Ukweli lazima usemwe, Tunahitaji Muungano wa Serikali 1 tu

Ukweli lazima usemwe, Tunahitaji Muungano wa Serikali 1 tu

Uchaguzi ujao pawekwe na kipengele Cha kupigia kura kuhusu muungano,yaani unapigia kura ,Kama ni unataka muungano wa serikari 1,au 2 ,au 3 ,unaweka vema (✓) pale unapopataka. hapo tutakuwa tumepata muafaka sahihi wa hili Jambo!! au ikiwezekana waweke na kipengele Cha kuvunja muungano .
bara na zanzibar ni kama urusi na ukraine siku zijazo
 
Kwa maelezo yake mwenyewe Karume alitaka nchi moja na Serikali moja. Hakuwa na mantiki kwenye kutaka Serikali mbili. Wingi wa Serikali ni wingi wa kodi za wananchi kuzihudumia hizo serikali

Quote maarufu ya Karume ni, "Muungano ni kama koti, ukiona linakubana basi unalivua tu"
Hiyo ya kwako ndio naisikia leo.

Tanganyika wakiona Muungano unawanyonya, si wauvunje tu. Mleta mada jitizame wewe mwenyewe kama umeweza kuunganisha familia yako na ya upande wa mke wako kwanza!
 
Nimefuatilia kwa muda sasa kuhusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na nilichogundua ni kuwa wale wengi wanaotaka Zanzibar iwe na Serikali au Tanganyika iwe na Serikali yake wengi ni wanasiasa na wanafanya yote hayo kwa maslahi ya kisiasa ili wapate vyeo vya kisiasa na kujinufaisha binafsi.
Mkuu umewaza sawa kabisa wanasiasa wanatamaa sana na wapo kufanya lolote ili tu wapate madaraka..

Huu muungano wetu upo kisiasa zaidi na hauna dhati ya uungano ndani yake.

Ni kama Tanzania bara imejiunga na kakikundii kadogo cha mapinduzi cha zanzibar ili kiwalinde bila kujali wananchi wengine.
 
Nitawapeni kisa kimoja. Once nilihamia mtaa mmoja ughaibini nikamkuta mwenyeji wangu sikujua ni mtu wa.wapi basi tukawa kunagonga ung'eng'e mara akaniuliza mwenzangu ni mtu kutoka wapi nikamwambia mie Mtanzania ,basi nae akasema alaa !!! Then akanijibu mie mzanzibari, tangu wakati huo hii kitu ilinifikirisha sana .its true story imenitokea mimi escrow.
Dah,
Yaani Ni ngumu kabisa kwa Mtanzania aishiye Zanzibar kung'amua kuwa yeye Ni Mtanzania!

Muungano uvunjwe haraka sana

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Wazee wetu walifanikiwa kuunganisha udongo wa Tanganyika na Zanzibar kwa mafanikio makubwa. Walinia kuunganisha Vyama 2 vya Siasa, TANU na ASP wakafanikiwa kwa asilimia mia moja, hatimaye CCM ikazaliwa.

Yote hayo walifanikiwa, ila Sina uhakika kama mitazamo ya Watanganyika na Wazanzibar iliunganishwa ipasavyo!

Eti Mimi ni "Mtanzania" na yule ni "Mzanzibar". Mbona kama sielewi?
kama zbar Ina rais na serikali ,na bendera na wimbo wao Kama wa taifa ,Basi Wana haki kijiita wao ni wanzanzibari,Hilo ndo kosa lililofanya na hayati karume na mwal.nyerere,ilitakiwa zbar itambulike Kama mkoa ,hapo lqbda wangejiona wao ni sehemu ya Tanzania .huu muungano umekaa kisiasa Sana kuliko uhalisia .
 
Kati ya vitu vinavyofanya sisi waafrika tuendelee kuwa maskini ni kutotumia akili zetu vizuri na pia kupenda sana madaraka/ vyeo.

Nimefuatilia kwa muda sasa kuhusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na nilichogundua ni kuwa wale wengi wanaotaka Zanzibar iwe na Serikali au Tanganyika iwe na Serikali yake wengi ni wanasiasa na wanafanya yote hayo kwa maslahi ya kisiasa ili wapate vyeo vya kisiasa na kujinufaisha binafsi.

Pili, nimegundua uwepo wa Serikali 2 au 3 unawanufaisha zaidi hao wanasiasa kwa sababu uwepo wa Serikali hizo unawahikishia kupata nafasi za kisiasa ili waendelee kunufaika na kodi za wananchi kama vile Uwaziri, Ukuu wa Mikoa , Wilaya katika Serikali hizo mbili/tatu.

Mwisho katika ufuatiliaji wangu nimegundua kero hizi zinazoitwa za Muungano kama wabara kutoweza kumiliki Ardhi Zanzibar kama Wa Zanzibar wanavyomiliki Ardhi huku bara dawa yake ni moja tu yaaani Kuwa na Nchi 1 na Serikali 1 tu na Raisi 1 tu.

Ni vizuri tukiwa tunaenda kujenga daraja la kuunganisha Zanzibar na Tanzania tukafikiria pia kuwa sasa tuwe na nchi 1 na serikali 1 tu ili kuepusha sehemu kubwa ya kodi za wananchi kwenda kuhudumia Serikali 2/3 tena ambazo kiuhalisia hazina manufaa yeyote kwa mwananchi wa kawaida

Heri ya Siku ya Wafanyakazi
Muungano ni wa nini? Mimi napendekeza uvunjwe na kila nchi na watu wake.
 
Tukiamua twende kwenye serikali moja, then we just go ahead!, watu wanaitwa Wazanzibari ni ndani tuu ya muungano, nje ya muungano, hakuna Wanzanzibari wala Watanganyika, kuna Watanzania tuu.
P
Kama tunataka muungano wa haki, basi twende kwenye muungano wa mkataba.
 
Kati ya vitu vinavyofanya sisi waafrika tuendelee kuwa maskini ni kutotumia akili zetu vizuri na pia kupenda sana madaraka/ vyeo.

Nimefuatilia kwa muda sasa kuhusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na nilichogundua ni kuwa wale wengi wanaotaka Zanzibar iwe na Serikali au Tanganyika iwe na Serikali yake wengi ni wanasiasa na wanafanya yote hayo kwa maslahi ya kisiasa ili wapate vyeo vya kisiasa na kujinufaisha binafsi.

Pili, nimegundua uwepo wa Serikali 2 au 3 unawanufaisha zaidi hao wanasiasa kwa sababu uwepo wa Serikali hizo unawahikishia kupata nafasi za kisiasa ili waendelee kunufaika na kodi za wananchi kama vile Uwaziri, Ukuu wa Mikoa , Wilaya katika Serikali hizo mbili/tatu.

Mwisho katika ufuatiliaji wangu nimegundua kero hizi zinazoitwa za Muungano kama wabara kutoweza kumiliki Ardhi Zanzibar kama Wa Zanzibar wanavyomiliki Ardhi huku bara dawa yake ni moja tu yaaani Kuwa na Nchi 1 na Serikali 1 tu na Raisi 1 tu.

Ni vizuri tukiwa tunaenda kujenga daraja la kuunganisha Zanzibar na Tanzania tukafikiria pia kuwa sasa tuwe na nchi 1 na serikali 1 tu ili kuepusha sehemu kubwa ya kodi za wananchi kwenda kuhudumia Serikali 2/3 tena ambazo kiuhalisia hazina manufaa yeyote kwa mwananchi wa kawaida

Heri ya Siku ya Wafanyakazi

SULUHISHO LA KUDUMU LA MUUNGANO HUU WENYE KERO ZISIZOISHA:

1. Watu wa Tanganyika wenye makazi ya kudumu Zanzibar na Wazanzibar wenye makazi ya kudumu Tanganyika, wapewe uhiari, haki na uraia wa kuendelea kuishi Zanzibar au Tanganyika mtawalia.

2. Endapo Tanganyika na Zanzibar zitaendelea kuwa na uraia wa nchi moja, basi nchi hizi mbili ziwe na makubaliano maalum ya uraia maalum wa nchi mbili (Duo Exclusive Treaty on Special Dual Citizenship) kwa Watanganyika na Wazanzibar ambao watahiari kuwa na uraia wa nchi mbili baina ya Tanganyika na Zanzibar pekee.

3. Tanganyika na Zanzibar ziwe madola huru yenye mamlaka kamili kama ilivyokuwa kabla ya muungano na zijiunge katika jumuiya au taasisi mbalimbali za kikanda au kimataifa ikiwa pamoja na Umoja wa Mataifa (UN), FIFA, nk.

4. Pasiwepo viza ya kusafiria kati ya Tanganyika na Zanzibar isipokuwa vitambulisho vya uraia au hati za kusafiria (passports) zitumike kumtambua Mtanganyika au Mzanzibar.

5. Iundwe Tume ya Mahusiano na Ujirani Mwema baina ya Tanganyika na Zanzibar (Commission for Relations and Good Neighbourhood). Tume hii pamoja na mambo yatakayojitokeza, ifanye yafuatayo:

(a) Kuweka utaratibu wa kuimarisha uhusiano na ulinzi wa pamoja wa Majeshi ya Ulinzi ya Watu wa Zanzibar (Zanzibar People’s Defence Forces - ZPDF) na Majeshi ya Ulinzi ya Watu wa Tanganyika (Tanganyika People’s Defence Forces -TPDF). Wanajeshi wa Tanganyika na Zanzibar wataendelea kutumika kwa pamoja kulinda watu na mipaka ya Tanganyika na Zanzibar.

(b) Kugawanya madeni ya nje kulingana na uwiano halisi wa jinsi yalivyotumika kusaidia nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar.

(c) Kuratibu balozi za nje ili ziendelee kutumiwa pamoja kiofisi (shared consulates) kwa Tanganyika na Zanzibar hadi wakati ambapo uwezo wa kila nchi utaruhusu kuwa na ubalozi wake.

(d) Kuratibu fedha na/au sarafu za aina moja ili ziendelee kutumika kihalali kati ya Tanganyika na Zanzibar ili kudumisha uhusiano na utambulisho wa kihistoria.

Hitimisho

Nikiwa mwanafunzi wa Mwalimu Nyerere nihitimishe kwa kusema alichokataza ni kufukuzana baina ya Watanganyika na Wazanzibar. Akaita dhambi kubwa sawa na kula nyama ya mtu. Hakukataza maelewano na makubaliano ya kuagana kwa amani. Na sitegemei watu wanaokubaliana kwa amani watafukuzana au kupigana. Wala si sahihi kulinganisha hilo na Sudan ambao walipigana miongo kadhaa wagawane nchi.

Wakati vita vya Uganda na Tanzania vikielekea ukingoni kabisa, Mwalimu Nyerere alilaumiwa kuwa anataka kuimeza Uganda, wengine wakadiriki kusema kama alivyoimeza Zanzibar. Yeye alijibu kuwa lililo la msingi ni kudumisha amani na nchi jirani na kuwa na uhusiano mwema - si kuunganisha nchi. Tubakie majirani wema kama ilivyo kwa Zambia, Msumbiji, Malawi, Rwanda, Kenya na kwingineko. Kuwa na mahusiano mema na jirani ni jambo la msingi na si lazima muunganishe nchi.

Kuna nchi nyingi tunahusiana nazo vizuri sana na kwa ukaribu japo haziko jirani, sembuse Zanzibar na Tanganyika! Undugu ni mahusiano mema si kuunganisha nchi. Na ujirani na udugu wa kihistoria upo kwa nchi zote tunazopakana nazo, si Tanganyika na Zanzibar pekee.

Muungano usilindwe kwa vitisho, kulazimishana, kubanana, kufinyana, kupunjana na kulaumiana, bali kwa kujenga na kuimarisha mahusiano na ushirikiano mwema wa viongozi na wananchi wa hizi nchi mbili.

Kuna faida nyingi za kitaifa na kimataifa kwetu sisi Watanganyika kuwa nchi kamili, na vivyo hivyo kwa Zanzibar. Tusizibiane fursa na kuendelea kukerana au kulalamikiana!
 
SULUHISHO LA KUDUMU LA MUUNGANO HUU WENYE KERO ZISIZOISHA:

1. Watu wa Tanganyika wenye makazi ya kudumu Zanzibar na Wazanzibar wenye makazi ya kudumu Tanganyika, wapewe uhiari, haki na uraia wa kuendelea kuishi Zanzibar au Tanganyika mtawalia.

2. Endapo Tanganyika na Zanzibar zitaendelea kuwa na uraia wa nchi moja, basi nchi hizi mbili ziwe na makubaliano maalum ya uraia maalum wa nchi mbili (Duo Exclusive Treaty on Special Dual Citizenship) kwa Watanganyika na Wazanzibar ambao watahiari kuwa na uraia wa nchi mbili baina ya Tanganyika na Zanzibar pekee.

3. Tanganyika na Zanzibar ziwe madola huru yenye mamlaka kamili kama ilivyokuwa kabla ya muungano na zijiunge katika jumuiya au taasisi mbalimbali za kikanda au kimataifa ikiwa pamoja na Umoja wa Mataifa (UN), FIFA, nk.

4. Pasiwepo viza ya kusafiria kati ya Tanganyika na Zanzibar isipokuwa vitambulisho vya uraia au hati za kusafiria (passports) zitumike kumtambua Mtanganyika au Mzanzibar.

5. Iundwe Tume ya Mahusiano na Ujirani Mwema baina ya Tanganyika na Zanzibar (Commission for Relations and Good Neighbourhood). Tume hii pamoja na mambo yatakayojitokeza, ifanye yafuatayo:

(a) Kuweka utaratibu wa kuimarisha uhusiano na ulinzi wa pamoja wa Majeshi ya Ulinzi ya Watu wa Zanzibar (Zanzibar People’s Defence Forces - ZPDF) na Majeshi ya Ulinzi ya Watu wa Tanganyika (Tanganyika People’s Defence Forces -TPDF). Wanajeshi wa Tanganyika na Zanzibar wataendelea kutumika kwa pamoja kulinda watu na mipaka ya Tanganyika na Zanzibar.

(b) Kugawanya madeni ya nje kulingana na uwiano halisi wa jinsi yalivyotumika kusaidia nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar.

(c) Kuratibu balozi za nje ili ziendelee kutumiwa pamoja kiofisi (shared consulates) kwa Tanganyika na Zanzibar hadi wakati ambapo uwezo wa kila nchi utaruhusu kuwa na ubalozi wake.

(d) Kuratibu fedha na/au sarafu za aina moja ili ziendelee kutumika kihalali kati ya Tanganyika na Zanzibar ili kudumisha uhusiano na utambulisho wa kihistoria.

Hitimisho

Nikiwa mwanafunzi wa Mwalimu Nyerere nihitimishe kwa kusema alichokataza ni kufukuzana baina ya Watanganyika na Wazanzibar. Akaita dhambi kubwa sawa na kula nyama ya mtu. Hakukataza maelewano na makubaliano ya kuagana kwa amani. Na sitegemei watu wanaokubaliana kwa amani watafukuzana au kupigana. Wala si sahihi kulinganisha hilo na Sudan ambao walipigana miongo kadhaa wagawane nchi.

Wakati vita vya Uganda na Tanzania vikielekea ukingoni kabisa, Mwalimu Nyerere alilaumiwa kuwa anataka kuimeza Uganda, wengine wakadiriki kusema kama alivyoimeza Zanzibar. Yeye alijibu kuwa lililo la msingi ni kudumisha amani na nchi jirani na kuwa na uhusiano mwema - si kuunganisha nchi. Tubakie majirani wema kama ilivyo kwa Zambia, Msumbiji, Malawi, Rwanda, Kenya na kwingineko. Kuwa na mahusiano mema na jirani ni jambo la msingi na si lazima muunganishe nchi.

Kuna nchi nyingi tunahusiana nazo vizuri sana na kwa ukaribu japo haziko jirani, sembuse Zanzibar na Tanganyika! Undugu ni mahusiano mema si kuunganisha nchi. Na ujirani na udugu wa kihistoria upo kwa nchi zote tunazopakana nazo, si Tanganyika na Zanzibar pekee.

Muungano usilindwe kwa vitisho, kulazimishana, kubanana, kufinyana, kupunjana na KULAUMIANA, bali kujenga na kuimarisha mahusiano na ushirikiano mwema wa viongozi na wananchi wa hizi nchi mbili.

Kuna faida nyingi za kitaifa na kimataifa kwetu sisi Watanganyika kuwa nchi kamili, na vivyo hivyo kwa Zanzibar. Tusizibiane fursa na kuendelea kukerana au kulalamikiana!
hivi tunafaidika nini watz (bara) na huu muungano ,hivi Kuna mtu anaweza kutoa faida za huu muungano kwa upande wa bara!!? kwa upande wa zbar najua wao wanafaidika Sana ,je huku bara ,tunapata faida gani!!?
 
hivi tunafaidika nini watz (bara) na huu muungano ,hivi Kuna mtu anaweza kutoa faida za huu muungano kwa upande wa bara!!? kwa upande wa zbar najua wao wanafaidika Sana ,je huku bara ,tunapata faida gani!!?
Hakuna faida, isipokuwa watawala, hasa wa kutoka Zanzibar.
 
Tukiamua twende kwenye serikali moja, then we just go ahead!, watu wanaitwa Wazanzibari ni ndani tuu ya muungano, nje ya muungano, hakuna Wanzanzibari wala Watanganyika, kuna Watanzania tuu.
P
Muunganonuvubjwe tu, una faida gani kwa Tanganyika na Zanzibar?

Tena irudishwe mipaka ya kabla ya iliyowekwa na Wajerumani.
 
SULUHISHO LA KUDUMU LA MUUNGANO HUU WENYE KERO ZISIZOISHA:

1. Watu wa Tanganyika wenye makazi ya kudumu Zanzibar na Wazanzibar wenye makazi ya kudumu Tanganyika, wapewe uhiari, haki na uraia wa kuendelea kuishi Zanzibar au Tanganyika mtawalia.

2. Endapo Tanganyika na Zanzibar zitaendelea kuwa na uraia wa nchi moja, basi nchi hizi mbili ziwe na makubaliano maalum ya uraia maalum wa nchi mbili (Duo Exclusive Treaty on Special Dual Citizenship) kwa Watanganyika na Wazanzibar ambao watahiari kuwa na uraia wa nchi mbili baina ya Tanganyika na Zanzibar pekee.

3. Tanganyika na Zanzibar ziwe madola huru yenye mamlaka kamili kama ilivyokuwa kabla ya muungano na zijiunge katika jumuiya au taasisi mbalimbali za kikanda au kimataifa ikiwa pamoja na Umoja wa Mataifa (UN), FIFA, nk.

4. Pasiwepo viza ya kusafiria kati ya Tanganyika na Zanzibar isipokuwa vitambulisho vya uraia au hati za kusafiria (passports) zitumike kumtambua Mtanganyika au Mzanzibar.

5. Iundwe Tume ya Mahusiano na Ujirani Mwema baina ya Tanganyika na Zanzibar (Commission for Relations and Good Neighbourhood). Tume hii pamoja na mambo yatakayojitokeza, ifanye yafuatayo:

(a) Kuweka utaratibu wa kuimarisha uhusiano na ulinzi wa pamoja wa Majeshi ya Ulinzi ya Watu wa Zanzibar (Zanzibar People’s Defence Forces - ZPDF) na Majeshi ya Ulinzi ya Watu wa Tanganyika (Tanganyika People’s Defence Forces -TPDF). Wanajeshi wa Tanganyika na Zanzibar wataendelea kutumika kwa pamoja kulinda watu na mipaka ya Tanganyika na Zanzibar.

(b) Kugawanya madeni ya nje kulingana na uwiano halisi wa jinsi yalivyotumika kusaidia nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar.

(c) Kuratibu balozi za nje ili ziendelee kutumiwa pamoja kiofisi (shared consulates) kwa Tanganyika na Zanzibar hadi wakati ambapo uwezo wa kila nchi utaruhusu kuwa na ubalozi wake.

(d) Kuratibu fedha na/au sarafu za aina moja ili ziendelee kutumika kihalali kati ya Tanganyika na Zanzibar ili kudumisha uhusiano na utambulisho wa kihistoria.

Hitimisho

Nikiwa mwanafunzi wa Mwalimu Nyerere nihitimishe kwa kusema alichokataza ni kufukuzana baina ya Watanganyika na Wazanzibar. Akaita dhambi kubwa sawa na kula nyama ya mtu. Hakukataza maelewano na makubaliano ya kuagana kwa amani. Na sitegemei watu wanaokubaliana kwa amani watafukuzana au kupigana. Wala si sahihi kulinganisha hilo na Sudan ambao walipigana miongo kadhaa wagawane nchi.

Wakati vita vya Uganda na Tanzania vikielekea ukingoni kabisa, Mwalimu Nyerere alilaumiwa kuwa anataka kuimeza Uganda, wengine wakadiriki kusema kama alivyoimeza Zanzibar. Yeye alijibu kuwa lililo la msingi ni kudumisha amani na nchi jirani na kuwa na uhusiano mwema - si kuunganisha nchi. Tubakie majirani wema kama ilivyo kwa Zambia, Msumbiji, Malawi, Rwanda, Kenya na kwingineko. Kuwa na mahusiano mema na jirani ni jambo la msingi na si lazima muunganishe nchi.

Kuna nchi nyingi tunahusiana nazo vizuri sana na kwa ukaribu japo haziko jirani, sembuse Zanzibar na Tanganyika! Undugu ni mahusiano mema si kuunganisha nchi. Na ujirani na udugu wa kihistoria upo kwa nchi zote tunazopakana nazo, si Tanganyika na Zanzibar pekee.

Muungano usilindwe kwa vitisho, kulazimishana, kubanana, kufinyana, kupunjana na kulaumiana, bali kwa kujenga na kuimarisha mahusiano na ushirikiano mwema wa viongozi na wananchi wa hizi nchi mbili.

Kuna faida nyingi za kitaifa na kimataifa kwetu sisi Watanganyika kuwa nchi kamili, na vivyo hivyo kwa Zanzibar. Tusizibiane fursa na kuendelea kukerana au kulalamikiana!
Umeongea point.
 
Back
Top Bottom