Ukweli kuhusu Mradi wa NSSF wa Dege Beach Kigamboni

Ukweli kuhusu Mradi wa NSSF wa Dege Beach Kigamboni

Azimio na NSSF wakishindwa kwenye huu ubia na wakaamua kuuza huu mradi wanufaika wakubwa watakuwa ni Azimio.

Azimio watapa asilimia 20 yao ya milioni 800 kwa kila kiwanja lakini wanunuaji watakuwa tayari kulipa milioni 20 kwa kila kiwanja!
hamna mkuu,hawatauza kwa milioni 20,kumbuka kuna tayari nyumba 300 ziko tayari juu ya hiyo ardhi,kwahiyo thamani ya ardhi imeongezeka maradufu
 
mkuu,hiyo ardhi sio kwamba hao,azimio washakula hiyo milion 800 kila heka,

yaani pale itapoanza kuzalisha sasa,
thamani ya ardhi halisi ni milioni 25 ikiwa dormant,
sasa umeingia ubia na mtu mkajenga hotel kwa ushirikiano,bado katika kugawana mapato wewe utadai hiyohiyo milioni 25?.

Hao azimio ni expert wa real estate which means NSSF wanafaidi pia consultation toka azimio,

ieleweke sitetei mtu nachangia navyoona ni sawa,
nijuavyo mimi NSSF bado hawajanunua ardhi kwa milioni 800 kwa heka toka kwa azimio
Mkuu,
You are missing the point again. Unaangalia huu ubia kwa jicho la Azimio na NSSF!

Azimio wao wameona opportunity wameitumia! Lakini kwanini NSSF didn't go alone kwa dhamani ya milioni 20 kwa kiwanja badala ya milioni 800?!

Lakini umedai Azimio ni Expert wa real estate. Je, una ushahidi wowote wa mafanikio yao ya nyuma unaweza kuweka hapa?
I doubt it, kampuni ambayo hata wamiliki wake wamejificha!
 
Kigamboni kipindi huu ubia wa kishetani unafanyika bei ya ardhi iliyokuwa sokoni ni kati ya 1,500,000/= na 4,500,000/= kwa eka kutegemea na sehemu husika! na ardhi ilikuwa inapatikana sana! Sasa katika mazingira hayo ni mwekezaji ibilisi tu ambaye ataamua kutokununua ardhi mwenyewe halafu aingie ubia na mtu au kampuni inayothaminisha ardhi yake kwa sh 775,000,000/= kwa eka badala ya kuinunua mwenyewe kwa sh 5,000,000/= kwa eka!.
Hiyo ni tisa lakini kumi huyo mbia aliyethaminisha ardhi yake kwa sh 775,000,000/= bado anakutaka wewe umkopeshe pesa na ndiye anayemiliki share nyingi zaidi!
Ninachokiona hapa ni ufisadi uliokubuhu! Yaani nakopa pesa kwako halafu nanunua ardhi kwa bei chee halafu naingia ubia na wewe na kuithàminisha ardhi niliyonunua kwa hela niliyokopa kwako kwa bei mbaya kisha mimi ndo nakuwa mmiliki wa mradi mwenye hisa nyingi wakati kimsingi pesa yote ya mradi imetoka kwako!
 
hamna mkuu,hawatauza kwa milioni 20,kumbuka kuna tayari nyumba 300 ziko tayari juu ya hiyo ardhi,kwahiyo thamani ya ardhi imeongezeka maradufu
Mkuu,
Labda ni kujibu kwa mfano, kama dhamani halisi ya kiwanja ni milioni 20 lakini ukaingia ubia kwenye hicho kiwanja kwa thamani ya milioni 800 na mkaweza milioni 700 na mradi haijaisha. Hiyo ni jumla ya bilioni 1.5 mume invest.

Kwa hiyo kama ni kuuza ili kutokupa hasara ni lazima iwe bilioni 1.5 au zaidi.

Kwa mtu yoyote mwenye akili timamu atayetaka kununua anaangalia gharama zako na anapiga mahesabu yake kuanzia na ukubwa wa eneo na thamani halisi ya eneo ndio ana decide.

Kwa bilioni 1.5 mtu atajiuliza kwa nini nisinunue kiwanja kwa milioni 20 halafu ni wekeze milioni 700 ambapo atakuwa ameokoa milioni 780!

Mwekezaji yoyote atakayeta kununu atajiuliza ili swali, kwa nini hasinunue viwanja kwa milioni 20 ndio hawekeze?
 
Kigamboni kipindi huu ubia wa kishetani unafanyika bei ya ardhi iliyokuwa sokoni ni kati ya 1,500,000/= na 4,500,000/= kwa eka kutegemea na sehemu husika! na ardhi ilikuwa inapatikana sana! Sasa katika mazingira hayo ni mwekezaji ibilisi tu ambaye ataamua kutokununua ardhi mwenyewe halafu aingie ubia na mtu au kampuni inayothaminisha ardhi yake kwa sh 775,000,000/= kwa eka badala ya kuinunua mwenyewe kwa sh 5,000,000/= kwa eka!.
Hiyo ni tisa lakini kumi huyo mbia aliyethaminisha ardhi yake kwa sh 775,000,000/= bado anakutaka wewe umkopeshe pesa na ndiye anayemiliki share nyingi zaidi!
Ninachokiona hapa ni ufisadi uliokubuhu! Yaani nakopa pesa kwako halafu nanunua ardhi kwa bei chee halafu naingia ubia na wewe na kuithàminisha ardhi niliyonunua kwa hela niliyokopa kwako kwa bei mbaya kisha mimi ndo nakuwa mmiliki wa mradi mwenye hisa nyingi wakati kimsingi pesa yote ya mradi imetoka kwako!

huo ndio ufirauni wa NSSF wao huwa10% ndio kitu kinachowaongoza na wengine nasikia wanasomesha watoto huko uingereza , kwa 10% za fedha zetu
 
Nlisema ilo hizi ishu unaokota vihabar kwa njaa tu unaIleta huku hazina hata IJ thn unachafua tu watu,sasa huu UZI umejtosheleza haswa.nakila ishu ya NSSF ikitupwa huku majibu hua hayakos baada ya muda,namtaka mfuga njaa yule aje na investigation jounalism IJ ya majungu yake,na kwa hizi nondo hatorud.
 
Hata hili nalo mtu anajipanga kutetea?
1.Tatizo sio joint venture,hakuna popote ambapo watu wameona joint venture kati ya nssf na azimio ni tatizo.
2. Tatizo ni ulaghai uliofanyika,azimio haina eneo sawa na linalotajwa kwenye mkataba na pili thamani ya kiwanja milioni 800 sio sahihi.
Tuwe tunatulia na kutafakari hata kama tumetumwa na kulipwa ili kusafisha watu.
 
Maelezo yana substance, lakini kwa kuwa ujinga na majungu vinashabikiwa mno katika awamu hii ya Baba Ubaya, na kwa kuwa imeamuliwa kuwa NSSF ni lazima ichafuke na pengine hatimaye ifilisike kama ilivyo Twiga Bancorp, basi mleta mada hata tarajia matusi, kejeli na vijembe na usishangae Baba Ubaya naye akajitokeza na kutokwa mapovu!
 
Hivyo eeeeh

Lione kwanza...Na Tanesco ile pesa iliyowatoka ni binafsi siyo?

Two wrongs don't make a right!!

Halafu Rugemalila aliingia ubia na IPTL ni shirika binafsi tofauti na NSSF ambalo linaendeshwa kwa pesa zetu.
Makampuni kama IPTL tanapingia ubia ya aina hiyo wanajua wenyewe cha kufanya ili kurudisha gharama zao na tumeona walichofanya!!
 
Hata hili nalo mtu anajipanga kutetea?
1.Tatizo sio joint venture,hakuna popote ambapo watu wameona joint venture kati ya nssf na azimio ni tatizo.
2. Tatizo ni ulaghai uliofanyika,azimio haina eneo sawa na linalotajwa kwenye mkataba na pili thamani ya kiwanja milioni 800 sio sahihi.
Tuwe tunatulia na kutafakari hata kama tumetumwa na kulipwa ili kusafisha watu.
ndo maana kuna mahakama za biashara ambayo kama mbia mmoja amekiuka makubaliano mahakama inaamua,
mimi tatizo langu lipo katika milioni 800 kwa kiwanja,kama nakumbuka hesabu hiyo ilipatikana kwa kugawa eneo gawa kwa gharama zote za mradi,kama ni kweli,na eneo likawa pungufu inamaana itatakiwa recalculation na kuset upya hisa,kama unakumbuka hiyo hesabu waliipata vipi tuambie,
ila nijuavyo huwezi kutumia lugha ya nssf imenunua heka kwa milioni 800 ikakubalika kisheria,kwani hawajanunua ardhi
 
Mkuu hawa tutaenda nao taratibu taratibu tuh mwsho wa siku wataelewa tuuh

Naona wanachotaka kuaminisha umma ni hiyo million 800 kwa heka kwa mfananisho wa million 25 hapa hawatapa pa kutokea
Rugemalila na iptl deal halikua wrong,ndo biashara inavyoenda,yaani uje usimike mitambo kiwanjani kwangu tuseme heka moja,uanze kuungurumisha mashine na kuuza umeme miaka nenda rudi juu ya kiwanja changu halafu mimi unilipe milion 25?,,

keep in mind hayo mahesabu ya hisa mtu anaanza kupata mapato baada la mradi kukamilika na kuanza kuingiza mapato,

sasa unapodai wamenunua heka kwa milion 800,hiyo ni misleading
 
Bado maelezo yako hayaonyeshi ni kwa nini NSSF ilazimike kuingia mkataba na mwekezaji huyo kwa thamani hiyo ya ardhi...

Ina maana NSSF hawakuwa na uwezo wa kupata ardhi wenyewe na kusiwe na mbia mwingine?
 
Na mimi ninachokiona huyu jamaa na wenzake wengi hawajaelewa uhalisia ulivyo

Ni mwendawazimu gan anaweza nunua heka moja kwa shilling 800?

Na hata wanapoelezwa uhalisia bado hawataki kuukubali ukweli...

Shida yao sijui ni nin

Kuna kitu gan Dr Dau alichowakosea
ndo maana kuna mahakama za biashara ambayo kama mbia mmoja amekiuka makubaliano mahakama inaamua,
mimi tatizo langu lipo katika milioni 800 kwa kiwanja,kama nakumbuka hesabu hiyo ilipatikana kwa kugawa eneo gawa kwa gharama zote za mradi,kama ni kweli,na eneo likawa pungufu inamaana itatakiwa recalculation na kuset upya hisa,kama unakumbuka hiyo hesabu waliipata vipi tuambie,
ila nijuavyo huwezi kutumia lugha ya nssf imenunua heka kwa milioni 800 ikakubalika kisheria,kwani hawajanunua ardhi
 
Naona unatumia nguvu nyingi kutetea uozo, hapo waliponunua hakuna chochote special ndio maana unaambiwa few metres kutoka hapo viwanja vilikuwa vinauzwa 25m.

Sasa aliekuambia Nssf amenunua hiyo ardhi ni nan?

Walichofanya Nssf ni kuingia ubia na mwenye hiyo ardhi kisha baada ya mradi kukamilika na kuanza kuleta faida wagawane kwenye shares

Sidhan kama unakifaham unachokiongelea
 
Sasa aliekuambia Nssf amenunua hiyo ardhi ni nan?

Walichofanya Nssf ni kuingia ubia na mwenye hiyo ardhi kisha baada ya mradi kukamilika na kuanza kuleta faida wagawane kwenye shares

Sidhan kama unakifaham unachokiongelea
Haya mkuu.
 
Naona unatumia nguvu nyingi kutetea uozo, hapo waliponunua hakuna chochote special ndio maana unaambiwa few metres kutoka hapo viwanja vilikuwa vinauzwa 25m.

Usipojua Maana ya Asset to Equity huwezi kujua hii kadhia ya NSSF Matokeo yake mtakuja kusema Dr. Dau anaogopwa au analindwa. NSSF haikutoa fedha kununua Ardhi hiyo kilichofanyika ni kuingiza Ardhi hiyo kwny Mradi kwa Makubaliano kuwa thamani ya ardhi hiyo iwe converted kwenda kwny Hisa watazokuwa wanamiliki kwa Ubia. Hakuna Malipo yaliyofanyika kilichofanyika ni Evaluation ya Ardhi hiyo kwa thamani hiyo tajwa ambayo wapo wanaoihoji wakiamini imethaminishwa kwa thamani ya juu!
 
Usipojua Maana ya Asset to Equity huwezi kujua hii kadhia ya NSSF Matokeo yake mtakuja kusema Dr. Dau anaogopwa au analindwa. NSSF haikutoa fedha kununua Ardhi hiyo kilichofanyika ni kuingiza Ardhi hiyo kwny Mradi kwa Makubaliano kuwa thamani ya ardhi hiyo iwe converted kwenda kwny Hisa watazokuwa wanamiliki kwa Ubia. Hakuna Malipo yaliyofanyika kilichofanyika ni Evaluation ya Ardhi hiyo kwa thamani hiyo tajwa ambayo wapo wanaoihoji wakiamini imethaminishwa kwa thamani ya juu!
Vipi wangenunua ardhi yao kwa bei nafuu kuliko thamani ya hisa walizompa mbia? Yaani mfano wanunue ardhi eneo hilo hilo kwa mfano m100 badala ya kuchukua ya huyo mtu na kumpa share za thamani ya bilioni kadhaa? Au kulikuwa hamna ardhi ingine zaidi ya hio ya mbia?
 
Kuna watu ambao kwa nguvu zote wanataka kumtete Dau, NSSF ni mali ya wafanyakazi wa changiaji wa mfuko, tuna haja ya kuoji hii miradi maana ni pesa zetu, Hii kampuni ya azimio ni ya wapiga dili na kina Dau wamo, sasa nyinyi mnatoa povu kutetea, itakua ndio ninyi mlio nufaika na ajira za kiudini na undugu pale NSSF . Shame on u. Ipo siku utasikia Dau anatoka milango ya kisutu, apo ndio utajua jamaa alikua mpiga dili
 
Vipi wangenunua ardhi yao kwa bei nafuu kuliko thamani ya hisa walizompa mbia? Yaani mfano wanunue ardhi eneo hilo hilo kwa mfano m100 badala ya kuchukua ya huyo mtu na kumpa share za thamani ya bilioni kadhaa? Au kulikuwa hamna ardhi ingine zaidi ya hio ya mbia?

Kama Wangenunua wenyewe neno Ubia lisingekuwepo!
Sasa Uliza kwa nini Ubia nikupe tena Darsa Duara bila ya kashfa wala kejeli.
 
Back
Top Bottom