Ukweli ni kwamba bodaboda ana fursa na anamzidi kipato Mwalimu

Ukweli ni kwamba bodaboda ana fursa na anamzidi kipato Mwalimu

Lazima wewe utakua mwalimu unaandamwa na mikopo mbalimbali jumlisha bodi ya mikopo, nmb wachukue chao, salary laki na 30 kazi haina overtime, wala allowance yoyote hapo ndio utaona kivumbi na jasho
Hhhahaha
 
Tuseme ukweli either muongezewe mishahara na stahiki nyingine lakini mwalimu unachomshinda Bodaboda ni uwezo wa kukopa tena uwe unakopesheka sasa, mwalimu kumaliza mwaka ana balance ya milioni mbili huyo anatakiwa heshima
 
Why mwl na boda
Why isiwe mwl na magereza?au zimamoto
Au nurse


Unamfahamu walimu wanalipwa mishara mizur sana kuliko unachokijua?
Wapo walimu wanalamba mpaka milion 1.6

Laki 9 ndo wengi sana laki 4 idara zote za selikal wapo
Afya
Ulinzi na usalama
Nk
Hasa kwa local government

Mshahara mkubwa unatokana na kiwango cha elimu
Muda wa kazini nk

Kwa idara zote
Mtoe usalama humo Hawa watu mishahara Yao wanalipwa Sawa na wakuu wa wilaya
 
Walimu hawana hela,..bora mwalimu wa kike anaolewa!mwalimu anakopa mkopo ananunua gari atatumikia mkopo wake miaka 15 mpka amalize...kingine walimu wengi hawajipendi wanakuja shuleni hawabadili nguo...wanawaza kuwahi wanafunzi wawachape ...sio makosa Yao ila ilibidi serikali iwaangalie upya ...mwalimu amekadiliwa mshahara ili mradi isife na njaa tu!

Au naongea uwongo wakuu!
 
Wakati nikiwa sekondari niliupenda ualimu. Baada ya kwenda high schoo niliuchukia. Chuo kikuu sikuchukuwa ualimu, lakini baadaye nilijikuta nimekuwa mwalimu, na hadi leo sijatamani kazi nyingine zaidi ya kufundisha, ndiyo maana nimefundisha zaidi ya miaka 40.

Ni kweli kuwa ualimu, hasa siku hizi hauheshimiwi kama kazi nyingione. Waalimu wengi hasa shule za msingi na sekondari za kata wanafanya kazi katika mazingira magumu. Lakini kudai kuwa hiyo kazi ni mbaya kuliko kuendesha bodaboda ni kuidhalalisha hiyo fani. Yeyote anayesema hii fani ni mbaya basi akumbuke kuna fani nyingi ambazo ziko chini ya hizo. Kuna watu wanaitwa clerical officer, messenger, typist, n.k. huwe kulinganisha na ualimu.

Watu wengi wanadhani ualimu ndiyo wenye kipato cha chini. Kwa taarifa yako kuna waalimu wa shule za msingi wenye mishahara mikubwa kuliko wakubwa wao makao makuu. Ualimu unaa ngazi na wengi hupanda na kufikia mishara inayoweza kuwakaribia makatibu wakuu, mameneja wa kati, n.k. Bodaboda anaweza kupata kipato kikubwa na kujiendeleza na kuwa na pesa nyingi (tajiri) kuliko hata engineer, daktari, n.k. Hiyo hutokea katika kada zote. Mimi nimeshuhudumia wahudumu ofisi waklifanikiwa na kutajirika, lakini hii haina maana wahudumu ofisi kazi yao/maisha yao ni bora kuliko maofisa wao. Ni mtu mmoja mmoja. Hii ndiyo maana tuna watu wana masters/Ph.D. lakini bado kati ya hao hali zao zinaweza kuwa duni kuliko wachache wa darasa la saba au la 12.

Mimi nakubaliana na wewe uwezekano wa bodaboda kumzidi mwalimu upo, lakini huwezi kumlinganisha au kuwalinganisha walimu na bodaboda. Mimi nimefanikiwa kwenye ualimu na hata siku mopja sitajilinganisha na bodaboda na bodaboda hawanikaribii kwa vyovyote vile (generally). Lakini nakubali kuna bodaboda mmoja mmoja ambao inawezekana kufanikiwa kuliko mimi. Pia huenda kuna wahudumu offisi weamepata kufanikiwa kuliko mimi. Na hao ni wale waliyopata pesa na kufanya investment zenye kulipa. Walimu nao wapo waliyotumia vipato vyao na kuytajirika!
Umeongea Kwa busara sana. Mungu akubariki
 
Mbona unaruka [emoji23][emoji23][emoji23]

Mfanyakazi ili arndelee nchi za dunia ya tatu ni lazima kwanza awe mwizi na aibe sana, ndio maana walikoendelea kwanza malipo kwa kazi nyingi ni kwa saa na sio mwezi wewe piga hesabu mwalimu anaelipwa kwa mwezi 470k ukigawa kwa siku 30 analamba elfu kumi na tano kwa siku, ukigawa kwa 22 siku baada ya kutoa siku nane za weekend analamba elfu 21 na kitu, sasa 15k au 21k kwa bodaboda mbona ni pesa ndogo sana na hapo huyo ana barchelor kabisa
 
Mfanyakazi ili arndelee nchi za dunia ya tatu ni lazima kwanza awe mwizi na aibe sana, ndio maana walikoendelea kwanza malipo kwa kazi nyingi ni kwa saa na sio mwezi wewe piga hesabu mwalimu anaelipwa kwa mwezi 470k ukigawa kwa siku 30 analamba elfu kumi na tano kwa siku, ukigawa kwa 22 siku baada ya kutoa siku nane za weekend analamba elfu 21 na kitu, sasa 15k au 21k kwa bodaboda mbona ni pesa ndogo sana na hapo huyo ana barchelor kabisa
Kabisa mkuu bora umefafanua
 
Mwalimu pekee Tanzania niliewahi kumkuta na kumuona anaakili ni mchaga mmoja yuko mpanda huko, alipofika kule wenzake wanahangaika kuhama kule yeye akaanza kutafuta mashamba akawa anapanda miti ya mbao, alivonihadithia haraka sana akaanza kutafuta mashamba akawa analima mpunga, kila mwaka anaongeza ardhi, kiasi miaka ile nafika kule yule mchaga alikua miti hajaanza kuvuna lakini mpunga ana stock hadi gunia 700, huyo nilikaa chini kumsikiliza nikaona hakuna mchaga fala hasa akikuta kuna ardhi sehemu, yule kwa sasa nadhani atakua mbali sana,
 
Walimu hawana hela,..bora mwalimu wa kike anaolewa!mwalimu anakopa mkopo ananunua gari atatumikia mkopo wake miaka 15 mpka amalize...kingine walimu wengi hawajipendi wanakuja shuleni hawabadili nguo...wanawaza kuwahi wanafunzi wawachape ...sio makosa Yao ila ilibidi serikali iwaangalie upya ...mwalimu amekadiliwa mshahara ili mradi isife na njaa tu!

Au naongea uwongo wakuu!
Kweli kabisa [emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
 
Mwalimu pekee Tanzania niliewahi kumkuta na kumuona anaakili ni mchaga mmoja yuko mpanda huko, alipofika kule wenzake wanahangaika kuhama kule yeye akaanza kutafuta mashamba akawa anapanda miti ya mbao, alivonihadithia haraka sana akaanza kutafuta mashamba akawa analima mpunga, kila mwaka anaongeza ardhi, kiasi miaka ile nafika kule yule mchaga alikua miti hajaanza kuvuna lakini mpunga ana stock hadi gunia 700, huyo nilikaa chini kumsikiliza nikaona hakuna mchaga fala hasa akikuta kuna ardhi sehemu, yule kwa sasa nadhani atakua mbali sana,
Bora huyu alijiongeza Hawa wengine akili Hawana
 
Bora huyu alijiongeza Hawa wengine akili Hawana

Kabisa shida ajira za ndugu zetu akifika bush anawaza ahame, muda unakimbia mara miaka minne yupo pale pale, na hajafanya chochote kwa kuamini white color job inalipa, wakati kwa dunia ya tatu sio, wako wachache sana waliopenya kwa juhudi japo wengi wanakula msoto tu
 
Ni kweli kabisa,boda boda wanapata pesa nyingi halafu kwa mda mchache ila tatizo hawa binadamu wanapenda sana chini.Nashauri serikali iwape elimu hawa watu namna ya ku-manage pesa zao.
 
Walimu hawana hela,..bora mwalimu wa kike anaolewa!mwalimu anakopa mkopo ananunua gari atatumikia mkopo wake miaka 15 mpka amalize...kingine walimu wengi hawajipendi wanakuja shuleni hawabadili nguo...wanawaza kuwahi wanafunzi wawachape ...sio makosa Yao ila ilibidi serikali iwaangalie upya ...mwalimu amekadiliwa mshahara ili mradi isife na njaa tu!

Au naongea uwongo wakuu!

Hata uvaaji wao vyuoni utawajua tu, tofauti na course nyingine watoto wa BBA, Sheria wakipita unajua kabisa huyu sio mwalimu, na akipita ticha unajua kabisa huyu kweli ticha maana atakupigia bwanga moja lenye panga, na shati la kung’ang’aa na ndula moja kisigino kiko upande na saa yake ya buku tatu jero, hapo utawafaidi wakiwa ndio first year maana wakizoea mazingira wanachapa Kadet za mtumba
 
Japo ukipata mke mwalimu chukua oa haraka sana hua wanatunza familia vizuri walio wengi maana saikolojia inawasaidia
 
Ni kweli kabisa,boda boda wanapata pesa nyingi halafu kwa mda mchache ila tatizo hawa binadamu wanapenda sana chini.Nashauri serikali iwape elimu hawa watu namna ya ku-manage pesa zao.
Ila Kwa pesa mwalimu hanusi
 
Back
Top Bottom