Ukweli ni kwamba kama Nchi tunahitaji watu kama Tundu Lissu na Hayati Magufuli walioboreshwa

Ukweli ni kwamba kama Nchi tunahitaji watu kama Tundu Lissu na Hayati Magufuli walioboreshwa

Tofauti: Lissu kwake utawala wa sheria ndio kila kitu. Hakuna aliye juu ya sheria na hakuna huruma katika kutekeleza sheria. Hakuna mtu kusamehewa hata kama kakosea kwa “nia njema”. No flexibility, no leniency, no double standards. Ni adhabu tu. Hapo ndipo ulipo udikteta wa Tundu Lissu.
Kama ni wa kufuata sheria, sioni ni jinsi gani unaweza kuwa u-dikteta.

Lakini hata tukiupa jina la udikteta; udikteta huu ni mzuri sana kwa mazingira kama yaliyopo Tanzania. Watu hapa wanapenda kusukumwa ndipo waweke bidii kwenye maisha yao. Maofisini, hivyo hivyo.

Unajuwa, pamoja na kuwa na kinachoitwa 'Democracy' katika baadhi ya nchi, lakini viongozi wa nchi hizo walionekana kufanya udikteta ilipohitajika kuwa hivyo ili kuleta mabadilko ya haraka katika nchi zao. Korea Kusini ni mfano mzuri sana wa hali hii.

Tanzania sasa hivi tunataka sana kiongozi asiyechezea mali za umma kwa njia yoyote. Tunahitaji kila hicho kidogo kusukuma mbele maendeleo ya nchi hii.
Kuchekacheka kwa akina Kikwete/Samia, hakutupeleki kokote.
 

Bado naamini TL ni presidential material aandaliwa .
Your browser is not able to display this video.
Yaliyosemwa hapa hata TL angekuwa CCM kwa nafasi ya JPM yasingekuwa na Tofauti .​
Huko unakokusema "kuandaliwa" ndiko "kuharibiwa," kama hujui.

Tundu Lissu hana hulka za kishetani shetani alizokuwa nazo Magufuli. Kwa upande huo kuna tofauti bayana.
 
Yaliyosemwa hapa hata TL angekuwa CCM kwa nafasi ya JPM yasingekuwa na Tofauti .
Dah, nilikuwa sijaisikiliza hii hotuba ya Magufuli.
Sasa nimeisikiliza na mara moja swali likaniijia kichwani: Hivi Samia alishawahi kuisikia hotuba hii?

Inawezekana sana alikwisha isikiliza na yeye akahitimisha, kama alivyofanya Magufuli, kwamba "aliyofanya Magufuli ni ya Magufuli, yeye Samia atafanya yake"

Lakini kuna tofauti kidogo. Samia hajawahi kusimama na kuomba uongozi kwa waTanzania ili akipewa fursa hiyo, afanye anayotaka kufanya yeye, na siyo yale Magufuli aliyochaguliwa ayafanye. Samia amefanya makosa, kutoendeleza yale yaliyokuwa yakifanywa na mwenye serikali yake, Magufuli; Samia akiwa msaidizi tu!
 
Habari JF , TL na JPM personality zao zinafanana sana ukiachana tofauti zilizopo za kisiasa na ni wazalendo kweli kweli

Hivyo Kiuhalisia hakuna zuri ambalo JPM alifanya Tundu lissu asingefanya ukiachana na matamshi ya TL kulingana na kuwa nje box .

Vivyo hivyo hakuna baya ambalo JPM alifanya TL hawezi fanya kama hatoboreshwa .

JPM pamoja kuwa Rais bora alihitaji maboresho yafuatayo ambayo hata TL anahitaji
1. Kupokea ushauri ,kuutafakari kama mzuri kuufanyia kazi .

2.Kukubari kukosolewa , yaani sio mtu akikosoa anakuwa adui

3.Kama binadamu huwezi kuwa sahihi muda wote ,hivyo ni vizuri kufikiri zaidi kabla ya kutenda au kusema .

Bado naamini TL ni presidential material aandaliwa .
View attachment 2985467
Yaliyosemwa hapa hata TL angekuwa CCM kwa nafasi ya JPM yasingekuwa na Tofauti .

Ni mtazamo tu wana CDM na CCM muelewe .​
Uko sawa kabisa mkuu, atakayebisha ameamua kubisha tu!
 
Tofauti: Lissu kwake utawala wa sheria ndio kila kitu. Hakuna aliye juu ya sheria na hakuna huruma katika kutekeleza sheria. Hakuna mtu kusamehewa hata kama kakosea kwa “nia njema”. No flexibility, no leniency, no double standards. Ni adhabu tu. Hapo ndipo ulipo udikteta wa Tundu Lissu.

Bila kusahau msimamo wa Lissu kuwa akiingia madarakani kazi yake ya kwanza itakuwa kukamilisha mchakato wa katiba mpya itakayoleta demokrasia ya kweli nchini. Tumuamini au tusimuamini?

Magufuli kwake sheria hazikuwa na maana bali “uzalendo” na “maslahi ya taifa”. Kwenye hayo ikibidi kwake yeye ni “hatufungwi na sheria”, zinaweza kupindishwa hata kutupiliwa mbali kama akiona zinapishana na mtazamo wake kuhusu uzalendo na maslahi ya nchi. Kwake sheria zinachagua mahali na watu wa kushughulikiwa kulingana na “maslahi ya taifa” - kwa uwazi hata gizani.

Hizo ndizo tofauti za udikteta wa Magufuli na unaodhaniwa kuwa wa Lissu akiwa madarakani. Na katika mazingira ya katiba iliyopo.
Lissu akiingia madarakani hata hizo sheria hawezi fuata
 
Lissu akiingia madarakani hata hizo sheria hawezi fuata
Sawa. Huenda unamfahamu zaidi. Sijui.

Mimi nilivyomuona miaka mingi ni kuwa Lissu anaogopwa sana kuwa “hana ustaarabu” sheria zinapovunjwa au kupindishwa. Hasiti kumuita hata Rais “mwizi” au “fisadi”. Fikiri mtu wa aina hiyo akiingia madarakani patashika itakayotokea.

Kama ulikuwepo utaikumbuka orodha ya mafisadi (List of Shame) iliyosomwa Mwembechai 2007 na Dr Slaa. Unajua ilivyovyoandaliwa? Pia unajua kuelekea uchaguzi wa 2010 Rais JK alisema “heri ya Dr Slaa kuwa Rais kuliko Lissu kuwa mbunge”. Unajua kwa nini?
 
Sawa. Huenda unamfahamu zaidi. Sijui.

Mimi nilivyomuona miaka mingi ni kuwa Lissu anaogopwa sana kuwa “hana ustaarabu” sheria zinapovunjwa au kupindishwa. Hasiti kumuita hata Rais “mwizi” au “fisadi”. Fikiri mtu wa aina hiyo akiingia madarakani patashika itakayotokea.

Kama ulikuwepo utaikumbuka orodha ya mafisadi (List of Shame) iliyosomwa Mwembechai 2007 na Dr Slaa. Unajua ilivyovyoandaliwa? Pia unajua kuelekea uchaguzi wa 2010 Rais JK alisema “heri ya Dr Slaa kuwa Rais kuliko Lissu kuwa mbunge”. Unajua kwa nini?
Huwezi fuata sheria na still ukaweza leta maendeleo na kusimamia haki ,ndio maana nchi kama China ,Russia hawasaini mikataba ya kimataifa ya haki za Binadamu .
 
Habari JF , TL na JPM personality zao zinafanana sana ukiachana tofauti zilizopo za kisiasa na ni wazalendo kweli kweli

Hivyo Kiuhalisia hakuna zuri ambalo JPM alifanya Tundu lissu asingefanya ukiachana na matamshi ya TL kulingana na kuwa nje box .

Vivyo hivyo hakuna baya ambalo JPM alifanya TL hawezi fanya kama hatoboreshwa .

JPM pamoja kuwa Rais bora alihitaji maboresho yafuatayo ambayo hata TL anahitaji
1. Kupokea ushauri ,kuutafakari kama mzuri kuufanyia kazi .

2.Kukubari kukosolewa , yaani sio mtu akikosoa anakuwa adui

3.Kama binadamu huwezi kuwa sahihi muda wote ,hivyo ni vizuri kufikiri zaidi kabla ya kutenda au kusema .

Bado naamini TL ni presidential material aandaliwa .
View attachment 2985467
Yaliyosemwa hapa hata TL angekuwa CCM kwa nafasi ya JPM yasingekuwa na Tofauti .

Ni mtazamo tu wana CDM na CCM muelewe .​
Naunga hoja mkono nanina uhakika kwa sasa hakuna anayeweza kuirudisha nchi kwenye mstari tofauti na lisu ili hata ccm wenyewe ukiwauliza watakueleza kwa lisu ndio mbadala wa jpm
 
Naunga hoja mkono nanina uhakika kwa sasa hakuna anayeweza kuirudisha nchi kwenye mstari tofauti na lisu ili hata ccm wenyewe ukiwauliza watakueleza kwa lisu ndio mbadala wa jpm
Usije ukawa ndio TL mwenyewe
 
Magufuli na Lissu wote ni watu wapgania haki Wazalendo na hawapendi kuburuzwa ila JPM hana mfano kwa hawa waliopo he was something else, special and very unique person.
 
Back
Top Bottom