent from my Infinix X6517 using JamiiForums mobile app
Hajra alikuwa mmisri. Ibrahim alikuwa toka Irani ya sasa. Israel imezalliwa ilitokea misri. Hivyo mwarabu ni mwagrika na Muiran.
 
Huwezi pata majibu ya haya maswali kwa vitabu vya hadithi na masimulizi....

All in all unaenda kuchukua ardhi ya mwenzako wakati nchini kwako hujamaliza changamoto za wananchi wako? Does this make sense?? Logically & reasoning
 
Hajra alikuwa mmisri. Ibrahim alikuwa toka Irani ya sasa. Israel imezalliwa ilitokea misri. Hivyo mwarabu ni mwagrika na Muiran.
Hajra anahusikaje hapo?? Tunamuongelea ismail ,uarabuni hawafati ukoo wa mama,pia iran sio waarabu wala hawaongei kiarabu ni waajemi wanaongea aramaic
 
Hajra anahusikaje hapo?? Tunamuongelea ismail ,uarabuni hawafati ukoo wa mama,pia iran sio waarabu wala hawaongei kiarabu ni waajemi wanaongea aramaic
Mama Ishamel anaitwa nani?. Yule aliyekuwa na mwanawe jangwani. Au hujui hata alipoambiwa atakuwa taifa kubwa. Soma vitabu vyote ujue.
 
Hicho ndio ukweli ibrahim alikuwa mwajemi na kujakazi hajra alikuwa mmisri.
Hajra anahusikaje hapo?? Tunamuongelea ismail ,uarabuni hawafati ukoo wa mama,pia iran sio waarabu wala hawaongei kiarabu ni waajemi wanaongea aramaic
 
Tupeane elimu kidogo, kuna watu wanachanganya mambo. Hapa tufundishane jambo moja. Kitu cha kwanza kabisa watu wanachokichanganya ni kuhusu Ibrahim, wengi wanasema Ibrahim alikuwa Mwarabu, ndugu yangu, nikwambie tu kwamba jamaa hakuwa Mwarabu.

Ibrahim baada ya kuzaa na kijakazi ambaye alikuwa Mwarabu, inamaanisha damu yake ilichanganyika na ya Kiarabu na ndiyo maana tunasema Ishmael ni baba wa Waarabu kwa sababu mama yake alikuwa Mwarabu.

Nchi za Kiarabu ambazo zipo kwenye umoja ni hizi, Algeria, Bahrain, Iraq, Jordan, Kuwait, Djibout, Saudi Arabia, Tunisia, United Arab Emirates, Yemen, Somalia, Sudan, Syria, Comoros, Misri, Maurtania, Qatar na Palestina.

Kwa nini Waarabu wanamchukia Israel? Ni kwa sababu si Mwarabu mwenzao. Na hao ndiyo wa kizazi cha Ibrahim. Kwa hiyo kama ulikuwa unahisi Ibrahim alikuwa Mwarabu, futa hiyo akilini mwako.

Hata Iran sio Waarabu, najua wengine mtakuwa hamlijui hili kwa undani. Miongoni mwa nchi za Kiarabu, Iran hayupo kwa sababu yeye si Mwarabu.

So Israel na Waarabu ni baba mmoja ila mama tofauti. Ibrahim alizaa na Muisrael mwenzake kwa kipindi hicho ilikuwa bado haijaitwa Israel na mtoto wake kuitwa Isaka ila yule aliyezaa na kijakazi ambaye ni Mwarabu anaitwa Ishmael. Tatizo kubwa la vita baina ya Mwarabu na Israel ni hapa.

Kama Israel angekuwa Mwarabu, leo usingesikia vita vinavyoendelea huko. Na mara zote Israel anawaambiaga kwamba nchi zote za Uarabuni ni mali ya Israel na ndiyo maana kila anapokwenda kupiga, anachukua ardhi na kutanua nchi yake.

Israel walipewa nchi ndogo sana wakae baada ya kutawanywa na Adolf Hitler, baada ya kuanza kurudi, wakaitaka nchi yao, lakini kwa bahati mbaya waliwaona Waarabu washajigawia ardhi yao. Walichokifanya ni kuanza kupigana nao.

Kama unakumbuka Umoja wa Mataifa uliingilia kati, ulichukizwa na kitendo cha Israel kuwapiga Waarabu, walichokifanya, wakawapelekea Biblia ambayo kwa nyuma kuna ramani ya Israel tangu enzi za Musa. Wakawaonyesha na kuwaambia kwamba nchi zote za Uarabuni ni Israel, tutakapokuwa wengi, tutaendelea kupiga na kuirudisha nchi yetu.

So jua hili. Ibrahim hakuwa Mwarabu. Musa hakuwa Mwarabu. Suleimani mtoto wa Daudi na baba yake huyo hawakuwa Waarabu. Ni Waisrael ambao bado wanaendelea kupigana na Waarabu ili wachukue nchi yao iliyowafanya waondoke Misri.

Uzao wa Ibrahim ndiyo uliomleta Yusufu ambaye akawachukua Waisrael kwenda kuishi Misri. Maisha yalikuwa ya raha sana, watu waliionjoi maisha lakini baada ya mfalme huyo kufa, ndipo akaja mfalme mwingine ambaye sasa hakuwataka Waisrael, akawafanya watumwa wake.

Wakafanyishwa kazi. Baadaye ndipo Musa akazaliwa ndani ya ardhi ya Kiarabu. Akapewa jukumu la kuwatoa Israel kutoka hapo Misri kwenda kwao. Wakati huo ndio ambao nao Waarabu walikuwa wamejinyakulia nchi, tena walikuwa ni watu wakubwa kimuonekano.

Musa akaanza mchakato wa kuwatoa Israel Uarabuni na kuwapelekea Israel. Waliishi Misri kwa miaka 400. Wakaondoka na kwenda Misri, na walitumia miaka 40.

Musa hakuingia Israel, alikufa jangwani na Mungu kumzika. Wale waliofanikiwa kuingia huko Israel ndio walioendelea kuipambania ardhi yao mpaka leo hii.

Hapa kuna jambo moja.

Vita ya Israel na Waarabu itapamba moto hapo baadaye. Itapigwa vita kali sana. Sasa kwa kuwa Israel ataonekana kuwa kiburi na mwenye nguvu sana, dunia nzima itaanza kumcharaza. Huyu Marekani anayeonekana kuwa karibu na Israel naye atamgeuka, kila nchi duniani itamgeuka na kumpiga.

Mwisho wa siku baada ya kuona wanapigwa sana, watakimbilia mpaka kwenye mlima ule aliopaa Yesu, wataomboleza na kulia, hapo ndipo Yesu atashuka kuimaliza vita hiyo, na huo ndiyo utakuwa mwisho wa kila kitu.
Mwarabu anamchukia muisraeli kwa sababu muisraeli si mwarabu

Hii Kali asee
 
Mwarabu anamchukia muisraeli kwa sababu muisraeli si mwarabu

Hii Kali asee
Hujawai kusikia ubaguzi wa utaifa, au wa rangi... Mbona ujiulizi Muafrika kuchukiwa na Mzungu

Kuchukiwa kwa sababu wewe sio wa jamii fulani ni jambo la kawaida... Fatilia taarifa mbalimbali utaona, watu wanachukiana kisa si wadini fulani, sembuse hii ya wewe kuwa si muarabu
 
Sijakuelewa hapo unaposema ismail ni baba wa waarabu kwa kuwa mama yake alikua mwarabu .inamaana waarabu wanafata koo zao kupitia kwa mama na si baba?? Kwanini ismael aendeleze ukoo wa waarabu wakati baba yake hakua mwarabu?? Kwanini asiendeleze ukoo wa kizazi chake cha babaake??

Sent from my Infinix X6517 using JamiiForums mobile app
Huyu analeta hadidhi za Bibili, alafu anataka kuaminisha watu wote, wasiamini imani yake na hata wasiokua na imani na hizi dini.
 
Mama Ishamel anaitwa nani?. Yule aliyekuwa na mwanawe jangwani. Au hujui hata alipoambiwa atakuwa taifa kubwa. Soma vitabu vyote ujue.
Nimekwambia mama wa kazi gani hapa? Hatutaki kusikia habari za mama maana kwenye ukoo mama hausiki.waarabu ,wasrael na mashariki ya kati yote mwanamke hata kuhesabiwa tu ni marufuku so ongelea ukoo wa baba achana na habari za wanawake.
 
Kwani Chief Borito Wanjagi, babu yake na Nyerere, alikuwa Mtanzania au sio Mtanzania?
 
Tupeane elimu kidogo, kuna watu wanachanganya mambo. Hapa tufundishane jambo moja. Kitu cha kwanza kabisa watu wanachokichanganya ni kuhusu Ibrahim, wengi wanasema Ibrahim alikuwa Mwarabu, ndugu yangu, nikwambie tu kwamba jamaa hakuwa Mwarabu.

Ibrahim baada ya kuzaa na kijakazi ambaye alikuwa Mwarabu, inamaanisha damu yake ilichanganyika na ya Kiarabu na ndiyo maana tunasema Ishmael ni baba wa Waarabu kwa sababu mama yake alikuwa Mwarabu.

Nchi za Kiarabu ambazo zipo kwenye umoja ni hizi, Algeria, Bahrain, Iraq, Jordan, Kuwait, Djibout, Saudi Arabia, Tunisia, United Arab Emirates, Yemen, Somalia, Sudan, Syria, Comoros, Misri, Maurtania, Qatar na Palestina.

Kwa nini Waarabu wanamchukia Israel? Ni kwa sababu si Mwarabu mwenzao. Na hao ndiyo wa kizazi cha Ibrahim. Kwa hiyo kama ulikuwa unahisi Ibrahim alikuwa Mwarabu, futa hiyo akilini mwako.

Hata Iran sio Waarabu, najua wengine mtakuwa hamlijui hili kwa undani. Miongoni mwa nchi za Kiarabu, Iran hayupo kwa sababu yeye si Mwarabu.

So Israel na Waarabu ni baba mmoja ila mama tofauti. Ibrahim alizaa na Muisrael mwenzake kwa kipindi hicho ilikuwa bado haijaitwa Israel na mtoto wake kuitwa Isaka ila yule aliyezaa na kijakazi ambaye ni Mwarabu anaitwa Ishmael. Tatizo kubwa la vita baina ya Mwarabu na Israel ni hapa.

Kama Israel angekuwa Mwarabu, leo usingesikia vita vinavyoendelea huko. Na mara zote Israel anawaambiaga kwamba nchi zote za Uarabuni ni mali ya Israel na ndiyo maana kila anapokwenda kupiga, anachukua ardhi na kutanua nchi yake.

Israel walipewa nchi ndogo sana wakae baada ya kutawanywa na Adolf Hitler, baada ya kuanza kurudi, wakaitaka nchi yao, lakini kwa bahati mbaya waliwaona Waarabu washajigawia ardhi yao. Walichokifanya ni kuanza kupigana nao.

Kama unakumbuka Umoja wa Mataifa uliingilia kati, ulichukizwa na kitendo cha Israel kuwapiga Waarabu, walichokifanya, wakawapelekea Biblia ambayo kwa nyuma kuna ramani ya Israel tangu enzi za Musa. Wakawaonyesha na kuwaambia kwamba nchi zote za Uarabuni ni Israel, tutakapokuwa wengi, tutaendelea kupiga na kuirudisha nchi yetu.

So jua hili. Ibrahim hakuwa Mwarabu. Musa hakuwa Mwarabu. Suleimani mtoto wa Daudi na baba yake huyo hawakuwa Waarabu. Ni Waisrael ambao bado wanaendelea kupigana na Waarabu ili wachukue nchi yao iliyowafanya waondoke Misri.

Uzao wa Ibrahim ndiyo uliomleta Yusufu ambaye akawachukua Waisrael kwenda kuishi Misri. Maisha yalikuwa ya raha sana, watu waliionjoi maisha lakini baada ya mfalme huyo kufa, ndipo akaja mfalme mwingine ambaye sasa hakuwataka Waisrael, akawafanya watumwa wake.

Wakafanyishwa kazi. Baadaye ndipo Musa akazaliwa ndani ya ardhi ya Kiarabu. Akapewa jukumu la kuwatoa Israel kutoka hapo Misri kwenda kwao. Wakati huo ndio ambao nao Waarabu walikuwa wamejinyakulia nchi, tena walikuwa ni watu wakubwa kimuonekano.

Musa akaanza mchakato wa kuwatoa Israel Uarabuni na kuwapelekea Israel. Waliishi Misri kwa miaka 400. Wakaondoka na kwenda Misri, na walitumia miaka 40.

Musa hakuingia Israel, alikufa jangwani na Mungu kumzika. Wale waliofanikiwa kuingia huko Israel ndio walioendelea kuipambania ardhi yao mpaka leo hii.

Hapa kuna jambo moja.

Vita ya Israel na Waarabu itapamba moto hapo baadaye. Itapigwa vita kali sana. Sasa kwa kuwa Israel ataonekana kuwa kiburi na mwenye nguvu sana, dunia nzima itaanza kumcharaza. Huyu Marekani anayeonekana kuwa karibu na Israel naye atamgeuka, kila nchi duniani itamgeuka na kumpiga.

Mwisho wa siku baada ya kuona wanapigwa sana, watakimbilia mpaka kwenye mlima ule aliopaa Yesu, wataomboleza na kulia, hapo ndipo Yesu atashuka kuimaliza vita hiyo, na huo ndiyo utakuwa mwisho wa kila kitu.

Umeanza vizuri umemalizia kijinga sana
 
Nimekwambia mama wa kazi gani hapa? Hatutaki kusikia habari za mama maana kwenye ukoo mama hausiki.waarabu ,wasrael na mashariki ya kati yote mwanamke hata kuhesabiwa tu ni marufuku so ongelea ukoo wa baba achana na habari za wanawake.
Tupe unavyoelewa wewe. Kuwa huyu mwarabu alitokea wapi
 
Ibrahim baada ya kuzaa na kijakazi ambaye alikuwa Mwarabu, inamaanisha damu yake ilichanganyika na ya Kiarabu na ndiyo maana tunasema Ishmael ni baba wa Waarabu kwa sababu mama yake alikuwa Mwarabu.
Punguza upotoshaji kwani waisrael ni watoto wa Abraham au Yakobo? Maana kama ni Abraham ana watoto wengi na wajukuu kibao nje ya Yakobo nao ni waisrael?

Tukirudi kwa Yakobo kumbuka alizaa na wajakazi wawili walitoka Syria ina maana hata hao wayahudi ni mixture ya Yakobo na Assyria sasa unaposema waisrael sio waarabu kivipi? Nachojua Israelites na Syrians or Egyptians wote ni SEMITES ni JAMII moja.

Ugomvi wa hapo ni wa kidini zaidi kuliko vinasaba otherwise Iran wangekua partners na Israel
 
Unaposema ibrahim ni muisrael unamaanisha alizaliwa baada ya isaka (israel)?
Kwani Isaka ndiye Israel? Utakuwa unachanganya madesa, Israel ni Yakobo mtoto mdogo wa Isaka! Kwa ufupi Ibrahim anapaswa aitwe Myahudi!
 
Back
Top Bottom