Ukweli kuhusu Israel, Waarabu, na Ibrahim

Ukweli kuhusu Israel, Waarabu, na Ibrahim

Wewe unasemaje? Kwamba ulikuwepo tanagu enzi za Adamu wakati Mohamad ambaye ni mtume na mwanziloishi wa Uislamu amezaliwa mwaka 570 yaani karne ya sita baada ya Yesu.
Waislamu wenyewe wanakuambia uislamu ulikuwepo tangu enzi za Adamu 😂
 
Mungu alibaliki vizazi vyote vya Ibrahim, baada ya Ibrahim kufariki ulitokea ugomvi wa urithi mmoja akidai ni mtoto mkubwa wa marehemu mwingine akidai ni mtoto aliyezaliwa kwenye ndoa.
 
Sawa sielewi nieleweshe,una maana gani kusema israel ilianza kwa yakub na baba yake asiwe ukoo huo?? Kinasaba unaweza kuwa kabila au ukoo ambao baba yako sio ?? Ina maana huyo mtu alikana nasaba damu na ukoo wa baba yake na babu yake anaanzisha kabila lake na ukoo wake ambao hauna uhusiano na baba yake na babu yake? Wewe hapo unaweza sasahivi ukaamua ukawa sio kabila wala ukoo wa baba yako ma babu yako?na huyo ismail huo ukoo wa waarabu alianza kwa nani?
Wewe umechanganyikiwa ama kwa kutotaka kufungua ubongo wako ukawa huru. Siyo lazima babu awe wa ukoo moja na mjukuu. na pia siyo lazima babu awe wa kabila moja na mtoto. Ndo maana watoto wa Yakobo kila moja alitengeneza kabila lake. Makabila 12 ya Israel yametokana na watoto 12 wa yakobo. Kwa mantiki hiyo Yakobo siyo wa kabila lolote kati ya hizo 12 za Israel. yakobo ni Mkaldayo kama ilivyo babu yake Ibrahimu na baba yake Isaka.
 
Sina uthibitisho wa moja kwa moja juu ya hilo... Yani vivid evidence, maana waarabu nao wanasema alikuwa muarabu
waarabu wazushi tu wanataka kulazimisha mambo ambayo history inawakataa haiwezekana kwa era aliyoishi Abram Misri watoke waarabu badala ya Khemet ambao ndio Black kama Nubian wa Kush
hivyo kusema Hajra alikua Mwarabu ni Uzushi mtupu!
 
Mjulishe kuwa hakuna nchi iliitwa Israel kabla na hata wakati wa Ibrahimu.
Nilimwambia hili akaanza kuleta siasa za Tanganyika na Tanzania...kipind cha falme zinagawanyika kulikuwa na samaria na Uyahudi ila hakukuwa na nchi inaitwa israel
 
Mungu alibaliki vizazi vyote vya Ibrahim, baada ya Ibrahim kufariki ulitokea ugomvi wa urithi mmoja akidai ni mtoto mkubwa wa marehemu mwingine akidai ni mtoto aliyezaliwa kwenye ndoa.
Wote walizaliwa kwenye ndoa mkuu Au hilo nalo unaoinga pia afu kumbuka Isaka ni chalii mdogo sana ni wana tofauti ya miaka 13 na ishmaili sio mwak mmoja au miwili kama unavyodhan
 
Bado haupo sahihi kwasababu mjakazi ambaye Ibrahim alizaa nae alikuwa Mmisri na wamisri wa nyakati hizo walikuwa ni weusi kwahiyo hawakuwa Waarabu Historia hii tuliyo nayo imepikwa kuficha jambo.
Nadhani uarabu siyo rangi ni kabira .
 
Waarabu ni marufuku kabisa kufata ukoo wa mama,kwanza mwanamke kule hatakiwi hata kusogea mbele za watu.
Kuna kabira na kuna taifa.
so alipozaliwa ndipo uraia wake ulipokuwa.ila inawezekana alineda taifa lingine akabadili uraia
 
Nomba mstwari tafadhali nijiweke fiti maana humu kuna wafia dini.
Bila shaka mkuu..
kwana kabisa kama utakumbuka Yakobo alivopata Tabu katika kuchunga wale Mifugo ili apate mke Ndipo alipofanikuwa kuondoka na Wake wawili na Vijakazi wawili...

watoto wa Yakobo wote wamezaliwa na Mama Wanne ambao ni;
  • Lea: Lea alikuwa mke wa kwanza wa Yakobo, na alimzalia watoto watano: Rubeni, Simeoni, Lawi, Yuda, Zabuloni, Isakari na Dinah
  • Raheli: Raheli alikuwa mke wa pili wa Yakobo, na alimzalia watoto wawili : Yusufu na Benyamini,
  • Bilha: Bilha alikuwa mjakazi wa Lea, na alimzalia Yakobo watoto wawili: Dani na Naftali.
  • Zilpa: Zilpa alikuwa mjakazi wa Raheli, na alimzalia Yakobo watoto wawili: Gadi na Asheri.
Ukitaka kupata uzao huu wote Kama nilivyoainisha Soma Manzo 30 yote...

kuhusu Huyo Dina...Mwanzo 30:19-21..

Screenshot_20231005-145503.png


SASA NARUDI KWA DINA STORY YA DINA NI UNDERRTAED SANA INAPATIKANAKUANZIA MWANZO 34 (MTOTO WA KIKE WA YAKOBO) JAPO IPO KWENYE BIBLIA HUWEZI KUTA WATU WAKIHADITHIA...

Dina alibikiriwa na Mtu wa asili ya Mhivi anaitwa Shekemu..
mwanzo 34:1-3 na jamaa akampenda sana Huyu msichana..

Screenshot_20231005-151159.png

kaka zake baada ya kusikia hivyo wakaanzisha vagi la kutosha nenda soma kisa kizima kipo huko Mwanzo 34....
 
Ndoa ilikuwa Kati ya Ibrahim na Sara
Una uhakika kaka Ngoja basi nikuonyeshe ndoa Zilizokuwepo...

Ndoa kati ya Ibrahimu na sarai ( Ama zama hizo abram na sarai)
Mkuu soma biblia yako Mwanzo 11 :28-30 hii ndo ndoa ya kwanza ya ibrahimu na sarai

Screenshot_20231005-153951.png


Ikumbukwe kwamba bibie Hagar/Hajiri hakuwa mtumwa ila alikuwa Mtoto wa mfalme ila kutokana na Mfalme kufanya aliyofanya na Mambo yakahafibika ilibidi amkirimu ibrahim kwa kumpa mali na mwanaye ili kupata radhi yake...

Ndoa ya pili ya Ibrahimu ipo hapaa...SOMA Mwanzo 16:3
basi unafikiri ni kwanini ilikuwa Lazima Sara ndo ampe Ibrahimu Huyo mwanamke...

sababu ni moja tu Hagar/hajiri alikuwa ni mtumwa wa sara kwa kuwa zamani zile mtumwa atatii kila kitu kutoka kwa Mwajiri wake au mtwana wake hivyo ilimpasa ibrahimu kusubiri kukabisdhiwa mke na sara na ndivyo ilivyokuwa ....

mwanzo 16:3..

"Sarai mkewe Abramu akamtwaa Hajiri Mmisri mjakazi wake, baada ya kukaa Abramu katika nchi ya Kanaani miaka kumi, akampa Abramu mumewe, awe mkewe."

Screenshot_20231005-154512.png


Kuna kitu kipya hapo kwamba awe mkewe
inakuchanganya mapenzi katika dini yasikutoa Ujuzi na uchambuzi wako wa kutafakari jitahidi usome na uelewee....

Na ndoa zote ni Takatifu na ndo maana Mungu mwenyewe alisema hivyo mkuu au nakoseaa.....
 
Mungu alibaliki vizazi vyote vya Ibrahim, baada ya Ibrahim kufariki ulitokea ugomvi wa urithi mmoja akidai ni mtoto mkubwa wa marehemu mwingine akidai ni mtoto aliyezaliwa kwenye ndoa.
Ugomvi ulizuka baadaye,lakini kabla Ibrahim hajafa,aligawa urithi kwa watoto wake kabla hajafa! Ibrahimu alimpa Urithi Isaka,watoto wengine(aliowazaa kwa mke mwingine) aliwapa zawadi na kuwatawanya kwenda mbali na Isaka,(Mwanzo25:5-6)! Sasa cha ajabu Ishmaeli hakupewa urithi wo wote na Ibrahim.
 
Sijakuelewa hapo unaposema ismail ni baba wa waarabu kwa kuwa mama yake alikua mwarabu .inamaana waarabu wanafata koo zao kupitia kwa mama na si baba?? Kwanini ismael aendeleze ukoo wa waarabu wakati baba yake hakua mwarabu?? Kwanini asiendeleze ukoo wa kizazi chake cha babaake??

Sent from my Infinix X6517 using JamiiForums mobile app
Hawezi jibu amejaza ushabiki akili mwake
 
Ismail anachukuliwa kuwa baba waarabu kulingana na mila ya Kiislamu. Imani hii imejikita katika Quran na Hadith za Mtume Mohammad, ambazo ni maandiko ya msingi katika Uislamu.

Kwa mujibu wa vyanzo hivi, Ismail alikuwa mtoto wa kwanza wa Nabii Ibrahimu na mkewe Hajiri (Hajar). Ibrahim ni mtu muhimu katika mila za Kiislamu na Kiyahudi-Kikristo.

Katika mapokeo ya Kiislamu, inaaminika kuwa Ismail aliishi katika maeneo ya Uarabuni, hasa katika eneo ambalo lingekuwa Makka. Uzao wake uliofata unaonekana ni wa Kiarabu ambao ni mababu wa waarabu wa hivi leo, na Quran inamtaja yeye na baba yake Ibrahim kama watu muhimu katika historia ya Uislamu.

Ni muhimu kutambua kwamba imani hii kimsingi inategemea maandiko ya kidini na ni suala la imani ndani ya mapokeo ya Kiislamu. Nje ya miktadha ya kidini, dhana ya Ismail kama baba wa Waarabu inaweza isiwe na maana sawa.

Ni kama Ibrahim anavyoitwa Baba wa mataifa, wakati yeye ni myahudi na mbona kuna wachina, waafrika, wa-mexico, walatini
Je yahudi ni kabila taifa kijiji?
 
Back
Top Bottom