Ukweli mchungu: Zanzibar tunaishi kwa kudra za Tanganyika!

mleta mada ni mzanzibari. namjua kwa uzuri. siwezi ku reveal identity yake hapa na faragha za pembeni za kufahamiana naye.
Kaskazini unatetea huyo sio mzanzibar , ukileta hapa nakupa pesa kwa uthbitisho ...Mkimbizi huyo anarudi kwao December.

Ukithibitisha nakupa pesa au ID yangi ifungiwe milele.
 
Nimesikia huko Arusha kuna wadudu, sasa haka kamuungano ketu siku kakifa nahisi hao wadudu watanitoa mkuku nirudi kwetu unguja na kugawana kibanda changu!
Tumia utambulisho wa kwenu , acha kejeli ...Usipagawe na JF watu unaweza kufuatiliwa.

Tumia akili hata comments zako zinaonyesha tu .
 
Japo sisi tumekuwa ndugu, marafiki nk lkn bado muungano wetu una mapengo mengi sana. Wanufaika ni wanasiasa tu ndio wanaokula. Kizazi cha kuhoji kinakuja, tusiombee. Nawaza Katiba mpya itibu hili. Na wanaokataa katiba mpya ni kwa maslshi yao kwa hofu zao, hasa wanasiasa wetu ambso wanaamini wao ndio kila kitu
 
Huijui Zanzibar. Ungetulia tu.
Sasa wewe mwenye kuijua Zanzibar embu tuambie basi, Zanzibar tutawezaje kutoboa kimaisha siku moja huu muungano ukafia baharini?

Yaani kama hata ulinzi, usalama na umeme kwa 100% Zanzibar tunategemea msaada wa pesa za mvuja jasho wa Tanganyika, ni kipi hasa tutaweza kukiendesha sisi wenyewe?

Ukweli usemwe, mtanganyika apewe maua yake kwa kuweza kutusitiri sisi wazenji kwa miaka 60.
 
Kaka mbona iko wazi kabisa anaeng'ang'ania huu muungano ni CCM na sio Watanganyika. Bahati mbaya hata huko hao CCM mnao.
 
Maneno haya Zitto Kabwe Mcongoman hataki kusikia.
 
Wewe ni mchaga kutoka machame upo Zanzibar kuuza vinyago toka lini umekua Mzanzibari?
 
Kaka mbona iko wazi kabisa anaeng'ang'ania huu muungano ni CCM na sio Watanganyika. Bahati mbaya hata huko hao CCM mnao.
Huko wapi ? Huyo ni mtanganyika mwenzako mchaga kutoka machame yupo Zanzibar anauza vinyago wala sio Mzanzibari
 
Zanzibar watapata pesa zao na misaada kwa 100%. chakula hata bongo kinaagizwa juzi tu hapa walipiga marufuku ndizi kutoka huku Tz mkaanza kupiga kelele, mipakani mpaka wakenya wanunua chakula na vivyo hivyo watanzania wananunua kutoka nje.

Mfanyabiashara anapeleka kwany soko hata ulaya hana shobo na muungano wanu, Umeme inaweza kununua mbona Tanzania inanua? Muulize Biteko.

Mikoa kibao ya karibu kama kupitia Dar, Tanga, Mtwara ....Basi kama lango la bidhaa hata magendo zenji ni namba moja ..

Hamna logic kwa vile kuvunja muungano sio ugomvi ushirikiano upo pale pale , unaweza kutoka bara ukaomba uraia kule kw kufuata taratibu, zanzibar ina diaspora wengi nje kuliko huku bara...Nchi za Asia wapo kibao ndugu zao wapo mikao ya pwani kwa sana maana wanafanana.

Biashara zipo pale pale watalii wataingia na wakule wtakuja huku.
 
Huyo jamaa znz Asp ni mchaga kutoka machame yupo Zanzibar anauza vinyago
Nionyeshe mzanzibar wa asili ili nikuonye mgeni wa kuja Zanzibar!
Wazanzibar wote ni watu wa kuja, Zanzibar haina mwenyewe, kihistoria ni kisiwa cha uvuvi, utumwa na ulanguzi. kuanzia Mzee Karume mwenyewe (mnyasa), Maalim (mshiraz wa kutoka Oman) mpaka Dr. Hussein (kutoka Mkuranga)

Sifa kubwa (na mbaya) ya Mzanzibar ni kubagua na kutumikisha, ubaguzi ni kama ngozi kwa mzanzibar. Mshirazi (mpemba!) atambagua mswahili (muunguja!) na muunguja atamdidimiza (mtumikisha) mpemba. Ngoma pia ipo siku itageuka. Yaani Zanzibar tumekaa kuviziana tu.
 
Nimekuuliza toka lini umekua Mzanzibari?
 
Mimi nataka tu siku moja huu muungano uvunjike ili wabaki kwao tuone wwtafsnya maajabu gani ..watu wanapewa kila ain y a upendeleo lakin hawaridhiki
 
Kwa hiyo na wewe ni Mzanzibari wa kuja au vipi ?
 
Ni sawa na kusema Tanzania bila ya misaada ya Ulaya isinge toboa.

Hivi kuna kisiwa duniani hakiwezi jiendesha wenyewe?.
Namshangaa huyu mpenda misaada ya bure. Hivi Zanzibar kabla ya 1964 ilikuwa inaishi vipi? Au hivyo visiwa vingi tu vinavyojitegemea wenyewe vinajiendesha vipi?

Na akumbuke tu kuwa Zanzibar ilikuwa mbele zaidi kielimu na kimaendeleo kabla ya muungano.
 
Nimesikia huko Arusha kuna wadudu, sasa haka kamuungano ketu siku kakifa nahisi hao wadudu watanitoa mkuku nirudi kwetu unguja na kugawana kibanda changu!
Shehee Wadudu wa huku ni Marasi
So hilo ni brand tu bro ya kazi zao wasikutishe waa amani sana Dingi hao Jomba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…