Ukweli usemwe: P Funk ndio mtu mnyonyaji zaidi kuwahi tokea kwenye historia ya Bongofleva

Ukweli usemwe: P Funk ndio mtu mnyonyaji zaidi kuwahi tokea kwenye historia ya Bongofleva

So yeye anaweza kukusanya watu wakufanya Production tu??? Kama Dj khaled anawaita mnatia verse mnakula mpunga wimbo wakee...
Afadhali dj Khaled mtu anapigwa mpunga wa maana pfunk studio kwake ana gym yeye anapiga gym choma embassy zakutosha,choma kaya bia zakutosha yeye anamalizia mixing pale studio kwake kunakuwa na mamluki wa kutosha njaa yako umaskini wako hela yakiboya bado anakuoshea hata hadharani
 
Nakumbuka sio movie, ni ngoma sijui nikusaidiaje ile biti akauziwa tena chameleone akaimbuia bomboclat.. Jay kuulizia p kaishakula hela, chameleone akataka kumpa tena hela Prof akaamua wapige kolabo, ngoma nimeisahau jina.
Nooo nooo nooo ni movie imefanyika Hollywood, awali jamaa Wenye movie walidhania kuwa mwenye haki ya beat ni chamilion , chamilion alitaka kupiga mpunga ndio p funky akasanukia mchongo akaenda usa kufuata haki yake
 
Pamoja na yote uloyoeleza P Funk_Majani ana mchango mkubwa kwenye game kuliko Sallama (Sallam),P ni bulldozer,ni miongoni mwa waandaaji wa muziki walioibeba Bongo fleva kwenye mabega yao mpk hapa ilipofika ame_inspire vijana wengi kuingia kwenye game,kwa kuimba,kuchana na kuwa na record label,tuheshimu wahenga
 
Nooo nooo nooo ni movie imefanyika Hollywood, awali jamaa Wenye movie walidhania kuwa mwenye haki ya beat ni chamilion , chamilion alitaka kupiga mpunga ndio p funky akasanukia mchongo akaenda usa kufuata haki yake
Umenikumbusha hii ishu, ni kweli P ndie alienda USA kufata pesa ambayo ilikua apewe Chamillion.... Nakumbuka aliporudi Watu walihoji sana kama alimpa chochote Jay na P mwenyewe alipotea kwa muda mrefu kabla ya kuibuka tena.
 
Kijana wa wcb mishipa imekusimama kweri-kweri.

Jibuni hoja za P.funk kwanini Mbosso halipwi pesa yake kama writer wa mashairi anayomuandikia ya Diamond?

Kwanini publishing rights za producer S2kizzy kwenye platforms zimechezeshwa ili asitambulike kama mbunifu wa midundo yote aliyofanya na wcb kiasi kwamba amekosa malipo yake zaidi ya million 110 ????

Mbosso anasepa soon, kaa mkao.
[emoji848][emoji28][emoji28][emoji28][emoji419]
 
hivi producer si anasikiliza wimbo na idea ya msanii ndo anatengeneza beat?? au msanii anapewa beat aweke mashairi??? maana kama unamlipa akutengenezee beat means utakuwa unaimiliki...lakini pia unaweza nunua beat may b kama huwa hela yake ni mamilion
Inategemea sio lazima asikilize nyimbo ya msanii kama siku hizi ndio hawafanyi hivyo kabisaaa now days pro ana nyonga beat Kwa feeling zake Kisha anampatia msanii ambaye ana mudu kupita humo
 
Wakuu kuna wakati ukweli lazima usemwe. Mambo ya kusema mtu aheshimiwe kwa kuwa alikuwa anatengeneza beats nzuri hizo ni heshima za uoga.

P Funk ambaye kiukweli zaidi ya kufanya production ya muziki na kupokea malipo hana jingine kubwa alilolifanyia bongofleva.

Kwa wasiofahamu wasanii wote waliokuwa chini ya bongo records hawana nyimbo au album wanazomiliki vyote anamiliki P Funk.

Ngwea amekufa maskini huku muziki wake unamilikiwa na P Funk mpaka leo anakula hela ya Ngwea.

Ukiona wimbo wa Juma Nature au Feruzi kwenye YouTube, Boomplay au digital platform yoyote usidhani ukisapoti unamsaidia msanii hiyo ni pesa ya Majani. Leo hii ikitokea bahati mbaya Juma Nature hatupo nae watoto wake watarithi nothing utajiri wake wa nyimbo ni mali ya watoto wa Majani kina Paula.

Huyu P Funk aliyekuwa anawapiga ngumi na mitama watoto wa kimaskini wakienda kuomba msaada wa kurekodi nyimbo zao.

Kumbuka pale bongo records kwenye utengenezaji wa beats waliusika watu wengi zeze ilitengenezwa na bizimani ila achukui hata sh 10, beat ya mikasi alitengeneza prof ludigo ila achukui hata sh 10 kina Marlon linje walikuwa wanapiga vinanda na vyombo vingine kwenye kutengeneza instrumental za wasanii haki zao za ubunifu anachukua nani kama sio mnyonyaji p Funk?

P Funk tunamuheshimu kwa kutengeneza beats ila zaidi ya production kaufanyia nini huu muziki?
P Funk uwa wakiitwa wasanii walipwe yeye anaenda kuchukua malipo kama nani? Kina Daz Baba wamekuwa vituko mtaani hela zao kwa nini unakula wewe PFunk?

Hii thread haiusiani na tukio lolote bali ukweli usiozungumzwa.
Kuna kitu kinaitwa mkataba unakifaamu? Kama hao wasanii waliona unayonyaji kwanini wali saini?
 
P Funk anakula mpaka hela za marehemu Ngwea. Yeye p Funk anajinadi kama anapaza sauti juu ya haki za wasanii vipi mbona yeye anawanyonya mpaka leo?

Haki za ubunifu kwenye midundo mbona anawatapeli wenzie?

Tukemee unyonyaji wa P Funk
Hujajibu hoja
 
Producer anasema ile beat aliyokupa unaweza kuitumia utakavyo (sasa ile sio master) lakini master anayo yeye na anasema anastahili kuitumia atakavyo.

Yaani ni sawa na kitabu, ukishanunua unaweza hata kukichana na kuwashia moto lakini mtunzi au mchapaji atauza nakala nyingine (sio nakala yako) ila ni nakala nyingine ya kitabu hichohicho. Kwa hiyo hata magari, unanunua na kumiliki nakala lakini kumiliki kwako wewe hakuwazuii toyota kumuuzia jirani yako gari kama unalomiliki wewe. Ndio muono wa maprodusa
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28] kazi kweli kweli
 
Mbona Mimi nilikuwa msanii wa diamond na napata pesa yangu always
 
Wanakuwa wameipenda wenyewe. Ila wakati mwingine huwa wanatoa tangazo watu walete kazi zao ili zitumike kama soundtrack, wanatoa idea ya movie na kusema nyimbo ziwe na maudhui hayo, ila mara nyingi ni kwa wao kupenda nyimbo zilizotoka tayari.

Kwenye Sometimes in April movie, walitumia kinyemela wimbo wa Dataz ft Soggy Doggy; Soggy alipofuatilia walilipwa hela yeye na Dataz
Walilipwa kiasi Gani!?
 
Nimebaki nacheka tu hapa Ndugu Mdau. Comment zako zinanifurahisha Sana. Eti "hakuwazuii Toyota kumuuzia jirani yako, gari Kama lako". Sipati picha jamaa anaenda Toyota kupiga mkwara jirani yake asiuziwe gari Kama yake yeye.
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
 
Kwa hiyo yeye kuwanyonya wenzie ndio sawa?
Kazi walizofanya kina Jay Moe, Nature, Feruzi, Mangwea etc unaona ni ndogo wasipate chochote kwenye ubunifu wao. Yeye kama ni producer mzuri angekuwa anatoa album za beats peke yake aone kama kuna mtu angenunua
Na hao wasanii wangetoa nyimbo zao bila biti waone kama zitauza.
 
Kwenye production na ubunifu kuna hakishiliki... walioshiriki kutengeneza beats mgao wao mbona hawapewi? Nyimbo nyingi pale yeye alikuwa anafanya mastering tu na mixing ila ubunifu wanafanya kina bizimani lakini anatepeli jasho lao. Huo ni unyonyaji na uzuri yeye amejipambanua kama mtetezi wa haki za wabunifu.
Ina maana hao akina bizman walikua hawajui kama wananyonywa?
 
Music publishing ni ishu tata sana. Sio huku kwetu tu bali hata huko kwa walioendelea. Kuna mifano kadhaa ya wanamuziki wakubwa ambao walitangaza kufilisika (bankruptcy) licha ya "kuuza" mamilioni ya kopi za rekodi. Mfano Toni Braxton, TLC n.k. Lakini huo ni mjadala wa siku nyingine.

Typical music production (unless kila kitu mpaka kuimba amefanya mtu mmoja) huwa inahusisha producers, composers, melody makers, session musicians na engineers. Hawa huwa wanakuwa na haki zinazoitwa mechanical rights za huo wimbo. Ukiangalia hapo sijamtaja mtu mmoja, MUIMBAJI/WAIMBAJI. Hawa wanakuwa na haki za uimbaji (singing right) kwenye huo wimbo.

Tafsiri ya rights zilizotajwa hapo juu ni kwamba kwa namna fulani KILA mtu aliyeshiriki kutengeneza huo wimbo (unless kwa sababu fulani amekubali kufanya bure) anatakiwa kulipwa. Analipwaje ndio mjadala ninaouona kwenye huu uzi. Suala la mshiriki kwenye production atalipwaje huwa liko kimkataba, inaweza kuwa malipo ya mara moja au percentage fulani ya publishing (wenzetu wanaitaga points). Kuna watu wamesema kwamba P Funk amepora haki ya watu aliofanya nao kazi ya production. Tutajuaje kama P alishamalizana nao kimalipo na wakaachia rights zao za publishing? Je, hizo haki zao zimesajiliwa kisheria? Hii ishu nitaijadili kidogo huko mbele.

Again, typical music production huwa inasimamiwa Producer. Kwenye music production kumekuwa na tatizo la watu kuchanganya producer na beat maker au session musician. Kwa kawaida huwa inategemewa producer awe pia musician ili awe na uwezo wa kuendesha zoezi zima la production. Lakini SIO lazima yeye apige vyombo au kufanya programming kwenye huo wimbo unaotengenezwa. Kuna mtu kasema "P Funk hajui hata kupiga kinanda", kwanza sio kweli, P Funk anaweza kupiga kinanda, pili ili awe ame-produce wimbo fulani sio lazima personally afanye beat making, yeye anahakikisha kila mhusika ana-play role yake na standard ya production inakuwa per exellent. Producers wengi wakubwa huko duniani huwa hawapigi vyombo wao wenyewe bali hutumia session musician au beat makers mfano Quincy Jones, Dr Dre, P Diddy, Irv Gotti etc.

Sasa tuje kwenye ishu tata ya hatimiliki aka publishing. Tofauti na watu wengi wanavyoamini, publishing rights sio automatic. Ni lazima ziwe zimesajiliwa kisheria (registered) ili zilindwe, kama umefanya kazi yoyote ya ubunifu bila kuisajili wakatokea wajanja wakasajili imekula kwako. Jamaa watapiga hela huku wewe ukipiga miayo. Huku kwetu nina uhakika kuanzia wasanii, wapiga vyombo na wengineo walikuwa hawalijui hilo ndio maana watu wengi wakiwemo wasanii wanaamini kwamba akienda studio akalipia kurekodi wimbo automatically unakuwa mali yake. Kitu ambacho sio kweli.

Sijajua mikataba ambayo wasanii wa hapa kwetu (wakiwemo wa WCB) huwa wanaingia na lebo huwa ina-address suala la publishing au hapana. Ambacho nina uhakika nacho ni kwamba wasanii wengi (hasa wa zamani) hawako aware kuhusu ishu ya publishing, na ndio mzozo wa Prof Jay na P Funk ulipoanzia.

Actually ishu ya Prof Jay na P Funk kuhusu beat ya nikusaidiaje haikuanzia kwenye beat hiyo kutumika kwenye movie. Baada ya Prof Jay kurekodi wimbo huo na kuhit, Chameleone akamfuata P akitaka atumie hiyo beat, P akamchaji Chameleone USD 2,000. Prof aliposikia akaja juu na kulalamika kwamba beat yake imeuzwa bila idhini yake. Lakini kiukweli Prof hakuwa ma haki yoyote kwa kuwa Chameleone alitumia beat tu, sio wimbo wote. Wimbo wa Chameleone ukaja kutumika kwenye movie ya Queen of Kitwe iliyotengenezwa na Disney na Chameleone akavuta mpunga. P akakomaa na Disney na kwa kuwa sheria ilikuwa upande wake alalipwa. Again Prof hakuwa na haki kwani wimbo uliotumika ni wa Chameleone na sio wa kwake.

Hitimisho ni kwamba music business is very shady, inatakiwa msanii ajifunze SANA sheria za hatimiliki na ahakikishe haki zake ziko documented na zimesajiliwa kisheria ili zilindwe.
Hii comment Iko na madini yote

Case closed, Uzi ufungwe
 
Ulisema kuwa P funk alikuwa hafanyi lolote zaidi ya kutengeneza beats na jamaa kakwambia alihusika hadi kwenye kusukuma kazi

Ukisikiliza interviews nyingi za producers wa zamani utajua kuwa walikuwa wanamsimamia msanii hadi sokoni na kuzipush nyimbo kwenye media houses. Inshort walikuwa wanafanya kazi hadi za managers

Wangekuwa ni beat makers tu bhasi majani na jay wasingepata hiyo heshima waliyonayo
Naam naam [emoji419][emoji16]🥱
 
Back
Top Bottom